Kuhusu Uwekezaji Tanzania

UWEKEZAJI TANZANIA ni mtandao unaokupatia maarifa na taarifa mbalimbali za uwekezaji kwa hapa nchini Tanzania.
Kupitia mtandao huu utajifunza fursa mbalimbali za uwekezaji na pia kupata taarifa zinazohusu uwekezaji.

 AINA ZA UWEKEZAJI TANZANIA.

Kwa bahati nzuri sana kuna aina nyingi sana za uwekezaji Tanzania. Kuna kila rasilimali na fursa mbalimbali za uwekezaji. Ugunduzi wa mafutra na gesi unaoendelea kufanyika Tanzania unaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi sana.
Kuna aina mbalimbali za uwekezaji zinazoweza kufanyika Tanzania.

1. Uwekezaji wa mali.

Tanzania kuna arhi kubwa sana ambapo mtu anaweza kununua na kuendeleza kwa kujenga majengo ya kibishara na hata makazi.
Pia ardhi hii inaruhusu kilimo na hivyo mtu unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha biashara.

2. Bishara.

Kwa kuwa uchumi wa tanzania unakua kwa kasi sana mtu yeyote anayweza kuwekeza kwenye biashara anaweza kuapata faida kubwa. Biashara za bidhaa na huduma zinakua kwa kasi sana kutokana na ongezeko la watu na muingiliano wa kimataifa.

3. Uwekezaji katika maliasili na gesi.

Tanzania ina gesi nyingi sana ambayo bado haijachimbwa. Hii inatoa fursa kubwa sana ya uwekezaji.

4. Uwekezaji wa hisa na vipande.

Hii ni fursa nzuri ya uwekezaji kwa watu ambao wana miotaji kidogo. Soko la hisa la dar es salaa limeorodhesha makampuni mbalimbali ambayo mtu anaweza kununua hisa.
Pia dhamana ya uwekezaji UTT, inatoa fursa kwa watu kununua vipande na vipande hivyo kuongezeka thamani na hivyo kunufaika zaidi.
Kuna fursa nyingi sana za uwekezaji ambazo utajifunza kupitia mtandao huu.

0 comments: