Matatizo Yote Kwenye Maisha Yako Yanatokana Na Kitu Hiki.

Kila mmoja wetu anapitia matatizo au changamoto mbalimbali kwenye maisha yake. Inawezekana unapitia matatizo ya kuumwa, au mwingine anapitia changamoto ya madeni na pia inawezekana unapitia changamoto ya migogoro kwenye familia.
Sasa matatizo yote haya huwa yanaanza na kitu kimoja.
Kabla sijakuambia kitu hiko naomba nikuoe mfano mmoja mzuri sana.
Ukitaka kumuua chura kwa maji ya moto huwezi kumuua kwa kumweka kwenye maji ya moto. Chura ni mnyama ambaye anavyopata joto kali anakuwa na nguvu ya kuweza kuchukua hatua haraka. Hivyo ukimweka kwenye maji ya moto ataruka haraka sana kuondoka kwenye maji hayo.
Sasa hapa kuna njia rahisi ya kumuua chura kwa maji ya moto. Unachukua maji ya baridi kabisa, tena yenye barafu halafu unamweka chura. Kwenye baridi chura hana nguvu ya kuondoka. Baada ya hapo unaanza kupasha maji yale taratibu, kadiri maji yanapata joto chura anakuwa anafurahia, anaona utamu. Akija kustuka maji yanakaribia kuchemka na mwili mzima umesaishiwa nguvu.
Hivi ndivyo matatizo uliyonayo yalivyoanza;
Hukujikuta siku moja unaumwa tu, bali zilianza dalili ndogo ndogo ukazipuuzia.
Hukujikuta kwenye madeni tu, bali ulianza uzembe mdogo mdogo kwenye fedha na ukapuuzia,
Hukujikuta kwenye mgogoro mkubwa wa kifamilia kwa mara moja tu, bali vilianza vitu vidogo vidogo ukavipuuzia.
Hatimaye mambo yamekuwa mambo na sasa upo katikati ya matatizo.
Kupuuzia dalili ndogo ndogo ambazo zingeweza kushughulikiwa ndio kunakufikisha kwenye matatizo makubwa.
Kama waswahili wanavyosema; usipoziba ufa....

Mambo Kumi Muhimu Kuhusu Maisha

1.Tupo hapa kujifunza, dunia ndio mwalimu wetu.

2. Ulimwengu hauna upendeleo.

3. Maisha yako ni matokeo ya imani yako.

4. Pale utakapoanza kutegemea zaidi vitu, watu au fedha unaharibu kila kitu.

5. Kila unachokiwekea mkazo kwenye maisha yako kinakua.

6. Fuata moyo wako.

7. Mungu hatoshuka kutoka mawinguni na kukuambia “sasa hivi una ruhusa ya kufanikiwa”

8. Unapopigana na maisha maisha siku zote yanashinda.

9. Unawapendaje watu? Kwa kuwakubali.

10. Mpango wetu hapa duniani sio kuibadili dunia bali kujibadili sisi wenyewe.

NENO LA LEO; Njia Isiyokuwa Na Foleni.

There are no traffic jams along the extra mile. –Roger Staubach

Hakuna foleni unapokwenda mbali zaidi.

Unapofanya kile ambacho kila mtu anafanya utakutana na ushindani mkubwa sana.

Unapofanya kitu chenye ubora mkubwa na wa kipekee utakuwa mwenyewe na hakutakuwa na ushindani.

Mara zote nenda maili ya ziada, fanya zaidi ya wengine na utapata zaidi.

Nakutakia siku njema.

Kitu Hiki Kimoja Kitakufanya Uweze Kujiajiri, Uishie Kuwa Mwajiriwa Au Uishie Jela.

Habari za jumatatu rafiki?
Tunaelekea kabisa ukingoni mwa mwaka 2014.
Najua unefanikiwa mengi, umepata changamoto kwenye machache na umejifujza mengi pia.
Najua pia unajiandaa vyema kwa mwaka 2015
Leo nataka tukumbusane kitu muhimu sana ambacho ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuzingatia.
Kitu hiko ni NIDHAMU...
Unapoweza kuwa na nidhamu ya kujisimamia wewe mwenyewe yaani jidhamu binafsi unaweza kujiajiri, kuwa mjasiriamali au kufanya biashara.
Unaposhindwa kuwa na nidhamu ya kujisimamia mwenyewe utahitaji mtu wa kukusimamia na hivyo utapata mtu wa kukuajiri na utakuwa muajiriwa, ukijaribu biashara itakushinda.
Unapokosa Nidhamu kabisa, yaani huna nidhamu kabisa unaishia kukaa jela.
Fanya maamuzi mazuri mwaka 2015, jijengee nidhamu binafsi.
Kama hujui uanzie wapi ili kujijengea nidhamu binafsi jiunge na KISIMA CHA MAARIFA, tumejadili hatua kwa hatua jinsi ya kujijengea tabia hii.
Tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz na ujiunge.
Nakutakia kila la kheri.
TUPO PAMOJA.

NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachohitaji Ili Kufanikiwa.

In order to succeed, your desire for success should be greater than your fear of failure. –Bill Cosby

Ili kufanikiwa, hamu yako ya mafanikio inabidi iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.

Kinachokufanya mpaka sasa hujafanikiwa ni hofu ya kushindwa. Una hofu kwamba ukijaribu kitu fulani unachokifikiria utashindwa.

Ili ufanikiwe inabidi uweze kuishinda hofu hiyo na utaweza kuishinda kama kiu yako ya kufanikiwa ni kubwa kuliko hofu ulizo nazo.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Hapa Ndio Pa Kuanzia, Hasa kwa mwaka 2015…

The way to get started is to quit talking and begin doing. –Walt Disney

Njia ya wewe kuanza ni kuacha kuongea na kuanza kufanya.

Ni rahisi sana kuongea, kila mtu anaweza kuongea..

Ni rahisi sana kupanga, kila mtu anapenda kupanga na kupanga tena baada ya kupanga.

Lakini kuongea na kupanga hakutofanya lolote, hakutokufikisha popote.

Kufanya ndio kutakutoa hapo ulipo, vitendo na sio maneno au mipango.

Acha kupanga na kuongea kila siku, 2015, maneno kidogo vitendo vingi..

Nakutakia siku njema.

Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.

Adui yako ni wewe mwenyewe na anaanza na hofu zako...
Una hofu ngapi leo asubuhi?
Una hofu kama utakula leo mchana na jioni?
Una hofu kama mshahara utaingia kabla ya krismas?
Una hofu kama krismasi yako itakuwa nzuri?
Una hofu kama baraza la mawaziri litabadilishwa au halitabadilishwa?
Una hofu kama serikali itafanya maisha kuwa rahisi zaidi?
Una hofu kama 2015 chama unachokipenda kitashika madaraka?
Una hofu kama mpenzi/mwenza wako atakusaliti/atakuacha?
Una hofu kama hofu zako zitaosha??
Karibu hofu zote hapo juu hazina msaada mkubwa kwako au huwezi kuziathiri. Na kuendelea kuziendekeza ndio zinakuzuia ushindwe kufikiria mambo makubwa yatakayokuwezesha kufikia mafanikio makubwa.
Yaani kichwa kimoja chenye hofu zote hizo kitapata wapi nafasi ya kuweka jambo la muhimu?
Hofu hizi ndio adui mkubwa wa mafanikio kwako...
Usizipeleke hofu hizi 2015....

Hiki Ni Kitu Unachotakiwa Kufanya Kila Siku...

Linapokuja swala la kuhamasika/kuhamasishwa sio kitu kinachotokea mara moja halafu ghafla unakuwa mtu uliyehamasika.
Hiki ni kitu ambacho kinatakiwa kutokea kila siku ya maisha yako.
Usifikiri unasoma kitabu kimoja unapata maarifa yote unayohitaji, unatakiwa kujifunza kila siku kila siku, yaani namaanisha KILA SIKU, kama jinsi ambavyo UNAOGA KILA SIKU na kama ambavyo UNAKULA KILA SIKU.
Ndio maana mambo haya sio rahisi, yanahitaji kujitoa, yanahitaji kujikana?
Je upo tayari?
Upo tayari kufanya mabadiliko kwenye maisha yako mwaka 2015?
Kama upo tayari niambie NDIO kwenye maoni hapo chini, halafu tuma email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz ukisema upo tayari halafu nitakupa mpango mzima.
Pia tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com ili kujifunza kitu kipya kila siku.
Karibu sana, TUPO PAMOJA.

Vyakula Vitano Ambavyo Vinaimarisha Afya Yako.

Sehemu kubwa ya magonjwa yanayotusumbua zama hizi yanatokana na mfumo wetu wa maisha. Magonjwa kama kisukari, presha ya kupanda na hata kansa yanatokana na mfumo wa maisha tunayoishi.

Vyakula tunavyokula, vitu tunavyokunywa na mtindo wa maisha tunaoendesha vimekuwa chanzo kikubwa cha magonjwa haya yanayosumbua watu wengi kwa sasa.

Ili kujikinga na magonjwa haya, kuna baadhi ya vitu unavyohitaji kubadili kwenye maisha yako. Leo tutajadili vyakula vitano ambavyo ukijenga tabia ya kuvitumia utajikinga na maginjwa mengi sana. Uzuri wa vyakula hivi ni kwamba vinapatikana kwa urahisi na havina gharama kubwa.

1. Nafaka ambazo hazijakobolewa.

Utumiaji wa nafaka ambazo hazijakobolewa unapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo. Pia nafaka hizi zinaondoa sumu kwenye mwili.

nafaka

2. Bisi(Popcorn).

Huenda umekuwa ukiziona bisi na kufikiri ni chakula cha watoto. Bisi zina virutubisho vinavyoitwa polyphenols ambavyo vinapambana na seli zinazosababisha kansa.

popcorn

3. Mayai.

Mayai yana virutubisho vinavyoitwa lutein ambavyo vinaondoa sumu mwilini. Virutubisho hivi vinaweza kuyalinda macho yako na upofu.

mayai

4. Maharage.

Maharage yana virutubisho vingi ambavyo vinaondoa sumu mwilini.

maharage

5. Sukari asili.

Vyakula vyenye sukari asili kama asali na sukari guru vina virutubisho vinavyoondoa sumu kwenye mwili.

asali

Fanya mabadiliko katika vyakula unavyokula ili uweze kuimarisha afya yako.

Kwa ushauri zaidi wa kiafya andika email kwenda afya@kisimachamaarifa.co.tz

NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachokiishi

Too many of us are not living our dreams because we are living our fears. –Les Brown

Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.

Acha sasa kuzuiwa na hofu na anza kuishi maisha ya ndoto zako. Hakuna kinachoshindikana kama kweli utakuwa umedhamiria.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Huwezi Kuanguka Kama Hutafanya Hivi.

You can’t fall if you don’t climb. But there’s no joy in living your whole life on the ground. –Unknown

Huwezi kuanguka kama hutopanda. Lakini hakuna furaha kwenye maisha kama utaishi maisha yako yote ukiwa chini.

Anza sasa kupanda na kuwa bora zaidi, ndio unaweza kuanguka ila utajifunza mengi na utaweza kufikia juu zaidi.

Ukiendelea kuogopa kuanguka, utaendelea kubaki hapo ulipo.

Nakutakia siku njema.

Vitu Vitamu Muhimu Unavyohitaji Ili Kuingia Kwenye Biashara.

Ili kuingia kwenye biashara zama hizi unahitaji vitu vitatu tu;
i. Kidadavuzi mpakato(laptop)
ii. Simu ya mkononi yenye uwezo mkubwa(smartphone)
iii. Wazo.
Na wazo sio lazima liwe kubwa sana, linaweza kuwa wazo la kawaida sana ambalo wengine wanalipuuza.
Kama una vitu hivyo vitatu na hujui uanzie wapi niandikie kwenye makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Angalizo; uwe tayari kufanya kazi, sio lelemama...

NENO LA LEO; Hiki Ndio Chanzo Cha Furaha.

Happiness is not something readymade. It comes from your own actions. –Dalai Lama

Furaha sio kitu ambacho kimetengenezwa tayari. Furaha inatokana na matendo yako mwenyewe.

Kama utakuwa na matendo yenye maana kwako na kwa wanaokuzunguka ni lazima yatakuletea furaha. Furaha hupewi na mtu mwingine.

Soma; HII NI HAKI YAKO YA KUZALIWA, USITEGEMEE KUPEWA NA WENGINE.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Mlango Mpya Wa Furaha

When one door of happiness closes, another opens, but often we look so long at the closed door that we do not see the one that has been opened for us. –Helen Keller

Mlango mmoja wa furaha unapojifunza, mlango mwingine unafunguka, lakini tunaishia kuangalia mlango uliojifunza kwa muda mrefu na hivyo kushindwa kuona mlango mpya uliofunguka.

Acha kuangalia matatizo yako tuu, angalia pembeni na utaona fursa nyingi za kubadili na kuboresha maisha yako.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Ni Mara Ngapi Unahitaji Kusimama Tena?

Fall seven times and stand up eight. –Japanese Proverb

Anguka mara saba, nyanyuka mara ya nane.

Haijalishi ni mara ngapi umeshindwa, cha msingi ni kuendelea tena.

Kukata tamaa ni mwiko kama kweli unataka kuyafikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Jambo Kubwa Na La Kushangaza.

We can easily forgive a child who is afraid of the dark; the real tragedy of life is when men are afraid of the light. –Plato

Tunaweza kumsamehe mtoto mdogo anayeogopa giza; ila jambo kubwa na la kushangaza kwenye maisha ni pale mtu mzima anapoogopa mwanga.

Ni kipi unachokiogopa kukifanya kwenye mwanga? Maana hiko ndio kinachokuzuia wewe kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Hapa Ndio Unapoweza Kuanzia Na Hiki Ndio Unachoweza Kufanya.

Start where you are. Use what you have. Do what you can. –Arthur Ashe

Anzia hapo ulipo. Tumia hiko ulicho nacho. Fanya unachoweza.

Usipoteze tena muda kufikiri ni wapi pa kuanzia, uanze na nini au ufanye nini. Unachohitaji ni kuanza kupiga hatua na mambo mengine yote yatakwenda vizuri.

Nakutakia siku njema.

KARIBU KWENYE MTANDAO WA AFYA IMARA

AFYA IMARA ni mtandao unaokupatia makala zinazohusiana na afya.
Kupitia mtandao huu utajifunza mbinu mbalimbali za kulinda na kuboresha afya yako.
Kama wote tunavyojua afya ni kiungo muhimu sana kwenye maisha yetu.
Bila kuwa na AFYA IMARA hatuwezi kufikia mipango na malengo tuliyojiwekea kwenye maisha yetu.
Tembelea mtandao huu kila siku ili uweze kujifunza kuhusu afya yako.

MAMBO UTAKAYOJIFUNZA KUPITIA AFYA IMARA.

Kupitia afya imara utajifunza mambo yafuatayo kuhusu afya;
1. Dalili za magonjwa mbalimbali.
2. Jinsi ya kujikinga na magonjwa.
3. Mazoezi na afya.
4. Lishe kwa makundi mbalimbali ya watu.
5. Afya kwa makundi mbalimbali kama watoto, wanawake na wazee.
MASWALI NA USHAURI ZAIDI.
Kama una tatizo la kiafya ambalo ungependa kupata ushauri zaidi unaweza kuandika na ukapewa ushauri wa kitaalamu. Andika email kwenda afya@kisimachamaarifa.co.tz
Tujenge AFYA IMARA ili tuweze kuwa na maisha bora.

Maswali matatu muhimu ya kujiuliza leo ili kujua muelekeo wa maisha yako.

Maswali matatu muhimu ya kujiuliza ili kujua ni nini unapaswa kufanya.
i. Ni kitu gani ambacho unajua unataka ukifanye ila bado unakipuuzia kukifanya?
ii. Ni kitu gani unaweza kukisimamia leo?
iii. Ni kitu gani haupo tayari kukiacha/kukiharibu hata kama kungetokea nini?
Kwa kujibu maswali haya utajua ni kipi muhimu kwako na anza kukifanyia kazi.
Kama bado unapata shida ya kujua ni kipi muhimu kwako karibu kwenye ushauri utakaokuwezesha kujijua zaidi. Andika email kwenda ushauri@kisimachamaarifa.co.tz
Nakutakia kila la kheri.

NENO LA LEO; Chochote Unachotaka Kuwa Kipo Huku

Everything you’ve ever wanted is on the other side of fear. –George Addair

Chochote ambacho umewahi kutaka kipo upande wa pili wa hofu.

Acha sasa kuwa na hofu na chukua hatua kupata kile unachotaka.

Kumbuka hakuna kingine zaidi ya kuchukua hatua.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Umepangiwa Kuwa Mtu huyu…

The only person you are destined to become is the person you decide to be. –Ralph Waldo Emerson

Mtu pekee uliyepangiwa kuwa ni yule unayeamua kuwa.

Kama unaamua kuwa na mafanikio utakuwa nayo kweli na kama unaamua kuwa wa hovyo utakuwa wa hovyo.

Maamuzi ni yako, uchaguzi ni wako.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Vikwazo.

Obstacles are those frightful things you see when you take your eyes off the goal. –Henry Ford

Vikwazo ni yale mambo ya kutisha unayoyaona pale unapoondoa macho yako kwenye malengo yako makubwa.

