Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

Warren Buffett ni mmoja wa watu matajiri sana duniani. Utajiri wake huu ameupata kupitia biashara na uwekezaji. Alianza biashara akiwa na miaka 11 na sasa ana miaka 83. Kwa miaka zaidi ya 60 ambapo amekuwa kwenye biashara una uzoefu wa kutosha kutufundisha sisi ni vitu gani vya kuzingatia kwenye biashara.

Hizi hapa ni sheria 8 za kufanikiwa kwenye biashara kutoka kwa Warren Buffett.

1. Tulia wakati wa matatizo/changamoto.

Katika biashara kuna wakati ambao utakutana na changamoto na matatizo mbalimbali. Huu ni wakati ambao Warren anatushauri tutulie badala ya kuvurugwa na hatimaye kuharibu kila kitu.

SOMA; Maswali Matatu Kwa Anayetaka Kuwa Mjasiriamali Kujiuliza Kutoka Kwa Richard Branson.

2. Zungukwa na watu wazuri.

Kama unafanya biashara kwa kushirikiana na mtu au watu wengine, hakikisha watu hawa  wana maadili mazuri na wanandoto kubwa ya mafanikio kama uliyonayo wewe.

3. Ng’ang’ania kile unachokitaka.

Warren anashauri kwamba usiache lengo lako kuu kwa sababu kuna vitu vizuri umeviona pembeni, kufanya hivi kutakuletea kushindwa.

4. Weka gharama chini.

Hakikisha gharama za kuendesha biashara yako zinakuwa chini sana ili uweze kuuza kwa bei ambayo wateja wako wanaweza kuimudu na wewe kupata faida.

SOMA; Hakuna Anayejua Anachofanya, Na Huo Ndio Uzuri Wa Maisha.

5. Toa zawadi kwa wafanyakazi wako.

Warren anashauri kwamba pale wafanyakazi wanapofanya vizuri uwape zawadi hata kama ni ndogo kiasi gani. Hii inawafanya waone unajali.

6. Epuka matatizo.

Warren aliwahi kumwandikia mshirika wake kwenye biashara hivi “nachotaka kujua ni wapi nitaenda kufa hivyo nisiende hapo kamwe”. Kama unataka kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuepuka matatizo maana matatizo mengi yanasababishwa na wewe mwenyewe.

7. Fanya kuwa ndogo.

Buffett anasema kwamba biashara inapokuwa kubwa sana inakuwa vigumu kubadilika na urasimu unakuwa mkubwa kiasi cha kuwachosha wafanyakazi na hata wateja. Anashauri kurahisisha uongozi wa biashara hivyo hata ikikua sana bado ionekane ni ndogo na rahisi kuongoza na kuwasiliana.

8. Linda heshima yako.

Buffett anasisitiza kwamba heshima yako ni kitu muhimu sana kwenye mafanikio ya biashara. Anashauri kuwa mwaminifu na kutofanya kitu chochote ambacho usingependa kiripotiwe kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti. Anasisitiza hili kwa kauli hizi mbili;

Poteza hela za biashara na nitakuelewa, poteza sifa ya biashara na nitakuwa mbaya sana kwako.

Inakuchukua miaka 20 kujenga heshima na dakika tano kuiharibu. Ukifikiria hili utafanya mambo kwa tofauti.

Tumia sheria hizi nane kwenye maisha yako ya kila siku na ya biashara na zitakusaidia sana kufikia mafanikio.

SOMA; Hii Ni Kazi Yenye Malipo Makubwa Sana Ambayo Unaweza Kujifunza Kuifanya

3 comments:

Unknown said...
This comment has been removed by the author.
Unknown said...

Mwalimu umenifumbua macho, nashukuru sn ubalikiwe

sahani media said...

Thank may God bless u