Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)

Watu wengi wanatamani kununua hisa kupitia soko la Hisa la Dar es salaam ila bado hawafahamu ni jinsi gani wanaweza kununua hisa wakiwa mahali popote pale Tanzania. Soko la Hisa limetengeneza njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kununua hisa akiwa sehemu yoyote ile Tanzania.

Unapohitaji kununua Hisa katika soko la Hisa unatakiwa kuwa na email, akaunti ya bank na kuwa na mawasiliano brocker yoyote Yule ambaye amesajiliwa katika soko la Hisa.

SOMA; Soko la Hisa la Dar: Fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wazalendo Tanzania

Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa

Baada ya kufanya maamuzi ya kampuni gani ya kununua katika soko la Hisa. Unaweza kutamfuta brocker ambaye amesajiliwa na soko la Hisa kwa ajili ya kununua hisa zako.

1. Wasiliana Brocker kwa ajili ya kununua hisa

Wasiliana na brocker yoyote ambaye amesajiliwa katika soko la hisa. Baada ya kuwasiliana na brocker ataomba email yako kwa ajili ya kukutumia fomu za kujaza. Utaprint fomu hizo ambazo zitakuwa mbili; moja kwa ajili ya taarifa zako binafsi na nyingine kwa ajili ya ununuzi wa hisa.

Hii ni orodha ya Brockers waliosajiliwa na soko la Hisa

· CORE securities Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 212 3103 au info@coresecurities.co.tz

· Orbit Securities Co. Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1758 au orbit@orbit.co.tz

· Rasilimali Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1711 au rasilimali@africaonline.co.tz

· Tanzania Securities Ltd; Tel: +255 22 211 2807 au info@tanzaniasecurities.co.tz

· Vertex International Securities Ltd; Tel: +255 22 211 6382 au vertex@vertex.co.tz

· Solomon Stockbrokers Co. Ltd; Tel: +255 22 211 2874 au solomon@simbanet.net

· E.A. Capital Ltd P.O. Box 20650, Dar es Salaam au Tel +255 779740818/ +255 784461759
EC@EACAPITAL-TZ.COM

· ZAN Securities  Ltd P.O. Box 5366, Dar es Salaam au Tel +255 22 2126415
info@zansec.com

2. Jaza fomu ulizopewa

Baada ya kuprint fomu ulizotumiwa utajaza kutokana na mahitaji ya fomu husika. Baada ya kumaliza kujaza fomu zako, utazi scan zote na kuzituma kama attachment kwenye email ya brocker na kusubiri majibu kutoka kwake.

SOMA; Msingi na ustadi wa kuwekeza kwenye Soko la Hisa

3. Utatumiwa kiasi cha kutuma na akaunti ya benki kwa ajili ya kuingiza pesa

Baada ya kutuma fomu zako kwa brocker atazipitia na kujua ni kiasi gani ulipie ili uweze kununua hisa hizo. Baada ya kupata akaunti ya benki ya utaingiza kiasi cha pesa ambacho umeambiwa kwenye akaunti ya kampuni ya brocker. Baada ya kulipia benki pesa za ununuzi wa hisa uta scan risiti ya benki.

4. Tuma risiti ya benki ambayo umescan kwenye email ya brocker

Baada ya kuscan risiti ya benki utatuma kwa brocker ili kuthibitisha kuwa umefanya malipo hayo kwenye akaunti yao na wewe ni muhusika. Baada ya kutuma atakujibu kuwa amepata na usubiri hisa zako kununuliwa.

SOMA; Hatua Muhimu Kuzifahamu Unapohitaji Kuwekeza Katika Hisa.

5. Subiri kununuliwa kwa hisa zako

Baada ya kupitia hatua zote, subiri kwa ajili ya kununuliwa kwa hisa zako. Kutoka na kupanda na kushuka kwa bei unaweza kumwambia kuwa brocker anunue hisa zako kulingana na bei ya soko hii ni kwa sababu wakati unajaza fomu ulipanga bei ya kununulia.

Kumbuka: Vitu vyote nilivyoelewa unaweza kufanya ndani ya siku moja ikiwa utawasiliana na brocker mapema na kufanya kwa uharaka. Vile vile unaweza tumia gmail akaunti kwa urahisi wa utumaji wa taarifa zako.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

Mambo Matatu Ya Kuzingatia Katika Msamaha.

Msamaha una pande mbili kuwasamehe waliokukosea na kusamehewa na wale uliowakosea. Ni tendo linalotokana na wawili ,mmoja amekosa na wa pili amekosewa. Hivyo Kusamehe au kusamehewa ndio msamaha ambao huweza kuleta maelewano kati ya pande hizo mbili yaani mkosaji na mkosewa .

Tatizo kubwa la mwanadammu ni ile tabia ya kutokukubali kosa. Watu wengi wanashindwa kusamehe au kukubali msamaha kwa sababu hawajui maana ya msamaha. Kusamehe sio kusema, bali ni zaidi ya kutamka kwa mdomo. Kusamehe ni kumaliza chuki yote na maumivu yote yaliyo ndani ya moyo. Pande hizi mbili zikisameheana ( mkosaji na mkosewa ) makosa yote hufutwa na haibakii tena hatia juu yao kutokana na makubaliano yaliyofanyika kati ya hao wawili.

YAJUE MAMBO MATATU AMBAYO LAZIMA YATOKEE KATIKA MSAMAHA WA KWELI

  1. KUMPENDA ALIYEKUKOSEA

Upendo huu sio ule wa mdomoni bali wa kutoka ndani na kutokuwa na uchungu tena moyoni, hasa kusaidiana katika shida na raha ili kudumisha upendo. Wapo watu wengi waliosema wanasamehe lakini hawana mawasiliano na wale waliowakosea, huu sio msamaha, kumpenda aliyekukosea itakufanya uwe huru.

  1. KUSAHAU KOSA

Ingawa kibinadamu inaonekana ni vigumu kusahau kosa ulilotendewa lakini mbele ya Mungu inawezekana . Hivyo basi ukijiona kuwa umetoa msamaha au umepokea msamaha lakini kosa lililotendeka bado linakurejea katika akili yako basi ujuwe msamaha huo bado haujawa msamaha. Jitaidi kusahau,rudisha moyo wa ukarimu juu yake ili kuboresha mawasiliano ya awali.

  1. KUMWOMBEA

Yampasa mtu aliyetoa msamaha wa kweli amwombee Yule aliyemkosea, sio kumlaani bali ni kumshauri na kumwombea baraka ili afanikiwe katika maisha yake. Watu wengine huwaombea adui zao mabaya huo sio msamaha unapomwombea mwenzako nawe unabarikiwa na kusahau kosa.

HASARA ZA KUTOSAMEHE

Kuna hasara nyingi sana kama mtu hujasamehe na hizi ni baadhi tu,

1. Tunajifungia milango ya baraka sisi wenyewe

2. Unashindwa kufikiria maendeleo

3. Unakuwa na chuki na maumivu moyoni mwako

4.Unakosa afya njema

5.unakuwa mtu wa mawazo tu

Hivyo basi kutosamehe katika maisha yetu tunajizibia milango ya baraka katika maisha yetu,mwandishi wa kitabu cha The Miracle of your Mind anasema kuwa ‘’ Do not poison yourself through hatred, begin to forgive’’ Maana ni kwamba usijiwekee sumu mwenyewe kwa kupitia chuki, pia ametuasa tuanze sasa kusamehe.

‘’The feeling of wealth produces wealth, the feeling of being successful produces success’’ hivyo basi hisia za kitajiri au mali huzaa mali au utajiri vivyo hivyo katika hisia za chuki huzaa chuki na siyo mafanikio, weka sana akilini mwako maneno hayo kila mara katika maisha yako.

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza ukawasiliana naye kupitia simu 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com

Jinsi Ya Kuondokana Na Hofu/ Woga

Hofu ni hali ya kuwa na wasiwasi wa kitu fulani kibaya kutokea lakini kitu hicho huwa bado hakija tokea.

Kama binadamu kila mmoja hupatwa na woga kwa nyakati tofauti. Woga huu hugusa maeneo mbalimbali katika maisha ya kila siku yaweza kuwa kazini, katika mahusiano, katika matembezi,kwenye ndoa. N.k.

Kila binadamu anahofu yake.

SOMA; Orodha Mpya Ya Mabilionea; Mambo Kumi Ya Kuzingati Ili Na Wewe Uweze Kuingia Kwenye Orodha Hii Siku Za Baadae.

Hofu inaweza kuwa mbaya au hofu nzuri kutegemeana na hofu uliyonayo. Mfano hofu ya kupoteza pesa baada ya kusikia kuna mahali ukihifadhi pesa kwa wiki moja utapewa mara tatu zaidi. Hii ni hofu nzuri. Inawezekana ukajiuliza kitu kama hiki kinaukweli gani, mbona hakuna utarartibu kama huu hapa ulimwenguni wa kuweka pesa na kukaa tu halafu baada ya wiki ukapewa maratatu ya pesa hizo.

Waswahili wanasema woga wako ndio umasikini wako. Kuna baadhi ya watu huogopa kufanya jambo lolote kwa kuwa na fikra hasi za baadae. Ni vizuri kuchukua tahadhari kwa kila jambo unalotaka kulifanya na sio kuogopa tuu. Kumbuka kuwa uoga ni wasiwasi wa kitu kuleta matokeo mabaya, sio kwamba jambo baya limeshatokea tayari.

NINI CHANZO CHA HOFU/WOGA

Chanzo cha hofu au woga ni hisia za ndani ambazo zimejengeka katika jamii yetu kutoka kwa wazazi wetu na watu wa karibu wanaotuzunguka au watu ambao wamepata matatizo fulani baada ya kufanya jambo fulani, hivyo kutufanya nasi kuwa na woga.. Mara nyingi tumekua tukiambiwa kuwa usiposoma huwezi kufanikiwa, huwezi kuwa kiongozi mkubwa,ukiwa tajiri utarogwa, matajiri wote ni wanyonyaji,huwezi kupata kazi kama huna mtu wa juu wa kukuunganishia,ndoa ni mbaya sana bora usioe au usiolewe na maneno mengine mengi ya kuogopesha. Maneno haya na mengine mengi yamejenga hofu za kila namna kwenye kila eneo la maisha yetu na hivyo kuyaona maisha ni magumu na mabaya kila tukikumbuka hofu hizo.

SOMA; Hizi ndio Hofu mbili ulizozaliwa nazo, nyingine ni uongo.

NAMNA YA KUONDOKANA NA HOFU NA KUISHI KWA FURAHA

Kuondokana na HOFU/WOGA huu sio jambo rahisi sana lakini habari njema ni kwamba kama ukiamua kwa dhati inawezekana kuishi bila hofu na woga utakaokufanya usitimize ndoto zako.

Kwanini sio rahisi, tumezungukwa na watu ambao wanatuogopesha hata ukijaribu kuondoa woga sauti zote zinazokuzunguka zitakuambia maneno ya kuogopesha. Inahitaji ufahamu kuwa wewe mwenyewe ndiye kiongozi wa maisha yako na unaweza kuamua kuachana na hofu hizo bila kusubiri mtu mwingine yeyote kukusaidia kuondo hofu hizo. Kwakua asilimia kubwa ya watu wanaotuzunguka wanahofu na woga. Wamekua katika mazingira hayo na woga na hofu imekuwa sehemu ya maisha yao.

SOMA; UKURASA WA 17; Hofu, Matumizi Mabaya Ya Ubunifu Wako.