Ukishaweka malengo na mipango yako usiangalie tena pembeni, utaona mambo mengi ambayo yatakukatisha tamaa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Njia Moja Ya Uhakika Ya Kuepuka Kupingwa.

There is only one way to avoid criticism: do nothing, say nothing, and be nothing. –Aristotle

Kuna njia moja pekee ya kuepuka kupingwa; usifanye chochote, usiseme chochote na usiwe chochote.

Vinginevyo chochote utakachofanya lazima kuna mtu atakupinga au kukukosoa.

Fanya kile unachoona ni sahihi kufanya na komaa nacho mapaka ufikie mafanikio.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Jinsi Ya Kuua Hofu

If you hear a voice within you say “you cannot paint,” then by all means paint and that voice will be silenced. –Vincent Van Gogh

Kama unasikia sauti ndani yako inayokuambia huwezi kuchora basi kwa njia yoyote ile hakikisha unachora na sauti hiyo itanyamazishwa.

Usikubali kukatishwa tamaa na nafsi yako mwenyewe. Fanya kile unachohofia na hofu itakufa yenyewe.

Natutakia siku njema.

SIKU YA UKIMWI DUNIANI; Mambo Kumi Unayotakiwa Kujua Kuhusu Ukimwi.

Kila tarehe 01/12 ya kila mwaka dunia inaadhimisha siku ya UKIMWI. Siku hii imepewa heshma yake kutokana na madhara yake makubwa kwa watu wanaoupata.

Wakati tukiwa kwenye siku hii ya UKIMWI jiongeze na mambo haya kumi muhimu.

1. UKIMWI HAUUI.

UKIMWI maana yake ni upungufu wa kinga mwilini. Hivyo kinga yako inapopungua unatoa nafasi ya magonjwa mengine kukushambulia. Hivyo kinachowaua wagonjwa wa ukimwi sio ukimwi wenyewe bali magonjwa nyemelezi.

2. UKIMWI ni tofauti na VIRUSI VYA UKIMWI.

Ukiambukizwa virusi vya ukimwi leo, hauna ukimwi. Unawez akukaa na vizsi hivi kwa muda hata wa miaka kumi na pale kinga ya mwili inaposhindwa kukulinda na magonjwa ndio unakuwa na UKIMWI.

3. Wagonjwa watatu wa kwanza wa UKIMWI Tanzania waligunduliwa katika hospitali ya Ndolange mkoani Kagera mwezi November 1983.

4. UKIMWI husambazwa kwa kupitia maji maji ya mwilini. Yanayoongoza ni damu, na yenye kiasi kidogo ni mate, machozi na majimaji ya ukeni.

UKIMWI TZ

5. Njia kuwa ya kusambaza ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine ni kufanya mapenzi bila ya kujikinga. Njia nyingine ni kuchangia vitu vikali kama sindano na pia mama kwenda kwa mtoto.

6. Mpaka leo hakuna tiba wala kinga ya UKIMWI. Baadhi ya tafiti zimeonesha matokeo mazuri ila hakuna ambayo imedhibitishwa kutumiwa kama kinga au dawa.

7. Afrika chini ya jangwa la sahara ndio sehemu yenye maambukizi makubwa ya UKIMWI, asilimia 80 ya watu wenye ukimwi duniani wako Africa chini ya jangwa la sahara. Wakati idadi ya wanachi walioko Afrika chini ya jangwa la sahara ni asilimia 10 tu ya idadi ya watu wote duniani.

8. Wanawake wana hatari mara nane zaidi ya kuambukizwa ukimwi kuliko wanaume.

9. Mikoa inayoongoza kwa UKIMWI Tanzania ni Njombe ukifuatiwa na Iringa na mikoa yenye maambukizi madogo ni Pemba, Unguja na Lindi.

10. Mapambano ya UKIMWI yanaanza na mimi na wewe. Njia nyingine za maambukizi zimeweza kuzuiwa kwa kiasi kikubwa ila njia moja ndiyo yenye changamoto na njia hiyo ni kupitia kufanya mapenzi.

Tushirikiane kuutokomeza UKIMWI.

NENO LA LEO; Kisasi Bora

The best revenge is massive success. –Frank Sinatra

Kisasi bora ni mafanikio makubwa.

Kama mtu amekufanyia jambo baya na unataka kulipa kisasi, kisasi bora kulipa ni kuhakikisha unafanikiwa sana.

Nakutakia siku njema.