Hatua Muhimu Kuzifahamu Unapohitaji Kuwekeza Katika Hisa.

Uwekezaji katika Hisa limekuwa jambo geni kwa watu wengi. Kwa kuwa mmiliki wa Hisa unapata fursa ya kuweza kuongeza kipato chako huku ukiendelea shughuli zako nyingine ambazo zinakuingizia kipato. Uwekezaji katika nchi yetu bado ni mchanga, kwa hiyo kuna fursa kubwa ya kuweza kutengeneza kipato. Kama unataka kuwa mwekezaji katika Hisa ni muhimu kufahamu hatua hizi.

SOMA; Soko la Hisa la Dar: Fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wazalendo Tanzania

Hatua Muhimu kuzifahamu unapohitaji kuwekeza katika Hisa

1. Fanya maamuzi kuwekeza

Kufanya maamuzi ni jambo zuri na inafanya akili yako kuwa tayari kwa ajilia ya kuingia kwenye uwekezaji huu.

2. Kufahamu ni sehemu gani ambayo unaweza kununua au kuuza Hisa

Ili uweze kuwa mmiliki wa Hisa ni lazima uweze kufahamu sehemu ambayo unaweza kununua Hisa zako. Kuna sehemu mbili ambazo unaweza kununua Hisa i) Kampuni inapouza Hisa zake kwa mara ya kwanza kabala kusajili katika soko la Hisa (IPO), ni vizuri ukanunua Hisa kwa kampuni ambayo inakaribia kusajiliwa katika Soko la Hisa; i) Unaweza kununua kupitia Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE) kwa kupitia mawakala wake.

SOMA; Msingi na ustadi wa kuwekeza kwenye Soko la Hisa

3. Kufahamu ni kampuni gani unahitaji kuwekeza

Katika soko la Hisa la Dar es salaam kuna kampuni ishirini na moja (21) ambazo zimesajiliwa na soko hilo. Unapohitaji kuwa mmiliki wa Hisa unatakiwa kuchagua Kampuni ambayo inakufaa kwa ajili ya uwekezaji wako. Katika kuchagua Kampuni unatakiwa kuwa na taarifa sahihi kuhusu kampuni hiyo na ufanisi wa kampuni hiyo katika soko la Hisa ili uweze kufanya uwekezaji wenye manufaa.

4. Muda mzuri kwa mwekezaji kununua Hisa

Kama mwekezaji ni vizuri ukafahamu muda mzuri kwako kununua Hisa wenye manufaa. Muda mzuri kwa mwekezaji kununua Hisa zake i) Kampuni inapouza hisa kwa mara ya kwanza kwa sababu mara nyingi kampuni bei zake huwa chini ya thamani halisi ili kuvutia wawekezaji ii) Kipindi cha januari hadi Machi kwa sababu watu wengi huuza hisa zao kwa shida mbali mbali na mara nyingi kipindi hiki Uchumi haufanya vizuri sana iii) Bei za Hisa zinaposhuka ila lazima utambue sababu ya kushuka kwa bei zake kama ni ya muda mfupi.

SOMA; Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

5. Muda mzuri kwa mwekezaji kuuza Hisa

Vile vile unapoingia kwenye uwekezaji katika Hisa ukafahamu muda mzuri wa kuuza hisa zako. Muda mzuri wa kuuza hisa zako ni pale kampuni inapokuwa haifanyi vizuri, bei zake zinaposhuka na zinaonyesha zitaendelea kushuka. Unapofanya maamuzi ya kuuza hisa zako ni vizuri ukawa na taarifa sahihi za Kampuni husika. Ni vizuri kwa mwekezaji akawa na malengo ya uwekezaji kwa kipindi cha muda mrefu.

6. Hatua ya mwisho unaweza kununua Hisa na kuwa mmiliki wa kampuni

Baada ya kupitia hatua zote hapo juu unaweza kufanya maamuzi ya kununua hisa katika soko la Hisa. Unaweza kununua hisa katika soko la Hisa kwa kupitia mawakala wa soko la hisa (Brockers) ambao wamesajiliwa na soko la Hisa au kununua hisa zinapouzwa na Kampuni kwa mara ya kwanza. Vitu vya msingi kuwa navyo unapohitaji kununua hisa i) uwe na email ambayo itakusaidia kutuma baadhi ya taarifa na akaunti ya benki.

SOMA; Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Hawa ni baadhi ya mawakala wa soko la Hisa (Brockers) ambao wamesajiliwa

CORE securities Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 212 3103 au info@coresecurities.co.tz

Orbit Securities Co. Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1758 au orbit@orbit.co.tz

Rasilimali Ltd; Mawasiliano Tel: +255 22 211 1711 au rasilimali@africaonline.co.tz

Tanzania Securities Ltd; Tel: +255 22 211 2807 au info@tanzaniasecurities.co.tz

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

0 comments: