Tabia KUMI Za Watu Waliofanikiwa Sana(PICHA)

Tabia ndio msingi wa mafanikio. Wote tunajua kwamba tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa inaanzia kwenye tabia. Ukiwalinganisha watu hawa wawili utaona utofauti mkubwa sana kwenye tabia zao.

Leo hapa UTAJIONGEZA na tabia kumi ambazo kama na wewe utaweza kujijengea utajiweka kwenye nafasi kubwa ya kuendelea kufanikiwa, KWA SABABU TAYARI UMESHAFANIKIWA.

Hapa nitaweka picha ambayo nimeipata kwenye mtandao wa ADDICTED TO SUCCESS, pitia tabia hizi kumi na zifanyie kazi.

Powerful-Habits-of-The-Ultra-Successful-Infographic

Kwa kifupi tabia hizi ni;

1. Kujifunza kila siku.

2. Kujijengea picha kwenye akili.

3. Weka vipaumbele.

4. Matumizi mazuri ya fedha.

5. Kuamka mapema.

6. Kuweka malengo.

7. Kula vizuri, kufanya mazoezi.

8. Kujiimarisha kiakili.

9. Kutengeneza mtandao.

10. Kujenga tabia nzuri.

Jijengee tabia hizi kumi na mafanikio hayataondoka kwako kamwe.

SOMA; Hizi Ndio Siri 21 Za Mafanikio

Tabia KUMI Za Watu Waliofanikiwa Sana(PICHA)

Tabia ndio msingi wa mafanikio. Wote tunajua kwamba tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa inaanzia kwenye tabia. Ukiwalinganisha watu hawa wawili utaona utofauti mkubwa sana kwenye tabia zao.

Leo hapa UTAJIONGEZA na tabia kumi ambazo kama na wewe utaweza kujijengea utajiweka kwenye nafasi kubwa ya kuendelea kufanikiwa, KWA SABABU TAYARI UMESHAFANIKIWA.

Hapa nitaweka picha ambayo nimeipata kwenye mtandao wa ADDICTED TO SUCCESS, pitia tabia hizi kumi na zifanyie kazi.

Powerful-Habits-of-The-Ultra-Successful-Infographic

Kwa kifupi tabia hizi ni;

1. Kujifunza kila siku.

2. Kujijengea picha kwenye akili.

3. Weka vipaumbele.

4. Matumizi mazuri ya fedha.

5. Kuamka mapema.

6. Kuweka malengo.

7. Kula vizuri, kufanya mazoezi.

8. Kujiimarisha kiakili.

9. Kutengeneza mtandao.

10. Kujenga tabia nzuri.

Jijengee tabia hizi kumi na mafanikio hayataondoka kwako kamwe.

SOMA; Hizi Ndio Siri 21 Za Mafanikio

Fikra TANO Zinazoua Mafanikio Na Jinsi Ya Kuziepuka.

Mpaka sasa unajua kwamba tofauti kubwa ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa inaanzia kwenye fikra zao. Kama bado hujajua ndio nakuwambia leo na nitakuambia mawazo ya aina tano ambayo yanaua kabisa mafanikio yako.

Tunajua kwamba kuwa na mawazo chanya ni kitu muhimu sana ili kufikia mafanikio. Hivyo kuepuka mawazo hasi ni hatua ya kwanza ya kufikia mafanikio. Ila mawazo ya aina tano tutakayokwenda kujifunz ahapa leo yanaweza yasionekane kama ni hasi na ndio maana watu wengi wanashindwa kuyatambua mapema.

SOMA; Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

Kwa kujua mawazo haya na jinsi ya kuyaepuka itakuwa msaada sana kwako kufikia mafanikio.

1. Mimi sio mtaalamu.

Mara nyingi sana umekuwa ukitumia sababu hii kwamba unashindwa kufanya zaidi kwenye kazi yako au biashara yako kwa sababu huna utaalamu mkubwa. Sawa huenda ni kweli huna utaalamu mkubwa ila je unachukua hatua gani?

Kumbuka hakuna mtu aliyezaliwa na utaalamu wowote, vitu vyote tunajifunza hapa duniani. Hivyo kama kuna utaalamu ambao unajua utakusaidia sana kwenye kazi au biashara zako anza kujifunza. Kwa bahati nzuri tunaishi kwenye dunia ambayo kujifunza sio lazima uende darasani, popote ulipo unaweza kujifunz ana kutendea kazi yale uliyojifunza na baada ya muda ukawa mtaalamu.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

2. Hicho kimeshafanyika.

Kuna wakati ambapo unapata wazo zuri la kufanya kitu ambacho kitakufaidisha sana kwenye kazi au biashara. Ila unapofuatilia kwa makini unagundua kwamba kuna watu wengine tayari wanafanya. Kwa kuwa na mawazo ya aina hii unajiondoa mwenyewe kwenye safari ya mafanikio.

Hata kama kitu kimefanyika na watu wengi kiasi gani, kama ndio kitakachokusaidia kifanye. Ila wewe kifanye kwa utofauti na upekee ili uweze kunufaika zaidi. Kama kuna biashara unayotaka kufanya na ukakuta wengine wanaifanya unatakiwa kufurahi kwa sababu tayari una uhakika kwamba soko lipo, hivyo kazi yako ni kujua jinsi gani utavutia na kuwabakiza wateja kwenye biashara yako.

3. Sina ‘connection’

Ni kweli kabisa na pia nilishaandika kwamba haijalishi unajua nini bali unamjua nani, mafanikio yako yatategemea sana na watu unaojuana nao na walioko kwenye mtandao wako. Hivyo ni rahisi sana kuamini kwamba kwa kuwa hujuani na watu waliofanikiwa basi huwezi kufanikiwa.

Swali ni kwamba unataka watu waliofanikiwa waje wakutafute wewe? Wakutafute kwa sababu gani? Wewe ndio unatakiw akuanzisha kitu hiki. Angalia ni watu gani ambao unahitaji kuwa nao kwenye mtandao wako, kisha angalia ni kitu gani unaweza kuwasaidia. Omba nafasi ya kuwasaidia kitu hiko na utakuwa umeanzisha connection muhimu sana kwako. Ndio watu wenye mafanikio ni vigumu sana kuwapata ila kama kweli unataka kuwapata utafanikiwa kuwapata.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

4. Sina hela.

Angalau hii ni sababu ambayo karibu kila mtu anaitumia wakati mmoja au mwingine. Kwa nini huanzi biashara, sina mtaji. Kwa nini biashara yako haikui, sina fedha. Kwa nini hujafikia mafanikio, sina fedha. Sawa huna fedha, swali ni je unataka nani aje akuletee fedha hapo ulipo? Hakuna, kama unasubiri unapoteza muda wako bure. Anzia hapo ulipo, anza na ulichonacho. Kama unataka kuanza biashara anza na kiasi kidogo unachoweza kuanzia, endelea kukua na pale unapokuwa makini utaanza kuona fursa nyingi za kukuza biashara yako. Lakini kama utasema huna fedha, huna mtaji na ukaendelea kulala, nakutakia usingizi mwema.

SOMA; Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

5. Nimejaribu sana lakini nashindwa.

Umesema nijifunze ili niwe mtaalamu, nimeshajifunza sana lakini siwezi.

JIBU; Bado hujajifunza vya kutosha, au haupo makini kwenye kujifunza kwako. Anza tena na jua ni nini hasa unachotaka. Usikate tamaa mpaka utakapofikia.

Umesema hata kama kitu kimefanywa naweza kukifanya na nikafanikiwa, nimeshajaribu hivyo lakini napata hasara tu.

JIBU; Unafanya kama kila mtu anavyofanya, weka ubunifu, jitofautishe, usiwe wa kawaida.

Unasema kama nahitaji connection nianze mimi kutafuta yule ninayetaka connection yake, nimejaribu sana, nimeenda ofisini kwa mtu niliyetaka kupata connection yake masecretary wamenizuia, wameniambia niandike barua na nieleze shida zangu nitapewa wa kunisaidia ila sio yule ninayemtaka.

JIBU; Ongeza juhudi, badili mbinu za kuweza kumpata mtu huyo, anza kufikiria ni jinsi gani unaweza kumsaidia, mwandikie kila unachofikiri kitamfanya atake kujua ni nani amempa mawazo hayo mazuri. Wakati huo huo kuwa bora kwenye kile unachokifanya, watu watakuongelea na moja kwa moja utapata nafasi ya kuonana na waliofanikiwa zaidi.

Unasema nianze kidogo hata kama mtaji sina, hata hicho kidogo sina, nilijaribu kuanz akidogo nimepata hasara na sasa sina hata pa kuanzia.

JIBU; Kama huna hata kidogo cha kuanzia kuna uwezekano mkubwa hujui unachotaka kufanya. Kama ulianza kidogo na umeshindwa, anza tena, ndio safari ya mafanikio ilivyo.

Hizo ndio fikra tano za kuondokana nazo ili uweze kufikia mafanikio. Kumbuka pamoja na yote haya maamuzi yanabaki kwenye mikono yako. Ukiamua kuyatumia haya kwenye maisha yako, utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufanikiwa. Ukiamua kuachana nayo utaendelea hivyo ulivyo.

Nakutakia kila la kheri.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

 

Njia KUMI Za Kuboresha Maisha Yako Ya Kibiashara.

Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara na hata kwenye maisha unahitaji kuwa na malengo na mipango, kufanya kazi kwa bidii na maarifa na hata kuwa na mtizamo chanya kwenye kile unachofanya na hata maisha yako kwa ujumla.

Hakuna kitu kinachowarudisha watu nyuma kama kutokuwa na malengo, uvivu na mtazamo hasi.

Pamoja na mambo hayo muhimu kuna njia kumi unazoweza kuzitumia na ukaboresha maisha yako ya kibiashara kwa kiasi kikubwa sana.

1. Kubali changamoto.

Hakuna barabara iliyonyooka, hivyo hivyo biashara yoyote utakayofanya, hata kama ingekuwa rahisi kiasi gani ina changamoto zake. Unapokutana na changamoto, ikubali na kisha anza kuitatua. Ukianza kuikimbia unajijengea matatizo makubwa baadae.

SOMA; Wajasiriamali Wenye Mafanikio Hufanya Mambo Haya Matano Kila Siku.

2. Jitegemee.

Ili uweze kufikia mafanikio kwenye biashara unayofanya, kuna wakati utahitaji kufanya maamuzi magumu na uweze kuyasimamia. Maamuzi hayo yanaweza yasiwe mazuri au yasiwapendeze wengi. Ni lazima uweze kujtegemea na kujisimamia kwenye biashara yako. Kama utaendesha biashara kwa kutegemea wengine wanafanya nini ndio uige, huwezi kufanikiwa.

3. Zione fursa.

Katika kila hali unayokutana nayo kwenye biashara, zione fursa mbalimbali zinapokuzunguka. Unapopata changamoto angalia ni fursa gani unayoweza kuitoa kwenye changamoto hizo. Kuwa na kiu ya kuangalia fursa na utaanza kuziona nyingi sana zinazokuzunguka.

4. Cheka.

Hata kama unafanya biashara inayokuhitaji uwe makini kw akiasi gani, unahitaji muda wa kucheka. Unahitaji muda ambao unawez akufanya utani wa hapa na pale na ukafurahia na kucheka. Kuna faida kubwa sana kwenye kucheka, inakuongezea kujiamini na kinga ya mwili pia.

SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

5. Wasaidie wengine.

Utapata chochote unachotaka kwenye maisha kama utaweza kuwasaidia watu wengi zaidi kupata kile wanachotaka. Ifanye biashara yako kuwa sehemu ambayo watu wanajua matatizo yao yatapata suluhisho na utapata wateja wengi sana.

6. Kuwa na dhumuni la maisha yako.

Mbali na malengo na mipango ya kibiashara na hata maisha, kuwa na dhumuni kubwa la maisha yako. Hiki ni kitu ambacho utakiishi na ndio kitakusukuma wewe kuweka juhudi zaidi ili kuweza kufikia dhumuni hilo.

7. Kuwa tayari kubadilika.

Unachoamini leo, kesho kinaweza kisiwepo kabisa. Biashara inayolipa leo, miaka michache inaweza isiwepo kabisa. Hivyo wakati wowote kuwa tayari kubadilika. Soma alama za nyakati na kuwa tayari kuchukua hatua kabla mambo hayajakwenda hovyo.

8. Zungukwa na watu chanya.

Hakikisha unazungukwa na watu ambao wana mtizamo chanya kama ulivyo wewe. Hawa watakuwezesha wewe kuendelea na mtizamo wako. Ila kama utazungukwa na watu wenye mtizamo hasi, ni vigumu sana kuweza kuendelea na mtizamo wako.

SOMA; Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

9. Fanya kazi kwa juhudi na maarifa.

Hili ndio hitaji la msingi kabisa, maelezo yanajitosheleza. Kama haupo tayari kufanya kazi kwa bidii na maarifa, achana na biashara, kafanye vitu vingine, na sina wazo ni kitu gani hakihitaji kazi. Kama utakipata tushirikishe.

10. Acha kuwa mwathirika.

Kama unataka kukuza biashara yako unahitaji kuacha kuwa na mawazo ya kiathirika. Pale jambo lolote linapotokea, acha kufikiri kwamba kwa nini limetokea kwako, au kwamba una bahati mbaya. Badala yake chukua hatua ya kubadili mambo. Kama umefanya makosa jifunze na usirudie tena.

Mafanikio kwenye biashara sio kitu rahisi sana ila pale unapojipanga vizuri utaona yanakuja yenyewe bila ya wewe kuteseka sana. Fanya mambo yale ya msingi na jali sana biashara yako na wale wanaokuzunguka. Bila kusahau, jifunze sana, wekeza sana kwenye rasilimali muhimu kwako ambayo ni akili yako.

SOMA; Kurasa 365 Za Mwaka 2015, Fursa Muhimu Kwako Kujifunza.

Mambo KUMI Ya Kufanya Ili Usiishi Maisha Ya Majuto.

Maisha ya majuto sio maisha mazuri kuishi. Ni maisha ambayo yatakufanya ukose furaha na hivyo kuona maisha yako hayana thamani.

Lakini pia majuto mengi ambayo watu wanaishi nayo ni ya kujitengenezea wenyewe iwe kwa matendo yao au kwa mitazamo yao.

Leo utajiongeza na mambo KUMI unayoweza kuanza kufanya leo ili uweze kusihi maisha yasiyokuwa na majuto.

1. Jali afya yako. Hiki ni kitu muhimu sana, ukiwa na afya mbovu utajutia mambo yote ya hovyo uliyofanya yakakupeleka kwenye afya mbovu.

SOMA; NENO LA LEO; Acha Kujiandaa Kuishi…

2. Tenga muda wa kufanya vitu unavyovipenda. Hata kama una kazi ngumu kiasi gani, tenga muda kila siku wa kufanya vitu ambavyo unavipenda kweli kwa moyo wako.

3. Pata muda wa kupumzika, cheka , cheza.

4. Sema kile ambacho unataka kusema. Unafiki utakufanya ujute sana baadae.

5. Badili mtazamo wako.

6. Usiumizwe na yaliyopitwa, usiogopeshwe na yajayo, ishi leo.

SOMA; UKURASA WA 19; Ishi Leo..

7. Kubali kwamba kuna vitu huwezi kuvibadili.

8. Acha kukimbiza fedha na mali, toa huduma nzuri na fedha zitakufuata zenyewe.

9. Shukuru kwa maisha uliyonayo, hata kama ni magumu kiasi gani.

10. Onesha upendo kwa kila mtu anayekuzunguka.

Maisha ni yako na una uamuzi wa kuyaishi vile unavyotaka kama tu hauvunji sheria na taratibu. Chagua kuishi maisha ambayo utayafurahia kila siku ili uweze kuwa na maisha bora. Fanya mambo hayo kumi kuanzia leo na maisha yako yataanza kubadilika.

SOMA; Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..

Sababu TATU Kwa Nini Watu Wengi Wanashinda Kufikia Mafanikio.

Kushindwa ni jambo ambalo haliwezi kukwepeka. Ila tofauti kubwa ya wale waliofanikiwa na ambao hawajafanikiwa ni wale waliofanikiwa waliweza kuendelea hata baada ya kushindwa na wasiofanikiwa walikata tamaa baada ya kushindwa.

Kila mmoja wetu anapenda kufikia mafanikio makubwa kwenye jambo analofanya, inaweza kuwa kazi, inaweza kuwa masomo, inaweza kuwa biashara, inaweza kuwa chochote ambacho ni muhimu kwako.

SOMA; Kitu Muhimu Cha Kufanya Kabla Ya Kutumia Muda Au Fedha.

Kuna vitu vitatu ambavyo vinawafanya watu wengi sana kushindwa kufikia mafanikio japo wanayatamani sana. Leo utajiongeza na vitu hivyo ili uweze kuviepuka na kufikia mafanikio unayotarajia.

1. Kuhsindwa kuendana na watu wengine.

Mafanikio sio kitu ambacho unaweza kukifikia wewe mwenyewe. Mafanikio yako yanategemea sana ushirikiano wako na watu wanaokuzunguka. Kama umeajiriwa kuna bosi wako, wafanyakazi wenzako na hata wafanyakazi walioko chini yako. Kama unafanya biashara kuna wateja, wafanyabiashara wenzako, wafanyakazi wako na kadhalika. Watu wote hawa wanaokuzunguka wana mchango mkubwa sana kwenye mafanikio yako. Ukiweza kushirikiana nao watakupa ushirikiano mzuri na utafikia mafanikio. Ukishindwa kushirikiana nao vizuri itakuwa vigumu sana kwako kufikia mafanikio.

SOMA; Naomba Ufanye Changamoto Hii Ya Siku Kumi, Utabadili Sana Maisha Yako.

2. Kukata tamaa.

Kama tulivyoona hapo juu, tofauti ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni kwamba waliofanikiwa huendelea kufanya hata wanapokutana na magumu, ila wasiofanikiwa hukata tamaa haraka wanapokutana na vikwazo au changamoto. Kama kweli una kiu ya kufanikiwa inabidi uwe king’ang’anizi hata pale mambo yanapoonekana ni magumu.

3. Kuahirisha mambo.

Tabia ya kuahirisha mambo imewazuia watu wengi sana kufikia mafanikio. Mtu anaweka malengo na mipango lakini inapofikia kweye utekelezaji anaahirisha. Tabia ya kuahirisha inamfanya mtu kushindwa kuchukua hatua haraka na hivyo kukosa fursa nzuri za kupata mafanikio.

Epuka mambo hayo matatu kama kweli una kiu ya kufikia mafanikio. Kama utaendele akuyaendekeza utaona siku zinapota ila hakuna mabadiliko kwenye maisha yako.

Mwaka huu 2015 unahitaji nini tena ili kufanikiwa? Kila unachohitaji unajifunza kupitia AMKA MTANZANIA, KISIMA CHA MAARIFA, JIONGEZE UFAHAMU, na MAKIRITA AMANI. Kilichobaki ni wewe tu kuchukua hatua.

Nakutakia kila la kheri.

SOMA; Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

 

Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Katika mfumo wa uchumi tunaoishi sasa hivi duniani, ni dhahiri kwamba kipato chako kinaathiriwa na vitu vingi sana.

Kipato chako kinaweza kuathiriwa na hali ya uchumi inavyokwenda. Kwa mfano mfumuko wa bei unapokuwa mkubwa, kipato chako kinaweza kisitoshe matumizi yako. Lakini hii ni nguvu ya nje ambayo huwezi kuiathiri.

Kipato chako pia kinaathiriwa na mambo ambayo yanatokana na wewe binafsi na mambo haya unawezakuyabadili ili kubadili kipato chako.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

Leo tutajadili vitu vitatu muhimu vinavyoathiri kipato chako na jinsi unavyoweza kuvitumia kubadili kipato chako.

Ni ukweli usiopingika kwamba kila mtu anapenda kipato chake kiongezeke, ila sasa unaanzia wapi kukiongeza? Jua vitu hivi vitatu na vifanyie kazi.

1. Unafanya nini.

Kitu cha kwanz akabisa kinachoathiri kipato chako ni unafanya kitu gani? Yaani ni shughuli gani unayofanya ili kujitengenezea kipato? Unafanya biashara? Umeajiriwa? Kama unafanya biashara je ni biashara gani? Na kama umeajiriwa je una utaalamu gani? Tunajua kabisa vipato vinatofautiana na kutokana na kile unachofanya. Kipato cha mwalimu hakiwezi kuwa sawa na cha daktari. Kipato cha boda boda hakiwezi kuwa sawa na cha dala dala.

Kuongeza kipato chako kwenye njia hii ni kuhakikisha unafanya kitu ambacho kina uwezekano mkubwa wa kutengeneza kipato kikubwa.

SOMA; HADITHI_FUNZO; Aliyenusurika Kufa Kutokana Na Tabia Yake Nzuri.

2. Unafanya kwa ubora gani?

Tumeona vipato vinatofautiana kutokana na vitu tofauti. Vile vile ndani ya fani moja au biashara moja, bado vipato havilingani. Watu wawili wanaweza wote kuwa walimu wenye kiwango sawa cha elimu lakini vipato vikawa tofauti. Watu wawili wanaweza kuwa wanaedesha boda boda na wanapaki eneo moja lakini vipato vikawa tofauti. Kwa yule ambaye anafanya kwa ubora wa hali ya juu kipato chake lazima kitakuwa kikubwa.

Hakikisha kile ambacho unakifanya unakifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.

3. Ugumu wa kukubadili.

Kipato chako pia kinaathiriwa na ugumu wa kukubadili wewe kwenye hiko unachofanya. Pata picha wewe unafanya kazi ambayo ni wewe tu unaweza kuifanya, hii ina maana kwamba kama usipokuwepo kazi yako haiwezi kufanywa na mtu mwingine hivyo thamani ya kipato chako inakuwa kubwa. Hali kadhalika kama unafanya biashara kwa kiwango ambacho mteja wako hawezi kukipata sehemu nyingine, lazima utakuwa na kipato kikubwa.

Anza sasa kujitengenezea mazingira ya wewe kuw avigumu kubadilishwa. Na sio ufanye hivyo kwa kuwafanyia wengine majungu, ila kwa kujiboresha zaidi na hivyo kufanya kazi au biashara yako kwa ubora wa hali ya juu.

Chukua hatua leo ili kuboresha kipato chako, acha kulalamika, maamuzi ni yako.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

Okoa Muda Huu Muhimu Ambao Unaupoteza Kila Siku Na Kukuchelewesha Kufikia Mafanikio.

Kuna muda mwingi sana ambao unaupoteza kila siku na kwa kufanya hivyo unajichelewesha kufikia mafanikio.

Kumbuka muda una thamani kubwa kuliko fedha kwa sababu muda ukishapotea haurudi tena, ila ukipoteza fedha leo kesho unaweza kupata nyingine.

SOMA; UKURASA WA 09; MUDA–Kitu Chenye Thamani Kubwa Ila Kisichothaminika Na Wengi.

Muda huo unaopoteza ni ule unaotumia kusema mabaya ya wengine, au kuonesha mapungufu ya wengine.

Ni kweli kwamba wengine wanaweza kuwa wana mapungufu makubwa, wanaweza kuwa wanakosea sana ila wewe kutumia muda wako kuyasemea hayo hakutakusaidia kwa vyovyote kufikia mafanikio unayotarajia.

Kwa mfano wewe ni mfanya biashara na unatumia muda wako mwingi kusema jinsi gani wafanyabiashara wengine wanakosea, au wanamadhaifu. Kwa kufanya hivi hauna tofauti na wao. Ni heri kutumia muda wako mwingi kuimarisha biashara yako.

SOMA; Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

Inawezekana wewe ni mchungaji ambae una kanisa, ila unatumia muda wako mwingi kusema jinsi gani wachungaji wengine wana mapungufu au wana mabaya. Ni vyema ukatumia muda huo vizuri kuwaonesha watu ni kipi sahihi kinachotakiwa kufanywa.

Inawezekana wewe ni mwanasiasa na unatumia muda mwingi kuonesha madhaifu ya chama kingine au mgombea mwingine. Hii haitakusaidia kushinda uchaguzi, ni vyema kutumia muda wako mwingi kuwaeleza watu utawafanyia nini na watakuona upo makini.

Sisemi tusikemee mabaya, ila hii isiwe agenda yetu kuu, labda kama ndio agenda yako na kama ndivyo hujui unachokifanya au itakuwa vigumu kifikia mafanikio.

Kumbuka kitu chochote ambacho hakipo kwenye malengo na mipango yako ni kelele kwako. Achana nacho mara moja na wekeza nguvu zako kwenye kukuza kile unachofanya.

SOMA; USHAURI ADIMU; Unapokutana Na Tatizo Jiulize Jambo Hili Moja La Msingi.

Vitu Vitatu Vitakavyokufanya Uwe Na Hamasa Ya Kufikia Mafanikio.

Hamasa ni kitu muhimu sana ili uweze kufikia mafanikio kwenye jambo lolote unalofanya.
Hii ni kwa sababu katika njia yoyote utakayopita utakutana na vikwazo na pia katika yale utakayofanya utapata changamoto.
Bila ya kuwa na hamasa kubwa utaishia njiani kwa kukata tamaa haraka sana.
Uzuri ni kwamba unaweza kuhamasishwa na pia unaweza kujihamasisha mwenyewe.
Unahamasishwa unaposoma vitabu ja makala nzuri kama hizi unazosoma hapa kwenye JIONGEZE UFAHAMU, MAKIRITA AMANI, AMKA MTANZANIA na KISIMA CHA MAARIFA.
Baada ya kupata hamasa hii unaweza sasa kuendelea kujihamasisha mwenyewe.
Ili kujihamasisha mwenyewe unahitaji kuwa na vitu hivi vitatu muhimu;
1. Kujisimamia.
Kama unajua kwamba unaweza kujisimamia mwenyewe unakuwa na hamasa kubwa sana ya kufanya vizuri. Hakuma mtu ambaye anapenda kupangiwa kila kitu cha kufanya, unapokuwa na nguvu ya kujipangia na kujisimamia unakuwa na hamasa ya kutekeleza mipango yako.
2. Kubobea.
Kama wewe ni mtaalamu wa kitu unachofanya unakuwa na hamasa kubwa ya kufanya kitu hiko. Kama umebobea na unatoa vitu ambavyo kila mtu anavikubali utahamasika kufanya zaidi ili wengi zaidi wanufaike na kile unachotoa.

SOMA; Kitu hiki kimoja ndio kitakufanya uanze.
3. Dhumuni.
Kama una dhumuni zuri la kuwasaidia wengine kwa kile unachofanya utahamasika kufanya zaidi. Kwa kuwa unajua watu wanakiutegemea kwa unachofanya na wanategemea kitu bora, hutotaka kuwaangusha. Hii itakuhamashisha ufanye zaidi na zaidi.
Hivyo ndio vitu vitatu muhimu unavyohitaji ili kujihamasisha. Habari njema ni kwamba kama huna vitu hivyo unaweza kujifunza. Na utajifumza kwa kujiunga ma KISIMA CHA MAARIFA ambapo mimi na wewe tutakuwa karibu zaidi.
Karibu sana.

Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

Warren Buffett ni mmoja wa watu matajiri sana duniani. Utajiri wake huu ameupata kupitia biashara na uwekezaji. Alianza biashara akiwa na miaka 11 na sasa ana miaka 83. Kwa miaka zaidi ya 60 ambapo amekuwa kwenye biashara una uzoefu wa kutosha kutufundisha sisi ni vitu gani vya kuzingatia kwenye biashara.

Hizi hapa ni sheria 8 za kufanikiwa kwenye biashara kutoka kwa Warren Buffett.

1. Tulia wakati wa matatizo/changamoto.

Katika biashara kuna wakati ambao utakutana na changamoto na matatizo mbalimbali. Huu ni wakati ambao Warren anatushauri tutulie badala ya kuvurugwa na hatimaye kuharibu kila kitu.

SOMA; Maswali Matatu Kwa Anayetaka Kuwa Mjasiriamali Kujiuliza Kutoka Kwa Richard Branson.

2. Zungukwa na watu wazuri.

Kama unafanya biashara kwa kushirikiana na mtu au watu wengine, hakikisha watu hawa  wana maadili mazuri na wanandoto kubwa ya mafanikio kama uliyonayo wewe.

3. Ng’ang’ania kile unachokitaka.

Warren anashauri kwamba usiache lengo lako kuu kwa sababu kuna vitu vizuri umeviona pembeni, kufanya hivi kutakuletea kushindwa.

4. Weka gharama chini.

Hakikisha gharama za kuendesha biashara yako zinakuwa chini sana ili uweze kuuza kwa bei ambayo wateja wako wanaweza kuimudu na wewe kupata faida.

SOMA; Hakuna Anayejua Anachofanya, Na Huo Ndio Uzuri Wa Maisha.

5. Toa zawadi kwa wafanyakazi wako.

Warren anashauri kwamba pale wafanyakazi wanapofanya vizuri uwape zawadi hata kama ni ndogo kiasi gani. Hii inawafanya waone unajali.

6. Epuka matatizo.

Warren aliwahi kumwandikia mshirika wake kwenye biashara hivi “nachotaka kujua ni wapi nitaenda kufa hivyo nisiende hapo kamwe”. Kama unataka kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuepuka matatizo maana matatizo mengi yanasababishwa na wewe mwenyewe.

7. Fanya kuwa ndogo.

Buffett anasema kwamba biashara inapokuwa kubwa sana inakuwa vigumu kubadilika na urasimu unakuwa mkubwa kiasi cha kuwachosha wafanyakazi na hata wateja. Anashauri kurahisisha uongozi wa biashara hivyo hata ikikua sana bado ionekane ni ndogo na rahisi kuongoza na kuwasiliana.

8. Linda heshima yako.

Buffett anasisitiza kwamba heshima yako ni kitu muhimu sana kwenye mafanikio ya biashara. Anashauri kuwa mwaminifu na kutofanya kitu chochote ambacho usingependa kiripotiwe kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti. Anasisitiza hili kwa kauli hizi mbili;

Poteza hela za biashara na nitakuelewa, poteza sifa ya biashara na nitakuwa mbaya sana kwako.

Inakuchukua miaka 20 kujenga heshima na dakika tano kuiharibu. Ukifikiria hili utafanya mambo kwa tofauti.

Tumia sheria hizi nane kwenye maisha yako ya kila siku na ya biashara na zitakusaidia sana kufikia mafanikio.

SOMA; Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

Kama kila siku una matatizo ya fedha, na karibu kila mtu ana matatizo haya, huenda kuna mambo mawili unayoyafanya kimakosa sana.

Jambo la kwanza kipato chako ni kidogo.

Jambo la pili matumizi yako yanazidi kipato chako.

Leo tutajadili jambo la pili na siku nyingine tutajadili jambo la kwanza. Hiyo endelea kutembelea mtandao huu wa JIONGEZE UFAHAMU ili uweze kujifunza mambo hayo mazuri ambayo yataboresha maisha yako.

Ili kuweza kurudisha usimamizi mzuri kwenye fedha zako, hatua ya kwanza kabisa ni kubana matumizi. Unaweza kufikiri kwa nini hatujaanza kujadili kuongeza kipato, ila kama utaongez akipato kwa tabia uliyonayo ya matumizi mabovu bado utarudi pale pale.

Leo tubane kwanz ama matumizi halafu kwenye makala ijayo tutaongeza kipato.

Zifuatazo ni njia kumi za kubana matumizi kwa mwaka huu 2015.

1. Tengeneza bajeti. Bajeti yako ni muhimu na ndio itakayokuongoza kwenye matumizi yako ya fedha. Jua kila mwezi utatumia kiasi gani na gawa kwenye wiki na hata siku. Iheshimu bajeti yako.

2. Nunua vitu kwa jumla. Kama ni vitu vinavyohusiana na matumizi muhimu ya nyumbani nunua kwa jumla. Hii itakufanya ununue kwa bei nzuri na pia kuweza kwenda na bajeti yako.

3. Sitisha huduma ambazo hutumii. Kama kuna huduma umejiunga nazo ambazo hutumii sana sitisha. Hii inaweza kuwa malipo ya kuangalia tv, malipo ya kuhudhuria mazoezi, malipo ya gharama za simu na kadhalika.

4. Usinunue vitu hovyo. Ukikutana na mtu anauza nguo hata kama umeipenda kiasi gani usiinunue kama hukuwa na ratiba hizo.

5. Epuka sana mikopo. Kama kitu sio muhimu sana kwao, usiingie kwenye mkopo ili kukipata, mikopo ni mzigo ambao unakupotezea fedha nyingi.

6. Punguza starehe. Punguza kiasi ambacho unatumia kwenye starehe kama kula kwenye hoteli kubwa, kutumia vilevi, kwenda kwenye kumbi za starehe na kadhalika.

7. Nunua vitu vyenye ubora, hata kama ni ghali. Unaweza kufikiri kununua vitu vya bei rahisi ni kubana matumizi ila ukawa ndio unaongeza matumizi zaidi. Nunua kitu chenye ubora hata kama ni bei ghali, utakaa nacho muda mrefu zaidi na hivyo kuepuka kupoteza fedha kwenye kununua mara kwa mara.

8. Nunua vitu ambavyo unavihitaji kweli na sio unavyotamani. Kwa mfano nguo, nusu ya nguo zako hujazivaa mwaka mmoja uliopita. Sasa unanunua nyingine za nini? Acha kupoteza fedha.

9. Andaa vitu unavyoweza kuandaa mwenyewe badala ya kufikiria kununua tu. Pendelea kupika chakula badala ya kununua chakula kilichopikwa.

10. Acha kutaka kuonekana. Usifanye mambo kwa sababu kila mtu anafanya. Usinunue simu mpya kwa sababu kila mtu ana simu mpya. Fanya kitu ambacho unakitaka kweli na sio kwa sababu kila mtu anakifanya.

Tumia mbinu hizi kumi na uanze kupunguza matumizi yako mwaka huu 2015. Katika makala ijayo tutajadili njia kumi za kuongeza kipato chako mwaka 2015.

Kila la kheri.

Wajasiriamali Wenye Mafanikio Hufanya Mambo Haya Matano Kila Siku.

Kila mtu ana maelezo yake ya mafanikio. Neno mafanikio lina maana tofauti kw akila mtu. Lakini licha ya utofauti huo bado kwa ujumla mafanikio ni kuwa bora kama unavyoweza kuwa.

Na mafanikio sio kitu ambacho kinatokea mara moja. Hutaamka siku moja asubuhi halafu paa mafanikio hao hapo.

SOMA; USHAURI; Jinsi Ya Kutoka Kimaisha Kwa Kuanza Na Mshahara Mdogo.

Mafanikio yanatokana na jinsi unavyoishi kila siku. Kuna tabia ndogo ndogo unazofanya kila siku ambazo zikikusanyika pamoja ndio zinaleta mafanikio au kushindwa.

Yafuatayo ni mambo matano ambayo wajasiriamali wenye mafanikio hufanya kila siku. Yasome na wewe uanze kuyafanya ili uweze kufikia mafanikio.

1. Wako tayari kujaribu tena hata pale wanaposhindwa.

Haijalishi wameshindwa mara ngapi, wajasiriamali wenye mafanikio huendelea kujaribu tena na tena. Na hawajaribu tu kama wajinga(kwa kurudia kile kile walichofanya) bali wanatumia walichojifunza na kubadili mbinu wanazotumia na hatimaye kupata mafanikio.

SOMA; NENO LA LEO; Hiki Ni Kitu Unachotakiwa Kufanya Kila Siku.

2. Huzikabili hofu zao.

Moja ya vitu vinavyowarudisha watu wengi nyuma ni hofu. Wajasiriamali wenye mafanikio sio kwamba hawana hofu, wanazo ila wanaamua kuzikabili. Wanaingiwa na hofu ila nwanajua hii ni hofu na wanaipuuza na kuendelea na mipango yao.

3. Wanajitengenezea nidhamu binafsi.

Wajasiriamali wenye mafanikio makubwa wanajua ya kwamba nidhamu binafsi ndio msingi wa mafanikio. Hivyo kila siku hujijengea nidhamu binafsi ili waweze kutekeleza majukumu yao, kuaminika zaidi na kuweza kufikia mafanikio. Wako tayari kufanya kazi ngumu leo ili baadae wapate matunda mazuri. Hawakimbilii kufanya vitu vya kuwafurahisha kwa sasa.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

4. Hutenga muda wa kupumzika.

Pamoja na kupenda kufanya kazi kwa bidii na maarifa, wajasiriamali wenye mafanikio wanajua kwamba miili yao haiwezi kufanya kazi muda wote. Hivyo hutenga muda maalumu kwa ajili ya kupumzika ili kurejesha nguvu kwenye miili yao.

5. Hutoa bila ya kutegema kupokea.

Wajasiriamali wenye mafanikio hutoa kwa wengine bila ya kutegemea kupokea. Kama ni bidhaa au huduma wanatoa, hutoa zaidi ya wanavyolipwa.Kwa njia hii huendelea kuwa bora zaidi na kutengeneza wateja wengi, faida kubwa na mafanikio makubwa.

Hayo ndio mambo matano yanayofanywa na wajasiriamali waliofanikiwa, anza sasa kuyafanya na wewe kila siku. Kitakachotokea utaona mwenyewe.

Vyanzo Viwili Vya Vikwazo Vinavyokuzuia Kufikia Mafanikio

Maisha ni magumu, angalau kila mtu wnalikubali hilo.
Kila jambo unalofanya kwenye maisha kuna vikwazo au changamoto ambazo utakutana nazo.
Lakini changamoto hizi haziyokei tu hewahi, bali zina vyanzo vyake.
Kuna vyanzo viwili vya changamoto zinazokufanya mpaka sasa hujafikia mafanikio makubwa.
1. Vikwazo vya kimwili.
Hivi ni vikwazo vinavyoonekana, ujana, uzee, ugonjwa, ulemavu, ufupi, kukosa uzoefu na vingine vingi ambavyo vinaweza kukufanya uone huwezi kuendelea na mapambano.
2. Vikwazo vya kiakili.
Hivi ni vikwazo ambavyo vipo kwenye mawazo yako. Hofu, kutokujiamini, wasiwasi na kukosa uvumilivu. Vikwazo hivi vinakufanya uamini kwamba huwezi kuendelea tena pale unapokutana na changamoto kubwa.
Jambo jema na la kufurahia ni kwamba vikwazo vyote hivi unaweza kuvishinda.
Kama utajifunza kutoka kwa walioshinda licha ya kuwa na vikwazo mbalimbali unaweza na wewe kuchukua hatua na kubadili maisha yako.
Anza sasa kujifunza ili uboreshe maisha yako.

Kitu Hiki Kimoja Ni Lazima Kitokee Kwenye Maisha Yako, Japo Hukipendi.

Tukiangalia historia ya dunia tokea enzi na enzi, tunaona jinsi ambavyo watu wamepitia changamoto mbalimbali.
Tunaona jinsi ambavyo tawala kubwa kama Roma zilivyopigania ukuaji wa utawala wao na hata kufikia kufa kabisa.
Tumeona watu wakitokea kwenye maisha magumu, kujaribu vitu vipya kushindwa lakini kuwa vinganganizi na hatimaye wakafanikiwa.
Kitu kimoja ambacho naweza kukuhakikishia kitatokea kwenye maisha yako ni changamoto au vikwazo.
Haijalishi utapata elimu kiasi gani, haijalishi utakuwa na fedha kiasi gani na haijalishi utakuwana na hadhi kiasi gani. Kila ngazi utakayokuwa unapitia kwenye maisha yako utakutana na changamoto na vikwazo.
Tunaweza kusema changamoto hizi ni njia ya dunia kutupa mitihani ili tuoneshe kama kweli tuko tayari kupata kile tunachotaka.
Katika changamoto yoyote utakayopitia hata iwe kubwa kiasi gani, unaweza kufanya moja kati ya haya mawili;
1. Kukubali changamoto hiyo iwe ndio mwisho wako na kutoendelea na mapambano ya kupata kile ulichotaka.
2. Kutumia changamoto hiyo kukua zaidi na kukupa nguvu na hasira ya kupata kile ulichokuwa unataka.
Uchaguzi ni wako, kama utaamua kukubali kukata tamaa kila la kheri.
Kama utaamua kiendelea na mapambano licha ya changamoto unazokutana nazo weka email yako hapo juu ili uendelee kupata mbinu za kupambana na changamoto hizo.
TUPO PAMOJA.

Mbinu 9 Za Kukuwezesha Kuamka Asubuhi Na Mapema Ukiwa Na Nguvu.

Kuamka asubuhi na mapema ni moja ya siri ya watu wenye mafanikio makubwa. Hii ni kwa sababu asubuhi na mapema akili inakuwa vizuri na hivyo kuweza kufanya majukumu yanayohitaji kutumia vizuri akili yako.

Pamoja na muda huu kuwa mzuri sana kwa kutekeleza majukumu, sio rahisi sana kuamka asubuhi. Watu wengi wamekuwa wakijaribu kuamka asubuhi lakini wanaishia kuzima alamu zao na kurudi kulala.

Leo hapa UTAJIONGEZA na mbinu 9 zitakazokuwezesha kuamka mapema na ukiwa na nguvu.

1. Soma kitabu au jarida dakika 30 kabla ya muda wa kulala.

2. Usile au kunywa pombe mda mfupi kabla ya kulala.

3. Weka simu au kompyuta yako mbali, mwanga wa simu na kompyuta hupunguza usingizi.

4. Usijiwekee majukumu mengi ya kufanya asubuhi. Fanya yale ambayo ni muhimu tu.

5. Panga kupata kifungua kinywa kizuri, hii itakuhamasisha kuamka mapema.

6. Fanya mazoezi, sio lazima yawe magumu.

7. Kunywa maji, itarudisha maji uliyopoteza kwa siku nzima.

8. Weka alarm yako kwenye chumba kingine ambapo utalazimika kuamka ili ukaifuate.

9. Pata jua la kutosha.

Unaweza kupitia mbinu hizi kwenye picha hapo chini.

how-to-wake-up-early

Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.

Kama mwaka huu 2015 umepanga kuanza biashara usifanye kosa moja ambalo huwa linafanywa na wafanyabiashara wengi wanapoanza.
Usianze biashara kama hujui miaka mitano ijayo biashara yako itakuwa imefika wapi.
Ni muhimu sana kuwa na picha kubwa ya biashara yako ili unapoanza usisahau ulipotaka kufika.
Kama utaanza biashara ukiwa hujui miaka mitano utakuwa wapi hutafika popote. Maana biashara itakapoanza kukuchanganya utajikuta ukihangaika na matatizo yanayokusonga na kusahau kukuza biashara yako.
Pata picha ya kule unakokwenda kabla hata ya kuanza safari.

Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Tumejifunza sana kuhusu tabia za mafanikio. Na fikiri utakuwa unajua tabia kadhaa ambazo ukiwa nazo unaweza kufikia mafanikio unayotarajia kwenye maisha yako.

Lakini pamoja na kujua tabia hizo mbona watu wengi bado wanashindwa kufikia mafanikio?

Jibu rahisi ni kwamba wanaendelea kung’ang’ania tabia zile zile ambazo zinawafanya wasipate mafanikio.

SOMA; Huu Ndio Ushauri Muhimu Sana Wa Kuishi Nao Kila Siku Kwenye Maisha Yako.

Tabia hizo ni zipi basi? Zipo nyingi kulingana na makundi mbalimbali ya watu ila hizi saba zipo kwa watu wote ambao hawana mafanikio.

1. Kuahirisha mambo. Watu wote ambao hawajafanikiwa wana tabia ya kuahirisha mambo. Wataweka malengo na mipango mizuri sana ila wanapofika kwenye utekelezaji wanaanza kuahurisha. Wanajishawishi watafanya kesho cha kusikitisha ni kwamba kesho yao huwa haifiki.

2. Kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja. Hii ni tabia nyingine ya watu wasiokuwa na mafanikio, wanataka wafanye kazi, huku wanaangalia tv, wanachat kwenye simu na kuwa kwenye mitandao ya kijamii. Akili moja huwezi kuigawa kwenye mambo yote hayo na bado ikawa na ufanisi mzuri.

SOMA; Kauli Mbili Za Kuacha Kutumia Leo, Maana Zinaashiria Kushindwa.

3. Kukubali kushindwa. Pale wanapokutana na changamoto au kikwazo wanakimbilia kusema wamejaribu ila wameshindwa.

4. Kupenda kuiga. Watu wasiokuwa na mafanikio hawana muda w akukaa na kufanya ubunifu wao wenyewe, wao hupenda kuiga kila kitu na mwishowe kujikuta kwenye wakati mgumu.

5. Hawajui njia bora za kujumuika na wengine. Watu wasiokuwa na mafanikio hawajui jinsi ya kujumuika na watu wenye mafanikio ili wajifunze mengi kutoka kwao.

6. Kufanya chochote ili waambiwe ndio. Watu wasiofanikiwa ni watu ambao wanapenda sana kuwaridhisha watu. Hujaribu kufanya chochote kile ili kuwafurahisha wengine na hivyo huishia kuwa na maisha magumu.

SOMA; Maisha Sio Rahisi Lakini Ni Mazuri Kama Hivi...

7. Kuhukumu. Watu wasiokuwa na mafanikio ni wazuri sana kuhukumu wengine. Hupend akufuatilia maisha ya wengine na kuhukumu kila jambo ambalo wanalifanya.

Epuka tabia hizi saba kama kweli unataka kufikia mafanikio kwenye maisha yako. Kama utaendelea kuzishikilia utajaribu kila mbinu lakini mafanikio hutoyaona.

Mbinu Kumi(10) Za Kuepuka Kuchoka Sana 2015.

Bado tupo kwenye mwanzo wa mwaka, na mwanzo wa mwaka kila mtu anakuwa na nguvu kubwa sana ya kufanya majukumu yake. Huu ni muda ambao kila mtu anakazana kujaribu kutimiza malengo yake.

Kadiri siku zinavyozidi kwenda watu wengi huanza kuchoka na mpaka kuja kufika mwezi wa kumi au kumi na moja asilimia kubwa ya watu wanakuwa wamechoka sana kiasi cha kushindwa kuwa na uzalishaji mzuri.

Hali hii ina madhara sana katika ufanisi wetu wa kazi na hata biashara. Na kama kweli unataka kufikia mafanikio makubwa, unahitaji kuwa kwenye ufanisi mkubwa kwa angalau mwaka mzima au wiki 50 kati ya wiki 52 za mwaka.

Leo hapa UTAJIONGEZA na mbinu 10 za kuepuka kuchoka sana mwaka huu 2015.

1. Upe mwili wako kazi. Kama kazi zako ni za ofisini au za kukaa, kufanya hivyo kila siku kutaufanya mwili wako uwe hovyo sana. Hivyo ni vyema kuupa mwili wako kazi, fanya mazoezi, cheza, tembea, kimbia, na hii ni kila siku.

2.Pata muda wa kutosha wa kulala. Kulingana na kazi zako unaweza ukasema huwezi kupata muda wa kutosha wa kulala, ila kulala kutaufanya mwili wako kuwa na nguvu na hata akili yako kuwa na ubunifu. Anza kulala nusu saa kabla ya muda wako wa kawaida wa kulala. Pia pata muda kidogo wa kulala mchana kama inawezekana kwako.

3. Pata dakika tano za kufanya tajuhudi/taamuli.

Hizi ni dakika chache ambapo unakaa kimya na kuondoa mawazo yote kwenye kichwa chako. Njia rahisi ya kufanya hili ni kukaa sehemu iliyotulia na kufunga macho yako kisha kuanza kuhesabu pumzi zako. Itakusaidia sana kusafisha akili yako.

4. Weka orodha ya vitu unavyoshukuru kuwa navyo. Haijalishi una matatizo kiasi gani kuna vitu unafurahi kuwa navyo, huenda ni familia inayokupenda, huenda ni biashara nzuri. Weka orodha hii na ipitie kila siku.

5. Kuwa na muda maalumu usiku ambapo unazima vifaa vyako vyote, yaani kompyuta, simu, tv na chochote kile. Fanya muda wako wa kupumzika kuwa wa kupumzika kweli.

6. Kuwa na picha inayokupa furaha na kukuhamasisha. Inaweza kuwa picha ya mtoto wako au kitu chochote. Itumie picha hii pale unapoona uvivu wa kufanya jambo.

7. Jisamehe. Kuna makosa mengi umeyafanya kwenye maisha yako, acha kuendelea kujitesa, jisamehe na songa mbele.

8. Kuwa mkarimu, wasaidie wengine, utaona mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yako.

9. Tumia kipaji ulichonacho. Hata kama kazi au biashara unayofanya sio inayohusisha kipaji chako, tenga muda ambao utafanya kipaji chako. Kwa kufanya hivi utakuwa na nguvu na hamasa kubwa utaporudi kwenye kazi yako.

10. Fanya jambo moja kwa wakati. Kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja kutachangia wewe kuchoka haraka sana. Fanya jambo moja likiisha ndio uanze jambo jingine.

Hizi ni mbinu rahisi unazoweza kuanza kuzitumia leo ili kuhakikisha mwaka mzima unakuwa na ufanisi mkubwa sana.

Nakutakia kila la kheri.

Vitu Vitatu Vinavyoathiri Kipato chako Kwenye Chochote Unachofanya.

Katika uchumi tunaoishi, kipato chako kitategemea vitu vitatu;

  1. Nini unafanya. Kama unachofanya ni muhimu sana, basi hata kipato chako kitakuwa kikubwa.
  2. Unakifanya kwa kiwango gani. Kama unafanya kwa viwango vya juu sana basi kipato chako kitakuwa kikubwa. Kama unafanya kawaida basi kipato chako kitakuwa cha kawaida.
  3. Ugumu wa kukubadilisha. Kama ni vigumu kupata mtu mwingine anayefanya kama wewe basi thamani yako itakuwa kubwa na kipato chako kitakuwa kikubwa pia. Kama ni rahisi kupata mwingine, yaani unachofanya kila mtu anaweza kukifanya thamani yako itakuwa ndogo na kipato chako kitakuwa kidogo pia.

Hii ni sahihi kwenye kazi, biashara na hata shughuli yoyote ya kiuchumi unayofanya. Jitahidi uwe bora zaidi na kipato chako kitakuwa kikubwa sana. Haijalishi ni kazi au biashara gani unayofanya, kinachojali ni ubora unaotoa.

Dunia inalipa ubora.

Hii Ndio Hasara Ya Kutokuwa Na Malengo.

Kama huna malengo kwenye maisha yako, mtu mwenye malengo atakuajiri umtimizie malengo yake.
Kama huna ndoto kubwa kwenye maisha yako, mtu mwenye ndoto atakuajiri umkamilishie ndoto yake.
Na kama hujui unaelekea wapi na maisha yako, utajikuta unafuata kundi ambalo pia halijui linaelekea wapi.
Ni wakati sasa wa wewe kuacha kupoteza muda.
Kaa chini leo na uandike malengo yako, kisha weka mipango na anza kufanyia kazi mipango hiyo mara moja.
Kumbuka kauli mbiu ya mwaka huu ni JUST DO IT...
Usipoteze muda, anza sasa.

Maswali 12 Muhimu Ya Kujiuliza Ili Kuweza Kufikia Mafanikio.

Mafanikio ni kitu ambacho kila mtu anakazana kukifikia. Japokuwa kila mmoja wetu ana maana yake ya mafanikio, kila mmoja kuna kitu ambacho anapifana kukipata kwenye maisha yake.

Kitu hiki ambacho kila mmoja wetu anakipigania sio rahisi kupatikana. Ndio maana kuna watu wengi wanahangaika lakini bado wanaishia kukata tamaa.

Leo hapa UTAJIONGEZA na maswali kumi na mbili muhimu ya kujiuliza ili uweze kufikia mafanikio kwenye jambo lolote unalofanya.

Jiulize na kujijibu maswali haya ili uweze kujua unaelekea wapi. Ingekuwa vizuri zaidi kama majibu yako utayaandika kwenye karatasi.

1. Ni kitu gani ninachotaka kwenye maisha?

2. Ni yapo machaguo yangu?

3. Ni dhana gani ambayo unatengeneza?

4. Nina majukumu gani?

5. Ninawezaje kufikiria tofauti na ninavyofikiri sasa?

6. Watu wengine wanafikirije kwa jambo hili ninalofikiri mimi?

7. Ni kitu gani ambacho nimejifunza kutokana na makosa ambayo nimewahi kufanya?

8. Ni kitu kitu gani ninachokosa au ninachokwepa?

9. Ni hatua gani ninazoweza kuchukua ili kuelekea kule ninakotaka?

10. Ni maswali gani muhimu nayotakiwa kuendelea kujiuliza na pia kuuliza wengine?

11. Nawezaje kubadili hali mbaya ninayopitia ili kuwa nzuri na kufaidika nayo?

12. Ni kitu gani kinawezekana?

Jiulize maswali hayo mara kwa mara kila wakati ambapo unakutana na changamoto au kikwazo na hata pale unapoweka malengo mapya.

Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

Mwaka huu nitaongeza kipato changu…

Mwaka huu nitafungua biashara yangu…

Nwaka huu nitaacha ulevi….

Mwaka huu nitaanza kufanya mazoezi…

Ndio tumekusikia na malengo yako ni mazuri sana, lakini je unakumbuka malengo haya haya uliyaweka mwaka jana? Na mwaka mwingine uliopita? Kwa nini hujayafikia mpaka sasa.

Kushindwa kujiuliza maswali haya kunakufanya uendelee kushindwa kufikia malengo yako.

Sababu kubwa ya watu kushindwa kufikia malengo yao inatokana na wao kutojua njia sahihi ya kuweka na kufikia malengo hayo. Leo hapa utajiongeza na sababu kumi kwa nini malengo yako hayatatimia mwaka huu 2015 ili uweze kuziepuka.

1. Unaweka malengo ambayo hayaeleweki.

Kwa mfano lengo “mwaka huu nitaongeza kipato” sasa kama kipato chako kwa mwezi kilikuwa milioni moja mwaka huu unaongeza na kufikia milioni moja na elfu kumi umetimiza malengo yako. Lakini kiuhalisia umeshindwa, unapoweka lengo hakikisha unajua ni kiasi gani unataka kufikia.

2. Huna njia ya kujipima.

Kama umeweka malengo halafu nuna njia ya kujipima kama kweli uko kwenye njia sahihi umejiandaa kushindwa. Kitu chochote ambacho hakiwezi kupimwa hakiwezi kufanyika. Jua ni kiwango gani unataka kufika na kila baada ya muda uweze kujitathmini umefika wapi.

3. Unaweka malengo ambayo hayapo ndani ya uwezo wako.

Japokuwa hakuna kisichowezekana, lakini ni vigumu sana kwako wewe kuweka malengo ya kutengeneza bilioni moja kwa mwaka huu wakati kwa sasa kipato chako ni laki mbili kwa mwezi. Kuweka lengo kama hili kunakukatisha tamaa badala ya kukusukuma kulifikia.

4. Huandiki malengo yako.

Kama unajisemea malengo yako na kuyaacha kichwani, subiri baada ya siku chache utakuwa umesahau kila kitu. Malengo na mipango yako yote ni lazima uiandike vizuri kwenye kitabu au karatasi.

5. Unaishi kwenye mazingira ambayo hayachochei malengo yako.

Kama watu wanaokuzunguka hawaoni umuhimu wa kuweka malengo na kuboresha maisha yao, upo kwenye hatari kubwa ya kushindwa kwenye malengo yao.

6. Unakata tamaa pale unapokutana na changamoto kidogo.

Changamoto ni sehemu ya safari hii ya kufikia mafanikio. Kama kila ukikutana na changamoto kidogo unakata tamaa itakuwa vigumu sana kwako kufikia mafanikio makubwa.

7. Unapoteza muda.

Muda ni muhimu sana kwako wewe kuweza kufikia malengo yako. Kama bado unaendelea kupoteza muda huwezi kufikia malengo yako.

8. Huna mfumo wa kukuwajibisha.

Kwa asili binadamu ni wavivu, kama ukijiwekea malengo yako mwenyewe kwa siri, hata usipoyafikia au kuyavunja unajua hakuna atakayejua au kukuuliza. Tafuta mtu ambaye anaweza kuwa anakufuatilia ili kujua kama unaendelea na malengo yako au la. Wakati mwingine tangaza hadharani, kwa mfano kama unataka kuacha pombe, mwambie kila mtu kwamba naacha kunywa pombe, kwa njia hii utaona aibu kunywa kwa sababu kila mtu anajua umesema unaacha.

9. Unaangalia na kusikiliza wengine wanafanya na kusema nini.

Popote ulipo umezungukwa na watu ambao hawajui maisha yao yanaelekea wapi. Hawana malengo yoyote na hawaoni umuhimu wake. Kama utajilinganisha na watu hawa huwezi klusonga mbele kamwe.

10. Umegoma kubadilika.

Kama unataka kuishi maisha yale yale ambayo umekuwa unaishi kila siku halafu unataka ufikie malengo yako nakushauri uache kujidanganya, hakuna kitu kama hiko. Unahitaji kubadilika wewe kwanza ndio mabadiliko mengine yatokee kwenye maisha yako.

Yafanyie mambo hayo kazi ili uweze kufurahia kufikia malengo yako.

Vipande Kumi Vya Ushauri Bora Kuwahi Kutolewa.

Tunaishi kwenye dunia ambayo kuna njia nyingi sana za kujifunza ili kufikia malengo yetu.

Unaweza kujifunza kwa kufundishwa, yaani kusoma au kukaa darasani au kupata aina yoyote ya mafunzo. Hii ni njia nzuri ya kujifunza.

Pia unaweza kujifunza kwa kushindwa kutokana na makosa yako. Yaani pale unapofanya jambo ukashindwa unajifunza njia ambayo imekufanya ushindwe ni nini na kutokurudia tena. Hii ni njia bora ya kujifunza maana hutosahau.

Njia nyingine unayowez akutumia kujifunza ni kupitia makosa au uzoefu wa watu wengine. Hapa unasoma au kuangalia kile ambacho watu waliofanikiwa wamefanya au hawafanyi na wewe kufanya kama wao. Hii ni njia bora sana ya kujifunza kwa sababu inakupunguzia muda ambao ungepoteza kwa kusubiri ujifunze kwa makosa yako mwenyewe.

Leo hapa utajiongeza kwa vipande kumi vya ushauri bora kuwahi kutolewa. Uchukue kama ulivyo na ufanyie kazi.

1. Haijalishi kama utatumia masaa 1000 kufanya kitu, kama unafanya kwa kukosea ulichojifunza ni jinsi ya kufanya kitu kwa kukosea.

2. Kama utamlaumu mtu mwingine usitegemee mabadiliko yoyote.

3. Usibishane na mjinga, atakayekuwa anaangalia kwa pembeni hatojua tofauti yenu.

4. Acha kuchukulia kila kitu binafsi, hakuna anayekufikiria wewe zaidi ya unavyojifikiria mwenyewe.

5. Kama unataka kukumbuka kitu kiandike mahali.

6. Fanya chochote unachofanya kama wewe ndio mtaalamu uliobobea, kila mtu atakuacha uendelee na kile unachofanya.

7. Jua ni kitu gani unachopenda kufanya, halafu fikiria ni jinsi gani mtu anaweza kukulipa kwa wewe kufanya kitu hiko.

8. Kama umekosea kubali kosa, kama uko sahihi kaa kimya.

9. Nunua kile ambacho utakitumia.

10. Mara zote kuwa na mpango, na mipango mingi itashindwa.

Hivyo ndio vipande kumi vya ushauri bora kuwahi kutolewa. Chukua ushauri huo na ufanyie kazi.

Hatua Tatu Za Kujua Kama Wazo Lako La Biashara Zuri.

Linapokuja swala la kufanya biashara watu wengi hupenda kutafuta ji wazo gani la biashara ni bora na linaweza kuwapatia faida.
Ukweli ni kwamba wazo moja la biashara haliwezi kuwa bora kwa watu wote. Wazo linaweza kuwa bora kwangu ila kwako likawa sio zuri au lisiweze kukuletea mafanikio.
Wazo bora la biashara linategemea na mtu anayetaka kufanya biashara yako.
Watanzania tumekuwa hatupendi kuumiza akili kutengeneza mawazo yetu ya biashara na hivyo kukimbilia kuiga, kitu ambacho kinatuumiza sana baadae.
Sasa leo hapa utajiongeza na hatua tatu za kutengeneza wazo lako la biashara ambalo litakuletea faida kubwa.
Wazo bora la biashara lina sifa hizi tatu;
1. Kitu unachopenda.
Hatua ya kwanza kabisa ya wazo bora la biashara ni kitu ambacho unapenda kufanya. Kama unapenda kitu unakuwa na shauku nacho na kupenda kukifuatilia zaidi.
2. Kitu ambacho upo tayari kukifanya.
Kupenda tu kitu hakutoshi, je upo tayari kukifanya? Je upo tayari kufanya kazi na kumwagika jasho? Je upo tayari kuvumilia hata pale mambo yatapokuwa magumu?
3. Kuleta thamani kwa wengine.
Sifa ya tatu ya wazo zuri la biashara ni kuwa thamani kwa wengine. Je watu wapo tayari kulipia bidhaa au huduma itakayotokana na wazo lako la biashara? Kama haliwezi kutengeneza thamani huna biashara.
Tumia njia hizi tatu kutengeneza wazo lako la biashara ambalo litakufikisha kwenye mafanikio.
Usiige tena, tumia akili yako, angalia mazingira yanayokuzunguka.

Njia Kumu(10) Za Kupata Utajiri Na Mafanikio.

Fedha ni muhimu na kila mmoja wetu anakazana kila siku ili kupata fedha za kumtosha kuendesha maisha yake. Na pia tunakazana kupata fedha zaidi ili angalau kuwa na uhakika wa chochote kitakachotokea mbeleni.

Hivyo kujua njia za kupata fedha na hata kuwa tajiri ni muhimu ili usijikute ukihangaika sana na mwishowe kushindwa kupata unachotaka.

Katika kitabu cha RICH HABITS, The daily success habits of wealthy individuals, mwandishi Tom Corley amechambua tabia ambazo ameziona kwa watu matajiri na hata masikini katika utafiti aliofanya.

Zifuatazo ni tabia ambazo watu wenye mafanikio wanazo;

1. Kuweka malengo.

Watu wenye mafanikio wanaongozwa kwa malengo na mipango, watu hawa wana malengo ya muda mfupi na ya muda mrefu na kila siku wanafanyia kazi malengo yao.

2. Kujifunza kila siku.

Watu waliofanikiwa wana tabia ya kujifunza kila siku. Huangalia njia za kuongeza maarifa yao, hujisomea na kuhudhuria semina mbalimbali zinazowafanya kuwa bora zaidi.

3. Kujali afya.

Watu waliofanikiwa wanajali sana afya zao. Wanakula vizuri na kufanya mazoezi mara kwa mara. Pia huepuka vyakula ambavyo sio vizuri kwa afya.

4. Kuweka mbele vitendo.

Watu wenye mafanikio ni watu wa kujali vitendo zaidi kuliko maneno. Ni watu ambao wakishasema wanafanya jambo fulani basi wanalifanya mara moja na sio kuvuta muda mpaka kusahau wanachotaka kufanya.

5. Wana mtizamo chanya muda wote.

Watu wenye mafanikio ni watu ambao wana mtizamo chanya juu yao binafsi na hata kuhusu maisha. Wanaamini wanaweza kufanya kile wanachotaka kufanya na hii huwafanya wafanikiwe zaidi.

6. Kuweka akiba.

Watu wenye mafanikio ni watu ambao huwa wanaweka akiba katika kila kipato wanachopata. Watu hawa huweka akiba kwanza na ndio kufanya matumizi. Wanaweka akiba asilimia 10 mpaka 20 ya kipato chao.

7. Kudhibiti matumizi.

Watu wenye mafanikio huishi chini ya kipato chao. Ni watu ambao hudhibiti matumizi na kuweza kuishi chini ya kipato wanachopata, wakitaka kuongeza matumizi wanaongeza kwanza kipato. Kwa njia hii wanaepuka kuingia kwenye madeni.

8. Kutokupoteza muda.

Watu wenye mafanikio wanaepuka sana kupoteza muda bila ya kufanya jambo la msingi. Watu wengi wenye mafanikio wanaangalia tv sio zaidi ya saa moja kwa siku.

9. Kufanya zaidi ya wanavyotegemewa.

Watu wenye mafanikio hufanya zaidi ya wanavyotegemewa kufanya. Kama wanategemewa kutoa huduma kwa kiwango fulani wao hupitiliza na kuwafanya kuwa wa thamani sana.

10. Kutokata tamaa.

Watu wenye mafanikio wameshindwa mara nyingi sana ila hawakukata tamaa. Wamekuwa na uvumilivu na pia ni vinganganizi mpaka wameweza kufikia mafanikio makubwa.

Je wewe unataka kufikia utajiri na mafanikio? Njia ndio hiyo hapo, kazi ni kwako sasa.

Nakutakia kila la kheri.

Maazimio Matano Muhimu Ya Fedha Kwa Kila Kijana Kuweka Mwaka Huu 2015.

Bado tupo kwenye msimu wa mwaka mpya na huu ni wakati muhimu wa kuweka maazimio na malengo mbalimbali ili kuboresha maisha yetu zaidi.

Huenda tayari umeshaweka malengo na mipango yako ya mwaka 2015, leo tutakumbushana mambo machache ambayo ni ya muhimu sana kuyajumuisha kwenye malengo yako ya mwaka huu 2015.

Kama bado hujaweka malengo mpaka leo bado hujachelewa, unaweza kukaa chini leo na kuandika malengo yako kwenye karatasi na kuanza kuyafanyia kazi.

Kama huna mpango wa kuweka malengo kabisa kwa mwaka huu pole…

100_7560 ED1

Yafuatayo ni maazimio muhimu kuweka kwenye malengo yako ya kifedha kwa mwaka huu 2015;

1. Weka akiba zaidi ya ulivyoweka mwaka jana.

Kama mwaka jana ilikuwa unaweka akiba, mwaka huu ongeza kiwango cha akiba unachoweka. Kama huna utaratibu wakujiwekea akiba kabisa anza na kuweka pembeni asilimia 10 ya kile unachopata. Ukipata elfu kumi, weka elfu moja pembeni. Ukipata laki moja weka elfu kumi pembeni. Baada ya muda mfupi utaona mabadiliko makubwa ya kifedha kwenye maisha yako.

2. Punguza madeni yako.

Madeni ni mzigo, madeni ni utumwa, mtu anayekudai anaweza kunyanyasa utu wako muda wowote. Mwaka huu weka azimio la kupunguza madeni yako na kama ikiwezekana lipa yote kabisa. Kaa chini na wale wanaokudai na wape pendekezo la njia rahisi kwako kuwalipa kisha anza kuwalipa. Utanunua uhuru wako ulioupoteza.

3. Tengeneza, badilisha bajeti yako.

Ni muhimu sana kuishi kwa bajeti, kama mpaka sasa huna bajeti tafadhali sana tengeneza bajeti yako leo. Amua ni kiasi gani utakachoishi nacho kwa siku, wiki na hatimaye mwezi. Na jitahidi sanakuishi kwa kiasi hiko, usinunue vitu kwa tamaa tu, nunu kile ulichopanga kwenye bajeti. Kama umepanga mwezi huu hununui nguo, usishawishike kununua nguo hata ukikutana nayo nzuri kiasi gani, nguo nzuri huwa haziishi. Siku ambayo bajeti yako inaruhusu utapata nzuri kuliko uliyokutana nayo.

4. Jifunze kuhusu uwekezaji.

Bila shaka uwekezaji ni somo gumu sana kwa vijana. Wengi hawapendi kusikia kitu hiki na huona ni kitu kinachohitaji elimu kubwa. Ukweli ni kwamba uwekezaji ni rahisi na ni njia rahisi kwako kukuza kipato chako. Kuna aina nyingi za uwekezaji, kuna uwekezaji wa kununua mali, uwekezaji wa fedha na kadhalika. Unaweza kuanza kujifunza hapa hapa kwa kubonyeza maandishi haya

Soma; Hivi ndivyo unavyoweza kutajirika kwa kuanza na shilingi elfu moja.

5. Jijengee nidhamu ya fedha.

Kama hutakuwa na nidhamu ya fedha, yote tuliyojadili hapo juu hayataweza kukusaidia. Mara zote tumia pungufu ya unachokipata, yaani matumizi yako yasizidi mapato yako. Na pia kwenye kuweka akiba weka akiba na inayobaki ndio ufanye matumizi. Ukifanya matumizi ili inayobaki ndio uweke akiba hutabakiwa na kitu.

Wewe kama kijana ni muhimu sana kwako kujijengea misingi imara ya kifedha na kiuchumi. Weka maazimio hayo matano muhimu mwaka huu 2015 na anza kuyafanyia kazi.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

kitabu-kava-tangazo4322

Mambo Kumi(10) Kuhusu Maisha Tunayoweza Kujifunza Kutoka Kwa Miti.

Miti niviumbe hai kama sisi, na ili kuendeleakuwa hai kuna mbinu mbalimbali ambazo viumbe hawa hutumia. Leo tutajiongeza na mambo kumi kuhusu maisha ambayo tunaweza kujifunza kwa kuangalia maisha ya miti.

1. Miti haijiwekei kikomo cha kukua, inakua mpaka mwisho wa uwezo wao.

Tofauti na mwanadamu ambaye anaweza kujiwekea kikomo cha mafanikio kwenye maisha yake, miti hukua biala ya kuchoka. Haijalishi hali ni mbaya kiasi gani miti huendelea kukua.

Ni muhimu kuendelea kukua kila siku.

2. Mapambano yao ya kuishi yanaifanya miti kuwa bora zaidi.

wakati baadhi ya watu wakikutana na matatizo wanazidi kuwa wadhaifu na wengine hata kukatisha maisha yao, miti inapokutana na matatizo ndio inazidi kuwa imara zaidi. Miti inapopata upepo ambao unatishiakuingoa kupeleka mizizi mbali zaidi ardhini. Inapokosa maji hupeleka mizizi mbali zaidi na hii yote huifanya kuwa imara.

3. Miti inachukua kile inachohitaji ili kuishi.

Miti inazungukwa na madini mbalimbali, lakinihuamua kuchukua madini yale inayohitaji kwa ukuaji wake tu. Ni muhimu kwetu kuwa wachaguzi wa vile ambavyo ni muhimu kwa maisha yetu.

4. Miti hufuata mwanga.

Bila ya kujali ni matatizo kiasi gani ambayo miti inapitia, mara zote huelekea upande wa mwanga. Mti unaweza kuwa umezungukwa na magugu, unawezakuwa unaliwa na wanyama wengine lakini hii haizuii yenyewe kuendelea kufuata mwanga ili kukua.

Ni muhimu kuangalia upande wa ukuaji hata kama upo kwenye matatizo.

5.Miti imejifunza kubadilika kutokana na mazingira.

Unapofika wakati wa kiangazi ambapo maji ni shida, miti hupunguza majani ili kupunguza maji yanayopotea kupitia majani hayo. Kiangazi kinapoisha na maji kuwa ya kutosha, hutoa tena majani.

Jifunze kubadilika kutokana na hali ya maisha.

6. Inatengeneza thamani kwa viumbe wengine.

Miti inatengeneza thamani kubwa sana kwenye maisha ya viumbe wengine. Miti inatoa hewa ya oksijeni ambayo ni muhimu sana kwa maisha ya viumbe hai wote, inatoa chakula, inatoa kivuli na mengine mengi.

Hakikisha maisha yako yanakuwa na thamani kwa  watu wengine.

7. Miti inaishi maisha yao wenyewe.

Mti hata ukiwa wenyewe unaendelea na maisha, na hata unapokuta kundi la miti, kila mti unakuwa na maisha yake wenyewe. Miti haiigani au kutaka kujionesha kwa wengine.

Ishi maisha yako, usiige ya wengine na wala usifanye mambo ili kuonekana.

8. Miti inatoa zaidi ya inavyopokea.

Miti inapokea maji, madini, na mwanga wa jua. Lakini inatoa chakula, hewa ya oksijeni, inaondoahewa ya kabondayoksaidi, inatoa kivuli, inatoa malazi na hata ikifa inatoa rutuba.

Mara zote penda kutoa zaidi ya unavyopokea, utapata mafanikio makubwa.

9. Miti ni vinganganizi.

Ili kuendelea kuwa hai miti ni vinganganizi na haikati tamaa. unaweza kukata mti leo na baada ya siku chache ukaota tena. Inajua kwamba maisha ni magumu na hivyo imejiandaa kushinda kwambinu zote.

Kuwa kinganganizi ili uweze kufikia malengo yako.

10. Miti imejijengea ulinzi wao wenyewe.

Kwa kuwa maisha ni magumu miti nayo imejifunza kuwa migumu. Ili isiliwe na viumbe wengine baadhi ya miti imejijengea vitu vya kuzuia isiliwe. Ili isipoteze maji mengi miti inayoota jangwani ina majani madogo sana ambayo pia ni miiba. Hii inaisaidia kuweza kuishi na pia kupunguza maji yanayopotea na kuepuka kuliwa na viumbe wengine.

Jipange najiwekee ulinzi kwa kuwa kuna watu wengi sana wanaokurudisha nyuma.

Tumia masomo hayo kumi kuboresha maisha yako.

Kumbuka kujifunza kila siku ni hitaji muhimu la wewe kufikia mafanikio.

Tabia Mbaya KUMI(10) Zinazopunguza Ufanisi Wako.

Huenda unatamani kufanya zaidi ya unavyofanya sasa lakini kila ukijitahidi huoni mabadiliko. Huenda una ufanisi mdogo kiasi kwamba kila mtu anakuona wewe ni mvivu sana.

Sio kweli kwamba wewe ni mvivu bali kuna tabia ambazo zinakufanya ushindwe kutekeleza majukumu yako kwa wakati.

Leo utajiongeza na tabia kumi mbaya ambazo zinakufanya uwe na uzalishaji mdogo na ukiweza kuziepuka utaongeza uzalishaji wako.

1. Unzanza siku yako bila ya kuipangilia. Usipopangilia siku yako utafanya nini utajikuta unafanya chochote kinachotokea mbele yako.

2. Unaangalia facebook au email kila baada ya dakika kumi. Kama mawasiliano yako yanakufanya uwe na shauku kubwa ya kutaka kujua ni nini kinaendelea kwenye mitandao ya kijamii itakuwa vigumu sana kwako kukamilisha majukumu yako kwa wakati.

3. Unasubiri muda muafaka ndio ufanye ulichopanga kufanya. Kuna wakati unafikiri kama kitu fulani kikitokea basi nitafanya kitu fulani, mwishowe unaishia kutokufanya kabisa.

4. Unajaribu kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja. Mwishowe unaishaia kushindwa kumaliza hata moja, kama mtu anayekimbiza sungura wawili, hakamati hata mmoja.

5. Unagoma kujifunza vitu vipya. Dunia ya sasa karibu kila kazi imerahisishwa sana. Kuna utaalamu mwingi ambao unaweza kuutumia kurahisisha kazi yako, ila unapogoma kujifunza unabaki nyuma.

6. Unasubiri mpaka dakika ya mwisho ndio ufanye jambo. Unapokuwa na muda wa kufanya jambo mara nyingi huwa unaona ni mwingi, ni mpaka muda unapokaribia kuisha unaona kwamba ulipoteza muda mwingi.

7. Unalaumu vifaa unavyofanyia kazi. Labda unasema kompyuta unayotumia ipo taratibu sana, mashine unayotumia inakurudisha nyuma. Hizi zote ni sababu ambazo hazina msingi.

8. Huna muda maalumu wa kula. Kama huna muda maalumu wa kula au wakati mwingine unaacha kula itakuwa vigumu sana kwako kuweza kuwa na nguvu ya kutekeleza majukumu yako.

9. Unatumia muda mwingi sana kupanga. Inawezekana unapanga, halafu unakaa unafikiria mipango yako, baadae unapanga tena. Kwa kupanga huwezi kutimiza chochote, unatakiwa kufanya kazi.

10. Huapati usingizi wa kutosha. Kama kila siku unachelewa kulala na kuamka umechoka ni vigumu sana kuweza kutekeleza majukumu yako.

Epuka tabia hizo kumi mwaka huu 2015 ili uweze kuongeza ufanisi wako.

Hatua Nne Muhimu Unazohitaji Kupitia Ili kufikia Mafanikio Makubwa 2015.

Mwaka umeanza na mwaka unakaribia kukomaa. Kila mwanzo wa mwaka watu wengi huweka malengo mablimbali ya kufanya kwenye mwaka husika. Huenda na wewe umeweka malengo mengi kama ambavyo umekuwa ukifanya miaka iliyopita.

Lakini pia watu wengi wanaoweka malengo huwa hawayafanyii kazi hata kidogo. Zaidi ya asilimia 85 ya watu wanaoweka malengo husahau malengo yao wiki sita baada ya mwaka mpya.

Ili na wewe usiwe mmoja wa watu ambao wanasahau malengo yao au wanashindwa kuyafikia kuna hatua nne muhimu za kufuata ili kuhakikisha unafikia mafanikio makubwa kwenyemaisha yako.

Hatua hizo nne ni kama ifuatavyo.

1. Amua ni nini unataka kwenye maisha yako.

Ni lazima uamue ni kitu gani hasa unataka kwenye maisha yako. Jua kwa usahihi na kwa uhakika na uweze kusema kwa sentensi fupi ni nini unataka kwenye maisha yako.

2. Amua ni gharama gani upo tayari kulipa.

Kama ulikuwa hujui ni kwamba HAKUNA KITU CHA BURE, yaani huwezi kupata kitu pasi na kutoa kitu. Hivyo ili uweze kupata kile unachotaka kwenye maisha lazima uwe tayari kulipa gharama. Inaweza kuwa unahitaji kufanya kazi zaidi, au gharama nyingine yoyote.

3. Weka vipaumbele vyako.

Baada ya kuamua unataka nini, na baada ya kujua ni gharama gani upo tayari kulipa, weka vipaumbele vyako. Amua ni vitu gani utafanya na vingine vyote sema hapana. Jifunze kusema hapana itakusaidia sana kwenye maisha yako.

Soma; Mambo 30 ya kusema hapana mwaka 2015.

4. Fanya kazi.

Yote hayo tuliyojadili hapo juu yanachangia asilimia 1 ya mafaniko. Asilimia 99 ya mafanikio yako itatokana na kazi. Ni lazima ufanye kazi sana, hakuna longolongo hakuna janja janja.

Soma; Misingi mitatu ya kujijengea mwaka 2015.

Fuata hatua hizo nne na anza haraka kufanyia kazi malengo yako. Nina hakika utaweza kufikia mafanikio makubwa. Ila kumbuka kwamba itakuchukua muda, maana mafanikio sio kitu cha kutokea papo kwa hapo.

Nakutakia kila la kheri,

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz