Kesho ni siku muhimu sana kwako, na itumie kufanya jambo hili moja muhimu.

Kesho ni tarehe moja mwezi wa kumi na mbili. Maana yake ni kwamba ni siku ya kwanza ya mwezi wa mwisho wa mwaka huu 2014.
Kuanzia kesho zitakuwa zimebaki siku 30 tu mwaka uishe!
Je mwaka huu 2014 uliendaje kwako?
Je malengo na mipango uliyojiwekea umeyatimiza!
Tumia siku ya kesho kutafakari mwaka huu umekwendaje.
Nakutakia kila la kheri,
TUPO PAMOJA.

Sheria Kumi Za Familia Za Kuzingatia


NENO LA LEO; Uwekezaji Unaolipa Riba Kubwa Sana

An investment in knowledge pays the best interest. –Benjamin Franklin

Uwekezaji kwenye elimu/ujuzi ndio uwekezaji unaolipa riba kubwa sana.

Anza sasa kuwekeza kwenye ujuzi na elimu yako, jifunze mambo mapya na yafanyie kazi.

Jinsi unavyojifunza zaidi ndivyo unavyoongeza thamani yako na hivyo kuongeza kipato chako.

Nakutakia siku njema.

UMUHIMU WA KUSOMA ZAIDI NA KUSOMA KILA MARA;

i. Jinsi unavyoishi jifunze jinsi ya kuishi, hakuna anayejua kila kitu.
ii. Viongozi bora wa uchumi mpya watakuwa ni wale wanaoweza kufikiri vizuri.
iii. Kufikiri vizuri kunajengwa na kusoma sana.
iv. Unachohitaji ili kubadili maisha yako moja kwa moja ni wazo moja tu kutoka kwenye kitabu sahihi.
v. Beba kitabu popote unapokuwa, ukiwa unamsubiri mtu soma, ukiwa kwenye foleni soma. Usipoteze muda wako kulalamika.
vi. Kama hujasoma kitu kizuri leo, hujaishi siku ya leo. Na kusoma huku sio habari, bali kitu kinachoweza kukusogeza karibu na malengo yako kweny maisha.
Kupata nafasi ya kusoma zaidi tembelea www.voraciousreaderstz.blogspot.com

Mambo matatu yatakayokufanya uishi maisha marefu.

Magonjwa mengi yanayowafanya watu kufa wakiwa na umri mdogo yanatokana na mtindo wa maisha tunaochagua.
Magonjwa kama presha ya juu, kisukari na hata kansa yanatokana na mitindo mbalimbali ya maisha.
Hapa nakushirikisha mambo matatu unayoweza kuanza kuyafanya leo na ukapunguza nafasi ya wewe kupata magonjwa haya na hivyo kuishi miaka mirefu.
1. Kula vizuri.
Naposema kula vizuri namaanisha ule mlo kamili. Kula mafita kidogo na kwa mtu mzima kula wanga kidogo. Kula matunda na mboga ,boga kwa wingi na pia kunywa maji mengi.
2. Fanya mazoezi.
Mazoezi ni muhimu sana kwa afya yako. Na mazoezi sio lazima ulipie gym au kukimbia barabarani japo hiyo ni sehemu nzuri ya mazoezi.
Unaweza kuchagua kutembea kwa miguu badala ya kupanda gari, kupanda ngazi badala ya kupanda lifti na kusimama na kufuata kitu mwenyewe badala ya kuagiza uletewe.
3. Usivute sigara.
Kila unapovuta sigara moja unapunguza dakika 14 za maisha yako. Sigara ina kemikali zaidi ya elfu moja zinazosababisha kansa. Karibu kila kansa inayompata binadamu inaweza kuchochewa na uvutaji wa sigara.
Na sigara sio lazima uvute wewe, hata ule moshi unaovuta kutoka kwa watu wanaovuta sigara una athari kubwa kwa afya yako.
Hayo ndio mambo matatu ambayo unaweza kuanza kuyafanya leo na ukaboresha afya yako na kyongeza siku zako za kuishi.
Nakutakia kila la kheri,
TUPO PAMOJA.
www.kisimachamaarifa.co.tz
www.amkamtanzania.com

NENO LA LEO; Siku Mbili Muhimu Sana Kwenye Maisha Yako.

The two most important days in your life are the day you are born and the day you find out why. –Mark Twain

Siku mbili muhimu sana kwenye maisha yako ni siku uliyozaliwa na siku uliyojua kwa nini ulizaliwa.

Najua wengi tunajua siku tulizozaliwa ila ni wachache sana wanaojua kwa nini walizaliwa.

Kama bado hujajua kwa nini ulizaliwa kwaribu tusaidiane kujua kwa nini ulizaliwa, yaani ni nini hasa unatakiwa kufanya na maisha yako.

Andika email yenye kichwa cha habari KWA NINI NILIZALIWA na maelezo mengine muhimu kuhusu wewe kisha tuma kwenye email ushauri@kisimachamaarifa.co.tz

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Kuhusu Kuendesha Siku Au Kuendeshwa na Siku.

Either you run the day, or the day runs you. –Jim Rohn

Kwenye siku yako ni labda unaiendesha siku au siku inakuendesha wewe.

Unaiendesha siku pale ambapo unakuwa na malengo na mipango yako ambayo unaifuata.

Unaendeshwa na siku pale ambapo unafanya kile kinachotokea mbele yako.

NINAJUA UNAJUA UNACHOTAKIWA KUFANYA, FANYA SASA, LEO HII ILI UWEZE KUIENDESHA SIKU YAKO.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Unachohitaji Ili Kubadili Maisha Yako.

You can never cross the ocean until you have the courage to lose sight of the shore. –Christopher Columbus

Huwezi kuivuka bahari mpaka pale utakapokuwa na ujasiri wa kupoteza taswira ya ufukwe.

Tunapenda vitu vizuri lakini tunaogopa kupoteza tulivyo navyo. Huwezi kupata vitu vipya kama hutaacha hivyo ulivyonavyo sasa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; MUDA MZURI WA KUPAMDA MTI.

The best time to plant a tree was 20 years ago. The second best time is now.

Muda mzuri wa kupanda mti ilikuwa miaka 20 iliyopita. Muda mwingine mzuri ni sasa.

Kila kitu kinahitaji maandalizi ya muda mrefu. Hivyo ili kuwa na maisha bora baadae inabidi uanze kufanya mabadiliko sasa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; FURSA UNAZOZIKOSA.

You miss 100% of the shots you don’t take. –Wayne Gretzky

Unakosa asilimia 100 ya fursa ambazo hujazichukulia hatua.

Acha kuendelea kusita sita, unapoteza fursa nyingi na muda wako pia.

Wakati wa kuchukua hatua ni sasa.

Nakutakia siku njema.

Hivi ndivyo shauku inavyokufanya kuwa mteja bila ya kupenda.

Sasa hivi tumekuwa watu wa kuendeshwa na shauku inayotokana na hisia. Na hii imetufanya tuwe wateja kwa wanaoweza kuzitumia hisia na shauku zetu.
Kwa mfano;
Kuna tofauti gani kwa anayenunua simu mpya iliyotoka leo kwa kusubiria muda mrefu na atakayekuja kuinunua kesho wakati kumetulia?
Kuna tofauti gani kati ya anayesikia habari mpya leo, BREAKING NEWS na atakayeisikia kesho?
Kuna tofauti gani kwa atakayekuwa wa kwanza kusambaza habari na ambae hatakuwa na haraka hiyo?
Yote haya na mengine mengi hayana tofauti ila yanatufanya tuwe wateja wa matoleo mapya, habari zilizovunjika na mbaya zaidi kusambaza habari ambazo hatuna uhakika nazo ili tu uwe wa kwanza......
Huna haja ya kuwa wa kwanza katika mambo haya, ni kujiongezea tu msongo.

NENO LA LEO; Kuhusu Fedha Kutonunua Furaha.

Watu wote wanaosema fedha haiwezi kununua furaha nao hawana fedha za kuwatosha. Sijawahi kumsikia tajiri akitumia kauli hiyo kwamba fedha haiwezi kununua furaha.

Hivyo basi badala ya kukubali tu kauli hiyo kwa nini usiifanyie majaribio? Kuwa na fedha nyingi halafu uone kama kweli zinaweza kununua furaha au la.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Tofauti Ya Washindi Na Washindwa.

Winners make goals... losers make excuses!

Washindi wanatengeneza malengo, washindwa wanatengeneza visingizio.

Amua leo kuwa mshindi na weka malengo na mipango mikubwa kwenye maisha yako. Acha sasa kutafuta visingizio.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Kuhusu Kujitetea.

It will do no good to argue if you're in the wrong. If you're right, you don't need to.

Kama umekosea au uko upande ambao sio sahihi, kujitetea hakuwezi kusaidia. Kama uko sahihi huna haja ya kujitetea.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Mwalimu Bora.

The best teachers teach from the heart, not from the
book.

Mwalimu bora anafundisha kutoka moyoni na sio kutoka kwenye vitabu.

Nakutakia siku njema.

Hivi ndivyo unavyoweza kuianza wiki yenye mafanikio.

Habari za asubuhi rafiki?
Ni siku nyingine mpya na mwanzo wa wiki mpya.
Naamini umeipangilia wiki yako vizuri kwa ajili ya kufikia mafanikio makubwa.
Wiki hii fanya kitu hiki kimoja;
Dhibiti kiwango cha taarifa unazopata, hasa kupitia vyombo vya habari. Hii ni kwa sababu taarifa nyingi ni;
i. Zinakula muda wako mwingi
ii. Ni hasi
iii. Hazina uhusiano na malengo yako.
iv. Huwezi kuziathiri, ziko nje ya uwezo wako.
Nakutakia wiki njema na yenye mafanikio makubwa.
TUPO PAMOJA.
Tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com kujifunza zaidi.

NENO LA LEO; Kuhusu Kuamini Uongo.

It is easier to believe a lie that you have heard a
thousand times, than the truth that you have only heard once.

Ni rahisi kuamini uongo uliousikia mara elfu moja kuliko kuamini ukweli uliousikia mara moja.

Ukweli utabaki kuwa ukweli, ukatae au ukubali.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Machozi

Tears are words the heart can't express.

Machozi ni maneno ambayo moyo hauwezi kuyaeleza.

Machozi ni hisia kubwa sana inayotolewa na mtu, inaweza kuwa furaha au inaweza kuwa huzuni. Hakikisha unaleta machozi ya furaha kwa watu wako wa karibu.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Chanzo Cha Mafanikio.

Achieving starts with believing in yourself.

Mafanikio huanza pale unapojiamini mwenyewe.

Anza sasa kujiamini na amini una uwezo mkubwa ulioko ndani yako wa kufikia mafanikio makubwa.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Mambo Unayotakiwa Kufanya.

You have to do what others won't. To achieve what others don't.

Unatakiwa kufanya mambo ambayo watu wengine hawafanyi ili kupata vitu ambavyo wengine hawapati.

Kupata mafanikio makubwa unahitaji kuwa tofauti na wengine.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Kuhusu Mtu Anayejua Kila Kitu.

Any man who knows all the answers most likely misunderstood the questions.

Mtu anayejua majibu yote kuna uwezekano mkubwa haelewi maswali.

Katika ulimwengu wa sasa ni vigumu sana kujua kila kitu, chagua vitu vichache unavyotaka kuvijua na vijue vizuri.

Nakutakia siku njema.

Mambo 21 muhimu ya kiufanya kila siku ili kuwa na maisha yenye mafanikio.

HABARI ZA LEO RAFIKI?
Naomba nikushirikishe Vitu 21 rahisi vya kufanya kila siku ili kuwa na maisha yenye furaha na mafanikio.
i. Lala masaa nane kwa siku.
ii. Kula milo miwili kwa siku.
iii. Usiangalie TV
iv. Usile vyakula vya haraka
v. Usilaumu wala kulalamika
vi. Usisengenye, usishiriki majungu na umbea.
vii. Onesha shukrani kwa marafiki.
viii. Andika orodha ya mawazo bora kila siku.
ix. Iambie nafsi yako unapoamka kwamba utakwenda kusaidia na kuokoa maisha ya watu kwa siku hiyo.
x. Andika mambo unayopanga kufanya kwa siku.
xi. Mshangaze mtu.
xii. Fikiria watu kumi ambao unashukuru kuwa nao kwenye maisha yako.
xiii. Msamehe mtu.
xiv. Panda ngazi badala ya lifti.
xv. Usiseme ndio wakati unafikiria kusema hapana.
xvi. Mwambie mtu kila siku kwamba unampenda.
xvii. Soma sura moja ya kitabu cha mtu anayekuhamasisha.
xviii. Weka mipango ya kutumia muda na rafiki yako.
xix. Pumua kwa kina na taratibu.
xx. Jifunze kitu kipya kila siku, pata walau saa moja ya kujisomea.
xxi. Fikiria watu wawili unaoweza kuwakutanisha na wakasaidiana na kushirikiana.
Kutoka kwa James Altucher - Choose Yourself.
Tembelea www.amkaconsultants.blogspot.com kujifunza zaidi.
TUPO PAMOJA, TUTAKUTANA KILELENI.