UFANYE NINI SASA

Vile unavyoamini toka ndani ndivyo inavyokuwa katika ulimwengu wa nje. Ukiwa na hofu kuwa kila tajiri ni mdhulumaji basi utawachukia matajiri wote na wewe pia utaishia kuwa masikini na kuridhika na hali uliyonayo lakini bado hautakuwa na furaha kwasababu huwezi kukidhi mahitaji yako ya kila siku,

Kaa mahali penye utulivu na ujiulize ni hofu gani inayotawala maisha yako na inayozuia maendeleo yako?

Ni hofu gani uliyonayo? Andika hofu hiyo katika karatasi.

Fikiria kama kuendelea kuwa na hofu hiyo kutaleta mabadiliko yoyote mazuri katika maisha yako,

Jiulize kama unataka kuendelea kushikilia hofu hiyo mwisho wake utakuwa mzuri?

Je kuna namna unavyoweza kuchukua tahadhari kwa kuondoa hofu na kufanya jambo ambalo unahitaji kulifanya na unaona ni muhimu na litakamilisha furaha ya moyo wako. Andika namna utavyofikiri ni njia nzuri ya kuondoa hofu hiyo na kupata nguvu ya kutimiza ndoto yako.

SOMA; SIRI YA 24 YA MAFANIKIO; Fanya Licha Ya Kuwa Na Hofu.

Acha kabisa kufikiria hofu hiyo badala yake fikiria matokeo ya mwisho mazuri ya jambo utakalolifanya na endelea kuwa makini ukichukua tahadhari.

Fanya hivi kwa kila hofu inayokuzuia kuzifia ndoto zako. Baada ya muda utahisi umefunguka na unaishi kwa amani na furaha na mambo mazuri yanaendelea kutokea katika maisha yako.

Maisha ya furaha na amani yanawezekana. Chukua hatua sasa.

Mwandishi: Esther Ngulwa.

Mawasiliano: estherngulwa87@gmail.com

0767 900 110/ 0714 900 110/ 0784 576 131

Hatua Muhimu Kuzifahamu Unapohitaji Kuwekeza Katika Hisa.

Uwekezaji katika Hisa limekuwa jambo geni kwa watu wengi. Kwa kuwa mmiliki wa Hisa unapata fursa ya kuweza kuongeza kipato chako huku ukiendelea shughuli zako nyingine ambazo zinakuingizia kipato. Uwekezaji katika nchi yetu bado ni mchanga, kwa hiyo kuna fursa kubwa ya kuweza kutengeneza kipato. Kama unataka kuwa mwekezaji katika Hisa ni muhimu kufahamu hatua hizi.

SOMA; Soko la Hisa la Dar: Fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wazalendo Tanzania

Hatua Muhimu kuzifahamu unapohitaji kuwekeza katika Hisa

1. Fanya maamuzi kuwekeza

Kufanya maamuzi ni jambo zuri na inafanya akili yako kuwa tayari kwa ajilia ya kuingia kwenye uwekezaji huu.

2. Kufahamu ni sehemu gani ambayo unaweza kununua au kuuza Hisa

Ili uweze kuwa mmiliki wa Hisa ni lazima uweze kufahamu sehemu ambayo unaweza kununua Hisa zako. Kuna sehemu mbili ambazo unaweza kununua Hisa i) Kampuni inapouza Hisa zake kwa mara ya kwanza kabala kusajili katika soko la Hisa (IPO), ni vizuri ukanunua Hisa kwa kampuni ambayo inakaribia kusajiliwa katika Soko la Hisa; i) Unaweza kununua kupitia Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE) kwa kupitia mawakala wake.

SOMA; Msingi na ustadi wa kuwekeza kwenye Soko la Hisa

3. Kufahamu ni kampuni gani unahitaji kuwekeza

Katika soko la Hisa la Dar es salaam kuna kampuni ishirini na moja (21) ambazo zimesajiliwa na soko hilo. Unapohitaji kuwa mmiliki wa Hisa unatakiwa kuchagua Kampuni ambayo inakufaa kwa ajili ya uwekezaji wako. Katika kuchagua Kampuni unatakiwa kuwa na taarifa sahihi kuhusu kampuni hiyo na ufanisi wa kampuni hiyo katika soko la Hisa ili uweze kufanya uwekezaji wenye manufaa.

4. Muda mzuri kwa mwekezaji kununua Hisa

Kama mwekezaji ni vizuri ukafahamu muda mzuri kwako kununua Hisa wenye manufaa. Muda mzuri kwa mwekezaji kununua Hisa zake i) Kampuni inapouza hisa kwa mara ya kwanza kwa sababu mara nyingi kampuni bei zake huwa chini ya thamani halisi ili kuvutia wawekezaji ii) Kipindi cha januari hadi Machi kwa sababu watu wengi huuza hisa zao kwa shida mbali mbali na mara nyingi kipindi hiki Uchumi haufanya vizuri sana iii) Bei za Hisa zinaposhuka ila lazima utambue sababu ya kushuka kwa bei zake kama ni ya muda mfupi.

SOMA; Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

5. Muda mzuri kwa mwekezaji kuuza Hisa

Vile vile unapoingia kwenye uwekezaji katika Hisa ukafahamu muda mzuri wa kuuza hisa zako. Muda mzuri wa kuuza hisa zako ni pale kampuni inapokuwa haifanyi vizuri, bei zake zinaposhuka na zinaonyesha zitaendelea kushuka. Unapofanya maamuzi ya kuuza hisa zako ni vizuri ukawa na taarifa sahihi za Kampuni husika. Ni vizuri kwa mwekezaji akawa na malengo ya uwekezaji kwa kipindi cha muda mrefu.

6. Hatua ya mwisho unaweza kununua Hisa na kuwa mmiliki wa kampuni

Baada ya kupitia hatua zote hapo juu unaweza kufanya maamuzi ya kununua hisa katika soko la Hisa. Unaweza kununua hisa katika soko la Hisa kwa kupitia mawakala wa soko la hisa (Brockers) ambao wamesajiliwa na soko la Hisa au kununua hisa zinapouzwa na Kampuni kwa mara ya kwanza. Vitu vya msingi kuwa navyo unapohitaji kununua hisa i) uwe na email ambayo itakusaidia kutuma baadhi ya taarifa na akaunti ya benki.

SOMA; Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Hawa ni baadhi ya mawakala wa soko la Hisa (Brockers) ambao wamesajiliwa

CORE securities Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 212 3103 au info@coresecurities.co.tz

Orbit Securities Co. Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1758 au orbit@orbit.co.tz

Rasilimali Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1711 au rasilimali@africaonline.co.tz

Tanzania Securities Ltd; Tel: +255 22 211 2807 au info@tanzaniasecurities.co.tz

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

Sababu 5 Zinazokufanya Wewe Kuishia Kukopa Kila Siku.

Watu wamekuwa wakifanya kazi kila siku ili kuweza kupata pesa ya kuendesha maisha yao ya kila siku . lakini wengi wao wamekuwa na desturi ya kuwa na madeni kila siku na kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo .Kuna madeni ya aina mbili nayo ni madeni ya Mabaya na mazuri .Mazuri ni yale unayokopa kwa ajili ya kuanzisha mradi Fulani na mabaya ni yale ya kukopa kwa ajili ya kula na siyo kuzalisha .Hivyo basi madeni haya ndio yana kufanya wewe kubaki kuwa masikini na kushindwa kufanya shughuli za uzalishaji.

Tuangalie sababu hizo ni zipi zinazokufanya wewe kila siku unaishia kukopa .

1. KUTOWEKA AKIBA.

Wahenga wanasema hivi Akiba haiozi ,hivyo basi kumbe kujiwekea akiba itakusaidia wewe kuondokana na madeni ya kila siku na kuachana na kukopa kabisa.Unaweza kujiwekea akiba kila siku kulingana na kipato chako ambacho una kipata kupitia biashara yako au mshahara wako wa mwezi .Haijalishi una kipato kikubwa kiasi gani kama wewe ni mtu wa kutumia tu bila kuweka akiba wewe ni masikini,

FAIDA ZA KUWEKA AKIBA

· Itakusaidia kwenye dharura ya ghafla inayoitaji hela

· Itakusaidia kupata mtaji

· Akiba haiozi

· Akiba ni ulinzi wako

SOMA; Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.

2. KUTEGEMEA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO

Hili ni tatizo kwa watu wengi kutegemea chanzo kimoja cha mapato mfano,mtu anategemea chanzo kimoja tu cha mapato yaani Ajira .Huwezi kufikia katika eneo la kujidai ,eneo la kuwa na uhuru wa kipesa (comfort zone)kwa kutegemea chanzo kimoja cha mapato.Ili kuepukana na madeni kila siku ambayo hayana tija kwako .Anza leo kuwa na vyanzo vya mapato yaani ’’ multiple streams of income ,money machines’’.

Fanya vyanzo vyako vya mapato kuwa kama matawi ya mti utakuwa na uhuru wa kifedha.

3. KUISHI JUU YA KIPATO CHAKO

Hili ni tatizo kwa watu wengi ,kujiingiza katika gharama zisizo za kilazima mfano ,mtu anapokea mshahara laki na nusu halafu matumizi yake ni zaidi ya laki tatu.

Je unafikiri mtu atayaepuka madeni ya kila siku?­­­­ jibu ni hapana. Anza kuishi chini ya kipato chako leo ,acha tabia ya kuigaiga Fulani amenunua simu mpya na wewe unataka ununue ili mradi tu na wewe uonekane upo kwenye chati kumbe unajimaliza mwenyewe bila kujijua. Haijalishi unakipato kikubwa kiasi gani yakupasa uishi chini ya kipato chako. “whatever your income live below your means

SOMA; Hii Ndio Sababu Kwa Nini Watu Wanafurahia Pale Unapoanguka...

4. KUTOJILIPA

Watu wengi wanafanya kazi sana na wana walipa watu wengine lakini wanajisahau kujilipa wao kwanza .Wewe ndio mfanyaji kazi unatakiwa kujilipa kwanza wewe.

pay yourself first” jilipe kwanza wewe 10% ya kipato chako hii itakusaidia sana kujiwekea akiba na kuondokana na kukopa kila siku.Anza leo kujilipa kama ulikuwa haujui hii fungua akaunti maalumu kwa ajili ya kuhifadhi pesa yako na usiiguse ndani ya miaka miwili utakuw mtu mwingine.

SOMA; Nafasi Ya Wewe Kuwa Bora Kila Siku… NA ZAWADI YA TSH 365,000/=

5. KUISHI BILA YA KUJIWEKEA BAJETI YA MATUMIZI YAKO

Kuishi bila ya kuwa na bajeti ya matumizi yako kwa mwezi ,wiki, siku ni sawa na kusafiri bila ya kujua unapokwenda. Ukiwa na bajeti itakusaidia kujua matumizi yako ya kila siku na kuweza kujiepusha na kukopa hivyo basi anza leo kuwa na bajeti yako ya matumizi.

‘’ ukijua unapokwenda katika safari yako utafika uendako’’

Makala hii imeandikwa na DEOGRATIUS KESSY ambaye ni mwandishi,mjasiriamali na mwamasishaji unaweza kuwasiliana naye kwa kupitia simu namba 0717101505 au kwa barua pepe (Email) deokessy.dk@gmail.com

ASANTE !

Siri Kubwa Unayotakiwa Kujua Kwenye Mahusiano Ya Kibiashara.

Mahusiano unayojenga na watu kibiashara yanaweza kuwa ya aina mbili;
1. Uhusiano ambao kila mmoja anafaidika(win - win)
2. Uhusiano ambao mmoja ananufaika zaidi ya mwingine(win - lose)
Kwa bahati mbaya sana kwenye mazingira yetu mahusiano yaliyotawala ni ya aina ya pili.
Watu wengi watakaotaka kujenga mahusiano ya kibiashara na wewe watataka kiunufaika zaidi yako.
Kuwa mjanja, angalia mbali.
Ukiona uhusiano wa aina hii kimbia, hautakufikisha mbali.

Siri Moja Kubwa Ya Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Unapokuwa mjasiriamali elimu yako ndio imeanza. Kwa kweli ili uweze kuwa juu kwenye ujasiriamali ni lazima uendelee kutafuta maarifa yatakayokufanya wewe na biashara yako kuwa bora zaidi.
Mjasiriamali anayeacha kujifunza ni mjasiriamali anayeacha kufaidika.
Wajasiriamali wanajifunza kupitia kusoma vitabu, kujifunza kuhusu watu waliofanikiwa, kusoma majarida yanayohusiana na wanachofanya, kuhudhuria semina na makongamano na njia nyingine nyingi.
Je wewe unatumia njia ipi kujifunza?

Siri Moja Kubwa Ya Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Unapokuwa mjasiriamali elimu yako ndio imeanza. Kwa kweli ili uweze kuwa juu kwenye ujasiriamali ni lazima uendelee kutafuta maarifa yatakayokufanya wewe na biashara yako kuwa bora zaidi.
Mjasiriamali anayeacha kujifunza ni mjasiriamali anayeacha kufaidika.
Wajasiriamali wanajifunza kupitia kusoma vitabu, kujifunza kuhusu watu waliofanikiwa, kusoma majarida yanayohusiana na wanachofanya, kuhudhuria semina na makongamano na njia nyingine nyingi.
Je wewe unatumia njia ipi kujifunza?

Unapokuwa Tayari Kuingia Kwenye Ujasiriamali Fanya Vitu Hivi Vitano.

Kuna watu ambao wangetamani kuwa wajasiriamali. Wanapoona mafanikio ya wajasiriamali wakubwa wanatamani sana kama wangekuwa wao.

Hijalishi unatamani kiasi gani kuwa mjasiriamali, tamaa yako tu haitakuwezesha kufikia mafanikio katika ujasiriamali. Ni lazima uwe na misingi ambayo utaisimamia ndio uweze kuona mafanikio makubw akupitia ujasiriamali.

Kwanza ni lazima uondoke kwenye kutamani na uingie kufanya na ukishaingia kufanya uwe tayari kukabiliana na lolote litakalojitokeza mbele yako.

SOMA; Maswali Matatu Muhimu Ya Kujiuliza Kwenye Wazo Lako La Biashara.

Leo hapa UTAJIONGEZA na vitu vitano muhimu vya kufanya unapokuwa tayari kuingia kwenye ujasiriamali.

1. Usianze tena kujishuku.

Ukishaamua kwamba wewe umechagua njia ya ujasiriamali, sahau kuhusu kujishuku na kuanza kuwa na wasi wasi kama kweli utaweza. Kikubwa ni nia yako ya kufikia mafanikio kupitia ujasiriamali. Matatizo, changamoto na vikwazo kila mtu anavipitia. Hivyo acha kuwa na wasi wasi kama utaweza na jitoe kwa asilimia 100 kufanya kile ambacho umeamua kufanya.

Kwenye ujasiriamali hakuna kujaribu, kuna kufanya. Fanya sasa na ondoa wasi wasi na hofu.

SOMA; SIRI YA 20 YA MAFANIKIO; Iendee Dhahabu...

2. Kuwa na mshauri.

Kuna ushauri wa bure ambao unapatikana kila mahali kwenye maisha yetu ya kitanzania. Ushauri kama, biashara fulani inalipa kweli yani, ukianza kuifanya tu, utapata mafanikio makubwa. Ukimuangalia anayekupa ushauri huo nae amesikia kwamba biashara hiyo inalipa.

Sasa hawa sio washauri ambao nakuambia uwe nao. Nakuambia uwe na mshauri ambaye anaelewa ni nini hasa anachokuambia. Mtu ambaye amekuwa kwenye safari ya ujasiriamali na anaujua ugumu wa safari hiyo. Mtu ambaye hatakuwa mnafiki kwako kukuambia mambo ili tu kukupa moyo na kukufurahisha, bali atakuambia ukweli, na ukweli huu utakufanya uweze kutumia mazingira yako vizuri kufikia mafanikio.

SOMA; UKURASA WA 43; Ushauri Wa Bure Una Gharama Kubwa.

3. Jitengenezee utaratibu wako wa kila siku, ambao utauheshimu.

Tofauti ya ujasiriamali na kazi zingine ni kwamba kwenye ujasiriamali wewe unajiongoza mwenyewe. Hakuna atakayekugombeza au kukutishia kukufukuza kazi kama utakuwa mzembe. Na hii ni hatari kubwa sana kwa sababu kama huwezi kujiongoza mwenyewe utashindwa kwenye ujasiriamali.

Njia rahisi ya kuweza kuanza kujiongoza mwenyewe ni kuwa na utaratibu wako wa kila siku ambao utaufuata na kuuheshimu. Ipangilie siku yako kabla hujaianza na weka vipaumbele kwenye malengo na mipango yako kwenye maisha na kupitia ujasiriamali unaofanya.

4. Acha kukaa na watu ambao wanakurusisha nyuma.

Tumeshajadili hili mara nyingi sana kwamba wewe ni wastani wa watu watano ambao wanakuzunguka. Hivyo kama umezungukwa na watu watano ambao hawana malengo yoyote kwenye maisha yako, ni vigumu sana wewe kuweka malengo na kuyasimamia. Hivyo wewe unapoamua kuingia kwenye ujasiriamali usikubali kukaa tena na watu ambao mawazo yao yanakurudisha wewe nyuma. Wewe unajua kwamba kwenye ujasiriamali, hasa wakati wa mwanzo unaweza kujikuta unafanya kazi mpaka masaa 16 au 20 kwa siku, lakini rafiki zako wanataka kila siku jioni mkutane mkipata moja moto na moja baridi, hii hutaiweza wewe kama mjasiriamali, niamini.

SOMA; UKURASA WA 11; Watu Hawa Wanakurudisha Nyuma.

5. Kuza mtandao wako.

Tumesema sana hili pia, haijalishi unajua nini bali unamjua nani. Unapoamua kuingia kwenye ujasiriamali hakikisha kila mtu anayehusika na aina ya ujasiriamali unaofanya anajua kuhusu wewe na kile unachofanya. Angalia watu muhimu ambao unahitaji ushirikiano wao, watafute, angalia ni jinsi gani unaweza kuwasaidia ili nao wakusaidie, kukua zaidi.

Kama unafikiri kwenye ujasiriamali utashinda kwa jeshi la mtu mmoja umepotea njia, ongea na watu wengi uwezavyo, wajue unachofanya na wao watakuunganisha na watu wengi zaidi.

Haya ndio mambo matano muhimu sana ya wewe kufanya pale unapoamua kwamba ujasiriamali ndio maisha yako. Na miaka sio mingi kila mtu atahitaji kuwa mjasiriamali, hivyo ni vyema kama utaanz akujiandaa mapema.

Kwa ushauri wowote kuhusu biashara na ujasiriamali tafadhali tuma email kwenda ushauri@kisimachamaarifa.co.tz

Nakutakia kila la kheri kwenye mafanikio kupitia ujasiriamali.

TUPO PAMOJA.

Makirita AMANI 

Maswali Matatu Muhimu Ya Kujiuliza Kwenye Wazo Lako La Biashara.

Hakuna changamoto kubwa kama kupata wazo zuri la biashara na ambalo litakuwezesha kupata mafanikio na mafanikio makubwa.

Japo nimeshaandika mara nyingi sana jinsi ya kutengeneza wazo zuri la biashara, bado maswali mengo ninayopata kutoka kwa wasomaji ni wazo gani la biashara ni zuri na lenye faida.

Leo tutajifunza maswali matatu muhimu ya kujiuliza kwenye wazo lolote la biashara ili kujua kama litakuletea faida.

SOMA; Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Muhimu ni kujua kwamba kila wazo la biashara ni zuri na linaweza kuleta faida. Changamoto ni jinsi gani unaweza kulitekeleza wazo hilo ili liweze kukuletea faida hiyo. Kupitia maswali haya matatu utaweza kuliweka wazo lako vizuri na hatimaye kuweza kutengeneza biashara kubw akupitia wazo hilo.

1. Je nawezaje kulipwa kwa wazo hili?

Jiulize swali hili muhimu sana kwamba unawezaje kulipwa kwa wazo ulilonalo. Unawezaje kulipwa kwa kile unachopenda kufanya?

Tuseme labda unapenda kuchora, je unawezaje kulipwa kwa kuchora? Hapa unaweza kupata majibu kama kuchora kazi za kisanaa, kuchora ramani za majengo, kuanzisha jarida la vibonzo na mengine mengi.

2. Je nitalipwa kiasi gani kutokana na wazo hili?

Kupata uhakika wa kulipwa kutokana na wazo bado hakutoshi wewe kujihakikishia biashara. Swali jingine muhimu la kujiuliza ni nitalipwa kiasi gani kwa wazo hili? Ni lazima ujue kiwango ambacho unaweza kulipwa kutokana na wazo lako. Na pia uone kiwango hiko unacholipwa kitakuwezesha kuendelea na biashara hiyo.

Kwenye mfano wetu wa kuchora hapo juu, huendakuchora vibonzo kunalipa, ila kuchora ramani za majengo kunaweza kulipa zaidi.

SOMA; Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

3. Je kuna njia ambayo naweza kulipwa zaidi ya mara moja?

Wazo zuri la biashara ni lile ambalo unaweza kulipwa zaidi ya mara moja. Kama una biashara ambayo mtu akishanunua ndio imetoka na hawezi kurudi kwako tena ni vigumu sana kutengeneza biashara endelevu.

Ila kama utakuwa na njia ya kuweza kulipwa zaidi ya mara moja, au mteja kuja tena na tena utaweza kujenga biashara nzuri na yenye mafanikio makubwa.

Jiulize na kujijibu maswali hayo matatu na utaweza kulijenga wazo lako la biashara na likakuletea mafanikio makubwa sana.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.

Weka Pamoja Vitu Hivi Vitatu Na Tayari Wewe Ni Mjasiriamali Mwenye Mafanikio Makubwa.

Kama tayari una kundi la watu wanaokufuata, na wanaosikiliza unachosema, ila huna cha kuwauzia, huna biashara.

Kama una bidhaa au huduma unayouza ila hakuna mtu yuko tayari kununua huna biashara.

SOMA; Sifa TATU Unazohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Kama una bidhaa au huduma unayouza na watu wapo tayari kununua ila huna njia rahisi ya wateja kuweza kukulipa huna biashara.

Kama ukiwa na bidhaa au huduma unayouza, ukawa na watu ambao wako tayari kuinunua, na ukawa na mfumo mzuri wa watu kukulipa ili kuipata, hongera una biashara kubwa ambayo itakuletea mafanikio.

Kwa kuweza kufikia vigezo hivyo vitatu na kuviweka pamoja wewe ni mjasiriamali mwenye mafanikio.

Kila la kheri.

SOMA; Huyu Ni Mjasiriamali Mwenye Hamasa Kubwa sana. Unaweza kujifunza kila kitu kutoka kwake.

Huyu Ni Mjasiriamali Mwenye Hamasa Kubwa sana. Unaweza kujifunza kila kitu kutoka kwake.

Moja ya vitu ambavyo vitakuwezesha wewe kufanikiwa kwenye ujasiriamali ni kupend akile unachokifanya. Kama kweli unapenda unachofanya, utakuwa na hamasa kubwa sana ya kukifanya.

Hamasa hii ndio inakuwezesha kuvuka vikwazo, kuwa mbunifu na kuweza kufikia mafanikio makubwa sana.

Kuna mjasiriamali mmoja mkubwa sana duniani ambaye ana hamasa kubwa sana ambayo huwa inawashangaza wengi. Pamoja na mafanikio makubwa aliyonayo, bado haoni shida kufanya mambo madogo madogo ambayo yanamfanya azidi kufikia mafanikio makubwa.

Mjasiriamali ninayemzungumzia ni Richard Branson. Huyu ni raia wa uingereza na anamiliki kampuni kubwa ya Virgin Group ambayo ina kampuni zaidi ya 400 chini yake. Huyu ni mmoja wa watu matajiri sana duniani, akikadiriwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 4.9.

branson

Leo hapa utajiongeza na baadhi ya mambo anayofanya Branson ambayo yatakufanya na wewe uwe na hamasa zaidi kwenye ujasiriamali unaofanya.

Katika ufunguzi wa hotel mpya chini ya kampuni yake ya Virgin, kulikuwa na tetesi kwamba Richard alikuwa anawatembelea wateja wake usiku na kuwafurahisha zaidi.

branson 2

Tetesi hizo zilithibitishwa na Branson mwenyewe pale alipowatembelea wateja chumbani kwao na kuwasomea hadithi wakati wa kulala. Kama ambavyo wazazi huwa wanawasomea watoto wao hadithi.

branson 3

Unaweza kuona ni kitu kidogo ila kinajenga picha kubwa sana kwake na kwa biashara zake. Hii inaonesha jinsi anavyojali biashara zake na anavyotoa huduma bora kwa wateja.

Angalia video ya tukio zima hapo chini;

Njia TATU Za Kufanya Moto Wa Ujasiriamali Uendelee Kuwaka Kwenye Nafsi Yako…

Hakuna maisha mazuri kama ya ujasiriamali, kama unajielewa na unaweza kujisimamia, ujasiriamali ni maisha yenye uhuru mkubwa sana.

Unapokuwa na wazo la ujasiriamali mwanzoni ni kama moto unawaka ndani yako. Unakuwa na hamasa kubwa sana ya kutekeleza wazo lako na unakuwa na mapenzi makubwa kwa unachofanya.

Ila kwa bahati mbaya sana unapoingia kwenye ujasiriamali na kuanza kufanya biashara zako za kila siku ni rahisi moto huu kuzimika na kujikuta unakosa hamasa ya kuendelea. Na pale unapokutana na changamoto, ambazo ni lazima ukutane nazo ni rahisi kukata tamaa.

Leo UTAJIONGEZA na njia tatu za kufanya moto wa ujasiriamali uendelee kuwaka kwenye nafsi yako. Hii itakufanya uendelee kuwa na hamasa kubwa na kupenda kile unachofanya. Hata utakapokutana na changamoto itakuwa rahisi sana kwako kuzitatua na kuendelea ili kufikia mafanikio makubwa zaidi.

SOMA; UKURASA WA 35; Usijaribu Kumfurahisha Kila Mtu.

1. Washa moto wa ujasiriamali kila siku.

Kila siku kabla ya kuanza siku yako, washa moto wa ujasiriamali kwenye nafsi yako. Unawashaje moto huu? Ni rahisi, kila siku jikumbushe ni nini ambacho kilikufanya uingie kwenye ujasiriamali unaofanya. Kama sababu yako ni kubwa, kwa kujikumbusha kila siku na kujiambia sababu hiyo itakuwa hamasa kubwa ya wewe kufanya mambo makubwa kwa siku hiyo.

Kila siku jikumbushe kilichokufanya uingie kwenye ujasiriamali.

2. Penda matatizo/changamoto.

Kwa sehemu kubwa kilichokufanya uingie kwenye ujasiriamali ni kutatua matatizo ya watu, au kuwapatia njia bora zaidi. Katika mchakato huu na wewe pia utaingia kwenye matatizo au changamoto mbalimbali.

Kama utaziogopa changamoto hizi, itakuwa rahisi kwa wewe kukosa hamasa ya kuendelea. Ila kama utayapenda matatizo na changamoto unazokutana nazo, utazipatia ufumbuzi na utaweza kuendelea na safari.

SOMA; NENO LA LEO; Viti Viwili Ambavyo Kila Mtu Anataka Kwenye Maisha.

3. Usikubali majukumu ya kila siku kukupoteza lengo lako.

Wewe kama mjasiriamali ulianza na wazo moja, lakini kwenye kutekeleza wazo hilo umeingia kwenye biashara ambayo ina vipengele vingi sana. Kwa kujaribu kufanya kila eneo la biashara yako kunaweza kukuchosha na ukasahau lengo lako kubwa lilikuwa nini.

Chagua mambo machache ambayo unayapenda kweli kuyafanya na yafanye vizuri sana, hii itakupatia hamasa kubwa ya kuendelea kufanya zaidi. Mambo mengine yote tafuta watu wanaoweza kufanya na waajiri wafanye mambo hayo.

Kadiri unavyofanya vitu vichache vinavyokuhamasisha, ndivyo unavyopata majibu mazuri na ndivyo moto wa ujasiriamali utaendelea kuwaka ndani yako.

SOMA; #HADITHI_FUNZO; Mbinu Rahisi Iliyomwezesha Jenerali Kushinda Vita Ngumu.

Hatua TANO Za Kuongeza Uzalishaji Wako Ili Kufikia Mafanikio.

Kuna usemi mmoja maarufu sana unaosema “ukiendelea kufanya unachofanya sasa, utaendelea kupata matokeo unayopata sasa”. Kwa lugha nyingine kama unataka kubadili matokeo yako, ni lazima uanze kwa kubadili kile unachofanya.

Ili uweze kufikia mafanikio zaidi ya uliyonayo sasa, kwa sababu mpaka hapo ulipo tayari una mafanikio, unahitaji kubadili njia unazotumia sasa. Na kitu cha kwanza kabisa kubadili ni uzalishaji wako.

Uzalishaji tunaozungumzia hapa ni ile kazi au thamani unayotoa kwa wengine kwa muda unaofanya kazi. Hivyo kama utazalisha thamani zaidi kwa muda mfupi maana yake una uzalishaji mkubwa. Na hii ni njia nzuri ya kufikia mafanikio kwenye chochote unafanya, iwe ni kazi au biashara.

