Jambo Moja Muhimu La Kuzingatia Ili Uwe Tajiri.

Kabla ya kitu chochote hakijaweza kuwa katika hali yake ya uhalisia huanza katika wazo. Nyumba haiwezi kujengwa kabla ya kuanza kuwa na mchoro unaongoza ujenzi wa hiyo nyumba. Katika maana nyingine rahisi unaweza kusema tunafikiri kwanza halafu tunafuata utekelezaji au kuweka katika matendo kile tunachokifikiri.

Jaribio rahisi ambalo linaweza kukufanya ujue kama mtu ataishia kuwa tajiri au tayari ni tajiri ni kwa kutazama yale mambo anayoyafanya kwa kuwa yale anayoyafanya yanaweza kutabiri matokeo yanayotarajiwa. Mambo anayoyafanya mtu huyafanya kutokana na mwongozo anaopata kutoka katika kiwanda chake cha kuzalisha mawazo.

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

Jaribio lenyewe ni kutazama mawazo ambayo anayatengeneza kupitia jinsi anavyoilisha akili yake. Chunguza ni mambo gani au vitabu vya aina gani au majarida ya aina gani au makala za aina gani huyo mtu anasoma. Katika hivyo vitabu au majarida mwangalie vipengele gani ambavyo anavyovisoma na pia uangalie vipengele gani katika majarida au vitabu hivyo hivyo huwa havipi mkazo kuvisoma. Katika vile vipengele anavyovisoma chunguza anavisoma katika mpangilio gani au mfuatano upi?

Jaribio hili unaweza kulifanya hata kwako binafsi kama kweli una kiu ya kubadili hali yako ya sasa kuwa tajiri au kama tayari ni tajiri basi kuufanya utajiri wako ukue zaidi. Watu ambao ni matajiri walio kaa chini kutafakari na kuamua kwa kusudia kuwa wanataka kuwa matajiri tofauti na wale ambao labda wameshinda bahati nasibu au wamerithishwa mali huchagua vitabu au majarida ambayo yanaongeza thamani katika utajiri wao, huchagua vipengele katika majarida au vitabu ambavyo kweli vinaongeza thamani katika maisha yao, havipi mkazo vipengele vile ambavyo haviongezi thamani na katika haya majarida au vitabu utagundua huwa wanasoma vipengele vinavyohusiana na fedha au biashara kwanza kabla ya kusoma vipengele vingine.

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Ukitaka kuwa daktari ni muhimu sana usomee udaktari, au ukitaka kuwa msanifu majengo ni muhimu sana usome kuhusu masuala ya usanifu majengo ili uwe na uwezo wa kufanya kazi yako kwa ufanisi na usiwe mbabaishaji katika eneo husika ulilolichagua. Matajiri wote ambao wamechagua kwa makusudi kuwa matajiri wamejifunza kwa njia mbalimbali kuhusu utajiri. Mmoja wa wana mafanikio maarufu duniani Jim Rohn hupenda kusema ukihitaji furaha nenda ujifunze furaha, ukihitaji uhuru wa kifedha nenda ujifunze kuhusu uhuru wa kifedha, ukihitaji afya bora nenda ujifunze kuhusu afya bora, orodha hii inaweza kuendelea zaidi lakini Jim alihitimisha kwa kusema kila kitu unachokihitaji ni kujifunza, ndiyo maana nikasema kama unataka utajiri jifunze utajiri. Kujifunza huku sio kwa kukaa darasani kwa sababu mifumo yetu ya elimu haina mitaala inayowaelekeza watu namna ya kuwa matajiri bali ina mitaala ambayo inawaandaa watu kuwa waajiriwa. Matajiri wengi waliamua kujiendeleza binafsi kwa kusoma makala, vitabu na majarida ambayo yanawapatia maarifa ambayo hayajawekwa katika mitaala ya mifumo wa elimu tulio nao.

Mafunzo makubwa ambayo wamejifunza ni namna ambavyo matajiri wengine kabla yao jinsi wanavyowaza kwa kudhibiti malighafi inayotumika katika kiwanda cha mawazo kupitia ulishaji wa akili zao kwa yale wanayoyasoma, wamejifunza namna matajiri waliotangulia wanavyofanya kazi, wanavyokula, wanavyoishi , wanavyoweka akiba, wanavyowekeza katika vitega uchumi mbalimbali. Wamejifunza kwa kujaribu kuongea na watu matajiri ili kuwapa mbinu za kufanikiwa kwa upande mmoja na kwa upande mwingine kuwaelekeza mambo ambayo wanatakiwa kuchukua tahadhari ili kuepuka kutetereka. Wamejifunza kwa kuuliza maswali sahihi, maswali sahihi ni yale maswali ambayo ukiuliza yanaenda kugusa na kubadili maeneo maisha yako moja kwa moja. Wamesoma mahojiano mbalimbali ambayo hawa matajiri waliotangulia wameyafanya, wamesoma kuhusu wasifu wa hawa matajiri waliotangulia. Hayo ndio masomo ambayo wanajifunza katika chuo cha utajiri.

SOMA; Jinsi Ya Kuondokana Na Tabia Ya Kuahirisha Mambo.

Kama kweli umeamua kwa makusudi kabisa unahitaji kuwa tajiri ni lazima ujiendeleze kwa kuwa na uelewa pamoja na maarifa ya kujitosheleza kuhusu utajiri.

Mwandishi: Goodluck Moshi

Mawasiliano: Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi

Pia unaweza kutembelea blogu yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.

Hivi Ndio Vitu Vinavyopelekea Ongezeko La Thamani Ya Hisa Kwa Mwekezaji.

Moja ya faida kwa mwekezaji kuwekeza katika Hisa ni pamoja na ongezeko la thamani ya hisa zake. Hisa ikiongezeka thamani kwa mwekezaji na uwekezaji wake unakua. Na ili uweze kufanya uwekezaji wenye manufaa ni vizuri ukawekeza kwenye Kampuni ambayo thamani ya Hisa inakua kwa kiwango cha chini kabisa 20% kwa mwaka. Ili thamani ya hisa iongezeke kuna vitu ambavyo huwa vinachochea kwa ukuaji wa thamani ya hisa hizo katika soko.

Vitu hivi hupelekea ongezeko la thamani ya Hisa kwa mwekezaji

Nguvu ya soko

Bei za hisa kuongezeka hutegemea ushindani kati ya wauzaji na wanunuzi wa hisa katika soko. Wanunuzi wakiwa wengi katika soko na wauzaji ni wachache hupelekea kupanda kwa bei kwa kuwa watashindana kwa bei. Ili hisa za kampuni hiyo ziwe na wanunuzi wengi hutegemea na ufanisi wa kampuni hiyo, hasa katika taarifa za fedha na utoaji wa gawio.

SOMA; Mambo 6 Yakukusaidia Kujua Shughuli Iliyokuleta Duniani.

Hali ya kiuchumi

Hali ya kiuchumi ya nchi hupelekea mwananchi kupata kipato ambacho hupelekea uwekezaji kuwa mkubwa. Mwenendo wa uchumi hupelekea ufanisi wa baadhi ya kampuni na kuchochea kuongezeka kwa bei zake katika soko kwa kuwa kampuni hiyo huwavutia wawekezaji kutokana na kufanya vizuri. Hali ya uchumi ikiwa sio nzuri hupelekea ufanisi katika soko kuwa mdogo na bei kushuka kwa baadhi ya kampuni.

Gawio

Gawio kwa mwekezaji ni kipato na faida mojawapo ya uwekezaji wake. Gawio hutolewa kutoka na faida ya Kampuni ambayo imepata na maamuzi wa wanahisa katika kikao na hutolewa mara moja au mara mbili. Kampuni ambazo hutoa gawio ambalo linaongezeka katika kiwango kizuri na kikubwa huchochea ukuaji wa bei zake. Wawekezaji wengi huvutiwa kuwekeza katika kampuni hizo na ushindani kuwa mkubwa na bei kuongezeka.

SOMA; USHAURI; Jinsi Unavyoweza Kuondokana Na Changamoto Za Kuendesha Biashara Na Kuweza Kufikia Mafanikio Makubwa.

Ufanisi wa kampuni

Utendaji wa kampuni husika katika kutoa huduma au bidhaa huwavutia wateja na kampuni kufanya vizuri. Vile vile ufanisi wa kampuni katika taarifa zake za fedha kama ukuaji wa mauzo, faida, gawio na uwezo wa kampuni katika kupunguza gharama na madeni. Kampuni ikifanya vizurihupelekea bei zake kupanda kwa kuwa wawekezaji wengi huvutiwa kuwekeza katika Kampuni hiyo.

Thamani inayotegemewa/Mipango ya kampuni

Mipango mizuri na yenye tija kwa kampuni kwa kipindi kijacho huwavutia wawekezaji wengi kununua hisa za kampuni kwa kuwa wanajua katika kipindi kijacho kampuni hiyo itafanya vizuri. Mfano pale kampuni inapotangaza kufungua matawi katika sehemu nyingine au inapotangaza kuongeza bidhaa mpya sokoni. Vitu hupelekea wawekezaji wengi kuvutiwa kununua hisa za kampuni hiyo na ushindani kuwa mkubwa na bei kuongezeka.

“Wekeza Inalipa”

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano: emmanuelmahundi@gmail.com au 0714 445510

Ukiwa Na Kitu Hiki Ni Mwanzo Mzuri Wa Kufanikiwa Katika Uwekezaji.

Kila mtu anatamani mafanikio. Hakuna chini ya jua mtu yeyote asiyependa kufanikiwa. Mafanikio si jambo la mara moja au jambo la kufanya leo na kuona matokeo kesho. Inahitaji kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kuweza kufikia katika lengo lako. Lengo lako ni kufanikiwa na kufanya kazi kwa pekee hakuwezi kukufanya ufanikiwe bila kuwa na uhitaji kutoka moyoni mwako (commitment). Mpaka kufikia hapa najua unatamani kujua ni kitu gani hicho cha muhimu unachopaswa kukijua ili uwemwekezaji bora na mfanyabiashara bora mwenye mafanikio. Jibu la kiu yako ni taarifa (information).Utashangaa kidogo lakini ndio ukweli huo. Watu wengi waliofanikiwa wamefanikiwa kwa sababu ya kupata taarifa.

SOMA; USHAURI; Jinsi Unavyoweza Kuondokana Na Changamoto Za Kuendesha Biashara Na Kuweza Kufikia Mafanikio Makubwa

Taarifa yaweza kuwa habari, fursa, nafasi ya kazi na hata elimu. Watu wamekuwa wakitafuta taarifa kwa udi na uvumba, wengi wamekuwa wakilipia kupata taarifa. Njia hizo zinazolipiwa kupata taarifa ni kama televisheni na magazeti. Taarifa imekuwa na soko kubwa katika karne hii. La kusikitisha ni kwamba watu wamekuwa wakifuatilia taarifa ambazo haziwasaidii katika kujikwamua katika maisha yao. Kufuatilia taarifa zisizokusaidia ni sawa na kujichimbia kaburi lako mwenyewe. Kwa hiyo basi ndipo sasa umuhimu wa kupata taarifa sahihi kwa wakati muafaka unapokuwa na umuhimu. Niseme tu kwamba kupitia taarifa sahihi unazopata unaweza kuamua kufanya uwekezaji unaouona unafaa zaidi. Taarifa kama hali ya hewa yaweza kukusaidia sana katika shughuli za kilimo na hata usafirishaji, utaweza kujua aina za mazao ya kulima na aina ya usafiri utakaoutumia kufikia wateja. Mfano mwingie ni uhitaji wa bidhaa mahali Fulani, ukipata taarifa hizo na wewe ni mzalishaji au msambazaji au mtu uliyeona fursa hiyo baada ya kupata taarifa sahihi unaweza kuchangamkia fursa hiyo na hivyo kuweza kufanikiwa. Taarifa sahihi inaweza kukuonyesha mapungufu yaliopo katika biashara Fulani au mahali Fulani na hivyo kuweza kuwekeza. Hivyo basi napenda kusisitiza taarifa sahihi kwani taarifa zisizo sahihi zaweza kukupelekea katika kushindwa kufikia mafanikio makubwa. Ili uweze kufanikiwa anza kutafuta taarifa sahihi kwa mafanikio yako. Acha kabisa kufuatilia taarifa ambazo zimekuwa zikikupotezea muda wako mfano taarifa za udaku na zinazofanana na hizo.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyojitengenezea Dharura.

Sehemu za kupata taarifa sahihi

Dunia ya sasa ni kama kijiji. Mawasiliano yamekuwa rahisi kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya mwanadamu. Kuamua kupata ama kutopata taarifa ni juu yako mwenyewe kwani kuna njia nyingi sana za kuzipata.

INTERNET

Nianze na njia ambayo ni maarufu sana ya INTERNET. Naamini wewe unayesoma Makala hii umeweza kuipata kupitia internet. Tumia internet vizuri kupata taarifa sahihi. Katika internet kuna taarifa nyingi sana za uongo na za kweli. Tumia akili yako na maarifa kuweza kuchambua taarifa sahihi.

VYOMBO VYA HABARI

Vyombo vya habari kama redio, televisheni na magazeti na hatabloguzinaweza kutangaza taarifa ambayo kwako ni fursa tosha. Tafuta taarifa sahihi hasa za kibiashara zinazotangazwa na vyombo hivi. Wakati mwingine majanga yanayotekea sehemu Fulani yaweza kuwa fursa yako ya kuweza kufanya biashara au kuwekeza. Mathalani sehemu yenye upungufu wa maji, unaweza kuwekeza kwa kuuza maji au kuchimba visima na kuwauzia wananchi.

WATU/MARAFIKI

Taarifa zimekuwa zikitoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Taarifa hizi zaweza kuwa sahihi au zisiwe sahihi hivyo kabla hujazitumia jitahidi kuzithibitisha. Ishi na watu vizuri na marafiki pia kwani bila watu na hasa marafiki ni vigumu kufanikiwa. Sahau kuhusu jeshi la mtu mmoja. Hakuna jeshi la namna hiyo duniani kote. Tumia taarifa unazopata kwa usahihi na naamini siku moja utakuwa umefanikiwa.

SOMA; Saikolojia Ya Kuuza, Uza Bei Ghali Kabla Ya Rahisi.

Kabla sijahitimisha nipende kurudia kuwa huhitaji taarifa peke yake bali unahitaji kupata taarifa sahihi. Kumbuka ‘Informationispower’ (taarifa ni nguvu) na mwenye taarifa sahihi ndiye aliyebeba mafanikio mikononi mwake.

Tukutane katika Makala nyingine muda mwingine.

Makala hii imeandikwa na Nickson Yohanes ambae ni mjasirimali na mhamasishaji.

Unaweza kuwasiliana na naye kwa: simu: 0712 843030/0753 843030

e-mail:nmyohanes@gmail.com

Pia unaweza kutembelea blogu yake: www.lifeadventurestz.blogspot.comkujifunza zaidi.

Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu; GO IT ALONE

Habari rafiki, ni matumaini yangu unaendelea vizuri. Wiki hii tunaendelea na utaratibu wetu wa kushirikishana mambo 20 nilijifunza kwenye kitabu. Leo tunajifunza kutoka kwenye kitabu kinachoitwa GO IT ALONE, Do what you do best let other do the rest. Kitabu kimeandikwa na Bruce Judson

1. Mawazo mazuri ya biashara yapo kila mahali. Unachotakiwa tu ni kufumbua macho. Ukiwa na jicho la fursa nakuhakikishia utaziona nyingi mpaka unawezashindwa kujua uanze na ipi. Tatizo ni kwamba tumekua watu wakulalamika mno, ikilalamika unafanya akili yako kushindwa kugundua fursa. Matatizo au changamoto zinazowakabili watu ndio fursa kwako, jikite kwenye kutafutasuluhisho la changamoto hizo, lazima watu watanunua suluhisho za changamoto zinazowakabili. Goodideasareeverywhere.

2. Katika biashara usijikite kutengeneza faida mwanzoni, bali jikite katika kutengeneza thamani ya biashara yako zaidi. Na pia Katika hatua za mwanzo usiitegemee biashara yako kama chanzo cha kipato. Faida inayopatikana itumike kwenye kuongeza thamani ya biashara na kuitanua zaidi.

3. Mjasiriamali unapaswa kua na mtazamo wa kufanya majaribio mara zote (experimentalattitude). Fanya majaribio tena na tena, fanya tena na tena mpaka umepata njia mpya. Hakuna jibu la kweli kwa wakati wote. Unaweza kugundua ukweli wa leo..lakini kesho ukawa haufanyi kazi au ukawa ni uongo. Bill gate wakati anaanza kutengeneza kompyuta miaka ila ya 70, watu walimwambia dunia nzima itahitaji kompyuta 5 tu, maana yake kutakua ni hakuna soko la hizo kompyuta anazotengeneza, pengine huo ndio ukweli wa kipindi kile. Lakini je ukweli wa leo ukoje, dunia inahitaji kompyuta kuliko ilivyofikiriwa mwanzoni. Kompyuta zimerahisisha mambo mengi sana. Laiti Bill Gate angesikiliza ushauri wao., leo tungekua nyuma sana. Alichofanya Bill Gate ni kuendelea kujaribu na kujaribu ili kupata ukweli mpya ambao ulikuja kubatilisha ukweli wa zamani.

4. Jiweke katika nafasi ya kutatua tatizo na si kulaumu. Sio kila wakati wewe ni mtu wa kunung’unika tu, hiyo hata Mungu hapendi. Kumbuka hata Mungu alitaka kulifutilia mbali taifa la Israel wakati walikua wakilalama. Ukilalamika ni ishara ya kukosa imani. Tumeumbwa na uwezo mkubwa sana, wa kutatua matatizo, sasa tunamuudhi hata aliyetuumba maana uwezo huo ameshatupa, ila tunakaa tu na kulalamika wengine waje watutoe tulipo au tunarudi kila saa kwake na kumuuliza tufanyeje wakati kila kitu tunacho. Dunia ina watu watatuzi wa matatizo wachache sana na ndio waliofanikiwa. Jitahidi uwe mtatuzi wa tatizo na si mkosoaji na mlalamikaji. Kumbuka wajasiriamaliwengi wanapata mawazo ya kibiashara wakati wanapojaribu kutatua matatizo yanayowakabili katika maisha.

SOMA; USHAURI; Jinsi Unavyoweza Kuondokana Na Changamoto Za Kuendesha Biashara Na Kuweza Kufikia Mafanikio Makubwa

5. Unapofanya mabadiliko ya biashara yako usiende mbali saana na wateja wako, usifanye mabadiliko makubwa sana ambayo yatafanya mteja kuingia gharama, au usumbufu. Mabadiliko yaendehatua kwa hatua. Hebu fikiri teknolojia ya simu, ingetoka kwenye kutumia simu za mezani na kwenda moja kwa moja kwenye Smartphones. Maana kwanza wakati huo hata simu za mkononi zilikua haizifahamiki na waliokua nazo walikua wachache sana. Hata kuongeza bei, ukifanya hivyo ghafla na kukawa na tofauti kubwa ni kwamba utapoteza wateja. Mabadiliko yeyote yatakayomgharimu mteja kwa ghafla hata kama yana nia njema, utapoteza wateja wako. Fikiria mabadiliko makubwa sana, ni sawa kabisa, lakini katika utekelezaji nenda hatua kwa hatua, ili wateja nao waweze kwenda na wewe vizuri.

6. Usiishie kufanya biashara na wateja unaowafahamu pekee. Ukiona unafanya biashara mwaka 1 na wateja wako ni wale unaowafahamu pekee basi ujue upo hatarini sana. Biashara inayokua ni ile inayoweza kuleta wateja wapya mara kwa mara, na wale waliopo wanarudiarudia kufanya biashara na wewe. Ongeza wigo wa wateja.

7. Huwezi kufanya kila kitu wewe. Kama biashara yako inakutegemea wewe kila kitu, hapo huna biashara. Ujasiriamali wa ukweli, ni kuweza kutumia uwezo wa watu wengine (leverage). Ukijishughulisha na kila kitu kwenye biashara yako ukadhani kwamba unaokoa fedha za kuwaajiri watu, ujue ndiounaelekea kubaya sana. Maana kila kitu kikikutegemea wewe, utakosa muda wa kufikiri, kuibua mawazo mapya. Maana ubunifu na mawazo mazuri yanaihitaji uwe na muda mzuri wa kufikiri, sasa kama kila siku huna muda, utaishia kua wakawaida tu. Cha kufanya tafuta watu wenye uwezo kukuzidi wewe wape zile nafasi zinazohitaji utaalamu, na wewe tafuta kitu kimoja ambacho unadhani unaweza kukifanya vizuri kuliko wengine, hapo weka nguvu zako zote, achia wengine wafanye. Napenda kutoa rai kwa wale hasa wenye mpango wa kuanzisha biashara, kua na fikra za kutafuta watu wa kuchukua nafasi zao wakati ili kupata muda wa kufanya mambo mengine kabisa nje ya kampuni. Mfano kama wewe ni MD, au CEO, fikiria nani atakuja kuchukua nafasi hiyo pale biashara itakapokua na uwezo wa kujiendesha, anza kumwandaa mapema. Hii itakupa kua na muda mzuri wa kufikiri mambo mengine mazuri ya kuendeleza biashara.

8. Hakuna kitu cha bahati. Hapa ndio nilipataga shida sana katika kuamini kwamba eti bahati inatengenezwa. Lakini hatimaye nilielewa falsafa yenyewe. Na sasa ni muumini wa kwamba bahati hutengenezwa. Kwa ufupi ni kwamba bahati ni pale maandalizi yanapokutana na fursa. Unapokutana na fursa unakua umejiandaa vya kutosha. Hii ina maana bahati zipo nyingi sana sema tunashindwa kuzipata maana hatuna maandalizi, tunaishia kusema.. “Haikuwa bahati yangu”. Ukikaa tu halafu usubiri bahati utaishia kusema mimi sina bahati. Sasa ngoja nikupe siri moja ya bahati, Ili upate bahati nyingi ongeza maandalizi, ongeza kujifunza vitu vipya usiishie kwenye vile unavyojua tu. Kumbuka fura hutoa upendeleo kwa wale waliojiandaa

9. Katika biashara kuna uchaguzi, aidha uwe mbunifu au ufunge biashara ukafanye kitu kingine. Maana tunaishi katika dunia yenye ushindani mkubwa wa kibiashara. Na Kinachotenganisha biashara moja kuonekana iko juu na nyingine iko mahututi (ICU) ni ubunifu. Unakuta ni biashara 2 au 3 hata 10 zinauzwa bidhaa au huduma sawa. Ila katika hizo kuna moja au mbili ndio zina wateja wengi, cha kufahamu ni kwamba kinachowafanya wawe vile ni ubunifu katika kutoa bidhaa au huduma bora. Na ubunifu huu unafanyika mara kwa mara.

10. Kufanikiwa kwenye biashara ni kutengeneza bidhaa au huduma ambayo wateja watarudi tena na tena. Mfano huduma ya kupiga simu. Mteja ili aweze kuwasiliana itabidi anunue vocha, kila akitaka kuwasiliana atahitaji kununua vocha. Hebu fikiri kama mitandao ya mawasiliano, ingekua inatoa huduma ya kununua vocha mara moja tu basi, ukishanunua ndio unawasiliana milele. Ukweli ni kwamba wangeshafunga ofisi zao kitambo. Kitu kidogo lakini chenye kujirudia rudia kina faida kuliko kikubwa ambacho ni cha mara moja tu. Na hapa ndipo unaweza kushangaa kwanini anayeuza unga, pipi, biskuti anapesa kuliko anayeuza samani za ndani (furnitures). Hapo ndio utaona kwanini Bwana CarlosSlimHelu tajiri namba 2 wa dunia anajihusisha na teknolojia ya mawasiliano ana pesa kuliko anayetengeneza magari ya BMW. Ndio maana hata kwenye biashara za mtandao zinazofanikiwa ni zile zenye bidhaa ambazo hutatumia maramoja tu, bali utahitaji tena na tena.

SOMA; Huyu Ndiye Mtu Ambaye Umasikini Huwezi Kumbugudhi.

11. Wapo wajasiriamali wengi wanaanzisha biashara zao kwenye muda wao wa ziada kabla ya kuacha kazi. Ukijaribu kuangalia wengi wa wajasiriamali kabla ya kua wajasiriamali walikua waajiriwa, waliweza kutumia muda wao wa ziada kuanzisha biashara zao. Hii inawasaidia kutokupata shida sana pale mwanzoni kama ana watu wanamtegemea. Wote tunajua kwamba biashara katika hatua ya mwanzo haitengenezi faida hata kama inatengeneza faida hiyo inatakiwa kutumika kwa ajili ya kuongeza biashara. Kama unafanya kazi ukaacha na hujaanza biashara yako ina maana utaitegemea sana hiyo biashara, wakati mwingine utalazimisha kupata faida pale mwanzoni ili uweze kujikimu, sasa hapo ndipo utajikuta unaharibu biashara. Maana mwanzoni mwa biashara watu hawajikiti kutengeneza faida, bali kutengeneza thamani ya biashara yao kwa wateja. Sasa haimaanishi kwamba hawapo wanaofanikiwa wanaoanzisha biashara kwa kuacha kazi kabla, wapo. Pia usipokua na hekima pointi hii inaweza kukufunga wewe mwajiriwa, ukawa unajifariji, kwamba utaanza kesho, utaanza kesho, kesho yenyewe unajishtukia miaka 15 ndani ya ajira. Ngoja ni kwambie kitu hichi ni ushauri wangu binafsi; ukiona mwajiri amekuongeza mshahara hapo sasa ndipo unatakiwa kuongeza spidi ya kuanza mikakati ya kuondoka, maana hapo ni amekufunga kamba mguu wa pili ili uzidi kutumika vizuri katika hali ya kujiona unapendwa zaidi. Ukiona kwenye ajira uko comfortable.. watchoutplease…

12. Imani sio lile wazo unalimiliki, bali ni wazo linakumiliki wewe. Na ndio maana inakua ngumu sana kuwatoa watu kwenye imani fulani, maana sio wao wanamiliki zile imani bali wanamilikiwa na zile imani. Mtu anatetea sana imani fulani, kwa vile yeye ni milki ya hiyo imani lazima amtumikie bosi wake vizuri. Kama una imani kwenye mambo ambayo sio sahihi ni hatari kubwa sana.

13. Hua tunajiaminisha kwamba mjasiriamali lazima awe na wazo zuri sana la kibiashara, mwishowe tunajikuta tunaona mawazo ya biashara yameisha. Wazo halihitaji kua zuri kivilee, hata lile unalolizarau laweza kua ni ukombozi wako.

14. Janga kubwa katika maisha sio kwamba hatuna nguvu za kutosha, ni kwamba tunashindwa kutumia nguvu tulizonazo. Sio kwamba huna mtaji wa kutosha, la hasha, ni kwamba umeshindwa kutumia mtaji uliona nao. Maana kwanza una imani kwamba mtaji ni fedha tu. Hujui kwamba mtaji namba moja ni muda ulionao, unaoutumia vibaya kwa kulalamikia serikali, halafu huwezi tatua chochote unabaki palepale, unasahau hata ujuzi ulionao ni mtaji mkubwa pia. Chochote unachokifahamu ambacho kinaweza kuwasaidiawengine ni mtaji tosha.

15. Wajasiriamali wengi wanashindwa kwasababu wana mielekeo mingi (toomanydirections) kwa wakati mmoja na mwishowe hawawezi kutekeleza vizuri chochote. Badala ya kulenga katika kufanya vizuri kuhudumia masoko yao makubwa, wanawagawanya watu/wateja wao na muda wao, kwa kujaribu kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyokaribisha Ushindani Kwenye Biashara Yako.

16. Siku za leo gharama na muda wa kuanzisha biashara na kuwa bosi wako mwenyewe zimepungua sana. Mtu anaweza kuanzisha biashara ikasimama ndani ya muda mfupi kuliko ilivyokua huko zamani. Leo hii kuna vitu vingi sana vya kutusaidia kufikisha huduma zetu kwenda kwa wateja kwa haraka. Moja wapo ni mawasiliano. Unaweza kutangaza biashara yako kwa bei nafuu zaidi na ikawafikia watu wengi ulimwenguni kuliko ilivyokuwa awali.

17. Intaneti ni nyenzo kubwa sana, yaani kubwa sana katika biashara. Leo hii dunia ingekua wapi kama intaneti isingekuwepo. Hata usingeweza kusoma haya mambo bila kuwepo intaneti. Hata hziwhataspp, facebook, twitter zote zinategemea intaneti. Leo hii unaweza kufanya biashara ukiwa nyumbani kwako, yaani nyumbani ndio ikawa ofisi yako na ukafanya biashara na dunia, hii ni kwasababu ya intaneti. Unaweza agiza gari toka pande yeyote ya dunia na ikakufikia hapo ulipo. Sasa tambua kwamba hii ni fursa kubwa sana. Sasa hii inatupa funzo kwamba intaneti ni utajiri tunaocheza nao pasipokujua, yaani unacheza na dhahabu halafu unalia umasikini. Mmiliki wa facebook ni tajiri kuliko hata mmiliki yeyote wa Mgodi wa Dhahabu au madini yeyote.

18. Chanzo kikuu kwa watu wengi kuhangaika sana kitaaluma au kimaisha binafsi, ni kukosa lengo (lackoffocus) hujui kwa kujikita ni wapi, unasubiria maisha yakuchagulie. Kuna nguvu kubwa sana kama utakua na focus

19. Pamoja namipango mizuri unayoweza kua nayo kama hamna vitendio, huna tofauti na Yule asiye na mipango kabisa. Watu hawatishwi na mipango, kila mtu anaweza sema mipango yake, lakini je vitendo vinavyoendana na hiyo mipango. Je hayo uliyapanga umeshaanza kuyatenda? Matendo ndio uhai wachemchemu ya kufanikiwa kwako. Hakuna Biashara inayokua imekamilika ikiwa kwenye makaratasi tu. Ondoka kwenye makaratasi anza utendaji. Kua mtu wa vitendo zaidi

20. Hofu ni adui mkubwa sana. Hofu imezika mawazo mengi sana. Hofu ndiyo sababu kubwa ya umaskini wa watu wengi. Watu wengi wameshindwa kuanzisha biashara kwa sababu kubwa ya kuhofia kushindwa na kuchekwa na watu. Ni bora ukashindwa na kuchekwa sasa hivi ukiwa kijana na nguvu zako, kuliko kuja kulazimika kujaribu ukiwa uzeeni, hata ukishindwa huna nguvu tena ya kujaribu. Hujaona mtu anastaafu ndio anaanza biashara, ya hardware ya vifaa vya pikipiki, au anaanza kufuga kuku wa mayai, hujawahi kujaribu, halafu unakuja kuweka pesayako ya mafao uliyokusanya miaka yote ya kutumikia watu. Sasa ukishindwa utaweza kurudi tena ukatumike ulikukusanya tena mafao kwa ajili ya mtaji?. Usikubali hofu ukufanye uje kupata fedheha uzeeni. Jaribu sasa. Wakati uliokubalika ni sasa

Asanteni

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana naye kwa simu 0763 071007 au barua pepedaudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com

Makala imeangaliwa ufasaha wa lugha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali Email: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.Tovuti http://rumishaelnjau.wix.com/editor

Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara - 2

Habari mpenzi msomaji wa mtandao huu wa JIONGEZE UFAHAMU. Natumaini unaendelea vema na karibu tena katika mwendelezo wa makala hii sehemu ya pili. Kama hukuisoma sehemu ya kwanza ya makala hii unaweza kuisoma hapa; Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara –1

Karibu kwenye sehemu ya pili ya makala hii ili upate kujifunza mengi zaidi.

3. Sigara

Ukiangalia paketi ya sigara wameandika uvutaji wa sigara ni hatari kwa maisha yako lakini watu bado hawasikii, mwingine anavuta hata paketi moja ya sigara kwa siku.

Lakini mtu huyo pengine hana hata mtaji wa biashara anaendelea kulalamika na kukaa vijiweni .Kumbe angeweza kuacha au kupunguza kuvuta sigara kila siku na kuweka akiba ya hela hiyo hatimaye kupata mtaji na kuanza biashara ndogondogo.

4. Matumizi ya Simu (vocha)

Mawasiliano ni muhimu sana ndio hatukatai je mawasiliano hayo yana tija kwako?

Kama kweli unataka kujikomboa na kupata mtaji wako punguza matumizi ya vocha kwa mwezi au miezi mitatu uone ni kiasi gani cha fedha unachoweza kupata na kufanya kuwa mtaji wako.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyojitengenezea Dharura.

Vijana wamekuwa na matumizi ya kununua vocha kila siku wengine zaidi hata ya elfu 2000 kwa siku je vocha hiyo inakuingizia? Au mawasiliano hayo yanakuingizia yanabadili maisha yako? yana tija kwako jiulize mwenyewe utapata jibu halafu fanya maamuzi haraka ya kubadilika , punguza matumizi hayo ya vocha kila siku iwekeze hiyo hela unayonunua nayo vocha kila siku uweke akiba ili upate mtaji na uache kulalamika kila siku mtaji uko mikononi mwako amka kijana.

Hivyo basi, kuna mambo mengi sana unaweza kuyapunguza yanayohusiana na somo hili ,punguza safari zisizokuwa na tija ,ununuaji wa vitu hovyo mfano unanunua nguo mpya kila mtindo mpya unapotoka jiulize una nguo ngapi ambazo huzivai na unanunua nyingine ? mtaji uko mikononi mwako ukiamua kupunguza na kuwekeza pesa hiyo utafika mbali.

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

Siri Hii Itakusaidia Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Wa Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi - 2

Habari ndugu msomaji. Ni imani yangu kuwa u mzima na unafuatilia mwendelezo wa makala hii. Wiki iliyopita tuliangalia siri mojawapo ya kuondokana na msongo wa mawazo wa kukosa muda ambayo ni kuandika ratiba ya kazi zako. Ni imani yangu kuwa ulipanga ratiba kwa wiki iliyopita na unaweza kutushirikisha matokeo ya upangaji wa ratiba yalikusaidia kiasi gani kwa kuweka maoni hapo chini. Kama hukusoma makala ya wiki iliyopita isome hapa; Siri Hii Itakusaidia Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Wa Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi.

Inawezekana mara nyingine ulisahau kama uliweka ratiba na kujikuta ukifanya vitu ambavyo si muhimu na viko nje ya ratiba yako. Usikate tama na kuamua kuacha kabisa kuandika ratiba. Endelea kuandika ratiba na kuifuatilia baada ya muda utazoea na kujikuta kila mara unaandika na kukamilisha ratiba yako uliyojiwekea.

Kama ulifanikiwa kuandika ratiba na kuifuata napenda kukupongeza sana. Endelea kufanya hivyo inakupa urahisi wa kukamilisha mipango yako bila ya kuzongwa na mawazo na kuchanganyikiwa. Tuendelee na siri nyingine.

2. Amka mapema asubuhi.

Hakikisha kuwa unaamka asubuhi sana, saa kumi na moja ni muda mzuri. Muda huu ni wa utulivu, akili bado inanguvu na hakunamtu anaweza kukusumbua kwa wakati huu. Angalia ratiba yako kwa siku husika na endelea na kukamilisha majukumu uliyojiwekea kwa siku hiyo. Kama una kazi za kusoma au kuandika basi huu ni muda mzuri sana wa kufanya hivyo kwani akili inakuwa na nguvu.

Ukiamka mapema siku nzima inakuwa ni ya kuchangamsha tofauti na mtu ambaye ataamua kuamka saa mbili asubuhi. Kuchelewa kuamka hukufanya ujisikie mchovu na kushindwa kufanya shughuli kwa ufanisi.

Wengi wetu huamka kwa mawazo tu na sio kimwili. Yaani unatega saa ikuamshe saa kumi na moja lakini kengele ikilia unaizima na kuanza kufikiri mawazo ya kuamka na fikra hizo zinakufanya ukae kitandani mpaka saa mbili asubuhi. Usifanye hivyo, kengele ikikuamsha amka kwakua unafanya hivyo kwa faida yako na ni kwaajili ya kupunguza wingi wa majukumu uliyonayo. Fanya zoezi la kuamka mapema asubuhi wiki hii na uzingatie ratiba yako ya siku.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuishi Maisha Yako Kwa Ukamilifu.

3. Lala masaa ya kutosha.

Kuna tofauti ya idadi ya masaa ya kulala kutokana na umri na aina mbalimbali ya watu. Watoto, vijana na wazee wanatofautiana katika idadi ya masaa wanayotakiwa walale. Kulingana na maelekezo ya wataalamubinadamu mwenye umri wa kati yaani ambaye si mtoto wala si mzee anashauriwa alale muda wa masaa saba hadi nane kwa usiku mmoja. Kupumzika huku ni salama kiafya kulingana na maelezo ya wataalamu. Si vizuri mtu kulala masaa chini ya sita, ingawa hali hii inatofautiana kati ya mtu na mtu.

clip_image002Kama utalala masaa saba na ukasinzia sana mchana basi inamaanisha hukupumzika vizuri hivyo jaribu kuongeza nusu saa. Na inawezekana pia baada ya masaa sita na nusu kuisha usingizi unakuishia. Huwezi kujilazimisha kuendelea kulala kwasababu inatakiwa ulale masaa saba. Amka na uendelee na ratiba zako.

Mapumziko ya kutosha ni mazuri kiafya pia huhuisha akili na mwili na kuvipa nguvu ya kufanya kazi tena.

SOMA; BIASHARA LEO; Hawa Ndio Wateja Rahisi Kuwapata Kwenye Biashara Yako.

Asante kwa kuwa nami naomba tukutane tena wiki ijayo. Endelea kufanyia mazoezi vitu hivi vitatu tulivyojadili na utupe maoni kama kunamabadiliko uliyoyapata.

Kama unaswali, maoni au ushauri usisite kuwasiliana nami.

MWANDISHI: ESTHER NGULWA

MAWASILIANO: 0767 900 110 / 0714 900 110

estherngulwa87@gmail.com

Makala imeangaliwa muundo na lugha fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali Email: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

KARIBU KWENYE SEMINA YA MAFANIKIO KUPITIA BIASHARA MWAKA 2015.

AMKA CONSULTANTS imekuandalia semina ya mafanikio kwenye biashara mwaka 2015. Katika semina hii utajifunza mambo yote muhimu yatakayokuwezesha kuanza, kukuza na kufikia mafanikio kwenye biashara yako. Semina itaanza tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima kwa njia ya mtandao(yaani email). Mwisho wa kujiunga na semina hii ni tarehe 01/05/2015. Wahi sasa kujiunga ili upate maarifa yatakayokuwezesha kufanikiwa kwenye biashara. Kwa maelezo zaidi na jinsi ya kujiunga bonyeza maandishi haya.

Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.

Inawezekana umefika katika hatua ambayo unaona kama ungekuwa na kiasi fulani cha fedha basi matatizo yako yote ambayo yamekuwa yanakusumbua au yanakukabili bila kujali yana umri kiasi gani yangekuwa yamepatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Kama ingekuwa kuwa na fedha ni kupata ufumbuzi wa matatizo tuliyonayo ina maana tungetarajia watu wenye fedha nyingi wangekuwa hawana matatizo kabisa. Lakini katika maisha ya leo baadhi ya hawa watu ambao wana fedha sana ndiyo ambao wana matatizo zaidi kama ya magonjwa, kukosa furaha n.k ukiwalinganisha na wale ambao hawana fedha au wana fedha kiasi kidogo.

SOMA; Najua Umeshasikia Hili Mara Nyingi, Sio Vibaya Ukasikia Tena Na Leo.

Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Kwa maana nyingine fedha haina ubaguzi kwamba wewe ni wa rangi gani au umetoka katika kundi gani la uchumi (mtu masikini au mtu wa daraja la kati au mtu tajiri) au wazazi wako walikuwa na hali gani ya kifedha au hata unafikiri kuwa wewe ni nani (nafasi yako katika jamii).

Fedha haiwezi kubagua kwa kuwa haijui mambo mengi yanayomhusu yule anayemiliki kiasi husika cha fedha. Fedha haijui una kiwango gani cha elimu au maarifa, fedha haina masikio wala macho wala uwezo wa kuhisi. Bali fedha ipo kwa ajili ya kutumiwa, kuwekwa akiba, kuwekezwa.

Kila mmoja wetu anayo haki na fursa sawa kuweka jitihada ya kupata fedha zaidi bila kujali jana yako ilikuwaje. Inawezekana ukaona ni ngumu na kuna changamoto na vikwazo zaidi lakini inawezekana kufanya na kuibadili maisha yako.

SOMA; Njia TANO Rahisi Za Kutangaza Biashara Yako.

Kwa hiyo ni muhimu sana kukaa chini na kutafakari na kufafanua kwa kina ni nini hasa kusudi la wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji. Kuwa na ufafanuzi au maana sahihi ya wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji itakusaidia kuendana vema na tabia hizo kuu tatu za fedha nilizoziainisha hapo juu (kutumiwa, kuwekwa akiba na kuwekezwa).

Mwandishi: Goodluck Moshi

Mawasiliano: Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi

Pia unaweza kutembelea blogu yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.

Makala imeangaliwa muundo na lugha fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na MjasiriamaliEmail: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

Hivi Ndivyo Unavyodhulumu Maisha Yako Wewe Mwenyewe.

Umezaliwa uishi wewe kama ulivyokusudiwa kuishi na kuwa. Usiishi maisha kufurahisha au kuwapendeza wengine tambua kwamba wewe ulivyozaliwa ulipewa uwezo wa kufanya kitu kilichokuleta hapa duniani. Acha kuishi ukitamani kuwa kama mtu fulani, acha kuigiza kuwa kama mtu fulani, acha kufanya mambo kama wengine wanavyofanya, unayo namna yako ya kufanya, unayo namna yako ya kuishi kama ulivyokusudiwa kuwa.

Huenda tangu uzaliwe umekuwa ukisikia sauti nyingi zikikuambia kuwa hauwezi kufanya kitu fulani kwa ajili ya sababu fulani, wengine wametumai mwonekano wako, umri wako kupima kwamba kuna vitu huwezi kufanya na wamekuambia sana habari hizo nawe umezipokea na kuziweka akilini mwako, umeamini hivyo na unaona huwezi kufanya jambo lolote kama walivyokuambia. Ndugu tambua hauwi kama watu wanavyokuambia upo, pengine unapenda kuimba sana lakini jamii yako imekuaminisha kuwa hauna sauti nzuri ya kuimbia nawe umekubali hilo hata ukijaribu kuimba unasikia sauti ikakuambia una sauti mbaya sana, hauwezi kuimba nawe unaiamini hiyo, unaacha kuimba.

SOMA; Kama Unataka Maisha Yako Yawe Bora Na Yenye Mafanikio, Acha Kufanya Kitu Hiki Kimoja.

Ndugu hatuendi hivyo hata kama kila mtu anaona hauwezi , hata kama hakuna hata mtu mmoja anayekuamini kuwa unaweza fanya jambo hilo, kama wewe mwenyewe unaamini kwamba unaweza, unajiamini, endelea kufanya hicho kitu, hata wasipokuelewa leo, wataelewa baadaye sana. Usiache kufanya jambo fulani kwasababu watu wamekuambia huwezi, usiache kufikia ndoto zako kwa kuwa tu umekutana na wasioielewa ndoto yako wakakukatisha tama, ndugu tambua ni wewe umeota/unaota hiyo ndoto hivyo usitegemee mwingine aielewe sana . Umeota wewe, ukiielewa iweke kwenye matendo, ndoto inaweza isieleweke sana lakini ukishaifanyia kazi watakuelewa tu.

Wengi wetu tumeishi maisha yetu tukijitahidi kuwa kama fulani kwa kuwa kuna vitu huyo mtu anavifanya na tunatamani kuvifanya bila kujali kama ndivyo vinavyotupa amani mioyoni mwetu, maana hata kama unapenda hicho kitu kama unakifanya kwa kuwa tu fulani anakifanya huwezi furahia na utatumia nguvu nyingi sana kukifanya, wengine wanafanya vitu fulani kwa kuwalabda wazazi wametaka ufanye , au jamii imemlazimisha afanye au pengine kwa kuwa atapata pesa, lakini hafanyi kwa kuwa ndicho kitu anatakiwa kukifanya, hafanyi kwa kuwa ndicho kitu ameumbwa akifanye na kwa kufanya hivyo wengi wamekuwa wakipata ugumu sana kufanya vitu hivyo kwa ukamilifu maana havipo ndani mwao, nguvu ya kufanya hivyo vitu inatokea nje na si ndani, hivyo lazima waumize akili sana kuweza kupata kitu kipya kila leo.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuishi Maisha Yako Kwa Ukamilifu.

Wewe kama ulivyo una uwezo wa kufanya hicho kitu unachopenda na unachotaka kufanya bila kuangalia kinakulipa nini, kile kitu ambacho ukifanya unafurahia, basi amini unaweza kukifanya bila kusikiliza sauti na kelele zinazokuambia kinyume, zipuuze, chagua na amua usikie sauti gani maishani mwako ili iwe rahisi kwako kufanya kile umeletwa kufanya kwa ukamilifu na kuishi maisha yale umekusudiwa uishi, yaani kuishi wewe na si mwingine.

Angalia ni watu gani wamekuzunguka na maneno yao yamejaa nini? Je ni watu wanaokufanya ujione duni zaidi, ujione huwezi kufanya hilo? Kuwa na marafiki wenye mitazamo sahihi maana mtazamo chanya tu hautoshi, wale ambao wanakukubali na kuamini kuwa nawe una kitu cha kuwaambia, wanaamini kuwa nawe unacho kitu cha maana cha kuwafaa maishani mwao, wanaoweza kukaa chini kukusikiliza na kuona thamani yako, wale watu wanaokufanya uzidi kujikubali kujiamini na kufanya kile unafanya kwa ujasiri zaidi. Watu wenye mitazamo isiyo sahihi si salama sana kwa afya yako labda kama unakaa nao kwa ajili ya wewe kuwasaidia nao waweze kuishi maisha yao, waweze kuwa wao.

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Jambo la msingi ili uweze kuwa wewe maishani mwako ni pamoja na wewe kuwa na muda wa kutosha wa kuwa na wewe ili uweze kujielewa zaidi. Wengi wetu tuna muda wa kutosha kukaa na watu wengine, kuangalia televisheni, kusikiliza radio au kukaa kwenye mitandao ya kijamii lakini hatuna muda na sisi wenyewe, hakikisha unapata muda wa kuwa na wewe kwanza ndipo utakapoweza kujielewa zaidi na hata watuwa je watakuona wewe halisi ukiishi.

Makala hii imeandikwa na Beatrice Mwaijengo Mawasiliano; 0755350772/bberrums@gmail.com Pia unaweza kutembelea blog yake www.jitambueunani.blogspot.com kujifunza zaidi.

Makala imeangaliwa muundona lugha fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na MjasiriamaliEmail: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

Kama Unataka Maisha Yako Yawe Bora Na Yenye Mafanikio, Acha Kufanya Kitu Hiki Kimoja.

AMKA MTANZANIA.!

By Malisa GJ & Makirita Amani,

Ni mara ngapi umewahi kuangalia watu ambao mmekua pamoja au mmesoma pamoja na kuona wao wamefanikiwa sana kwenye maisha kuliko wewe?

Unakutana na rafiki yako ambae mlipotezana miaka mitano au hata iliyopita. Katika kuzungumza kuhusu maisha anakwambia yeye ana kazi au biashara inayolipa sana, ana nyumba mbili, magari matatu na mashamba.

Ukijifikiria wewe huna kazi wala biashara ya kueleweka, bado unaishi kwenye chumba kimoja cha kupanga na usafiri wako ni daladala. Kiatu tangu ununue mwaka jana hujawahi kubadili. Hichohicho ndo ibadani, kwny harusi, msibani, kazini etc. Suruali unazo mbili unabadilisha pale unapopata mtoko.

Unajisikiaje baada ya kukutana na mwenzio mliyesoma nae na amefanikiwa kimaisha.?

Mbaya zaidi unakuta mtu huyo alikuwa hana uwezo sana darasani. Ulikuwa unafaulu zaidi yake. Unapata hasira na kujiona umeshapoteza maisha! Unajiona wewe si mwenye bahati. Unajiona huna future. Unajiona mwenye mikosi. Hiki ndicho kinachotokea kwa watu wengi.

UFANYE NINI?

Ktk maisha yako usijaribu kujilinganisha na mtu mwingine. Kila mtu ana nafasi yake ktk maisha ya kumuwezesha kufanikiwa. Kama si leo basi kesho.

Kama wewe kila siku ni kujilinganisha na wengine, kosa hili ni baya sana na litakugharimu sana kwenye maisha yako. Unaweza kusema kujilinganisha na wengine kunakupa wivu wa maendeleo au kunakufanya ukazane zaidi, huo sio ukweli hata kidogo.

Kujilinganisha na wengine na hasa pale wanapokuwa wamefanikiwa kushinda wewe ndio unazidi kujirudisha nyuma. Unajisikia vibaya sana kuona mtu uliyemfundisha kusoma na kuandika mlipokuwa shule ya msingi, unamfuta makamasi eti leo anatembelea Ford Explorer wewe huna hata baiskeli. Hapa ndipo unapoanza kuona labda wewe una kisirani na yeye ana bahati au kuanza kuhisi alibebwa.

Hapana. Usiwaze hivyo. Kila mtu ni wa pekee. Dunia ina watu zaidi ya bilioni saba, lakini kati ya watu hao hakuna hata mmoja anayefanana na mwenzie. Hata mapacha hawana ufanano wa asilimia 100.

Wewe ni wa pekee, una uwezo mkubwa na vipaji vya kipekee. Hakuna mtu yeyote duniani anayeweza kufanya vitu fulani kama unavyoweza kufanya wewe. Tatizo ni kwamba hujaweza kujua ni jinsi gani utumie vipaji vya pekee ulivyonavyo ili kutimiza ndoto zako.

Ni muhimu kuelewa kuwa duniani hatupo sawa hivyo hatuwezi kufanikiwa kwa usawa. Wewe ni wa pekee (unique) na una vitu unique ambavyo unaweza kuvitumia kupata mafanikio. Unahitaji tu kushikwa mkono ujue potentials ulizonazo na uweze kufanikiwa.

We unadhani Jotti hakupenda kusoma? Hakupenda kuwa na "digrii" au "mastazi" kama wewe? Hakupenda siku moja nae aitwe "Dokta Joti?". Sasa kwanini hakusoma?

Ni kwa sababu elimu kwake haikuwa one of his unique potetials. Yeye alijua potential yake ipo kwenye "comedy" do akawekeza nguvu na akili yake yote kwenye "comedy" na hatimaye amefanikiwa.

Je wewe umejua potential yako iko wapi? Kama hujui huwezi kufanikiwa. Unaforce utangazaji kumbe ur potential ipo kwenye ufundi magari. Unaforce kusomea sheria ili na wewe uitwe "advocate" kumbe potential yako ipo kwenye ualimu.

Matokeo yake unakuwa mtangazaji, au mwanasheria usiye na mvuto. Miaka kumi Hufanikiwi. Kwa sababu umefanya kitu ambacho si potential yako.

Kuna mtu ana kipaji cha ualimu. Akikufundisha unaelewa kuliko mwalimu mwenye uzoefu. Anachohitaji ni kwenda kusomea taaluma tu ya ualimu aweze kusave potential yake. Lakini ukimuuliza anasema "siwezi kusoma ualimu kamwe. Naenda kusoma Sociology"

Anamaliza Sociology anakaa miaka mitano bila kazi. Anatafuta hata mahali pa kuvolunteer hapati. Ni kwa sababu aliserve potential isiyo yake.

Kuna wengine wanaishi kwa kukariri. Umeona umesomea sheria ukafanikiwa, naye anataka akasome sheria eti awe kama wewe. Anaona umesomea uhasibu nae anasema "nataka kusoma uhasibu niwe kama fulani". Acha mawazo potofu. Nani alikuambia maisha yana formular? Usisafirie nyota ya mwenzio. Kila mtu anasafiri kwenye njia yake binafsi.

Kama potential yako ni ualimu, somea ualimu kisha fanya kwa bidii utafanikiwa. Mbona wako walimu wanatembelea "Vorgue" na kuna wahasibu, wanasheria au wengine wanaosomea taaluma zinazoonekana zina hela lakini hawana hata na baiskeli.

Jitambue na jiamini. Tambua potential yako na uanze kuifanyia kazi mapema. Mwanamuziki wa Congo Koffi Olomide alisomea degree ya kwanza ya uchumi. Alipomaliza akaajiriwa bank. Lakini akaona kukaa bank si potential yake. Akaamua kufanya mziki ambao ndio ilikua potentia yake.

Akaanza kuimba na amepata mafanikio kupitia sanaa ya muziki. Baadae akarudi chuoni akasomea "masters" ya uchumi ili aweze kufanya kazi yake ya muziki vizuri. Na amefanikiwa sn.!

Sasa wewe unajua potential yako ipo kwenye kucheza soka lakini unalazimisha shule. Unaishia kufeli. Umefeli form four lakini hukubali unarisiti mara tatu. Baadae unapata "credit" na kwenda form five. Unajilazimisha kukariri na inafika chuo kikuu.

Unafurahi kuwa sasa na wewe ni mwanachuo. Unasomea degree ya Marketing. Hujui hata Marketing ni kitu gani lakini unaforce kisa umesikia wati wakisema "Marketing ina hela balaa"

Unamaliza na kuishia kutembea na vyeti juani miaka mitano. Wenzio uliokuwa ukicheza nao soka wapo TP Mazembe au timu nyingine kubwa na wanafanya vzr. Wewe uling'ang'ania "digrii". Nani alikuambia "digrii" ndio njia ya mafanikio? Muulize Wyne Rooney wa Manchester kama ana digrii au diploma? Acha kukariri maisha.!

Kila mtu anasafiri kwenye njia yake binafsi. Kuna ambao watafanya kazi na kufanikiwa sana, kuna ambao watafanya biashara na kufanikiwa mno. Pia kuna wengine watatumia vipaji vyao na kufanikiwa pia.

Muhimu ni kujua njia yako ya kufanikiwa ni ipi. Unapojaribu kujilinganisha na watu ambao wako kwenye njia tofauti hujitendei haki wewe mwenyewe.

Kama hujafanikiwa kama wenzako walivyofanikiwa huenda hujajua ni kitu gani unachofanya kwenye maisha yako. Huenda hujajua ni kitu gani cha kipekee unachoweza kufanya na ukafanikiwa sana. Na kwa asilimia kubwa huenda unaiga maisha ya watu wengine.

Usipende kujilinganisha na mtu. Jilinganishe na wewe mwenyewe. Tumia mfano wa Christian Bella aliulizwa na waandishi wa habari anapenda kuwa kama nani. Akajibu "napenda kuwa kama Christian Bella". Hii ni kwa sababu anajikubali. Na hii imemsaidia kufanikiwa sn kwny muziki wake.

Lakini wewe kila siku ni kujilinganisha na wengine. Eti fulani alimaliza chuo akaenda kugombea ubunge akashinda, na mimi nikimaliza chuo naenda kugombea ubunge kule kwetu. Acha ujinga. Utapata kura yako na ya girlfriend wako. Kama potential yako ipo kwenye biashara kwanini unalazimisha kufanya siasa?

Siri ya mafanikio ni kutambua potential yako na kuanza kuitumia kupata mafanikio but pia kujiamini wewe mwenyewe. Kuanzia leo anza kujilinganisha na wewe mwenyewe. Usijilinganishe na mtu.

Jiulize hicho unachofanya kwenye maisha yako je unakifurahia? Kumbuka ni vigumu sana kufanikiwa kama unafanya kitu ambacho hukipendi. Jiulize ni vipaji gani ulivyonavyo, jua ya kwamba una uwezo mkubwa na ubunifu wa hali ya juu. Vijue na kutumia vitu hivi ili kuboresha maisha yako.

Shindana na wewe mwenyewe. hakikisha kila siku mpya unakuwa bora zaidi ya siku iliyopita. Unapomaliza siku ya leo hakikisha umefanya vitu unavyofanya kwa ubora zaidi ya ulivyofanya jana. Kwa njia hii utajikuta ufanisi wako unaongezeka kila siku na mwishowe unapata mafanikio makubwa.
Kama unafanya vitu kwa mazoea tayari upo nje ya njia ya kuelekea kwenye mafanikio. Kama sababu pekee inayokufanya uende kwenye shughuli zako leo ni kwa sababu jana ulienda upo kwenye hatari kubwa.

Hakikisha kila siku una kitu cha kuongeza kwenye ujuzi na ufanisi wako wa kazi. Hakikisha kila siku kuna kitu kipya unajifunza ambacho kitakusaidia kwenye maisha yako. Tambua "potential" zako na uzitumie.

AMKA MTANZANIA.!

Malisa G odlisten J || Your Partner In Critical Thinking.!

Credits kwa Makirita Amani ambaye ameandika sehemu kubwa ya makala hii nami nikongezea tu.!

Huu Ndio Uwekezaji Bora Zaidi Unaoweza Kuufanya.

Uwekezaji kama tunavyofahamu ni njia ya kupata kipato ambayo imekuwa ikihubiriwa na watu wengi sana kuanzia mashuleni, vyombo vya habari na hata mitaani. Lakini watu wengi wamekuwa wakitaja vitu vya kufanya hasa katika kuwekeza pesa kama mtaji. Sipingani nao katika hilo lakini kabla ya kuwekeza katika pesa lazima kwanza uwekeze katika hili. Najua utashangaa sana na kudhani kuwa ningekutajia eneo la kuweka pesa zako, la hasha.

Ukweli ni kwamba kabla hujawekeza katika pesa wekeza katika akili yako. Ukiwekeza katika akili yako kamwe hutafilisika, kwa sababu kuwekeza kwingine kabla ya akili ni sawa na kucheza masumbwi bila kujiandaa, ni lazima tu utashindwa tena katika mizunguko ya awali kabisa. Ubongo wako ndio kompyuta yenye nguvu na kasi zaidi kuliko zote hapa duniani. Lakini kama vile kompyuta inavyofanya kazi kwa kuelekezwa ndivyo na akili yako inavyofanya kazi kwa kuelekezwa pia. Kama utaelekeza akili yako ikuletee utajiri italeta utajiri, kama utaelekeza ikuletee umasikini vile vile itafanya hivyo. Kama utahitaji huzuni ndivyo na akili yako itakavyokuletea. Kila kitu kinaanza katika akili yako. Kila utakachowaza ndivyo utakavyokuwa.

SOMA; Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

Namna ya kuwekeza katika akili

Waza katika uwezekano (possibility thinking)

Ili uweze kufanikiwa ni lazima ujaze akili yako na vitu vizuri vyenye kukujenga na si kinyume chake. Huhitaji mtu kuwekeza katika akili yako kama hujaamua mwenyewe moyoni mwako kuwekeza. Kwanza kabisa ondoa takataka zote zilizopo akili mwako kwa kuwaza uwezekano wa kufanikiwa yaani kuwaza katika mambo chanya zaidi na kuachana na mambo hasi. Pili tafuta marafiki ambao watakujenga katika kukukosoa kwa mazuri, kukutia moyo pale unapokuwa katika hali ngumu au unapotaka kujaribu jambo jipya. Kama marafiki ulio nao ni wale wa kukurudisha nyuma basi unakosea sana na inakubidi ubadili jeshi lako la marafiki. Bila kufanya hivyo akili yako itajazwa kukata tamaa, kukwazwa na hata kurudishwa nyuma na mafanikio kuwa ndoto za Ali Nacha kwako.

SOMA; Watu Hawa Wanakurudisha Nyuma.

Hudhuria semina za kuelimisha

Jitahidi kuhudhuria semina za uwekezaji na za kujenga tabia. Jitahidi kuhudhuria semina za kujenga tabia kwanza kabla hujaanza kuhudhuria za kuwekeza katika fedha kwani kama hujawekeza katika kubadili baadhi ya tabia ambazo ni adui kwa mwekezaji kama nidhamu ya fedha na uongozi, utakuwa sawa na kujenga nyumba nzuri bila msingi imara.

Jifunze kwa watu waliofanikiwa

Hakuna mtu aliyefanikiwa kwa kufanya kila kitu peke yake. Unahitaji kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa hasa kwenye fursa, changamoto, biashara na hata tabia zao. Usiende kwa mtu aliyefanikiwa ili ukaombe fedha kwani tatizo lako sio pesa bali elimu kuhusu pesa (financial education). Watu wengi waliofanikiwa ni watu ambao wako tayari kusaidia watu wengine waweze kufanikiwa. Watu waliofanikiwa huonekana kuringa ama kujisikia lakini sababu kubwa ni kutingwa kwao na vitu vingi vya kufanya. Kama wapo wanaoringa basi ni tabia zao tu hivyo usiogope kuwafuata ili ujifunze kutoka kwao.

SOMA; Kozi 1100 Unazoweza Kujifunza Bure Kupitia Mtandao.

Soma sana vitabu

Kama kuna njia ya nzuri na ya kwanza kukushauri katika kujenga akili yako ni kusoma vitabu. Narudia tena soma vitabu sana kadiri unavyoweza. Kwa mara ya kwaza itaonekana ni kazi ngumu lakini ukiwa na nia ya dhati ya kujenga akili yako basi hili litakuwa rahisi na ukizoea itakuwa rahisi zaidi. Soma vitabu vya uwekezaji, tabia, uongozi na hata vitabu vya kutia moyo (inspirational books). Soma kila siku na kufanyia kazi ulivyosema. Matatizo yote ya dunia hii siyo mapya na karibu yote yashapata utatuzi na watu wakaandika katika vitabu. Kumbuka pia ‘’Mtu anayetoa vya mfukoni kwake na kuwekeza katika akili yake hatafilisika kamwe’’. Naamini na wewe utafanya hivyo, watu waliofanikiwa husoma sana vitabu na kusikiliza ‘’vitabu sauti’’ (audio books) kila siku. Anza leo na utaona mafanikio mlangoni kwako. Kumbuka hakuna njia ya mkato ya kufanikiwa na kila kitu kina gharama zake ambazo lazima uwe tayari kuzilipa ili ufanikiwe.

Nakutakia kila la kheri na uwekezaji mwema.

Makala hii imeandikwa na Nickson Yohanes ambae ni mjasirimali na mhamasishaji. Unaweza kuwasiliana na naye kwa: simu: 0712 843030/0753 843030 Barua pepe: nmyohanes@gmail.com Pia unaweza kutembelea blogu yake: www.lifeadventurestz.blogspot.com kujifunza zaidi.

Imesahihishwa kwa kiswahili sanifu na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali barua pepe: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu The One Thing.

Habari rafiki, ni matumaini yangu waendelea vizuri. Wiki hii tunaendelea na utaratibu wetu wa kushirikishana mambo 20 nilijifunza kwenye kitabu. Leo tunajifunza kutoka kwenye kitabu kinaitwa The ONE THING- the surprisingly truth behind the extraordinary results. Kitabu kimeandikwa na Gary Keller pamaoja na Jay Papasan.

Kwa ufupi kitabu hiki ni kizuri sana. Hupaswi kukosa mambo ya wiki hii. Karibu tujifunze.

1. Muda hausubiri mtu. Muda hauna cha VIP , maskini au tajiri hauna wa kumuogopa wala wa kumuonea huruma. Kwahiyo tunapaswa kuuthamini sana muda maana ni bidhaa hadimu sana na tumepewa bidhaa hii sawa kwa watu wote. Tofauti zetu zinatokana na jinsi tunavyotumia muda tulionao. Muda haukusubiri ufanikiwe kwanza ndio uzeeke, au hausubiri kwanza ustaafu ndo ukaanze biashara. Hata ukilala na usifanye chochote muda unayoyoma. Time waits for no one.

SOMA; Fanya Mambo haya matatu kuwa na maisha bora na yenye furaha.

2. Unapomuoana mtu ana maarifa mengi ujue imemchukua muda kujifunza kufikia hapo. Ukiona mtu amefanya vitu vingi au amefanikisha vitu vingi ujue kwamba alitumia muda fulani kuvifanikisha, na vilevile Ukiona mtu mwenye fedha nyingi ujue imemchukua muda kuzipata. Suala kubwa hapa ni muda. Kila kitu kinahitaji muda, hakuna kitu cha kulala usiku na kuamka asubuhi umekua tajiri hakuna kitu kama hicho. Mafanikio yeyote yanahitaji muda. Unaowaona wamefanikiwa iliwachukua miaka kadhaa kufika hapo walipo. Walikua na upeo wa mbali wa miaka kuanzia 20 mbele.. wakati wengi wetu hata mwakani hatujui tutakua wapi tunaishi maisha ya pata potea, kutafuta na kula kuoa au kuolewa na kujenga kanyumba kamoja na kagari kwisha kazi.. Halafu tunajiona vidume kweli.. na kukaa na kusema usiwaone wale kina Bill gates ni Freemason wale mali zao ni za kishetani… Tuna sahau kwamba wenzetu walikua na Malengo na mipango ya muda mrefu na kila siku walikua hawapotezi muda kuyafanyia kazi malengo yao. It’s just a matter of time

3. Kampuni nyingi zilizofanikiwa zinakua na bidhaa moja au huduma moja ambayo ndiyo inawafanya wajulikane na kuwatengezea fedha nyingi. Issue sio kua na bidhaa nyingi kama utitiri. Chagua kitu kimoja weka nguvu zako zote hapo lazma utaona mafanikio. Sasa kwetu unataka uuze mchele wewe, spear za pikipiki, duka la vyombo, sijui kibanda cha mpesa unataka. Fanya kitu kimoja kwanza kikishafanikiwa anza kingine. Success is sequential, not simultaneous.

4. Hakuna mtu anayefanikiwa peke yake. Kila mtu aliyefanikiwa katika Nyanja yeyote atakwambia kuna mtu aliyemshawishi, alimhamasisha au alimfunza hadi imepelekea kufika hapo alipo. Hata Albert Einstein mwanasayansi maarufu duniani, alikua akipata uongozi na maelekezo kutoka kwa bwana Max Talmud kwa muda wa miaka sita. Na ndio maana utasikia watu wakisema mentor wangu ni fulani, mentor wangu, mentor wangu.. je na wewe unayo mentor? Tafuta kocha na kaa chini ya kocha. Kumbuka No one is self-made. No one succeeds alone. No one.

5. Waliofanikiwa hawafanyi vitu tofauti la hasha wanafanya kwa utofauti. Wana jicho la umuhimu. Wanatulia na kuamua kipi ni cha muhimu katika maisha yao na ndicho wanachokipa nafasi kiendeshe maisha yao. Wanaofanikiwa Wanafanya kwanza vile vitu ambavyo wengine wanapanga kufanya baadaye, na ubaya ni kwamba hiyo baadaye hua haifiki inabaki tu baadaye. Achievers always work from a clear sense of priority.

SOMA; Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara -1

6. Orodha ya vitu vya kufanya (To do list) usipokua makini inaweza ikakupleka nje ya kuafanikiwa. Kwanza orodha ya mambo ya kufanya ni vitu vile tunavyodhani tunahitajika kufanya. Jambo la kwanza linalotokea kwenye orodha mara nyingi ni lile lililoanza kukujia kichwani. To do list nyingi ni kwa ajili ya kutufanya tuwepo tu(Survival list) , ni orodha ya kukufanya umalize siku yako na kujiona kwamba umefanya kazi..yani umeweza kufanya yote ulopanga kwenye orodha unajihisi umefanikisha mambo sana. Instead of a to-do list, you need a success list – a list that is purposefully created around extra ordinary results. Success list au orodha ya mafanikio ni ile inayojikita kwenye shughuli zenye matokeo makubwa na shughuli zenyewe ni chache tu. The majority of what you want will come from the minority of what you do. Kwisha habari

7. Kuwa bize au kua na mambo mengi ya kufanya hakumaanishi kufanikiwa. Mara nyingi tunapenda watu watuone kwamba tuko bize, tuna mabo mengi ya kufanya. Je umewahi kujiuliza toka uwe bize umepiga hatua gani ya maana kulingana na ubize wako? Don’t focus on being busy; focus on being productive. Allow what matters most to drive your day.

8. Jifunze kusema Hapana. Sio kila kitu unakubali tu, sio kila wakati unaawambiwa fanya hivi au vile na wewe unakubali tu. Mara nyingi vitu vya namna hiyo vinakujia ili kutimiza ndoto au mafanikio ya wengine. Jifunze kusema hapana, mpaka pale umemaliza kufanya jambo la muhumi kwanza. Mara nyingi hasa wafanyakazi walio ajiriwa wanadhani kukubali kila kitu kinachotoka kwa boss ndo unakua mfanyakazi bora au ndo utaambiwa uko flexible. Flexible wapi … wakati unajimaliza mwenyewe. utajikuta ni mtu wa kufanya vitu vya emergency tu… Usikimbilie kupata sifa za muda tu..ukaja kujutia maisha yako. Jifunze kusema hapana hata kwa boss wako. Mwanzoni ataweza asikuelewe lakin ipo siku utakua mfano, kwamba ni mtu unayejua kuweka vipaumbele mtu unayejua kusimimamia jambo lenye kipaumbele bila kujalisha ni dharura gani imetokea.

9. Kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja (Multitasking) ni uongo. Hii imekua dhana kila sehemu, utasikia watu wakijivunia mimi nafanya multitasks. Imefika mahali mpaka kwa waajiri multitasking imekua ni moja ya sifa ya mtu anatakiwa awe nayo ili kuajiriwa. Yaani wakati unaandika ripoti muda huhuo uwe unamhudumia mteja na tena uwe unaongea na simu. Ukifanya hivyo lazima utashindwa kimoja wapo au vyote, au utaishia kuapata matokeo ya kawaida sana. Katika ulimwengu wa leo ambapo unapimwa kwa matokeo (results/impacts) na sio kwa kazi uliyofanya Multitasking inawazika wengi sana. Ili uwe na matokeo makubwa fanya jambo la muhimui kuliko yote weka nguvu na umakini wako hapo. Hakikisha umemaliza alafu nenda kwenye jambo lingine. It’s not that we have too little time to do all the things we need to do, it’s that we feel the need to do too many things in the time we have.

10. Hatupaswi kuogopa mambo makubwa. Kwa kujua au kutokujua wengi wetu tumekua tunaogopa mambo makubwa tukidhani ni mabaya kumbe sio kweli. Mfano mtu anaogopa kuwa na mawazo ya kumiliki ndege, kumiliki makampuni makubwa duniani, akidhani kwamba ni mbaya au atapata madhara mabaya. Utasikia mtu anasema sasa pesa zote hizo nipeleke wapi? Mimi nataka tu za kunitosha sitaki presha mimi. Ukiwa na mawazo hayo ujue wewe ni mbinafsi (selfish) maana unajifikiria wewe tu. Huwazi kupata zaidi ya unachohitaji ili kuwasaidia wengine, mwisho wa upeo wako ni wewe kupata tu. Angalia kina Bill gate fedha walizonazo asilimia kubwa wala hatumii yeye. Anatumia kuwasaidia wengine katika sekta ya afya, kilimo n.k Ana malengo ya kufuta kabisa baadhi magonjwa yaliyoitesa dunia kama polio, malaria, ebola n.k. Ipo miradi mingi sana ya kilimo inayofadhiliwa na Bill Gate, na kiu yake kubwa nikuona wakulima wadogo wakiongeza vipato vyao kaika hali endelevu, mimi mwenyewe nimekua nikisimamia moja ya miradi ya kilimo inayofadhiliwa na Bill Gate. Don’t fear big. Fear mediocrity. Fear waste. Fear the lack of living to your fullest. “People who are crazy enough to think they can change the world are the only ones who do.”

SOMA; Huu Ndio Ukomo Unaojiwekea Wewe Mwenyewe.

11. Usiogope kushindwa maana ni sehemu ya safari yako ya kufanikiwa . Tazama kushindwa kwako kama shule ya kujifunzia alafu songa mbele. Mtu mmoja aliwahi sema hivi “ if you want to double your success, then you have to double your failures”. Akimaanisha kwamba kama unataka kupata mafanikio mara dufu, uwe tayari kushindwa maradufu. Maana katika kushindwa ndio unajua ipi sio njia sahihi na kuanza kutafuta njia sahihi.

12. Ubora wa maisha yako utatokana na maswali unayojiuliza. Unaweza jiuliza kwanini tujikite kwenye maswali wakati kwa kawaida hua tunahangaikia kupata majibu. Ni kweli Wengi tunawaza kupata majibu. Na mimi nakuuliza majibu ya kitu gani? Kama huna mawasli? Ukweli ni kwamba ubora wa majibu unatokana na ubora wa maswali. Hata waliobadilisha maisha yao, au waliobadilisha ulimwengu walianza kwanza kwa kujiuliza maswali makubwa na wakaanza kuyatafutia majibu. Je hapo ulipo ndipo ulipaswa uwepo? Maisha unayoishi ni ya kwako? Je kusudi la wewe kuwepo hapa duniani ni nini? Je unafikiri kama pangekua hakuna kikwazo chochote, na una kila kitu ili kufanya chochote au kupata chochote ungefanya nini? Au Ungetamani kua na maisha gani? Anza kujiuliza maswali hayo na mengine. Ukiona umekerwa ujue somo limeingia na uwezo wa kupata majibu unao. Fanyia kazi uone kama maisha yako yatabaki kama ulivyo. Great questions are the path to great answers.

13. Maisha ndio mwajiri wako mkuu, utakachopatana nae ndicho atakachokupa.. Unapopatana mshahara na mwajiri wako ndicho atakachokupa. Sasa cha ajabu umepatana mshahara na mwajiri baada ya muda unalalama mshahara mdogo. Kwani hukulijua hilo wakati wa mapatano? Bahati nzuri nimewafanyia watu wengi mahojiano ya kazi (job interview), na mara nyingi swali la mshahara linaulizwa mwishoni, na lengo lake kubwa ni kutaka kujua huyu mtu anajitathimini vipi. Yeye mwenyewe anajithaminisha je? Sasa wengi wakiulizwa swali la mshahara anajibu kwamba nitakua tayari au nitaridhika kwa mtakachonipa. Au anataja kiwango cha chini sana. Mimi mwenyewe niliwahi kukosa kazi kwa kutaja mshahara mdogo. Nikidhani ndo nitaonekana ninafaa au nitakua nimeangukia kweny bajeti yao. Duuh kwa masikitiko ndo nikawa nimejimaliza mwenyewe. Sasa wanachojiuliza waajiri ni kwamba kama mtu huyu haoni thamani yake sisi je tutawezaje? Sasa turudi kwenye pointi yetu ya msingi, Maisha ndio mwajiri wako, utakachopatana nae ndicho atakachokupa. Usiyaambie maisha nitakubaliana na chochote utakachonipa. Tambua thamani yako patana na mwajiri wako (maisha) ubora wa vitu unavyotaka.

14. Maisha yenye kusudi (Life with purpose) ndio maisha yenye furaha. Kama hujui kusudi lako hata ufanikiwe vipi huwezi furahia. Live with purpose and you know where you want to go.

15. Kuishi Maisha yenye vipaumbele (Live by priority). Tunaweza kuwa na kusudi la maisha, lakini tukikosa vipaumbele itakua ni pata potea. Kipaumbele au priority ina tafsiri kadhaa kama “kitu cha muhimu zaidi”, “kitu cha msingi”, “kitu cha kwanza”, “kitu cha juu” kitu kikuu” n.k Unaweza kua na tafsiri nyingi lakin zote zitalenga kaitka kitu kimoja kinachopaswa kutangulia ili kurahisisha vingine au hata kufanya hivyo vingne visiwe vya muhimu kivile. Kua na ndoto au malengo makubwa mengi sio kwamba ndo kufanikiwa, la hasha. Wengine wanajiuliza sasa mbona nina vipaumbele vingi, lakin unasahau kwamba katika vipaumbele ulivyonavyo ikichimba ndani zaidi una kimoja ni cha muhimu zaidi. Anza nacho hicho. The purpose without priority is powerless

SOMA; Kama Hutaki Kuwa Na Maadui Fanya Kitu Hiki Kimoja.

16. Kusudi la furaha. Ukweli ni kwamba kila tunachofanya kwenye maisha ni ili tupate furaha. Furaha ndio bidhaa ambayo imekua ukitafutwa na watu wengi sana, lakin ndio bidhaa ambayo wachache sana wanafanikiwa. Tatizo ni kwamba tunafikri furaha ni jambo la kufikia, yaani pale tunapopata kitu fulani,( kama mke, mume, mototo, nyumba, gari au kufaulu) ndo tunatakiwa kufurahi. Ndio maana ukipata kitu kile unafurahia kwa muda kidogo tu halafu unaanza kutafuta kingine ili upate furaha tena. Unapaswa kufurahia kila hatua unayopita kuelekea mafaniko. Kuna mtu aliwahi kusema hakuna njia ya mafanikio, bali mafanikio ndio njia. Kama mafanikio ni njia, basi tunapaswa kuwa na furaha kwenye njia hiyo. Happiness happens on the way to fulfillment.

17. Weka malengo yako kwenye kataratasi na uyaweke karibu na wewe. Watu wengi hatuna utaratibu wakuandika malengo yetu, yaani malengo yanakua kichwani tu, tena malengo mengi yanawekwa kipindi cha mwaka mpya, mwezi January ukiisha ulishasahau ulipanga nini. Swali la kujiuliza ni vitu ngani viko karibu na wewe zaidi? Wengi wetu simu ndo vitu vya karibu, simu ndo kitu cha mwisho kua nacho kabla ya kulala na cha kwanza kukishika kabla ya kuanza siku. Malengo yako ndo yanapaswa kua karibu na wewe kuliko unavyodhani. Kabla ya kulala yasome, kabla ya kuanza shughuli nyingne yasome. Kufanya hivyo kunaweka akili yako kua kwenye mstari sahihi wa kuhakikisha unajikita kwenye vitu vyenye mchango kwenye malengo husika. Pia utavutia watu au mazingira ambayo yanaendana na malengo yako hata yale ulodhani ni magumu utashangaa fursa zinafunguka hatua kwa hatua. Fanya hivyo ujionee mwenyewe

18. Dereva wa maisha yako ni wewe chukua umiliki wa matokeo yako (Take ownership of your outcomes). Wengi wetu tunaishi kama abiria kwenye maisha, halafu tunashangaa tunakoelekea, au tunalaumu kwa yanayotokea. Sasa acha kua abiria wa maisha yako, nenda kwenye kiti cha dereva chukua usukani wa masiha yako. Wajibika kwa matokeo unayopata.

19. Vitu vinavyozuia mafaniko ya mtu mara nyingi sio vile asivyovijua bali ni vile anavyovijua ambavyo sio kweli. Cha ajabu tunafahamu vingi sana. Ila vingi kati ya hivyo ni vya uongo na ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo. Halafu cha ajabu kingine vile vya uongo ndo tumeweka imani yetu huko, na ndivyo vinaamua maisha yetu. Kabla hujangundua usijokijua, anza kugundua unachokijua ambacho sio sahihi.

20. Jitahidi kuzungukwa na watu watakao kunyanyua juu zaidi. Ukweli ni Wengi tunapenda kukaa na watu tunaowazidi ili watuone vichwa kwelikweli. Tunapenda makundi ambayo sisi ndo tunakua wazungumzaji wa kuu tunaomiliki mazungumzo, kila ukisema uantaka watu waseme ndio mzee. Sasa kuna habari sio nzuri kama unatabia kama hiyo. Maana wewe ni wastani wa watu 5 wanaokuzunguka. Kama umezungukwa na vilaza 9 wewe utakua wa 10. Njia pekee ya kutoka hapo ulipo ni kuzungukwa na watu waliofanikiwa kukuzidi wewe ambapo utajifunza mbinu walizotumia kufika waliko. Sio lazima ukamtafute Bill gate au Buffet, vipo vitabu vizuri vinavyoelezea walivyoanza mpaka waliko fika. Zungukwa na vitabu vya watu wakubwa waliofanikiwa. Chimbua maarifa ya watu hao na tendea kazi unachojifunza, uone kama utabaki ulipokua .

Asanteni sana tukutane wiki ijayo. Kama utapenda kupata kitabu hiki cha The ONE THING wasiliana nami. Nitakupatia bure kabisa.

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana nae kwa simu 0763 071007 au 0658 587029 au email daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Huu ni wakati ambao karibu kila mtu anahitaji kuingia kwenye biashara. Haijalishi mtu ameajiriwa au hana ajira, haijalishi kiwango cha elimu mtu alichonacho na wala haijalishi umri wa mtu, kwa sasa kila mtu anahitaji kuwa kwenye biashara.

Ajira zimekuwa za shida kupatikana na hata wale wanaozipata bado haziwawezeshi kuyamudu maisha. Changamoto ni nyingi sana. Njia ya uhakika ya kuweza kupambana na changamoto hizi ni kuingia kwenye biashara,

Mazingira ya kuingia kwenye biashara nayo yamebadilika pia. Tofauti na zamani ambapo ilihitaji mtu kuwa na uwezo mkubwa sana wa kifedha ndio aweze kuingia kwenye biashara, sasa hivi unaweza kuingia kwenye biashara kwa mtaji kidogo sana.

Pamoja na umuhimu huu wa kuingia kwenye biashara na urahisi wa kufanya biashara, bado kuna changamoto kubwa sana wkenye biashara. Biashara nane kati ya kumi zinazoanzishwa zinakuwa zimeshakufa ndani ya miezi 18. Na hata zile ambazo zinapona kipindi hiki, nyingi hazifikii mafanikio makubwa.

Watu wengi wanaweka juhudi kubwa sana kwenye biashara ila bado hawaoni mafanikio waliyotarajia. Hili linawaangusha wengi sana na wengi kukata tamaa.

Matatizo haya mengi yanatokana na kukosekana kwa elimu sahihi ya biashara, kukosa mtazamo sahihi wa kufanikiwa kwenye biashara, kutokujua mbinu za mafanikio kwenye biashara na kufanya biashara kwa mazoea.

Ili kuwasaidia wafanyabiashara na wale ambao wanapanga kuingia wkenye biashara kuweza kuondokana na changamoto hizi, AMKA CONSULTANTS imeandaa SEMINA YA MAFANIKIO KWENYE BIASHARA 2015. Semina hii itakupatia wewe elimu sahihi, mbinu muhimu na mtazamo sahihi utakaokuwezesha kufanikiwa kwenye biashara yako.

Hii sio semina ya kukosa kwa sababu imejaa mambo mengi ambayo hujawahi kuyapata sehemu nyingine yoyote.

Semina hii imeandaliwa kuweza kukidhi mahitaji ya kufanikiwa kwenye biashara kwa mazingira yetu ya kitanzania. Semina hii itakuwezesha wewe kutoka hapo ulipo sasa na kupiga hatua kubwa sana kibiashara.

Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao na itaendeshwa kwa kipindi chote cha mwezi wa tano.

Washiriki wa semina hii watatumiwa email ya mafunzo kila siku asubuhi, kupata nafasi ya kuisoma na kuweza kuuliza swali popote ambapo hajaelewa. Email hizi zitakuwa na mafunzo yaliyofanyiwa utafiti w akina pamoja na mifano ambayo itamwezesha mshiriki kpata mawazo tofauti anayowez akuyatumia kwenye biashara yake na akafanikiwa sana.

Semina hii itafundisha mambo yafuatayo;

SEMINA YA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA.

Anza, kuza na fanikiwa kupitia biashara.

Yatakayofundishwa;

1. Utangulizi

1.1. Huu ni wakati mzuri wa wewe kuwa kwenye biashara.

1.2. Unawezakufanikiwa kwenye biashara.

1.3. Utakachokipata kwenye kozi hii.

2. Wazo la biashara

2.1. Biashara sahihi kwako kufanya

2.2. Jinsi ya kupata wazo bora la biashara

2.3. Jinsi ya kuboresha wazo lako la biashara

2.4. Baadhi ya mawazo ya biashara.

3. Mchanganuo wa biashara.

3.1. Umuhimu wa mchanganuo

3.2. Vitu muhimu vya kuweka kwenye mchanganuo wako

3.3. Udhaifu na uimara wako

3.4. Utafiti wa biashara yako

3.5. Ushindani.

3.6. Kuajiri wasaidizi bora kwenye biashara yako.

4. Mtaji na vyanzo vyake.

4.1. Aina za mtaji unaohitaji kwenye biashara

4.2. Mtaji wa fedha na vyanzo vyake

4.3. Njia bora za wewe kupata mtaji wa biashara.

5. Urasimishaji wa biashara

5.1. Umuhimu wa kusajili biashara yako.

5.2. Aina za usajili na faida zake

5.3. Hatua za kusajili biashara yako

5.4. Umuhimu na jinsi ya kulinda biashara yako.

6. Thamani ya biashara yako

6.1. Maandalizi ya bidhaa au huduma

6.2. Upatikanaji na upakiaji wa bidhaa au huduma

6.3. Upangaji wa bei.

7. Masoko na uuzaji.

7.1. Chagua soko la biashara yako

7.2. Mpango bora wa kutangaza biashara yako.

7.3. Njia rahisi za kutangaza biashara yako.

7.4. Mbinu za kuongeza mauzo kwenye biashara yako.

8. Mzunguko wa fedha.

8.1. Mauzo na faida.

8.2. Gharama muhimu za biashara

8.3. Gharama za kuepuka kwneye biashara

8.4. Kujilipa wewe mwenyewe.

8.5. Hesabu za fedha na umuhimu wa mhasibu.

9. Huduma kwa wateja.

9.1. Lengo la biashara ni kutengeneza wateja.

9.2. Jinsi ya kutoa huduma bora kwa mteja.

9.3. Mfanye mteja atangaze biashara yako.

9.4. Mteja ni mfalme na mwisho wa ufalme wake.

10. Changamoto za biashara.

10.1. Changamoto zinazoua biashara nyingi

10.2. Umuhimu wa mabadiliko

10.3. Mbinu za kufufua biashara inayokufa.

11. Mafanikio ya biashara yako

11.1. Jifunze kila siku

11.2. Matumizi mazuri ya muda

11.3. Kujihamasisha mwenyewe

11.4. Mafunzo kwa wafanyakazi wako

11.5. Usimamizi mzuri wa biashara yako.

11.6. Kununua uhuru wako kutoka kwenye biashara yako.

Gharama za kushiriki semina hii ni tsh elfu 30(30,000/=), ili kupata nafasi ya kushiriki semina hii tuma fedha za kushiriki kwa Mpesa 0755953887 au tigo pesa/airtel money 0717396253 kisha tuma majina yako na email kwenye moja ya namba hizo na utaandikishwa kwenye semina hii. Uandikishaji unaanza leo tarehe 20/04/2015 na utasitishwa tarehe 01/05/2015. Wahi kujiandikisha mapema kwani nafasi ni chache na zitakapojaa utakosa nafasi hii adimu ya kupata maarifa ya kukuwezesha kufanikiwa kwenye biashara yako.

Kumbuka semina inafanyika kwa njia ya mtandao hivyo popote ulipo Tanzania na hata nje ya Tanzania unaweza kushiriki semina hii.

Semina itaanza rasmi tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima.

Karibu kwenye semina hii ambayo itakupatia kila unachohitaji ili kufanikiwa kwenye biashara yako.

Kumbuka maarifa ni nguvu, pata maarifa sahihi kupitia semina hii ili uweze kuwa na nguvu za kutosha na zitakazokuletea mafanikio makubwa.

Karibu sana na hakikisha hukosi semina hii kwa sababu yoyote ile.

TUPO PAMOJA.

Makirita Amani 

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

kitabu-kava-tangazo4322

Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara -1

Vijana wengi wamekuwa wakilalamika ni wapi wanaweza kupata mtaji na kuweza kufanya biashara ili kuboresha maisha yao. Lakini vijana hao ndio watu wa kwanza wanaongoza kwa matumizi mbalimbali yasiyo na tija na kufanya starehe sana bila kujua kuwa hizo starehe wanazofanya wangezipunguza au kuacha kabisa na kuweka hiyo hela ili waweze kupata mtaji wa kufanya biashara wanazopenda .

Punguza Mambo Haya ili uweze kupata mtaji

1. Kamari (Kubeti)

Watu wazima hata vijana wengi siku hizi wanapoteza sana rasilimali muda katika kucheza kamari. Huwezi kuwa na uhuru wa kifedha (tajiri) kwa kucheza kamari, watu waliofanikiwa duniani na wenye uhuru wa kifedha hawajafanikiwa kwa kucheza kamari kama wewe unavyodhania na kuendelea kubeti kila siku na kuliwa kila siku katika mchezo huo.

SOMA; Hii Biashara Inaliangamiza Taifa, Tujiepushe Nayo.

Watu wengine wanaweza kubeti kwa siku zaidi hata ya elfu 20 kwa siku akitegemea atashinda hela nyingi na mambo humwendea mrama bila mafanikio yoyote. Kesho pia anajaribu tena kubeti akiwa na imani kuwa ipo siku ataweza kushinda. Mchezo huu wa kubeti anayefaidika ni Yule anayemiliki hiyo kampuni na siyo wewe bali wewe ndio una mtajirisha bila wewe kujua.

Je unaweza kujiuliza tokea uanze kubeti mpaka leo umepoteza shilingi ngapi?

Je kama ungeweza kuwekeza hela zako hizo kila siku bado tu hujapata mtaji? Mpaka hapo hujaweza kujiajiri?

Ni vema sana na ni bora sana ukaitumia fedha hiyo unayopoteza kila siku katika kamari na kuiwekeza fedha hiyo katika soko la hisa na kuendelea kupata faida bila kupoteza hela yako kama ulivyokuwa unapoteza katika kamari au kama unavyoendelea kupoteza fedha yako katika kamari.

Huu ni ushauri wa bure ambao unaweza ukautumia na kujikomboa kuliko kuendelea kucheza kamari.

SOMA; Hawa Ndio Wateja Rahisi Kuwapata Kwenye Biashara Yako.

2. Ulevi

Kitu chochote ukizidisha ni sumu, ulevi wa kupindukia ni sumu pia, siwezi kukuzuia kunywa ila kunywa kiasi punguza pombe au vilevi unavyotumia kila siku na kutumia hela hiyo unayopunguza kupitia pombe hizo unazonunua kila siku na kuweka akiba yako ili uweze kupata mtaji wako wa kufanya biashara halali unayoipenda na kuweza kupata kipato chako .

Vijana wengi wamekuwa ni watu wa starehe kupita kiasi ambayo baadaye inakuletea madhara makubwa utakuja kushtuka pale ambapo huwezi tena kufanya kazi. Ni vema ukautumia muda huu kufanya mabadiliko, amka kijana, amka Mtanzania ili uweze kuhalalisha ndoto yako.

Kama una uwezo wa kunywa bia tano au zaidi kwa siku kwa bei ya sasa ya bia moja na ukijinyima kwa mwezi bado hujapata mtaji?

Usisubiri mpaka upate mtaji mkubwa sana anza na mtaji mdogo na Ujasiriamali mdogo mdogo ambao utakupeleka juu kufikia mafanikio makubwa. Tunaweza kupata mfano kwa bilionea kutoka Afrika Alihaji Aliko Dangote ukisoma wasifu wake yaani wasifu wake alianza kupenda ujasiriamali tokea yuko darasa la tatu na alikuwa anauza pipi au peremende je leo yuko wapi?

SOMA; Ni Lipi Dhumuni Lako Kwenye Maisha? Langu Ni Hili Hapa.

Angalia mapinduzi anayofanya Mtwara kujenga bandari na kujenga kiwanda cha saruji ni jinsi gani mtu huyu ataweza kuwakomboa watanzania wa mahali husika ambapo anajenga vitu hivyo na kuleta mabadiliko chanya mengi. Hivyo usidharau kidogo anza nacho leo kipende na ujifunze utafanikiwa.

Mpenzi msomaji wa makala hii asante kwa muda wako na endelea kufuatilia tena mwendelezo wa makala hii wiki ijayo siku kama ya leo (Jumatatu).

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

Makala imehaririwa kwa Kiswahili fasaha na Rumishael Peter ambaye anatafsiri/kuhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali barua pepe: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422. tovuti http://rumishaelnjau.wix.com/editor

Siri Hii Itakusaidia Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Wa Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi.

Wiki iliyopita tuliona jinsi vituvingi tulivyonavyo katika maisha haya vinavyosababisha tushindwe kufanya majukumu yetu ya kila siku na hivyo kutufanya tuwe na msongo wa mawazo. Kama hukuisoma makala ile isome hapa; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Na Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi.

Leo tutaanza kuangalia jambo moja ambalo litasaidia kupunguza au kuondokana na msongo wa mawazo wa kukosa muda wa kufanya shughuli zako.

Andaa ratiba yako ya kazi

Kabla ya wiki kuanza, yaani mwisho wa wiki hakikisha umeandaa ratiba ya wiki inayofuatia. Tafuta daftari/kitabu chako kizuri ambacho utakuwa unakitunza kwaajili ya kuandikia ratiba zako. Usiandike kwenye karatasi kwakua karatasi ni rahisi kupotea. Tafuta kijitabu kizuri ili iwe rahisi kwako kukitunza. Andika ratiba zako za wiki kwa usafi kulingana na shughuli ambazo unaona ni muhimu kuzifanya kwa wiki iliyopo mbele yako. Unaweza kuandaa hata ratiba za wiki mbili au tatu zijazo ili usisahau vitu muhimu unavyotakiwa kufanya. Kunabaadhi ya shughuli zinahitaji maandalizi kabla hivyo ni vizuri kujua wiki Fulani utakua na shughuli hiyo hivyo kufanya maandalizi mapema . Baada ya kuandaa ratiba ya wiki andaa ratiba za siku. Wakati wa uandaaji wa ratiba ya siku unaweza kukumbuka shughuli zingine unazodhani pia ni vizuri kuziweka kwenye ratiba za wiki. Nenda kwenye ratiba za wiki ukizingatia ni wiki ipi ungehitaji kufanya kazi hiyo na uiweke hapo.

SOMA; Unajaribu Kumdanganya Nani?

Katika kitabu chako cha ratiba weka alama za kutenganisha kazi za wiki na kazi za siku. Weka karatasi itakayoonyesha hizi ni kazi za wiki ya tarehe ngapi hadi ngapi. Andika tarehe na siku za juma katika kazi za kila siku. Kabla ya kulala hakikisha unaandaa ratiba ya siku inayofuata na kupitia ratiba yako ya siku iliyoisha.