NENO LA LEO; Kuhusu Kikomo Cha Kasi Kwenye Njia Ya Mafanikio.

There are no speed limits on the road to excellence.

Hakuna kikomo cha kazi kwenye njia ya mafanikio.

Amua leo kwenda kwa kasi kubwa ili uweze kufikia mafanikio makubwa. Hakuna mda wa kupoteza.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Msamaha

Forgiveness is all about me giving up my right to hurt you for hurting me.

Msamaha ni pale ambapo mimi naamua kupoteza haki yangu ya kukuumiza wewe kwa kuniumiza mimi.

Unaposamehe unaepuka kutengeneza maumivu zaidi.

Amua leo kuwasamehe wote waliokuumiza, maana kuendelea kukaa na kinyongo unazidi kuumia wewe.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Mambo Mawili Muhimu Sana Kujua Kuhusu Maisha.

Life can either be accepted or changed. If it is not
accepted, it must be changed. If it cannot be changed, then it must be accepted.

Maisha yanaweza kukubaliwa au yanaweza kubadilishwa. Kama hayakubaliwi ni lazima yabadilishwe. Kama hayawezi kubadilishwa ni lazima yakubaliwe.

Usiendelee tena kuteseka na maisha yako, kama kuna kitu hukipendi kibadilishe na kama huwezi kukibadilisha kikubali. Ukiweza kufanya hivi maisha yako yatakuwa ya furaha.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Kukolea Kwenye Tabia Mbaya.

Bad habits are like a comfortable bed; they are easy to get into, but hard to get out of.

Tabia mbaya ni kama kitanda kizuri, ni rahisi kuingia ila ni vigumu sana kutoka.

Kama kuna tabia ambayo huipendi fanya jitihada kubwa kuondokana nayo.

Nakutakia siku njema.

NENO LA LEO; Mbinu Ya Kufikia Urefu Mkubwa.

To reach a great height a person needs to have great depth.

Kufikia urefu mkubwa mtu anahitaji kuwa na kina kikubwa.

Kiendacho juu kinategemea uimara wa kilichopo chini. Kama ilivyo kwamba ghorofa ndefu ina kina kikubwa na msingi imara.

Nakutakia siku njema.

LEO KATIKA HISTORIA; TAREHE 03/11/2014

November 3

1493
Christopher Columbus arrives at the Caribbee Isles (Dominica) during his second expedition.

1507
Leonardo da Vinci is commissioned to paint Lisa Gherardini ("Mona Lisa").

1529
The first parliament for five years opens in England and the Commons put forward bills against abuses amongst the clergy and in the church courts.

1794
Thomas Paine is released from a Parisian jail with help from the American ambassador James Monroe. He was arrested for having offended the Robespierre faction.

1813
American troops destroy the Indian village of Tallushatchee in the Mississippi Valley.

1868
Ulysses S. Grant elected the 18th president of the United States.

1883
A poorly trained Egyptian army, led by British General William Hicks, marches toward El Obeid in the Sudan–straight into a Mahdist ambush and massacre.

1883
The U.S. Supreme Court declares American Indians to be "dependent aliens."

1892
First automatic telephone exchange goes into operation in La Porte, Indiana.

1896
William McKinley is elected 25th president of the United States.

1912
The first all-metal plane flies near Issy, France, piloted by Ponche and Prinard.

1918
The German fleet at Kiel mutinies. This is the first act leading to Germany's capitulation in World War I.

1921
Milk drivers on strike dump thousands of gallons of milk onto New York City's streets.

1935
Left-wing groups in France form the Socialist and Republican Union.

1957
The Soviet Union launches Sputnik II with the dog Laika, the first animal in space, aboard.

1964
For the first time residents of Washington, D.C., are allowed to vote in a presidential election.

1964
Lyndon B. Johnson is elected the 36th president of the United States.

1964
Robert Kennedy, brother of the slain president, is elected as a senator from New York.

1967
The Battle of Dak To begins in Vietnam's Central Highlands; actually a series of engagements, the battle would continue through Nov. 22.