Kiuchumi, utajiri au thamani ya kampuni, mtu binafsi na hata jamii kwa ujumla unapimwa kwa ongezeko la uzalishaji.

SOMA; Sifa TATU Unazohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Leo UTAJIONGEZA na hatua tano unazoweza kutumia na ukaongeza uzalishaji wako na hatimaye kufikia mafanikio zaidi.

Hatua ya kwanza na rahisi kabisa ya kuongeza uzalishaji wako ni kuwa bora kwenye majukumu yako. Kufanya kazi kwa juhudi na maarifa na kuendelea kujifunza zaidi. Kama unafanya biashara, ijue vizuri biashara yako na ongeza juhudi. Kama umeajiriwa, unajua majukumu yako kikazi, yatekeleze vizuri.

Hatua ya pili ni kutafuta mtu ambae anaweza kufanya hiko unachofanya na kwa bei rahisi kisha unampa afanye. Kama ni mfanyabiashara maana yake unatafuta watu wa kukusaidia. Kama ni ajira unafanya kazi na watu wengine ambao wanakusaidia. Ukweli ni kwamba kazi inayofanyika kwa timu inafanyika kwa uzalishaji mkubwa.

SOMA; Tabia Mbaya KUMI(10) Zinazopunguza Ufanisi Wako.

Hatua ya tatu ya kuongeza uzalishaji ni kutumia teknolojia iliyopo. Hapa unatafuta njia ambayo teknolojia inaweza kurahisisha kazi unazofanya. Kwa mfano badala ya kuandika kila barua kwa mkono, inaweza kuandikwa moja na zikatolewa kopi na mashine. Kila kazi inaweza kusaidiwa na teknolojia.

Hatua ya nne ni kuvumbua teknolojia mpya inayoweza kurahisisha kazi zako. Na ukifikia hatua hii unakuwa umetatua tatizo la wengi. Inawezekana kwa kila kazi unayofanya kuvumbua njia rahisi ya kiteknolojia ya kuirahisisha.

Hatua ya tano na ya mwisho ya kuongeza uzalishaji wako ni kujua vitu vinavyoleta uzalishaji mkubwa kwako na kufanya hivyo tu. vingine vyote unaacha kuvifanya kwa sababu vinakupotezea muda. Kwa mfano asilimia 80 ya mafanikio yako inatokana na asilimia 20 ya kazi unazofanya. Je ni kazi zipi hizo zinakuletea faida kubwa? Zijue kazi hizi na zifanye kwa ufanisi mkubwa na utaongeza uzalishaji wako.

SOMA; SIRI YA 4 YA MAFANIKIO; Itumie Sheria Ya Wastani Kukuletea Mafanikio.

Mwisho wa siku kinachoongeza uzalishaji ni pale unapojua kile chenye faida kwako na kukifanya. Hii ndio inayoleta faida kwenye makampuni, biashara na hata kazi. Wale wanaojaribu kufanya kila kitu huishia kuwa na uzalishaji mdogo. Wale wanaochagua vichache na kuvifanya vizuri huwa na uzalishaji mkubwa.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Sifa TATU Unazohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Mafanikio kwenye ujasiriamali yanachangiwa na vitu vingi sana. Kupitia blog hii JIONGEZE UFAHAMU tumeshajifunza vitu vingi sana vinavyokuwezesha wewe mjasiriamali kufikia mafanikio makubwa.

Vitu kama kuweka malengo na mipango, kufanya kazi kwa juhudi na maarifa, kuwa mwaminifu, kutokata tamaa na vingine vingi ni muhimu sana kw akila mjasiriamali ili aweze kufanikiwa.

Leo UTAJIONGEZA na sifa tatu muhimu ambazo zitakuwezesha kufikia mafanikio kupitia ujasiriamali.

SIFA YA KWANZA; Kuwa Mtu Wa Watu.

Kuwa mjasiriamali maana yake wewe upo kwenye biashara ya watu. Mafanikio yako yote kwenye ujasiriamali yatatokana na watu wanaokuzunguka. Watu hao ni wateja wako, wafanyakazi wako, wawekezaji, washirika na hata watu wengine wa karibu.

Jinsi unavyoweza kwenda vizuri na watu wengi ndivyo utakavyoweza kutengeneza mafanikio makubwa.

SOMA; Hatua Tatu Za Kujua Kama Wazo Lako La Biashara Zuri.

SIFA YA PILI; Kuwa na Nidhamu.

Nidhamu ndio kila kitu ndugu yangu. Unapokuwa mjasiriamali hakuna wa kukusimamia utekeleze majukumu yako. Kama utakuwa mtu wa kujiendekeza utajikuta unabaki nyuma kila siku. Ni lazima uwe na nidhamu ambayo itakufanya uweze kufuata malengo na mipango yako hata kama mazingira ni magumu kiasi gani.

SOMA; Tabia Mbaya KUMI(10) Zinazopunguza Ufanisi Wako.

SIFA YA TATU; Penda Unachofanya.

Safari ya ujasiriamali inaweza kuwa ndio safari ngumu kuliko safari zote duniani. Kama ulikuwa hujui hilo jua leo. Na kinachofanya iwe ngumu ni ukweli kwamba utashindwa. Na utashindwa mara nyingi kiasi kwamba kama haupendi kile unachofanya kwa roho moja utaishia kukata tamaa.

Penda sana kile unachofanya, penda kujifunza zaidi na penda kuwasaidia wengine kupitia unachofanya na mafanikio hayatakuwa na ujanja wa kukukimbia.

Hizo ndio sifa tatu muhimu za kukuwezesha kufikia mafanikio makubwa kama mjasiriamali. Uzuri ni kwamba tabia hizi unawez akujitengenezea na kuweza kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia kila la kheri katika mafanikio yako kwenye ujasiriamali.

SOMA; SIRI 50 ZA MAFANIKIO.