Shughuli ambazo zilibaki siku ya nyuma hamishia kwenye ratiba ya siku inayofuatia. Angalia usiandike mambo mengi sana ambayo unadhani siyo rahisi kukamilisha ndani ya siku moja. Ukifanya hivi utajiongezea msongo wa mawazo kwani utaona ratiba yako bado imebana na hukuweza kukamilisha mambo mengi.

Katika ratiba yako ya siku anza na shughuli za muhimu sana kwa siku hiyo ambayo zinalenga moja kwa moja malengo yako uliyojiwekea katika maisha yako. Usisahau kutenga muda kwaajili ya familia na masuala ya kijamii kwa kua upweke pia husababisha msongo wa mawazo.

SOMA; KITABU; MEGA LIVING(Siku 30 Za Kuboresha Maisha Yako).

Kila mara pitia ratiba yako ya siku ili ufahamu ni nini unatakiwa ufanye ili mambo mengine yasikuzonge na kukufanya usahau mambo muhimu kwa siku hiyo. Usiibane sana ratiba yako ukakosa muda wa mazoezi na kupumzika. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa mazoezi na muda wa kutosha wa kupumzika hufanya akili ya binadamu kuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri. Jipe masaa saba ya kulala vizuri. Fanya mazoezi na usisahau kula vizuri na kunywa maji mengi.

Naomba ufanye zoezi hili kwa wiki hii. Tukutane tena wiki ijayo ili kuendelea na mambo mengine.

Kama unaswali, maoni au ushauri usisite kuwasiliana nami.

MWANDISHI: ESTHER NGULWA

MAWASILIANO: 0767 900 110 / 0714 900 110 estherngulwa87@gmail.com

Mambo 20 Niliyojifunza Kutoka Kwenye Kitabu Cha; The25 Sales Habits Of Highly Successful Salespeople

Habari za leo msomaji mwenzangu. Kama nilivyoahidi wiki iliyopita kwamba nitakua nikishirikisha mambo 20 kila wiki niliyojifunza kutoka kwenye kitabu kimoja kati ya 2; Wiki hii tunaendelea kama ufuatavyo.

Wiki hii nitakushirkisha mambo 20 niliyojifunza kutoka kwenye kitabu cha; The25 Sales Habits of Highly Successful Salespeople –Kiilichoandikwa na mwandishi Stephan Schiffman

Karibu

1. Wauzaji mashuhri ni wale wenye uwezo wa kutatua matatizo. Lazima uwe na mtazamo wa kutatua matatizo kwa kutoa suluhisho kwa wateja wako. Mfano kama unafanya biashara ya magari lazima uwe na matazamo wa kutatua tatizo la usafiri na usafirishaji. Kama unafanya biashara ya simu lazima uelewe kwamba upo ili kutatua tatizo la mawasliano. Kwa hiyo kabla hujaingia kwenye hiyo lazma uwe na mtazamo wa kutatua tatizo.Kwanza lazima ulitambue na kulielewa vizuri tatizo kabla ya kujaribu kulitatua. Hii itakusaidia kuwa mbunifu mzuri katika kuboresha huduma au bidhaa yako ili kutatua tatizo husika ipasavyo.

2. Je bidhaa au huduma unayouza unaweza kuibadilisha ikakidhi kusudi au uhitaji mwingne ili kupanua wigo? Je bidhaa au huduma yako unaweza kubadili kukidhi uhitaji wa watu wengne zaidi wa wale wa mwanzo? Mfano mwanzilishi wa Facebook bwana Mark Zuckerberg , wakati anaanzisha Facebook ilikua kwa minajili ya kuwasaidia wanafunzi wa chuo alipokua anasoma waweze kuwasiliana, lakin aligundua kua huduma anayoitoa anaweza kuiboresha na kufikia watu wengne wengi zaidi ya wanafunzi wa pale chuoni. Leo hii ni historia bwana Mark Zuckerberg ni ndio tajiri namba moja duniani mwenye umri mdogo.

SOMA; Kwa Nini Watu Hawawaambii Wengine Kuhusu Biashara Yako.

3. Unapo deal na mteja mpya usikimbilie kumuuzia tu huduma au bidhaa yako. Hakikisha unatengeneza mahusiano naye mazuri. Sio swala la kuuza tu, unatakiwa kumfanya mteja awe na hamasa ya kurudi tena na tena

4. Sikiliza, jifunze, Ongoza (Listen, learn, and lead). Ukisikiliza kutakufanya ujue nini tatizo la mteja wako. Ukijifunza unajiongezea maarifa unakua mwerevu zaidi hivyo kua na uwezo wa kuongoza wateja kule unakotaka waelekee.

5. Kuandika maelezo (taking Notes) wakati unapokutana na mteja mtarajiwa (prospect) ni nyenzo ya mazuzo yenye nguvu sana(powerful sales tool). Hakikisha wakati wa mazungumzo unaandika mahali ili kukusaidi kujua vizuri tatizo la mteja wako mtarajiwa. Kuchukua maelezo pia kutakusaidia yafuatayo:

· Kuandika kutakusaidia kusikiliza kwa makini, na itakua ngumu kusahau pointi muhimu

· Kuchukua maelezo kunakuweka katika hali ya kua na mamlaka na uthibiti

· Kutaimarisha uwezo wako wa uchambuzi. Maana unahusisha milango mitatu ya fahamau amabyo ni Kugusa( unapoandika), kusikia ( unaandika ulichokisikiliza kutoka kwa mteja wako), kuona (Unaona ulichokiandika)

· Kutakusaidia kuapta taarifa zaidi kutoka kwa mteja wako mtarajiwa. Maana atajisikia vizuri kufunguka maana anaona unajali anchoongea na upo serious katika kutatua changamoto aliyonayo

6. Tengeneza mpango wa kila mteja wako mtarajiwa. Mpango utakua pia unaonyesha jinsi gani ya kutatua tatizo lake kutokana na maelezo uliyokua ukiyaandika kwenye vikao vya nyuma kama ilivyoelezwa kwenye pointi ya hapo juu. Mpango utakua ni dira ya kufahamu ni kitu gani cha tofauti hasa unachoweza kufanya kwa huyo mteja wako. Kusikiliza ndio siri ya kwanza, na kutambua suluhisho zitakozokubaliwa na pande zote mbili ni siri ya pili.

7. Unatakiwa uwe daktari. Mfano: Unapokwenda hospitali labda tumbo linakuuma kisasawasawa , Unapofika kwa daktari hautojali kwamba amehudumia wagonjwa wangapi au wagonjwa wangapi wako wanamsubiri. Utakachopenda ni akuhudumie. Utataka akupeleke kwenye chumba cha matibabu kwa ajli ya uchunguzi na kukupatia matibabu sahihi kabla hajakimbia kwenda kuhangaikia wagonjwa wengine. Utataka akuulize unajisiakiaje, umekua na hali hii kwa muda gani, je ulishawahi kupatwa na tatizo kama hili nyakati zilizopita, nk. Kama daktari akikufanyia hayo yote na akakupa matibabu utafurahi na utakua na mtazamo mzuri zaidi kwake, na hata utapenda kuja kumuona wakati mwingne. Pia utapenda kuwashauri wengne wenye tatizo kama lako waende kwa daktari huyo kwa sababu ya huduma yake nzuri.

Hivyohivyo basi mtu wa mauzo (Salesperson) au muuzaji ni daktari. Haijalishi umehudumia wagonjwa (wateja) wangapi. Huyu mteja mtarajiwa (new propect/customer) ndio yeye tu ambaye unapaswa kumuona kwa wakati huo, na kumhudumia kipekee. Usimhudumie kwa harakaraka ili ukimbilie wengine, hakikisha umetatua tatizo lake na ameridhika. Mfanye ajione yeye ni wa pekee kwa wakati huo unaomhudumia. Kufanya hivyo hakuta fanya tu mazingira ya kaz yawe mazuri, bali pia kutaongeza kupendwa kwako na wateja na kupelekea watamani kurudi tena na tena.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuibadili Dunia.

8. Onyesha kua na shauku. Unapohudumia wateja wako, au unapokutana na mteja mtarajiwa onyesha shauku. Hii itamfanya asijiskike kwamba ni wa kawaida tu, atajisikia vizuri maana anona uko excited kukutana naye.

9. Jipe sifa unazo stahili. Ongea kuhusu wewe lakini katika hali ya unyenyekevu ili islitete tafsiri ya kua unajivuna. Uongee kwa ujasiri kuhusu biashara yako na mambo amabayo inaweza kutatua, cha muhimu epuka mbwembwe nyingi zisizokua na maana.

10. Jifunze kusoma hali na nyakati. Sio kila kinachofaa kwa mteja A kitafanya kazi kwa mteja B… You have to learn how to read the situation

11. Kwa wataalamu wengi wapo makundi mawili;

· Kundi la kwanza ni lile la wataalumu ambao wanaongeza thamani kwenye kila kitu wanchokigusa au kukifanya.

· Kundi la pili ni wale wanaofanya thamani ya kila wanachoguza ishuke.

Kama wewe ni mtaalamu thibitisha kwamba upo kwenye kundi la kwanza. Onyesha thamani yako. Hakikisha kila unachofanya unaongeza thamani yake.

12. Ukweli ni nyenzo muhimu. Unapaswa kua mkweli maana ndio rahisi kuukumbuka. Ukweli ni rahisi kuukumbuka kuliko uongo. Ndo maana wanasema ukiwa muongo uwe na kumbukumbu vizuri, maana utaumbuka tu siku moja. Hakikisha unajenga uaminifu na wateja wako kwa kua mkweli. Tell the truth; it’s easier to remember. Don’t promise your customer what you can’t deliver

13. Jiuze kwako mwenyewe (Sell Yourself on Yourself). Jihamasishe mwenyewe kwanza kabla ya kuhamasisha wengine. Kabla hujajiuza kwa wengine anza kujiuza kwako kwanza. Taswira yako mwenyewe (Your self-image) ni ya muhimu sana. Utakavyojiona ndivyo na wengine watakavyokuona.

14. Mhusishe mteja. Usiwe wewe ndo muongeaji tu mwanzo mwisho. Mfanye aongee kuhusu yeye mwenyewe. Hii itafanya akupe taarifa ambazo utajua ni suluhisho gani anahitaji. Hata kama unaongea usijisahau ukaongea tu kuhusu wewe na biashara yako. Hakikisha kunakua kwa faida yake. Mpe nafasi pia atoe maoni yake.

SOMA; Hizi Ndizo Sifa Saba Za Kiongozi Bora.

15. Anza mapema siku yako. Hii ni moja ya siri za watu waliofanikiwa. Unapoanza mapema unashauriwa kupata wasaa wa kutulia pekee yako na kutafakari. Wakati huu ni wa kwako na wewe, unahojiana na wewe mwenyewe. Unaichaji akili yako na utaona utofauti. Ukichunguza watu wanoamka alfjiri na mapema na wale wanoamka sa 2 asubuhi utendaji wao wa kazi ni tofauti sana. Kwa watu wengi alfajiri ndio wakati akili inakua na nguvu. Mimi mweneywe siku nikiamka mapema afajiri hua nakua na hamasa kubwa ya kazi. Lakini siku umechelewa kuamka, kwanza unakua huna raha, unaona umechelewa, unakosa muda wa kutafakari au kumuomba Mungu, na hata ukitafakari wakati umeamka kwa kuchelewa akili yako haitakua imetulia maana muda wote inawaza saa ngapi utafika kazini. Ukijijengea tabia hii ya kuamka mapema na kuutumia muda huo kufanya vitu vya maana lazima utaongoza kwenye sehemu uliyopo, iwe biashara, kazini n.k

16. Usisikilize redio au kuangalia TV asubuhi. Habari nyingi utakazosikia au kuziona wakati huo ni habari mbaya (hasi) amabazo zitakutia hofu na kukukatisha tamaa. Badala yake tafuta CD au video au chochote kile cha kuhamasisha. Hakikisha siku yako unaianza kwa hamasa kubwa.

17. Soma vitabu, majarida au machapisho yanayohusiana na biashara au kazi unayofanya. Hii ndiyo njia ya uhakika ya kukuweka juu, Maana utakua na maarifa makubwa ambapo yatakusaidia katika ubunifu. Ukisoma ukafikisha vitabu au machapisho 500 utakua kati ya watu 1% ya wale waliofanikiwa sana katika hiyo biashara au kazi. Pia hii itakuongezea kujiamini maana utakua umebobea na utakua mtaalamu wa kutegemewa maana unataarifa nyingi zenye thamani kubwa.

18. Mteja sio mara zote yuko sahihi. “Mteja mara zote yuko sahihi “ Hii ni moja kati ya amri kumi za mauzo, na amri hii ya kwamba mteja yuko sahihi imekua ikivuka kizazi hadi kizazi. Lakini si kweli kwamba mteja yuko sahihi mara zote. Lakini haimaanishi kwamba umwambie mteja wako kwamba hayuko sahihi. Kua mbunifu katika kuonyesha usahihi, aidha kwa kutoa kama pendekezo. Forget the conventional wisdom. I t’s okay to tell a customer that there’s a better way.

19. Makosa hua yanatokea. Unapokosea haipaswi kujuuta mpaka unaharibu mambo mengine. Kua muwazi kukiri kosa omba msamaha na kusonga mbele. Jifunze kutokana na kosa fanya maboresho husika.

20. Ona fahari ya kile unachokifanya au unachouza. Mwambie kila unyekutana naye kuhusu kampuni unayofanya kazi na bidhaa au huduma zinazopatikana.

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana nae kwa simu 0763 071007 au 0658 587029 au email daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com