1969
US President Richard Nixon, speaking on TV and radio, asks the "silent majority" of the American people to support his policies and the continuing war effort in Vietnam.

1973
NASA launches Mariner 10, which will become the first probe to reach Mercury.

1979
Ku Klux Klansmen and neo-Nazis kill 5 and wound 7 members of the Communist Workers Party during a "Death to the Klan" rally in Greensboro, NC; the incident becomes known as the Greensboro Massacre.

1983
Jesse Jackson announces his candidacy for the office of president of the United States.

1986
The Lebanese magazine Ash-Shiraa reports the US has secretly been selling weapons to Iran in order to secure the release of 7 American hostages being held by pro-Iranian groups in Lebanon.

1992
Arkansas Governor Bill (William Jefferson) Clinton is elected 42nd president of the United States.

1997
US imposes economic sanctions against Sudan in response to human rights abuses and support of Islamic extremist groups.

Born on November 3

1718
John Montague, fourth Earl of Sandwich and inventor of the sandwich.

1794
William Cullen Bryant, poet and journalist.

1801
Karl Baedeker, German publisher, well known for travel guides.

1831
Ignatius Donnelly, American social reformer best known for his book Atlantis: The Antediluvian World.

1901
Andre Malraux, French novelist (Man's Fate).

1903
Walker Evans, photographer.

1909
James "Scotty" Reston, New York Times reporter, editor and columnist.

1918
Russell Long, U.S. senator from Louisiana from 1951 to 1968 and son of Huey P. Long.

1920
Oodgeroo Noonuccal [Kath Walker], Australian Aboriginal poet.

1933
Jeremy Brett, actor; best known for his portrayal of Sherlock Holmes in the Granada TV productions of Sir Arthur Conan Doyle's stories about the detective.

1933
Michael Dukakis, politician; the longest-serving governor in the history of the State of Massachusetts (1975-79, 1983-91); unsuccessful Democratic candidate for US presidency (1988).

1933
Amartya Sen, Indian economist, winner of Nobel Memorial Prize in Economic Sciences (1998) for his work on economic theories of famines and social justice and indexes for measuring the well-being of citizens in developing countries.

1942
Martin Cruz Smith, novelist (Gorky Park).

1949
Larry Holmes, professional boxer known as The Easton Assassin; his 20 successful defenses of his heavyweight title is second only to Joe Louis' record 25.

1952
Roseanne Barr, comedian, actress, producer; best known for her starring role in the TV series Roseanne, for which she won both an Emmy and a Golden Globe.

1952
David Ho, virologist, AIDS researcher.

1956
Gary Ross, film director, screenwriter (The Hunger Games, Seabiscuit).

NENO LA LEO; Kuhusu Dunia Kutokukuzuia.

The whole world steps aside for the man who knows where he is going.

Dunia nzima hukaa pembeni na kumpisha mtu anayejua anakoelekea.

Kuwa na ujasiri wa kujua unakoelekea na hakuna kitakachoweza kukuzuia.

Nakutakia siku njema.

Soko la Hisa la Dar: Fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wazalendo Tanzania

 

Soko letu limekuwa likiwanufaisha zaidi wageni na wananchi wa nchi jirani ambao hulitumia kikamilifu kujinufaisha na wazalendo wengi kutoelewa nini kinachoendelea. Kwa wale waliokwisha jitosa, huwezi amaini jinsi wanavonufaika na kuwekeza zaidi na zaidi.

Leo kidogo tutupe jicho kwenye hii sekta ya hisa… Si sekta ngeni sana ila kwa hapa nchini wananchi wengi hawajaigundua na kushiriki kikamilifu kama nchi jirani na Tanzania. Wenzetu Kenya wamejitahidi kwenye ushiriki wa soko lao la Hisa la Nairobi (Nairobi Stock Exchange). Na kwa Afrika Mashariki, hili Soko la Hisa la Nairobi ndilo soko kubwa kuliko yote.

Dar-es-Salaam-Stock-Exchange

Pamoja na changamoto zake, hili soko lina faida kubwa kwa wale walioligundua na wanaoendelea kulitumia. Kuna mjasiriamali mmoja, yeye alinunua hisa za Twiga mwishoni mwa miaka ya 90 au mwanzoni mwa miaka ya 2000 zikiwa zinauzwa kati ya 200-300 kwa kipande. Leo hii kipande hicho hicho cha Twiga Cement kinauzwa kati ya 2500-2006 kiasi cha miaka 13 tu mbele.

Mdau huyu wa soko hilo anakiri kama angejua ukuaji ni wa kiasi hiki basi angenunua zaidi ya hizo alizonunuaga. Na ameendelea kuongeza vipande vyake kila awezapo. Anadai yeye hupenda kuwekeza kwenye hisa sababu hakuna usumbufu wa uendeshaji . Ukishanunua hisa unakaa na kungoja zipande ama zishuke ili na wewe uuze za kwako. Anakiri kuwa soko hili limemnufaisha sana na anawashauri wengine wajiunge nalo wapate kunufaika pia.

Wengi wetu wenye mitaji midogo midogo tunaweza kunufaika kwa kujiunga na hili soko la hisa la Dar es Salaam na kununua vipande kwa pesa tuliyonayo. Vipande vingi vimeonesha kupanda thamani yake ikiwemo hisa za makampuni ya bia (TBL na SBL), Saruji (Twiga  na Simba ) na Bank kama NMB. Kama mwekezaji mzalendo, ukijitosa ukanunua hisa zako za 2,000,000 leo, baada ya miaka 4 unaweza kuziuza hata kwa faida kubwa tu bila kuteseka na usumbufu wa uendeshaji kama zilivyo biashara nyingine.

Upande wa pili soko hili la hisa pia lina magumu yake kama kupotea kwa mtaji wako kutokana na kushuka kwa thamani ya vipande. Hili kwa mfano, limewaathiri wawekezaji walionunua hisa za CRDB na TOL ambazo zimekuwa zikikumbwa na kushuka kwa thamani mara kwa mara. Muhimu ni kuwa makini tu kwa kuchagua vyema ni hisa zipi ununue na kampuni ipi uwekeze.

Soko letu limekuwa likiwanufaisha zaidi wageni na wananchi wa nchi jirani ambao hulitumia kikamilifu kujinufaisha na wazalendo wengi kutoelewa nini kinachoendelea. Kwa wale waliokwisha jitosa, huwezi amaini jinsi wanavonufaika na kuwekeza zaidi na zaidi.

Huu ni wito wangu kwenu wazalendo wenzangu, mkajiunge na soko la hisa la Dar es Salaam na kufaidi matunda yake!

Chanzo cha makala haya ni FIKRA PEVU.

Msingi na ustadi wa kuwekeza kwenye Soko la Hisa

JE ukiwa kama mwananchi wa kawaida usingependelea kuwa mmiliki wa kampuni bila ya kuwa na ulazima wa kufika kazini na kufanya kazi za kila siku?

Hebu tafakari kwa kina, upo nyumbani kwako umepumzika au ukifanya shughuli zako nyingine na ukiiangalia kampuni yako inakua kwa ufanisi na tija na baada ya muda unachukua hundi yako ya gawio huku mtaji wako ukiendelea kukua kila kukicha.

Jambo hili linaweza kuonekana kama ni njozi au ndoto, lakini ukweli ni kwamba lina ukweli usiopingika na jawabu lake ni kuwa na hisa hususani katika kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Kwa hiyo ili kutimiza ndoto yako ya kukidhi mahitaji yako ya fedha na kuanza safari yako ya kumiliki kampuni kupitia Soko la Hisa unatakiwa kuwa na uelewa mzuri wa jinsi gani hisa zinavyouzwa na kununuliwa katika soko la hisa.

Katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja uliopita, wananchi wengi wa kawaida nchini Tanzania wamekuwa na shauku ya kununua hisa kwenye kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam na kulifanya soko hilo kukua kwa haraka. Hivi sasa hisa zinaonekana ya kwamba ndiyo chombo kinachoweza kuwapatia wananchi ukuaji wa uchumi binafsi kutokana na kumiliki kampuni zilizo katika sekta muhimu katika uchumi wa nchi yetu.

Pamoja na kuwa hisa zimeanza kupata umaarufu mkubwa, lakini watu wengi bado hawajaweza kuwa na uelewa mkubwa kuhusiana na hisa na jinsi ya kuweza kununua na kuuza hisa hizo. 

Nadhani mara nyingi mmeweza kusikia baadhi ya watu wakisema maneno yafuatayo:

"Umesikia, mjomba wake Marwa ametengeneza pesa nyingi sana katika hisa za NMB; na kwa sasa atapata bahashishi nyingine..." au vile utasikia "Chukua tahadhari kubwa kwenye hisa zako, kwa sababu unaweza ukapoteza hisa zako ndani ya siku chache!"

Maneno yote haya ni upotoshaji mkubwa kwa sababu yanasababishwa na mawazo potofu ya kupata utajiri wa haraka haraka. Mara nyingi baadhi ya watu wanafikiri ya kwamba ununuaji wa hisa ni njia ya mkato ya kupata utajiri na hakuna hatari ya kupata hasara.

Marwa dse

Msukosuko wa masuala ya fedha duniani uliotokea hivi karibuni umeweza kuthibitisha ya kwamba soko la hisa pia linaweza kuyumba.

Ukweli ni kwamba hisa zinaweza kuleta utajiri mkubwa lakini si kwamba hakuna hatari ya kupata hasara. Jambo la msingi la kujilinda ili kutokupata hasara na ni vyema kabla hujanunua hisa, ni vyema ukajua unawekeza pesa zako kwenye hisa za kampuni ipi. Na ndiyo maana kutokana na suala hilo, Soko la Hisa la Dar es Salaam limeanzisha programu inayomsaidia mwanahisa kuweza kufanya maamuzi yake binafsi kujua anafanya uwekezaji katika kampuni ipi bila ya kuwa na shinikizo.

Je, hisa ni kitu gani? Hisa ni nini?

Elimu ya msingi ambayo unatakiwa kuwa nayo kabla ya kufanya uwekezaji katika soko la hisa nikujua hisa ni kitu gani, aina tofauti za hisa na soko la hisa lenyewe linafanyaje kazi.

Kwa hiyo ni vyema tukaanza kwa kujua hisa ni kitu gani.

Kwa kutumia lugha nyepesi ukinunua hisa unathibitisha umilikaji wa kampuni. Hisa zinathibitisha kumiliki mali za kampuni na mapato yake. Jinsi unavyonunua na kuwekeza hisa katika kampuni ndivyo jinsi umiliki wako katika kampuni hiyo unavyoongezeka thamani.   

Kwa hiyo, hakuna utofauti wowote kati ya hisa na mtaji; vyote ni sawa na vinawakilisha umiliki wa kampuni.

Aidha, kwa kununua hisa, fedha ambayo ingekuwa imekaa tu bila kufanyiwa kazi au ipo katika akaunti ya akiba na kupata riba ndogo, inaingia katika mzunguko wa fedha ambao unakuwa na tija katika uchumi.

Kuwa mmiliki wa kampuni na faida zake

Kumiliki hisa za kampuni inamaanisha ya kwamba wewe unakuwa miongoni mwa wanahisa wengi ambao wana haki ya kumiliki kila kitu ambacho kampuni inamiliki.

Kisheria inamaanisha ya kwamba wewe ni mmoja wao wanaomiliki rasilimali, samani, vifaa, nembo ya biashara na mikataba yote ya kampuni. Kama mmiliki wa kampuni una haki ya kupata sehemu yako ya mapato ya kampuni na una haki ya kupiga kura kama ilivyoanishwa kwenye hati ya umiliki wa hisa zako.

Hisa kwa kawaida huwakilishwa na hati ya hisa ambayo ndiyo inayothibitisha umiliki wako wa kampuni.  Wakati unaponunua hisa unakuwa tayari mwekezaji na hivyo unakuwa mmiliki wa mali za kampuni, faida na hasara za kampuni hiyo.

Pamoja na hayo, kuwa mwanahisa katika moja ya kampuni zilizosajiliwa katika Soko la Hisa hakukufanyi wewe mwanahisa kufanya shughuli za kila siku za kampuni. Haki uliyo nayo ni kupiga kura ya kuwachagua wakurugenzi wa bodi katika mkutano mkuu wa mwaka na si vinginevyo.

Kwa mfano, ukiwa mwanahisa wa Benki ya CRDB, haimaanishi ya kwamba unayo haki ya kumpigia simu mkurugenzi mtendaji na kumwelekeza jinsi ya kuendesha benki hiyo. Pia kwa mwendo huo huo kama mwanahisa wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) hauna ruksa ya kuingia kiwandani na kwenda kudai upewe kreti la bia bure!

Kinachotakiwa ni menejimenti ya kampuni kufanya kazi kwa bidii na kuiongezea thamani kampuni kwa faida ya wanahisa waliowekeza fedha zao. Kama menejimenti ikishindwa kufanya hivyo wanahisa wanauwezo wa kupiga kura na kuiondoa. Kwa muundo huu wa kununua hisa hutakiwi kufanya kazi ili upate fedha, menejimenti inatakiwa kukufanyia kazi.

Suala hili la mwisho ni la msingi na ni lazima nilifafanue, ni kwamba umuhimu wa kununua hisa ndani ya kampuni unakupatia haki ya kumiliki mali na faida inayopatikana ndani ya kampuni hiyo bila hivyo hisa zisingekuwa na maana yoyote na hati yake isingekuwa na thamani yoyote.

Jambo jingine la msingi ni ya kwamba kama mwanahisa, kama mtu binafsi huwajibiki kisheria kutokana na kampuni kushindwa kulipa madeni yake. Katika biashara zingine kama za ubia (partnerships) zinasajiliwa kwa kanuni ambazo kama zinafilisika wadai kisheria wanaweza kuwafuata wamiliki wa ubia na kuuza mali zao kama nyumba, gari, vifaa, samani na kadhalika ili kurudisha fedha zao.

Kwa hiyo kisheria, kumiliki hisa ndani ya kampuni kunamaanisha ya kwamba kitu pekee ambacho mwanahisa anaweza kupoteza kama kampuni ikifilisika ni kupoteza thamani ya hisa zako ulizowekeza ndani ya kampuni na si vinginevyo. Huwezi ukapoteza mali zako binafsi.

Moremi Marwa ni Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE)

Email: moremi@dse.co.tz

Kuhusu Uwekezaji Tanzania

UWEKEZAJI TANZANIA ni mtandao unaokupatia maarifa na taarifa mbalimbali za uwekezaji kwa hapa nchini Tanzania.
Kupitia mtandao huu utajifunza fursa mbalimbali za uwekezaji na pia kupata taarifa zinazohusu uwekezaji.

 AINA ZA UWEKEZAJI TANZANIA.

Kwa bahati nzuri sana kuna aina nyingi sana za uwekezaji Tanzania. Kuna kila rasilimali na fursa mbalimbali za uwekezaji. Ugunduzi wa mafutra na gesi unaoendelea kufanyika Tanzania unaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi sana.
Kuna aina mbalimbali za uwekezaji zinazoweza kufanyika Tanzania.

1. Uwekezaji wa mali.

Tanzania kuna arhi kubwa sana ambapo mtu anaweza kununua na kuendeleza kwa kujenga majengo ya kibishara na hata makazi.
Pia ardhi hii inaruhusu kilimo na hivyo mtu unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha biashara.

2. Bishara.

Kwa kuwa uchumi wa tanzania unakua kwa kasi sana mtu yeyote anayweza kuwekeza kwenye biashara anaweza kuapata faida kubwa. Biashara za bidhaa na huduma zinakua kwa kasi sana kutokana na ongezeko la watu na muingiliano wa kimataifa.

3. Uwekezaji katika maliasili na gesi.

Tanzania ina gesi nyingi sana ambayo bado haijachimbwa. Hii inatoa fursa kubwa sana ya uwekezaji.

4. Uwekezaji wa hisa na vipande.

Hii ni fursa nzuri ya uwekezaji kwa watu ambao wana miotaji kidogo. Soko la hisa la dar es salaa limeorodhesha makampuni mbalimbali ambayo mtu anaweza kununua hisa.
Pia dhamana ya uwekezaji UTT, inatoa fursa kwa watu kununua vipande na vipande hivyo kuongezeka thamani na hivyo kunufaika zaidi.
Kuna fursa nyingi sana za uwekezaji ambazo utajifunza kupitia mtandao huu.

NENO LA LEO; Sehemu Ambapo Hofu Itakuwahisha.

Perpetual worry will get you to one place ahead of time - the cemetery.

Hofu ya kila mara itakusaidia kuwahi sehemu moja – kaburini.

Ni kweli hofu inaweza kukusababishia kifo.

Kuwa makini.

Nakutakia siku njema.