Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)

Watu wengi wanatamani kununua hisa kupitia soko la Hisa la Dar es salaam ila bado hawafahamu ni jinsi gani wanaweza kununua hisa wakiwa mahali popote pale Tanzania. Soko la Hisa limetengeneza njia rahisi ambayo kila mtu anaweza kununua hisa akiwa sehemu yoyote ile Tanzania.

Unapohitaji kununua Hisa katika soko la Hisa unatakiwa kuwa na email, akaunti ya bank na kuwa na mawasiliano brocker yoyote Yule ambaye amesajiliwa katika soko la Hisa.

SOMA; Soko la Hisa la Dar: Fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wazalendo Tanzania

Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa

Baada ya kufanya maamuzi ya kampuni gani ya kununua katika soko la Hisa. Unaweza kutamfuta brocker ambaye amesajiliwa na soko la Hisa kwa ajili ya kununua hisa zako.

1. Wasiliana Brocker kwa ajili ya kununua hisa

Wasiliana na brocker yoyote ambaye amesajiliwa katika soko la hisa. Baada ya kuwasiliana na brocker ataomba email yako kwa ajili ya kukutumia fomu za kujaza. Utaprint fomu hizo ambazo zitakuwa mbili; moja kwa ajili ya taarifa zako binafsi na nyingine kwa ajili ya ununuzi wa hisa.

Hii ni orodha ya Brockers waliosajiliwa na soko la Hisa

· CORE securities Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 212 3103 au info@coresecurities.co.tz

· Orbit Securities Co. Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1758 au orbit@orbit.co.tz

· Rasilimali Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1711 au rasilimali@africaonline.co.tz

· Tanzania Securities Ltd; Tel: +255 22 211 2807 au info@tanzaniasecurities.co.tz

· Vertex International Securities Ltd; Tel: +255 22 211 6382 au vertex@vertex.co.tz

· Solomon Stockbrokers Co. Ltd; Tel: +255 22 211 2874 au solomon@simbanet.net

· E.A. Capital Ltd P.O. Box 20650, Dar es Salaam au Tel +255 779740818/ +255 784461759
EC@EACAPITAL-TZ.COM

· ZAN Securities  Ltd P.O. Box 5366, Dar es Salaam au Tel +255 22 2126415
info@zansec.com

2. Jaza fomu ulizopewa

Baada ya kuprint fomu ulizotumiwa utajaza kutokana na mahitaji ya fomu husika. Baada ya kumaliza kujaza fomu zako, utazi scan zote na kuzituma kama attachment kwenye email ya brocker na kusubiri majibu kutoka kwake.

SOMA; Msingi na ustadi wa kuwekeza kwenye Soko la Hisa

3. Utatumiwa kiasi cha kutuma na akaunti ya benki kwa ajili ya kuingiza pesa

Baada ya kutuma fomu zako kwa brocker atazipitia na kujua ni kiasi gani ulipie ili uweze kununua hisa hizo. Baada ya kupata akaunti ya benki ya utaingiza kiasi cha pesa ambacho umeambiwa kwenye akaunti ya kampuni ya brocker. Baada ya kulipia benki pesa za ununuzi wa hisa uta scan risiti ya benki.

4. Tuma risiti ya benki ambayo umescan kwenye email ya brocker

Baada ya kuscan risiti ya benki utatuma kwa brocker ili kuthibitisha kuwa umefanya malipo hayo kwenye akaunti yao na wewe ni muhusika. Baada ya kutuma atakujibu kuwa amepata na usubiri hisa zako kununuliwa.

SOMA; Hatua Muhimu Kuzifahamu Unapohitaji Kuwekeza Katika Hisa.

5. Subiri kununuliwa kwa hisa zako

Baada ya kupitia hatua zote, subiri kwa ajili ya kununuliwa kwa hisa zako. Kutoka na kupanda na kushuka kwa bei unaweza kumwambia kuwa brocker anunue hisa zako kulingana na bei ya soko hii ni kwa sababu wakati unajaza fomu ulipanga bei ya kununulia.

Kumbuka: Vitu vyote nilivyoelewa unaweza kufanya ndani ya siku moja ikiwa utawasiliana na brocker mapema na kufanya kwa uharaka. Vile vile unaweza tumia gmail akaunti kwa urahisi wa utumaji wa taarifa zako.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

0 comments: