Showing posts with label UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT). Show all posts
Showing posts with label UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT). Show all posts
Yafahamu Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Kwenye Eneo La Ujenzi Kabla Hujajenga Nyumba Yako
Na Kimbe Nickas
Mwonekano wa Tanzania ya sasa na ya miaka kumi iliyopita ni tofauti sana, mafanikio haya ni kutokana na msukumo mkubwa wa maendeleo ya sekta mbalimbali ukiwemo uwekezaji wa ardhi na majengo unaoshika kasi kubwa ndani na pembezoni mwa miji mikubwa ya Tanzania. Ndugu msomaji wa makala hii usiachwe nyuma bali uwe sehemu ya mafanikio ya kubadili uchumi wa nchi yetu na uchumi wako binafsi, kama wewe ni miongoni mwa watu wengi wanaojiuliza wawekeze kwenye biashara gani itakayokufanya uwe huru kiuchumi na kijamii, jibu ni rahisi sana, isikilize nafsi yako na itendee haki kwa kuwajibika. Nina mengi ya kukushirikisha lakini Leo nakupa mambo muhimu ya kuzingatia kwenye eneo la uwekezaji kabla hujajenga unachotaka kujenga. Mambo haya yatakusaidia kufanya tathmini na hatimaye kufanya maamuzi sahihi ya aina gani ya uwekezaji uweze kufanya, hapa namaanisha aina na matumizi ya majengo kama vile ofisi, maduka, nyumba ya kuishi, mgahawa, hoteli, zahanati au shule.
Mzunguko wa watu
Mzunguko wa watu huathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya uchumi na jamii katika eneo lolote, mara nyingi maeneo yenye mzunguko mkubwa wa watu ni maeneo yenye huduma bora za kijamii na kiuchumi. Maeneo haya watu huingia na kutoka kutafuta huduma muhimu za kimaisha. Maeneo yenye ofisi za serikali, taasisi mbalimbali, viwanda, makampuni binafsi na umma huwa na mzunguko mkubwa wa watu. Huduma hizo huvuta watu kutoka sehemu mbalimbali kuingia ili kukidhi mahitaji yao ya kimaisha yanayopatikana maeneo hayo. Unapowekeza maeneo kama haya unapaswa kuangalia mapungufu yaliyopo ili kukidhi mahitaji ya watu wa eneo hilo, mfano, kama hakuna hoteli utajenga hoteli, hakuna pakingi utajenga pakingi. Muhimu ni kuangalia namna gani utaondoa tatizo na utakidhi mahitaji ya wengi huku kwa upande wa pili unajijengea uwezo wa kuwa mwenye mafanikio kifedha kwa kuwa umewekeza kilicho sahihi kwa wakati huo.
SOMA; Kama Umewekeza Kwenye Majengo Yafahamu Magonjwa Sugu Yanayo Athiri Majengo.
Aina za nyumba zilizopo
Popote unapotaka kuwekeza nyumba yako lazima utajifunza kitu kutoka kwa waliotangulia kujenga kwenye eneo hilo, mazuri na mapungufu mengi utayaona, yapo mengi ya kujifunza endapo utakuwa makini na kuzingatia ubora, mpangilio na mwonekano wa nyumba za jirani. Lengo la kutathmini nyumba zilizopo ni kuchukua yale mazuri na kuepuka kurudia mapungufu yaliyojitokeza kwa wengine. Mfano, nyumba nyingi za hivi karibuni zimejengewa vyumba vya biashara yaani frem, na wengi wameiga hivyo, lakini wanasahau kuwa wapo wafanyabiashara wengi wanao hitaji aina tofauti ya “fremu” hizo kukidhi mahitaji yao ya kibiashara, tambua kuwa kuna taasisi, kampuni na mashirika mbalimbali yanayohitaji majengo ili kuwafikia wateja wao waliopo sehemu mbalimbali za nchi. Hivyo ili uwe na uwanja mpana wa kupata wateja kwenye majengo ya biashara, lazima ujenge nyumba itakayokidhi mahitaji mbalimbali ambayo pia ni rahisi kwa kubadili matumizi pasipo ubomoaji wowote. Hakikisha ujenzi utakaofanya unaongeza thamani katika eneo hilo, hii ndiyo sababu mojawapo ya wewe kutumia wataalamu kwenye mipango yako ya uwekezaji ili wakushauri namna gani ya kujenga kutokana na mabadiliko makubwa yanayojitokeza kwa sasa. Jitahidi kuwa bora zaidi ya wengine ili upate wateja zaidi na mafanikio zaidi.
Miundombinu iliyopo
Kabla ya kununua ardhi au kuanzisha ujenzi wako ni muhimu sana ukazingatia na kutathmini miundombinu iliyopo ili isisababishe ukinzani wowote wa ujenzi wako unaotaka kufanya. Kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, ardhi yote ya jamhuri inasimamiwa na rais wa jamhuri, hivyo kama kuna miundombinu yoyote yenye manufaa kwa wengi jaribu kuikwepa maana kwa namna yoyote ile utaondoka wewe ili miundombinu hiyo iendelee kuwanufaisha wengi. Zingatia sana hifadhi za barabara, misitu, nishati za umeme na miundombinu iliyofukiwa. Miundombinu iliyofukiwa juu ya ardhi huwekwa alama (bikoni) kila baada ya umbali fulani kuonesha mwelekeo wa miundombinu hiyo. Pia maeneo yenye miundombinu ya uhakika huwa ni kivutio kikubwa kwa watu tofauti na maeneo ambayo bado hakuna miundombinu ya uhakika.
Fanya uthamini binafsi
Jijengee utaratibu wa kufanya tathmini kabla ya kufanya uwekezaji wowote ule, kabla ya kununua eneo au nyumba jipe muda wa kutosha wa kufikiri na kufanya tafiti ili uwe na taarifa sahihi la eneo husika. Tathmini yako izingatie ulinganifu wa bei za manunuzi au gharama za ujenzi, matumizi rasmi ya eneo hilo, umiliki rasmi wa eneo hilo, hata ramani ya nyumba yako lazima izingatie mazingira ya eneo husika. Jipe muda wa kutosha kupata taarifa sahihi kabla ya kufanya maamuzi ya kununua au kujenga, Hii itakusaidia wewe kufanya uwekezaji wako kihalali na kwa kufuata taratibu zote, pia utaepuka gharama kubwa kutokana na udanganyifu wa watu au faini kutoka kwa mamlaka husika endapo utakiuka jambo lolote kwa kukosa taarifa sahihi.
Zione mamlaka husika za kisheria na usimamizi
Daima unaponunua au kuwekeza nyumba au kufanya chochote kwenye ardhi zione mamlaka husika ili upate taratibu rasmi za kufuata ili malengo yako yatimie pasipo misuguano na mamlaka hizo za serikali. Hakuna jambo linalokosa taratibu za kimfumo, hata kwenye ujenzi zipo mamlaka zinazosimamia mfumo na vibali kabla na wakati wa ujenzi na baada ya ujenzi. Pia taratibu hizo hutofautiana kutokana na sera na taratibu za kimfumo za mamlaka za usimamizi wa eneo husika. Watu wengi hawajui kuhusu taratibu hizi, hujikuta wameletewa barua za kusimamisha ujenzi wao (stop order) pasipo kujua nini cha kufanya. Ni muhimu sana ukazifahamu taratibu za mahali husika kabla hujaamua kujenga, tofauti na hivyo utabomolewa na kujikuta umepoteza fedha nyingi pasipo msaada wowote.
Washirikishe wataalam wa Ardhi na ujenzi
Ni muhimu sana kuwashirikisha wataalamu wa fani husika ili wakushauri namna gani uweze kufikia lengo lako huku ukitabasamu kwa furaha. Watu wengi wamejikuta wapo kwenye majuto makubwa baada ya kutapeliwa fedha zao na watu wasio na ufahamu wowote kuhusiana na ardhi na ujenzi wa nyumba. Watafute sasa maana wanapatikana kila mahali, wathamini ardhi (land valuer) watakusaidia namna gani ya kumiliki ardhi yako, wasanifu majengo(Architects) watakuchorea ramani ya nyumba yako, wakadiriaji majenzi (Quantity Surveyors) watakusaidia kupanga na kusimamia gharama za ujenzi wako, wahandisi (ujenzi, umeme na maji) watasimamia ujenzi wa nyumba yako. Hawa wote kwa pamoja ni timu yenye uwezo wa kuhakikisha mjasiriamali unapata ulichotarajia kupata kwa uhalisia wake. Kama unataka mafanikio ya kweli watumie wataalamu kwenye mambo yako.
Tuendelee kuwa pamoja kupitia JIONGEZE UFAHAMU tufike kwenye kilele cha mafanikio, pia endelea kufuatilia makala zijazo ili ujifunze zaidi.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
Mwonekano wa Tanzania ya sasa na ya miaka kumi iliyopita ni tofauti sana, mafanikio haya ni kutokana na msukumo mkubwa wa maendeleo ya sekta mbalimbali ukiwemo uwekezaji wa ardhi na majengo unaoshika kasi kubwa ndani na pembezoni mwa miji mikubwa ya Tanzania. Ndugu msomaji wa makala hii usiachwe nyuma bali uwe sehemu ya mafanikio ya kubadili uchumi wa nchi yetu na uchumi wako binafsi, kama wewe ni miongoni mwa watu wengi wanaojiuliza wawekeze kwenye biashara gani itakayokufanya uwe huru kiuchumi na kijamii, jibu ni rahisi sana, isikilize nafsi yako na itendee haki kwa kuwajibika. Nina mengi ya kukushirikisha lakini Leo nakupa mambo muhimu ya kuzingatia kwenye eneo la uwekezaji kabla hujajenga unachotaka kujenga. Mambo haya yatakusaidia kufanya tathmini na hatimaye kufanya maamuzi sahihi ya aina gani ya uwekezaji uweze kufanya, hapa namaanisha aina na matumizi ya majengo kama vile ofisi, maduka, nyumba ya kuishi, mgahawa, hoteli, zahanati au shule.
Mzunguko wa watu
Mzunguko wa watu huathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya uchumi na jamii katika eneo lolote, mara nyingi maeneo yenye mzunguko mkubwa wa watu ni maeneo yenye huduma bora za kijamii na kiuchumi. Maeneo haya watu huingia na kutoka kutafuta huduma muhimu za kimaisha. Maeneo yenye ofisi za serikali, taasisi mbalimbali, viwanda, makampuni binafsi na umma huwa na mzunguko mkubwa wa watu. Huduma hizo huvuta watu kutoka sehemu mbalimbali kuingia ili kukidhi mahitaji yao ya kimaisha yanayopatikana maeneo hayo. Unapowekeza maeneo kama haya unapaswa kuangalia mapungufu yaliyopo ili kukidhi mahitaji ya watu wa eneo hilo, mfano, kama hakuna hoteli utajenga hoteli, hakuna pakingi utajenga pakingi. Muhimu ni kuangalia namna gani utaondoa tatizo na utakidhi mahitaji ya wengi huku kwa upande wa pili unajijengea uwezo wa kuwa mwenye mafanikio kifedha kwa kuwa umewekeza kilicho sahihi kwa wakati huo.
SOMA; Kama Umewekeza Kwenye Majengo Yafahamu Magonjwa Sugu Yanayo Athiri Majengo.
Aina za nyumba zilizopo
Popote unapotaka kuwekeza nyumba yako lazima utajifunza kitu kutoka kwa waliotangulia kujenga kwenye eneo hilo, mazuri na mapungufu mengi utayaona, yapo mengi ya kujifunza endapo utakuwa makini na kuzingatia ubora, mpangilio na mwonekano wa nyumba za jirani. Lengo la kutathmini nyumba zilizopo ni kuchukua yale mazuri na kuepuka kurudia mapungufu yaliyojitokeza kwa wengine. Mfano, nyumba nyingi za hivi karibuni zimejengewa vyumba vya biashara yaani frem, na wengi wameiga hivyo, lakini wanasahau kuwa wapo wafanyabiashara wengi wanao hitaji aina tofauti ya “fremu” hizo kukidhi mahitaji yao ya kibiashara, tambua kuwa kuna taasisi, kampuni na mashirika mbalimbali yanayohitaji majengo ili kuwafikia wateja wao waliopo sehemu mbalimbali za nchi. Hivyo ili uwe na uwanja mpana wa kupata wateja kwenye majengo ya biashara, lazima ujenge nyumba itakayokidhi mahitaji mbalimbali ambayo pia ni rahisi kwa kubadili matumizi pasipo ubomoaji wowote. Hakikisha ujenzi utakaofanya unaongeza thamani katika eneo hilo, hii ndiyo sababu mojawapo ya wewe kutumia wataalamu kwenye mipango yako ya uwekezaji ili wakushauri namna gani ya kujenga kutokana na mabadiliko makubwa yanayojitokeza kwa sasa. Jitahidi kuwa bora zaidi ya wengine ili upate wateja zaidi na mafanikio zaidi.
Miundombinu iliyopo
Kabla ya kununua ardhi au kuanzisha ujenzi wako ni muhimu sana ukazingatia na kutathmini miundombinu iliyopo ili isisababishe ukinzani wowote wa ujenzi wako unaotaka kufanya. Kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, ardhi yote ya jamhuri inasimamiwa na rais wa jamhuri, hivyo kama kuna miundombinu yoyote yenye manufaa kwa wengi jaribu kuikwepa maana kwa namna yoyote ile utaondoka wewe ili miundombinu hiyo iendelee kuwanufaisha wengi. Zingatia sana hifadhi za barabara, misitu, nishati za umeme na miundombinu iliyofukiwa. Miundombinu iliyofukiwa juu ya ardhi huwekwa alama (bikoni) kila baada ya umbali fulani kuonesha mwelekeo wa miundombinu hiyo. Pia maeneo yenye miundombinu ya uhakika huwa ni kivutio kikubwa kwa watu tofauti na maeneo ambayo bado hakuna miundombinu ya uhakika.
Fanya uthamini binafsi
Jijengee utaratibu wa kufanya tathmini kabla ya kufanya uwekezaji wowote ule, kabla ya kununua eneo au nyumba jipe muda wa kutosha wa kufikiri na kufanya tafiti ili uwe na taarifa sahihi la eneo husika. Tathmini yako izingatie ulinganifu wa bei za manunuzi au gharama za ujenzi, matumizi rasmi ya eneo hilo, umiliki rasmi wa eneo hilo, hata ramani ya nyumba yako lazima izingatie mazingira ya eneo husika. Jipe muda wa kutosha kupata taarifa sahihi kabla ya kufanya maamuzi ya kununua au kujenga, Hii itakusaidia wewe kufanya uwekezaji wako kihalali na kwa kufuata taratibu zote, pia utaepuka gharama kubwa kutokana na udanganyifu wa watu au faini kutoka kwa mamlaka husika endapo utakiuka jambo lolote kwa kukosa taarifa sahihi.
Zione mamlaka husika za kisheria na usimamizi
Daima unaponunua au kuwekeza nyumba au kufanya chochote kwenye ardhi zione mamlaka husika ili upate taratibu rasmi za kufuata ili malengo yako yatimie pasipo misuguano na mamlaka hizo za serikali. Hakuna jambo linalokosa taratibu za kimfumo, hata kwenye ujenzi zipo mamlaka zinazosimamia mfumo na vibali kabla na wakati wa ujenzi na baada ya ujenzi. Pia taratibu hizo hutofautiana kutokana na sera na taratibu za kimfumo za mamlaka za usimamizi wa eneo husika. Watu wengi hawajui kuhusu taratibu hizi, hujikuta wameletewa barua za kusimamisha ujenzi wao (stop order) pasipo kujua nini cha kufanya. Ni muhimu sana ukazifahamu taratibu za mahali husika kabla hujaamua kujenga, tofauti na hivyo utabomolewa na kujikuta umepoteza fedha nyingi pasipo msaada wowote.
Washirikishe wataalam wa Ardhi na ujenzi
Ni muhimu sana kuwashirikisha wataalamu wa fani husika ili wakushauri namna gani uweze kufikia lengo lako huku ukitabasamu kwa furaha. Watu wengi wamejikuta wapo kwenye majuto makubwa baada ya kutapeliwa fedha zao na watu wasio na ufahamu wowote kuhusiana na ardhi na ujenzi wa nyumba. Watafute sasa maana wanapatikana kila mahali, wathamini ardhi (land valuer) watakusaidia namna gani ya kumiliki ardhi yako, wasanifu majengo(Architects) watakuchorea ramani ya nyumba yako, wakadiriaji majenzi (Quantity Surveyors) watakusaidia kupanga na kusimamia gharama za ujenzi wako, wahandisi (ujenzi, umeme na maji) watasimamia ujenzi wa nyumba yako. Hawa wote kwa pamoja ni timu yenye uwezo wa kuhakikisha mjasiriamali unapata ulichotarajia kupata kwa uhalisia wake. Kama unataka mafanikio ya kweli watumie wataalamu kwenye mambo yako.
Tuendelee kuwa pamoja kupitia JIONGEZE UFAHAMU tufike kwenye kilele cha mafanikio, pia endelea kufuatilia makala zijazo ili ujifunze zaidi.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
7/14/2015 07:30:00 AM | Labels: UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
Kama Umewekeza Kwenye Majengo Yafahamu Magonjwa Sugu Yanayo Athiri Majengo.
Kama ilivyo kwa viumbe hai kuathiriwa na mazingira wanayoishi
ndivyo ilivyo kwa viumbe visivyo hai ikiwemo majengo. Majengo huweza kuhimili
mazingira kutokana na namna yalivyobuniwa na kujengwa katika mazingira yaliyopo.
Hata ujenge majengo mazuri na makubwa kiasi gani, kama hayajabuniwa na kujengwa
kutokana na mazingira husika majengo hayo huwa hatarini na watumiaji wa majengo
hayo huwa kwenye majanga mazito kwa kujua au kwa kutokujua. Mbaya zaidi huwa
hasara kwa mmiliki wa jengo husika. Kwa mujibu wa taaluma na ufahamu nilionao
unaweza kujenga majengo mahali popote iwe ardhi tambalale, mabondeni, milimani,
kando ya mito na hata baharini maadamu ikidhi ubunifu na ujenzi uzingatie
mazingira husika. Kwenye makala zijazo nitaeleza hayo kwa ufasaha zaidi, lakini
leo naomba uyafahamu magonjwa yanayoathiri majengo yako ili uweze kuyakinga na
yadumu kwa muda mrefu kwa kuwa ujenzi ni uwekezaji na hugharimu fedha
nyingi.
Nyufa
Nyufa ni uwazi unaosababishwa na utengano wa mihimili ya jengo uliokuwa muunganiko hapo awali. Nyufa zinapotokea kwenye jengo tambua kuwa jengo lako lipo katika tabu fulani, nyufa ni lugha kuu ya majengo kumjulisha mtumiaji kuwa lipo kwenye kashkashi. Nyufa husababishwa na matokeo mengi na utagundua tatizo kutokana na mwelekeo wa nyufa hizo na mahali ulipotokea. Kama nilivyoeleza hapo awali udhaifu wa majengo ni matokeo mabovu ya ubunifu na ujenzi kwa mazingira husika. Unachopaswa kufanya hapa ni kugundua tatizo na kuliweka sawa ndipo uzibe ufa. Watu wengi huishia kuziba ufa pasipo kushugulikia chanzo chake, kitendo hiki ni sawa na kuuficha ufa ili usiendelee kuuona machoni lakini tatizo linabaki palepale.
SOMA; Mambo Ya Kuzingatia Na Njia Bora Za Uwekezaji Wa Majengo Kwa Gharama Nafuu.
Kutitia kwa majengo
Ni kawaida kutitia kwa majengo lakini linapozidi kiwango huwa ni tatizo na hatari kwa watumiaji. Tatizo hili husababishwa na ukadiriaji hafifu wa tabia za udongo kwenye kiwanja cha jengo husika. Mara nyingi jengo hutitia kutokana na aina tofauti za udongo kwenye kiwanja kimoja au kimo cha msawazo wa msingi kuwa tofauti, pia ubunifu hafifu wa udongo kulingana na uzito wa jengo husika. Hatari kuu huwa kwenye majengo marefu na kwenye vyoo vya shimo. Cha kusikitisha mara zote serikali yetu huwajengea watoto wetu vyoo vya mashimo lukuki mashuleni jambo ambalo ni hatari kutokana na udhaifu wa muundo wa vyoo hivyo. Ni muhimu kutenganisha shimo na chumba cha choo kwa usalama wa watumiaji ili tusiendelee kupoteza watu na kufunga shule eti vyoo vimebomoka.
Majengo kupitisha maji
Maeneo mengi ya Tanzania yamezungukwa na vyanzo vya maji ambavyo ni bahari mito na maziwa hali inayosababisha ardhi yake kusharabu maji karibu majira yote ya mwaka na mbaya zaidi wakati wa mvua. Maeneo mengi ya pwani majengo mengi yameathiriwa na tatizo hili na hata limekuwa kero kwa wakazi na watumiaji wa majengo hayo. Majengo hupitisha maji kwa njia ya sakafu na kuta mithili ya chujio au chemchemu. Mara nyingi utagundua kwa kuona ardhi yake imetota maji wakati wote wa majira ya mwaka. Pia majengo mengi ya maeneo haya yanaoza na kutitia kwa haraka na hata mashimo ya vyoo vya maeneo hayo huinuka kwenda juu na siyo chini jambo ambalo ni hatari kwa afya za wakazi. Katika hali hii kuta na sakafu huoza kwa haraka kutokana na maji yaliyopo chini ya ardhi kuwa na kemikali mbalimbali zilizopo kwenye maji hayo. Katika mazingira haya lazima yatumike malighafi sahihi za kuzuia maji hasa wakati wa ujenzi.
SOMA; Kama Utashindwa Kufanya Chochote Utakachojifunza, Basi Fanya Hiki Kimoja Tu, Na Maisha Yako Yatagusa Wengine.
Kuoza kwa kuta
Moja ya masahibu yanayoyakumba majengo ni kuoza kwa kuta za tofali au chuma. Hali hii hutokana na unyevunyevu na kemikali mbalimbali kupitia maji kukaa kwa muda mrefu kwenye kuta hali inayoathiri ubora wakuta hizo. Pia hali hiyo husababishwa na kumea kwa mimea au kupanda maua kwenye viambaza vya kuta ambapo baadhi ya mimea hiyo kusababisha ukungu wa kijani kwenye kuta ambao huzalisha fangasi mbalimbali wanaokula kuta. Pia kitendo cha kumwagilia maua kwenye kuta huozesha kuta haraka. Kinga kuta zote zithiathiriwe na hali ya hewa na maji pale inapolazimu na Usiruhusu mimea kumea kwenye viambaza vya kuta.
Kuoza kwa paa
Unapaswa kutambua kuwa kila kilichoumbwa kina mwisho, ndivyo ilivyo hata kwenye majengo, kila aina ya malighafi iliyotumika hufika mwisho wake kwa wakati tofauti kulingana na ubora na namna yalivyotumika katika ujenzi. Kuoza kwa paa hutegemea ubora na aina ya malighafi zilizotumika bila kusahau na kimo cha mwinuko wa paa hilo. Paa huathiriwa na hali ya mazingira ya eneo husika, mfano paa zilizopo ukanda wa pwani huthiriwa na chumvichumvi zinazobebwa na mikondo ya upepo uvumao kutoka baharini hali inayosababisha paa kuoza haraka, pia hali ya mwinuko ukiwa mdogo husadia paa kuhifadhi takataka mbalimbali ikiwemo majani ya mimea, hali hii ya uchafu kukaa muda mrefu huozesha paa haraka. Unapaswa kuweka paa lenye ubora kulingana na mazingira halisi. Inasikitisha kuona hadi leo hii bado kuna nyumba za serikali zimeezekwa vigae vya asbestos ambavyo ni hatari na vimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu.
Kusinyaa na kutanuka kwa milango na madirisha
Kuna shida sana hapa, watu wengi hujikuta wakiwalalamikia sana mafundi kuwa hawafai na wamewatia hasara. Kuna aina nyingi za malighafi zinazotumika kutengenezea milango na madirisha, kila aina ya malighafi hizo zina faida na hasara zake. Karibu aina zote za malighafi zina tabia ya kusinyaa na kutanuka kutokana na hali ya hewa (jotiridi) ya mazingira nyumba zilipo. Tumia mbao ngumu (treated hardwood) ili kuondokana na tatizo hili, usitumie mbao mbichi zitakusumbua sana siku zijazo. Kwa wale wanaotumia madirisha na milango ya vioo na aluminiam ni lazima wayapachike na kufitisha kwenye mbao na siyo moja kwa moja kwenye kuta ili kuruhusu hali ya kusinyaa na kutanuka, usipo fanya hivyo aluminiam hupinda na kuleta shida ya kufunga na kufungua. Pia kama unatumia madirisha haya ya vioo (sliding windows) ni lazima yawe makubwa ili kuruhusu hewa kuingia na kutoka kwa haraka kwa kuwa madirisha haya hufunguka nusu tu. Kumbuka kuweka vitasa sahihi kulingana na matumizi, Zingatia sana haya kwa kuwa kila unachoweka kwenye nyumba ni fedha hivyo usiache watu wafanye hovyohovyo tu, ni kero na hasara, wewe na wateja wako hamtafurahia mazingira ya nyumba hiyo.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
Nyufa
Nyufa ni uwazi unaosababishwa na utengano wa mihimili ya jengo uliokuwa muunganiko hapo awali. Nyufa zinapotokea kwenye jengo tambua kuwa jengo lako lipo katika tabu fulani, nyufa ni lugha kuu ya majengo kumjulisha mtumiaji kuwa lipo kwenye kashkashi. Nyufa husababishwa na matokeo mengi na utagundua tatizo kutokana na mwelekeo wa nyufa hizo na mahali ulipotokea. Kama nilivyoeleza hapo awali udhaifu wa majengo ni matokeo mabovu ya ubunifu na ujenzi kwa mazingira husika. Unachopaswa kufanya hapa ni kugundua tatizo na kuliweka sawa ndipo uzibe ufa. Watu wengi huishia kuziba ufa pasipo kushugulikia chanzo chake, kitendo hiki ni sawa na kuuficha ufa ili usiendelee kuuona machoni lakini tatizo linabaki palepale.
SOMA; Mambo Ya Kuzingatia Na Njia Bora Za Uwekezaji Wa Majengo Kwa Gharama Nafuu.
Kutitia kwa majengo
Ni kawaida kutitia kwa majengo lakini linapozidi kiwango huwa ni tatizo na hatari kwa watumiaji. Tatizo hili husababishwa na ukadiriaji hafifu wa tabia za udongo kwenye kiwanja cha jengo husika. Mara nyingi jengo hutitia kutokana na aina tofauti za udongo kwenye kiwanja kimoja au kimo cha msawazo wa msingi kuwa tofauti, pia ubunifu hafifu wa udongo kulingana na uzito wa jengo husika. Hatari kuu huwa kwenye majengo marefu na kwenye vyoo vya shimo. Cha kusikitisha mara zote serikali yetu huwajengea watoto wetu vyoo vya mashimo lukuki mashuleni jambo ambalo ni hatari kutokana na udhaifu wa muundo wa vyoo hivyo. Ni muhimu kutenganisha shimo na chumba cha choo kwa usalama wa watumiaji ili tusiendelee kupoteza watu na kufunga shule eti vyoo vimebomoka.
Majengo kupitisha maji
Maeneo mengi ya Tanzania yamezungukwa na vyanzo vya maji ambavyo ni bahari mito na maziwa hali inayosababisha ardhi yake kusharabu maji karibu majira yote ya mwaka na mbaya zaidi wakati wa mvua. Maeneo mengi ya pwani majengo mengi yameathiriwa na tatizo hili na hata limekuwa kero kwa wakazi na watumiaji wa majengo hayo. Majengo hupitisha maji kwa njia ya sakafu na kuta mithili ya chujio au chemchemu. Mara nyingi utagundua kwa kuona ardhi yake imetota maji wakati wote wa majira ya mwaka. Pia majengo mengi ya maeneo haya yanaoza na kutitia kwa haraka na hata mashimo ya vyoo vya maeneo hayo huinuka kwenda juu na siyo chini jambo ambalo ni hatari kwa afya za wakazi. Katika hali hii kuta na sakafu huoza kwa haraka kutokana na maji yaliyopo chini ya ardhi kuwa na kemikali mbalimbali zilizopo kwenye maji hayo. Katika mazingira haya lazima yatumike malighafi sahihi za kuzuia maji hasa wakati wa ujenzi.
SOMA; Kama Utashindwa Kufanya Chochote Utakachojifunza, Basi Fanya Hiki Kimoja Tu, Na Maisha Yako Yatagusa Wengine.
Kuoza kwa kuta
Moja ya masahibu yanayoyakumba majengo ni kuoza kwa kuta za tofali au chuma. Hali hii hutokana na unyevunyevu na kemikali mbalimbali kupitia maji kukaa kwa muda mrefu kwenye kuta hali inayoathiri ubora wakuta hizo. Pia hali hiyo husababishwa na kumea kwa mimea au kupanda maua kwenye viambaza vya kuta ambapo baadhi ya mimea hiyo kusababisha ukungu wa kijani kwenye kuta ambao huzalisha fangasi mbalimbali wanaokula kuta. Pia kitendo cha kumwagilia maua kwenye kuta huozesha kuta haraka. Kinga kuta zote zithiathiriwe na hali ya hewa na maji pale inapolazimu na Usiruhusu mimea kumea kwenye viambaza vya kuta.
Kuoza kwa paa
Unapaswa kutambua kuwa kila kilichoumbwa kina mwisho, ndivyo ilivyo hata kwenye majengo, kila aina ya malighafi iliyotumika hufika mwisho wake kwa wakati tofauti kulingana na ubora na namna yalivyotumika katika ujenzi. Kuoza kwa paa hutegemea ubora na aina ya malighafi zilizotumika bila kusahau na kimo cha mwinuko wa paa hilo. Paa huathiriwa na hali ya mazingira ya eneo husika, mfano paa zilizopo ukanda wa pwani huthiriwa na chumvichumvi zinazobebwa na mikondo ya upepo uvumao kutoka baharini hali inayosababisha paa kuoza haraka, pia hali ya mwinuko ukiwa mdogo husadia paa kuhifadhi takataka mbalimbali ikiwemo majani ya mimea, hali hii ya uchafu kukaa muda mrefu huozesha paa haraka. Unapaswa kuweka paa lenye ubora kulingana na mazingira halisi. Inasikitisha kuona hadi leo hii bado kuna nyumba za serikali zimeezekwa vigae vya asbestos ambavyo ni hatari na vimepigwa marufuku kwa matumizi ya binadamu.
Kusinyaa na kutanuka kwa milango na madirisha
Kuna shida sana hapa, watu wengi hujikuta wakiwalalamikia sana mafundi kuwa hawafai na wamewatia hasara. Kuna aina nyingi za malighafi zinazotumika kutengenezea milango na madirisha, kila aina ya malighafi hizo zina faida na hasara zake. Karibu aina zote za malighafi zina tabia ya kusinyaa na kutanuka kutokana na hali ya hewa (jotiridi) ya mazingira nyumba zilipo. Tumia mbao ngumu (treated hardwood) ili kuondokana na tatizo hili, usitumie mbao mbichi zitakusumbua sana siku zijazo. Kwa wale wanaotumia madirisha na milango ya vioo na aluminiam ni lazima wayapachike na kufitisha kwenye mbao na siyo moja kwa moja kwenye kuta ili kuruhusu hali ya kusinyaa na kutanuka, usipo fanya hivyo aluminiam hupinda na kuleta shida ya kufunga na kufungua. Pia kama unatumia madirisha haya ya vioo (sliding windows) ni lazima yawe makubwa ili kuruhusu hewa kuingia na kutoka kwa haraka kwa kuwa madirisha haya hufunguka nusu tu. Kumbuka kuweka vitasa sahihi kulingana na matumizi, Zingatia sana haya kwa kuwa kila unachoweka kwenye nyumba ni fedha hivyo usiache watu wafanye hovyohovyo tu, ni kero na hasara, wewe na wateja wako hamtafurahia mazingira ya nyumba hiyo.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
7/07/2015 08:18:00 AM | Labels: UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
Mambo Ya Kuzingatia Na Njia Bora Za Uwekezaji Wa Majengo Kwa Gharama Nafuu.
Nina kila sababu ya kumshukuru mungu kwa afya njema niliyonayo
ambayo inaniwezesha kumudu kufanya yote ikiwemo kuandika makala hii kwa wasomaji
wa JIONGEZE UFAHAMU, Chochote unachokifanya huwa ni msukumo wa ndani
kutokana na hamasa kubwa uliyonayo ya kufikia malengo yako, mara nyingi umekuwa
ukipata wazo la kujenga aina fulani ya jengo kwa makazi, ofisi au biashara na
hujui uanzie wapi, napenda nikukumbushe msomaji wa makala hii kuwa biashara ni
ushindani, ili ushinde lazima uwe bora/tofauti dhidi ya wengine, leo nimekuletea
njia bora za wewe kuzitumia ili zikusaidie kutimiza ndoto zako kwa ubora
zaidi.
Wazo la uwekezaji wa majengo
Kama ilivyo kwenye safari yoyote ile lazima kuwe na mipango na mikakati madhubuti ya kufika mahali husika, haijalishi utatumia usafiri gani lazima iwepo dira itakayokuongoza. Ndivyo ilivyo hata kwenye ujenzi, unataka kujenga nyumba ya kupangisha, hoteli, shule, zahanati, ofisi mbalimbali, mgahawa, makazi ya mifugo, gereji, kiwanda au stoo ya kuhifadhia bidhaa na malighafi mbalimbali lazima upate dira itakayokidhi hitaji husika kabla hujatoa kiasi chochote katika uwekezaji wako. Katika ujenzi ramani huwa ndiyo dira kuu inayowaongoza anayewekeza na mafundi wanaojenga. Kuna faida kubwa sana katika ujenzi wa kutumia ramani pasipo kujali unajenga jengo kubwa au dogo, hii husaidia kupata taswira mapema kabla hujaanza kuwekeza. Usinunue ramani mitaani, tumia wasanifu majengo ili wakushauri kulingana na eneo lako na aina ya uwekezaji unaotaka kuwekeza.
Makadirio ya gharama za ujenzi
Watu wengi wameshindwa kuwekeza kutokana na kipengele hiki na walioanza wamejikuta wakiishia njiani pasipo kutimiza ndoto zao kutokana na kutokuwa na mikakati madhubuti ya kifedha. Uwekezaji wowote hugharimu fedha na muda. Kabla ya kufanya uwekezaji huu tafadhali wasiliana na wakadiriaji majenzi ambao ni wataalamu wa uwekezaji na wachumi majenzi uwape wazo lako na namna unavyotaka uwekezaji wako uwe. Hawa ni watu wa ajabu sana, watakushauri namna gani ya kufanya ili uwekeze kulingana na kipato chako pasipo kubadili wazo lako na kukidhi ndoto zako kwa wakati muafaka kulingana na eneo husika la uwekezaji. Hii itakusaidia kuratibu fedha kabla na wakati wa ujenzi na namna utakavyoendesha mradi huo na hatimaye kupata faida baada ya ujenzi huo kukamilika. Pia Kupitia wakadiriaji majenzi wanaweza kukushauri kutafuta vyanzo vingine vya mapato kukidhi aina ya uwekezaji wako.
SOMA; Vitu Vya Msingi Vya Kuzingatia Ili Uweze Kuwa Mwekezaji Mzuri
Namna ya kuwapata mafundi bora
Watu wengi wamenitafuta pale mambo yao yameshaharibika, hajui aanzie wapi kutatua tatizo hilo, hatimaye hujikuta akiongeza gharama zaidi ya mara tatu vile angepaswa kutokana na uhalisia wa mambo yalivyoharibika kutokana na kuwatumia mafundi wasiokidhi ubora. Kwenye ujenzi ni hatari sana kutumia watu wa hovyohovyo kwa kuwa ujenzi ni gharama na wakati mwingine hugharimu hata uhai wa watu na mali zao kitu ambacho hakikubaliki. Kama kazi yako ni ndogo na ya fedha kidogo tafadhali tafuta mafundi wazuri waliofundishwa na makandarasi katika fani husika, iwe tofali, bomba, umeme, milango, paa, madirisha au rangi na mengineyo. Pia kama ujenzi ni mkubwa tafuta mkandarasi anayekidhi vigezo husika. Endapo utawatumia wasanifu majengo na wakadiriaji majenzi katika hatua za awali watakushauri hayo yote kwa kuwa wanajua nini unachohitaji katika uwekezaji wako. Pia endapo utapewa mafundi na watu unaowaamini ni vizuri ukawasaili kulingana na aina ya ramani uliyonayo kama wataimudu au laa! Usiendeshwe na hisia bali akili iwe timamu katika kufikiri na kuamua kutenda ili usilie na kujuta kutokana na mafundi wasio waaminifu na wasiokidhi viwango.
Kabla ya kujenga zingatia haya
Tatizo ni nini: Hali ya sasa imekuwa mbaya sana kutokana na ujenzi holela unaoendelea hapa nchini na hasa miji mikubwa inayoendelea na kukua kwa kasi. Maeneo mengi hayajapimwa kwa matumizi husika na hata yaliyopimwa hayakidhi viwango husika kwa sasa. Kutokana na ongezeko kubwa la watu mijini hasa kwenye miji mikubwa limesababisha tatizo kubwa la matumizi na migogoro ya ardhi hali iliyosababishwa na watu kununua maeneo yasiyopimwa maarufu kama “skwata”. Serikali ya Tanzania imeshindwa kwenda sambamba na kasi ya maendeleo yaliyopo hali inayosababisha kila mwananchi kufanya vile anavyofikiri. Hapa nazungumzia upangaji mji na miji, ni serikali pekee ndiyo ina mamlaka ya kazi hii ya kupanga miji. Leo kuna idadi kubwa ya watu wanaohitaji ardhi kwa matumizi tofauti tofauti hivyo hujikuta wamenunua mahali panapokinzana na matumizi ya watu wengine. Upangaji miji hutofautisha matumizi ya maeneo ya makazi, biashara, kilimo, mifugo, viwanda, maeneo ya wazi na huduma za jamii (zahanati, shule, masoko, makanisa, misikiti, viwanja vya michezo). Wengi wamefariki na wengine wamelia na wapo watakao fariki kwa presha katika hili, kwa ujumla hili ni tatizo kubwa ambalo mzizi wake ni udhaifu wa serikali na uelewa mdogo wa watu wake.
SOMA; Ili Upate Mafanikio Ya Kudumu, Wekeza Kwenye Ardhi Na Majengo.
Nini cha kufanya: popote unaponunua ardhi jiulize mambo mengi sana, hasa maeneo ya “skwata”, tafakari kuhusu miundombinu iliyopo ili ikuongoze kufanya maamuzi.
Kama unanunua skwata, tumia tape mita na siyo hatua kupima urefu na mapana ya maeneo hayo, dalali anakwambia ni 20 kwa 20 na wewe unamwambia fundi wako kiwanja chako ni 20 kwa 20 miguu haina uhalisia na vipimo vya metriki mtazungumzia jambo moja lakini uhalisia ni tofauti kwa sababu watu hawalingani urefu wa miguu.
Kama unaponunua tayari kuna miundombinu hasa ya barabara, zingatia matumizi ya barabara hizo, kama barabara hiyo ina zaidi ya kilometa 20 na inaunganisha maeneo makuu basi jenga mbali zaidi ya mita 30 kutoka barabara hiyo. Na kama barabara ni chini ya kilometa 5 inaunganisha makazi ya watu unapaswa uache umbali usiopungua mita 3 kutoka barabara hiyo na pande zote za jirani angalau mita 2 ndipo ujenge kuta zako. Pia zunguka eneo hilo zaidi ya mita 500 kutoka eneo lako kutazama kama kuna alama inayokutambulisha kama kuna miundombinu yoyote iliyofukiwa kukatisha eneo hilo. Miundombinu inayofukiwa huwekwa alama kila baada ya mita 100 kuonesha mwelekeo wake (miundombinu ya maji safi na maji taka, mafuta, gesi na nyaya za mawasiliano). Ukifanya hivyo utaepukana na dhana ya kubomolewa kutoka kwa mamlaka husika za miundombinu jambo ambalo ni hatari na linaloumiza uchumi wa watu. Hakuna fidia utakayolipwa katika hayo kwa kuwa umeikuta miundominu hiyo.
Pia waeleze na kuwaelimisha wengine ili wajenge kwa mpangilio kuepusha kukosekana kwa njia kutoka nyumba moja na nyingine na viongozi wa mtaa washirikishwe katika kusimamia ujenzi huu usio rasmi kuhakikisha kila anayetaka kujenga aache njia inayokidhi mahitaji ya wengine. Yapo mengi ya kuzingatia kulingana na eneo husika na namna gani utajenga unachotaka kuwekeza (nyumba ya makazi, biashara, shule, zahanati, ofisi mbalimbali, hoteli, migahawa gereji na stoo za malighafi)
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
Wazo la uwekezaji wa majengo
Kama ilivyo kwenye safari yoyote ile lazima kuwe na mipango na mikakati madhubuti ya kufika mahali husika, haijalishi utatumia usafiri gani lazima iwepo dira itakayokuongoza. Ndivyo ilivyo hata kwenye ujenzi, unataka kujenga nyumba ya kupangisha, hoteli, shule, zahanati, ofisi mbalimbali, mgahawa, makazi ya mifugo, gereji, kiwanda au stoo ya kuhifadhia bidhaa na malighafi mbalimbali lazima upate dira itakayokidhi hitaji husika kabla hujatoa kiasi chochote katika uwekezaji wako. Katika ujenzi ramani huwa ndiyo dira kuu inayowaongoza anayewekeza na mafundi wanaojenga. Kuna faida kubwa sana katika ujenzi wa kutumia ramani pasipo kujali unajenga jengo kubwa au dogo, hii husaidia kupata taswira mapema kabla hujaanza kuwekeza. Usinunue ramani mitaani, tumia wasanifu majengo ili wakushauri kulingana na eneo lako na aina ya uwekezaji unaotaka kuwekeza.
Makadirio ya gharama za ujenzi
Watu wengi wameshindwa kuwekeza kutokana na kipengele hiki na walioanza wamejikuta wakiishia njiani pasipo kutimiza ndoto zao kutokana na kutokuwa na mikakati madhubuti ya kifedha. Uwekezaji wowote hugharimu fedha na muda. Kabla ya kufanya uwekezaji huu tafadhali wasiliana na wakadiriaji majenzi ambao ni wataalamu wa uwekezaji na wachumi majenzi uwape wazo lako na namna unavyotaka uwekezaji wako uwe. Hawa ni watu wa ajabu sana, watakushauri namna gani ya kufanya ili uwekeze kulingana na kipato chako pasipo kubadili wazo lako na kukidhi ndoto zako kwa wakati muafaka kulingana na eneo husika la uwekezaji. Hii itakusaidia kuratibu fedha kabla na wakati wa ujenzi na namna utakavyoendesha mradi huo na hatimaye kupata faida baada ya ujenzi huo kukamilika. Pia Kupitia wakadiriaji majenzi wanaweza kukushauri kutafuta vyanzo vingine vya mapato kukidhi aina ya uwekezaji wako.
SOMA; Vitu Vya Msingi Vya Kuzingatia Ili Uweze Kuwa Mwekezaji Mzuri
Namna ya kuwapata mafundi bora
Watu wengi wamenitafuta pale mambo yao yameshaharibika, hajui aanzie wapi kutatua tatizo hilo, hatimaye hujikuta akiongeza gharama zaidi ya mara tatu vile angepaswa kutokana na uhalisia wa mambo yalivyoharibika kutokana na kuwatumia mafundi wasiokidhi ubora. Kwenye ujenzi ni hatari sana kutumia watu wa hovyohovyo kwa kuwa ujenzi ni gharama na wakati mwingine hugharimu hata uhai wa watu na mali zao kitu ambacho hakikubaliki. Kama kazi yako ni ndogo na ya fedha kidogo tafadhali tafuta mafundi wazuri waliofundishwa na makandarasi katika fani husika, iwe tofali, bomba, umeme, milango, paa, madirisha au rangi na mengineyo. Pia kama ujenzi ni mkubwa tafuta mkandarasi anayekidhi vigezo husika. Endapo utawatumia wasanifu majengo na wakadiriaji majenzi katika hatua za awali watakushauri hayo yote kwa kuwa wanajua nini unachohitaji katika uwekezaji wako. Pia endapo utapewa mafundi na watu unaowaamini ni vizuri ukawasaili kulingana na aina ya ramani uliyonayo kama wataimudu au laa! Usiendeshwe na hisia bali akili iwe timamu katika kufikiri na kuamua kutenda ili usilie na kujuta kutokana na mafundi wasio waaminifu na wasiokidhi viwango.
Kabla ya kujenga zingatia haya
Tatizo ni nini: Hali ya sasa imekuwa mbaya sana kutokana na ujenzi holela unaoendelea hapa nchini na hasa miji mikubwa inayoendelea na kukua kwa kasi. Maeneo mengi hayajapimwa kwa matumizi husika na hata yaliyopimwa hayakidhi viwango husika kwa sasa. Kutokana na ongezeko kubwa la watu mijini hasa kwenye miji mikubwa limesababisha tatizo kubwa la matumizi na migogoro ya ardhi hali iliyosababishwa na watu kununua maeneo yasiyopimwa maarufu kama “skwata”. Serikali ya Tanzania imeshindwa kwenda sambamba na kasi ya maendeleo yaliyopo hali inayosababisha kila mwananchi kufanya vile anavyofikiri. Hapa nazungumzia upangaji mji na miji, ni serikali pekee ndiyo ina mamlaka ya kazi hii ya kupanga miji. Leo kuna idadi kubwa ya watu wanaohitaji ardhi kwa matumizi tofauti tofauti hivyo hujikuta wamenunua mahali panapokinzana na matumizi ya watu wengine. Upangaji miji hutofautisha matumizi ya maeneo ya makazi, biashara, kilimo, mifugo, viwanda, maeneo ya wazi na huduma za jamii (zahanati, shule, masoko, makanisa, misikiti, viwanja vya michezo). Wengi wamefariki na wengine wamelia na wapo watakao fariki kwa presha katika hili, kwa ujumla hili ni tatizo kubwa ambalo mzizi wake ni udhaifu wa serikali na uelewa mdogo wa watu wake.
SOMA; Ili Upate Mafanikio Ya Kudumu, Wekeza Kwenye Ardhi Na Majengo.
Nini cha kufanya: popote unaponunua ardhi jiulize mambo mengi sana, hasa maeneo ya “skwata”, tafakari kuhusu miundombinu iliyopo ili ikuongoze kufanya maamuzi.
Kama unanunua skwata, tumia tape mita na siyo hatua kupima urefu na mapana ya maeneo hayo, dalali anakwambia ni 20 kwa 20 na wewe unamwambia fundi wako kiwanja chako ni 20 kwa 20 miguu haina uhalisia na vipimo vya metriki mtazungumzia jambo moja lakini uhalisia ni tofauti kwa sababu watu hawalingani urefu wa miguu.
Kama unaponunua tayari kuna miundombinu hasa ya barabara, zingatia matumizi ya barabara hizo, kama barabara hiyo ina zaidi ya kilometa 20 na inaunganisha maeneo makuu basi jenga mbali zaidi ya mita 30 kutoka barabara hiyo. Na kama barabara ni chini ya kilometa 5 inaunganisha makazi ya watu unapaswa uache umbali usiopungua mita 3 kutoka barabara hiyo na pande zote za jirani angalau mita 2 ndipo ujenge kuta zako. Pia zunguka eneo hilo zaidi ya mita 500 kutoka eneo lako kutazama kama kuna alama inayokutambulisha kama kuna miundombinu yoyote iliyofukiwa kukatisha eneo hilo. Miundombinu inayofukiwa huwekwa alama kila baada ya mita 100 kuonesha mwelekeo wake (miundombinu ya maji safi na maji taka, mafuta, gesi na nyaya za mawasiliano). Ukifanya hivyo utaepukana na dhana ya kubomolewa kutoka kwa mamlaka husika za miundombinu jambo ambalo ni hatari na linaloumiza uchumi wa watu. Hakuna fidia utakayolipwa katika hayo kwa kuwa umeikuta miundominu hiyo.
Pia waeleze na kuwaelimisha wengine ili wajenge kwa mpangilio kuepusha kukosekana kwa njia kutoka nyumba moja na nyingine na viongozi wa mtaa washirikishwe katika kusimamia ujenzi huu usio rasmi kuhakikisha kila anayetaka kujenga aache njia inayokidhi mahitaji ya wengine. Yapo mengi ya kuzingatia kulingana na eneo husika na namna gani utajenga unachotaka kuwekeza (nyumba ya makazi, biashara, shule, zahanati, ofisi mbalimbali, hoteli, migahawa gereji na stoo za malighafi)
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
6/30/2015 07:19:00 AM | Labels: UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
Ili Upate Mafanikio Ya Kudumu, Wekeza Kwenye Ardhi Na Majengo.
Daima namshukuru mungu kwa namna ambavyo amekuwa akinipa pumzi
pasipo malipo, Baraka hizi ndizo zinazonisukuma niweze kuwatazama wengine kama
sehemu yangu ya maisha hapa duniani. Ndugu Mtanzania mwenzangu ambaye umekuwa
ukitumia muda mwingi kufikiri namna gani utatoka hapo ulipo na kuweza kufikia
ndoto zako, usikate tamaa endelea kusonga mbele kwa kuwa unajua unakoenenda, ni
furaha isiyo kifani ikiwa unasafiri na unajua unakokwenda na unatambua lengo la
safari hiyo ni nini. Leo naungana na wale wote ambao lengo lao ni uwekezaji
katika ardhi na majengo. Napenda kukushirikisha ili upate njia rahisi ya wewe
kufikia malengo kwa njia ya ardhi au majengo kwa kuwa nimekuwa katika sekta hii
kwa muda na nimewasaidia wengi katika hili.
Kwa nini uwekeze kwenye ardhi na majengo
Katika Tanzania hali ya sasa ni rahisi kwa uwekezaji huu lakini inazidi kuwa ngumu katika siku zijazo kutokana na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa, ndiyo; uwekezaji wowote ule hutegemea hali ya uchumi ikiambatana na sheria, sera na taratibu za wakati huo. Idadi ya watu inaongezeka kwa kasi sana tofauti na miaka iliyopita, hivyo ongezeko hilo huenda sambamba na mahitaji ya kibinadamu kama vile makazi na huduma mbalimbali za kijamii, mahitaji hayo hufanyika kwenye ardhi na majengo, hivyo hali ya sasa inahitaji sana ardhi na majengo kwa matumizi mbalimbali nchini kote iwe mijini au vijijini, hali hii ya uhitaji husababisha gharama ya ardhi kupanda kwa haraka sana kwa kuwa bidhaa hiyo ni adimu na ina ukomo (ardhi haiongezeki wala haizalishwi).
SOMA; Njia Kumu(10) Za Kupata Utajiri Na Mafanikio.
Inasikitisha kuona mtanzania anayetaka kujikwamua kiuchumi anakuwa mpangaji kwenye nyumba ya kuishi na hata kwenye ofisi za biashara zake. Wengi Hujikuta wakiyumba pale gharama hizo zinapobadilika mara kwa mara kutoka kwa wamiliki kutokana na uhitaji mkubwa wa makazi na ofisi za biashara. Pia wengi huyumba kibiashara kutokana na kuhamahama kwa ofisi jambo ambalo huwa usumbufu kwa wateja. Amua kumiliki ardhi, amua sasa kujenga ili umiliki ofisi za biashara zako au makazi na kuwapangisha wengine.
Fursa zilizopo kwenye ardhi na majengo
Udalali wa nyumba na viwanja
Haijalishi upo wapi na upo katika hali gani ya uchumi kazi hii unaweza kuifanya, uwe mjini au kijijini pia unaweza fanya endapo utaamua kutenda kwa uadilifu. Unaweza kuwa dalali wa viwanja, mashamba na nyumba kwa kununua au kupangishwa, hapa dalali unajipatia fedha kwa kazi ya kuwaunganisha mteja na mwenye mali, kazi kubwa hapa ya dalali ni kuitangaza bidhaa hiyo kwa makubaliano ya mwenye mali na mteja kulingana na hitaji husika. Fungua ofisi yako na uisajili kwa mamlaka husika ili upate fursa kubwa zaidi na hata ufanye kazi na makampuni ya ndani na nje ya nchi yanayohitaji huduma hii. Usifanye kazi hii kwa ubabaishaji bali kwa weledi na ndipo utakapoona mafanikio yako.
Ununuaji na uuzaji wa viwanja na majengo
Katika njia hii unaweza kununua ardhi au nyumba kwa bei rahisi baada ya kufanya marekebisho kadhaa unaweza kuiuza kwa gharama ya juu zaidi tofauti na ulivyonunua. Kwa wale waliopo vijijini wanaweza kununua mashamba/mapori na kuyaongezea thamani/kuyasajili kulingana na eneo husika baada ya miezi au miaka kadhaa unaweza kuuza kwa thamani kubwa zaidi tofauti na ulivyo nunua na huu ndiyo uwekezaji unaolipa zaidi. Watu wengi wamenufaika sana kwa uwekezaji huu na hata wameweza kufanya makubwa zaidi ya walivyotarajia.
SOMA; Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)
Kuongeza thamani za viwanja na majengo
Kwa bahati ni watanzania wachache sana wanaoifahamu njia hii ya uwekezaji, miongoni mwa watanzania wachache niliokutana nao walijilaumu sana kuwa wamechelelewa kupata wazo hili na eti wamechelewesha mafanikio yao. Napenda nikueleze msomaji wa makala hii kuwa hujachelewa na wala hujawahi, amua sasa kuwekeza. Katika njia hii unaweza kununua shamba ukaliwekea miundombinu ya kilimo cha aina fulani ya kuboresha shamba hilo baadae ukalikodisha kwa wahitaji wa aina hiyo ya miundombinu uliyoiweka, pia unaweza kununua kiwanja ukaweka miundombinu ya uwekezaji wa aina fulani ili kuvutia wawekezaji wengine katika ardhi hiyo, pia unaweza nunua nyumba kwa bei rahisi ukaiboresha au ukaibadili matumizi kulingana na hali ya uhitaji wa mahali husika. Katika njia hii ya uwekezaji ukishaongeza thamani ya mali yako unaweza kuikodisha au kuiuza kwa wahitaji au wawekezaji wengine. Kwa njia hii watu wengi wameingia ubia na makampuni makubwa hasa taasisi za fedha kwa kuwakodisha na kuwauzia maeneo na majengo yao na hali wao wakiendelea kunufaika ilihali wametulia au wanafanya mengine huku kipato kinaingia kutokana na kodi hizo.
Umiliki wa rasilimali ardhi na ofisi za biashara
Mwisho kabisa, hatimaye utakuwa ni mmiliki wa ardhi ndani ya nchi yako mwenyewe itakayokupa fursa nyingi ya kufanya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Inasikitisha Mtanzania unaishi kama mkimbizi ndani ya nchi yako kwa kuhamahama mahali pasipo na ulazima. Wewe unapanga mambo yako namna utakavyoijenga biashara yako hapo ulipopanga ofisi wakati huohuo pia mmiliki wako anawaza namna gani atakuondoa ili aweke ofisi zake au ampe mwingine mwenye uwezo wa kumlipa zaidi yako. Ondokana na haya masahibu kwa kumiliki makazi na ofisi zako mwenyewe. Kumiliki inawezekana amua sasa ili upange maendeleo yako kwa uhakika na ufasaha zaidi.
Mtaji utapata wapi?
Napenda nikupe habari njema msomaji wa makala hii, tumia akiba yako kutimiza ndoto zako pia taasisi na mashirika mengi hapa nchini yanahitaji watu wenye malengo haya ili iwawezeshe katika kutimiza ndoto zao, pia taasisi nyingi za kifedha na mashirika mengi hapa nchini yameanza kushindana kutafuta watu wenye malengo kama haya ili iwawezeshe katika uwekezaji huu. Pia hata mashirika mengi hapa nchini yameanza kuwasaidia wananchi kwa kujenga na kuwauzia nyumba wafanyakazi wake na hata wadau wengine wanao hitaji. Uwekezaji huu huchochea ukuaji uchumi wa nchi kwa haraka sana tofauti na uwekezaji mwingine. Unachofanya wewe ni kuandika nia na lengo la aina ya uwekezaji unaotaka kufanya na namna gani utakavyonufaika katika uwekezaji huo na taasisi hiyo namna ambavyo utakavyorudisha fedha hizo (business plan). Ni rahisi sana, wengi wametumia njia hizi za kuomba fedha kwa mashirika na taasisi za kifedha kwa masharti nafuu na kuweza kufanya makubwa tofauti na walivyofikiri.
Nakusihi msomaji wa JIONGEZE UFAHAMU, Wekeza kwenye ardhi na majengo upate mafanikio ya kudumu ukuze uchumi wa wako na uchumi wa nchi.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
Kwa nini uwekeze kwenye ardhi na majengo
Katika Tanzania hali ya sasa ni rahisi kwa uwekezaji huu lakini inazidi kuwa ngumu katika siku zijazo kutokana na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa, ndiyo; uwekezaji wowote ule hutegemea hali ya uchumi ikiambatana na sheria, sera na taratibu za wakati huo. Idadi ya watu inaongezeka kwa kasi sana tofauti na miaka iliyopita, hivyo ongezeko hilo huenda sambamba na mahitaji ya kibinadamu kama vile makazi na huduma mbalimbali za kijamii, mahitaji hayo hufanyika kwenye ardhi na majengo, hivyo hali ya sasa inahitaji sana ardhi na majengo kwa matumizi mbalimbali nchini kote iwe mijini au vijijini, hali hii ya uhitaji husababisha gharama ya ardhi kupanda kwa haraka sana kwa kuwa bidhaa hiyo ni adimu na ina ukomo (ardhi haiongezeki wala haizalishwi).
SOMA; Njia Kumu(10) Za Kupata Utajiri Na Mafanikio.
Inasikitisha kuona mtanzania anayetaka kujikwamua kiuchumi anakuwa mpangaji kwenye nyumba ya kuishi na hata kwenye ofisi za biashara zake. Wengi Hujikuta wakiyumba pale gharama hizo zinapobadilika mara kwa mara kutoka kwa wamiliki kutokana na uhitaji mkubwa wa makazi na ofisi za biashara. Pia wengi huyumba kibiashara kutokana na kuhamahama kwa ofisi jambo ambalo huwa usumbufu kwa wateja. Amua kumiliki ardhi, amua sasa kujenga ili umiliki ofisi za biashara zako au makazi na kuwapangisha wengine.
Fursa zilizopo kwenye ardhi na majengo
Udalali wa nyumba na viwanja
Haijalishi upo wapi na upo katika hali gani ya uchumi kazi hii unaweza kuifanya, uwe mjini au kijijini pia unaweza fanya endapo utaamua kutenda kwa uadilifu. Unaweza kuwa dalali wa viwanja, mashamba na nyumba kwa kununua au kupangishwa, hapa dalali unajipatia fedha kwa kazi ya kuwaunganisha mteja na mwenye mali, kazi kubwa hapa ya dalali ni kuitangaza bidhaa hiyo kwa makubaliano ya mwenye mali na mteja kulingana na hitaji husika. Fungua ofisi yako na uisajili kwa mamlaka husika ili upate fursa kubwa zaidi na hata ufanye kazi na makampuni ya ndani na nje ya nchi yanayohitaji huduma hii. Usifanye kazi hii kwa ubabaishaji bali kwa weledi na ndipo utakapoona mafanikio yako.
Ununuaji na uuzaji wa viwanja na majengo
Katika njia hii unaweza kununua ardhi au nyumba kwa bei rahisi baada ya kufanya marekebisho kadhaa unaweza kuiuza kwa gharama ya juu zaidi tofauti na ulivyonunua. Kwa wale waliopo vijijini wanaweza kununua mashamba/mapori na kuyaongezea thamani/kuyasajili kulingana na eneo husika baada ya miezi au miaka kadhaa unaweza kuuza kwa thamani kubwa zaidi tofauti na ulivyo nunua na huu ndiyo uwekezaji unaolipa zaidi. Watu wengi wamenufaika sana kwa uwekezaji huu na hata wameweza kufanya makubwa zaidi ya walivyotarajia.
SOMA; Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)
Kuongeza thamani za viwanja na majengo
Kwa bahati ni watanzania wachache sana wanaoifahamu njia hii ya uwekezaji, miongoni mwa watanzania wachache niliokutana nao walijilaumu sana kuwa wamechelelewa kupata wazo hili na eti wamechelewesha mafanikio yao. Napenda nikueleze msomaji wa makala hii kuwa hujachelewa na wala hujawahi, amua sasa kuwekeza. Katika njia hii unaweza kununua shamba ukaliwekea miundombinu ya kilimo cha aina fulani ya kuboresha shamba hilo baadae ukalikodisha kwa wahitaji wa aina hiyo ya miundombinu uliyoiweka, pia unaweza kununua kiwanja ukaweka miundombinu ya uwekezaji wa aina fulani ili kuvutia wawekezaji wengine katika ardhi hiyo, pia unaweza nunua nyumba kwa bei rahisi ukaiboresha au ukaibadili matumizi kulingana na hali ya uhitaji wa mahali husika. Katika njia hii ya uwekezaji ukishaongeza thamani ya mali yako unaweza kuikodisha au kuiuza kwa wahitaji au wawekezaji wengine. Kwa njia hii watu wengi wameingia ubia na makampuni makubwa hasa taasisi za fedha kwa kuwakodisha na kuwauzia maeneo na majengo yao na hali wao wakiendelea kunufaika ilihali wametulia au wanafanya mengine huku kipato kinaingia kutokana na kodi hizo.
Umiliki wa rasilimali ardhi na ofisi za biashara
Mwisho kabisa, hatimaye utakuwa ni mmiliki wa ardhi ndani ya nchi yako mwenyewe itakayokupa fursa nyingi ya kufanya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Inasikitisha Mtanzania unaishi kama mkimbizi ndani ya nchi yako kwa kuhamahama mahali pasipo na ulazima. Wewe unapanga mambo yako namna utakavyoijenga biashara yako hapo ulipopanga ofisi wakati huohuo pia mmiliki wako anawaza namna gani atakuondoa ili aweke ofisi zake au ampe mwingine mwenye uwezo wa kumlipa zaidi yako. Ondokana na haya masahibu kwa kumiliki makazi na ofisi zako mwenyewe. Kumiliki inawezekana amua sasa ili upange maendeleo yako kwa uhakika na ufasaha zaidi.
Mtaji utapata wapi?
Napenda nikupe habari njema msomaji wa makala hii, tumia akiba yako kutimiza ndoto zako pia taasisi na mashirika mengi hapa nchini yanahitaji watu wenye malengo haya ili iwawezeshe katika kutimiza ndoto zao, pia taasisi nyingi za kifedha na mashirika mengi hapa nchini yameanza kushindana kutafuta watu wenye malengo kama haya ili iwawezeshe katika uwekezaji huu. Pia hata mashirika mengi hapa nchini yameanza kuwasaidia wananchi kwa kujenga na kuwauzia nyumba wafanyakazi wake na hata wadau wengine wanao hitaji. Uwekezaji huu huchochea ukuaji uchumi wa nchi kwa haraka sana tofauti na uwekezaji mwingine. Unachofanya wewe ni kuandika nia na lengo la aina ya uwekezaji unaotaka kufanya na namna gani utakavyonufaika katika uwekezaji huo na taasisi hiyo namna ambavyo utakavyorudisha fedha hizo (business plan). Ni rahisi sana, wengi wametumia njia hizi za kuomba fedha kwa mashirika na taasisi za kifedha kwa masharti nafuu na kuweza kufanya makubwa tofauti na walivyofikiri.
Nakusihi msomaji wa JIONGEZE UFAHAMU, Wekeza kwenye ardhi na majengo upate mafanikio ya kudumu ukuze uchumi wa wako na uchumi wa nchi.
Mwandishi wa makala hii ni mwanataaluma na mshauri wa ujenzi.
Anapatikana kwa: Simu: +255 685 729 888, Email: kimbenickas@yahoo.com
6/23/2015 07:30:00 AM | Labels: UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
Kuhusu Uwekezaji Tanzania
UWEKEZAJI TANZANIA ni mtandao unaokupatia maarifa na taarifa mbalimbali za uwekezaji kwa hapa nchini Tanzania.
Kupitia mtandao huu utajifunza fursa mbalimbali za uwekezaji na pia kupata taarifa zinazohusu uwekezaji.
Kuna aina mbalimbali za uwekezaji zinazoweza kufanyika Tanzania.
Pia ardhi hii inaruhusu kilimo na hivyo mtu unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha biashara.
Pia dhamana ya uwekezaji UTT, inatoa fursa kwa watu kununua vipande na vipande hivyo kuongezeka thamani na hivyo kunufaika zaidi.
Kuna fursa nyingi sana za uwekezaji ambazo utajifunza kupitia mtandao huu.
Kupitia mtandao huu utajifunza fursa mbalimbali za uwekezaji na pia kupata taarifa zinazohusu uwekezaji.
AINA ZA UWEKEZAJI TANZANIA.
Kwa bahati nzuri sana kuna aina nyingi sana za uwekezaji Tanzania. Kuna kila rasilimali na fursa mbalimbali za uwekezaji. Ugunduzi wa mafutra na gesi unaoendelea kufanyika Tanzania unaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi sana.Kuna aina mbalimbali za uwekezaji zinazoweza kufanyika Tanzania.
1. Uwekezaji wa mali.
Tanzania kuna arhi kubwa sana ambapo mtu anaweza kununua na kuendeleza kwa kujenga majengo ya kibishara na hata makazi.Pia ardhi hii inaruhusu kilimo na hivyo mtu unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha biashara.
2. Bishara.
Kwa kuwa uchumi wa tanzania unakua kwa kasi sana mtu yeyote anayweza kuwekeza kwenye biashara anaweza kuapata faida kubwa. Biashara za bidhaa na huduma zinakua kwa kasi sana kutokana na ongezeko la watu na muingiliano wa kimataifa.3. Uwekezaji katika maliasili na gesi.
Tanzania ina gesi nyingi sana ambayo bado haijachimbwa. Hii inatoa fursa kubwa sana ya uwekezaji.4. Uwekezaji wa hisa na vipande.
Hii ni fursa nzuri ya uwekezaji kwa watu ambao wana miotaji kidogo. Soko la hisa la dar es salaa limeorodhesha makampuni mbalimbali ambayo mtu anaweza kununua hisa.Pia dhamana ya uwekezaji UTT, inatoa fursa kwa watu kununua vipande na vipande hivyo kuongezeka thamani na hivyo kunufaika zaidi.
Kuna fursa nyingi sana za uwekezaji ambazo utajifunza kupitia mtandao huu.
11/02/2014 04:58:00 PM | Labels: BIASHARA, DHAMANA YA UWEKEZAJI(UTT), FEDHA, HABARI ZA UWEKEZAJI, SOKO LA HISA(DSE), UCHUMI, UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
Subscribe to:
Posts (Atom)


