Tofauti ya mtazamo Kati ya Mtu wa Hali ya kati na Mtu wa hali Juu.
Kuna tofauti nyingi sana kati ya tajiri na masikini jinsi wanavyofikiri na kuwa na mitazamo tofauti. Mitazamo chanya na kufikri kichanya zaidi kwa matajiri kunawafanya wajizidi kuwa juu ukilinganisha na masikini jinsi wanavyofikiria. Zifuatazo ni mitazamo mbalimbali kati ya tajiri(world class ) na watu wa kipato cha kati yaani (middle class).
Masikini huwa wanaamini kuwa pesa ndio mzizi wa maovu yote lakini matajiri huwa wanaamini kuwa umasikini ndio mzizi wa maovu yote. Kwa hiyo amua kujivunia kuwa tajiri na dharau kauli za watu wa kipato cha chini wanaokuambia kuwa tajiri sio sahihi .
Masikini huwa wanaamini kuwa pesa ni ngumu sana kuipata wakati matajiri huwa wanaamini kuwa pesa ni rahisi kuipata kama ukiitega.
Masikini huwa wanaamini kuwa kama wakiwa matajiri watapoteza marafiki wao lakini Matajiri huwa wanaamini kuwa na marafiki kutawaongezea mtandao mkubwa zaidi wa kuwa tajiri.
Masikini huwa wanawafundisha watoto wao jinsi ya kuishi lakini matajiri huwafundisha watoto wao jinsi ya kupata au jinsi ya kuwa tajiri.
Masikini huwa wanaamini kuwa pesa inambadilisha mtu Lakini Tajiri anaamini kuwa pesa inaonesha mtu alivyo.
Tajiri anaamini kuwa kuwajibika au kujituma ndio njia salama pekee ya kupata pesa wakati masikini huwa wanaamini kuwa kazi ndiyo njia salama pekee ya kupata pesa.
SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.
Watu wa kipato cha kati huwa wanaamini kuwa na pesa nyingi inakutengenezea matatizo mengi lakini watu wa kipato cha juu yaani (world class) wenye uhuru wa kifedha wanaamini kuwa na pesa nyingi inakupunguzia kuwa na matatizo mengi au kuwa na matatizo machache.
Masikini huwa wanaamini kuwa ukipata fedha nyingi kutakupelekea kuwa na mawazo (stress) lakini tajiri anaamini kuwa na fedha nyingi inasaidia kupunguza mawazo (stress) au kutokuwa na mawazo .
Matajiri wanafikiri kirefu au kikubwa (think big) wakati masikini wanafikri kidogo u kifupi (think small).
Matajiri wanaishi chini ya kipato chao lakini masikini wanaishi juu ya kipato chao. Hii ndio sababu ambayo inawafanya watu wengi kutofikia malengo yao kwa sababu wanaishi juu ya kipato chao na kupelekea kuwa na madeni mengi.
Watu wa kipato cha kati wanaamini kuwa matajiri lazima wasaidie masikini lakini matajiri wanaamini katika kujitegemea.
Watu wa kipato cha kati wanaamini tajiri wana akili sana lakini watu wa kipato cha juu wanaamini kuwa na akili sana kuna uhusiano mdogo sana katika kupata utajiri au kuwa tajiri.
SOMA; Jambo Muhimu La Kila Mfanyabiashara Kufanya Kila Siku.
Watu wa kipato cha kati wanaamini kuwa na pesa ndio kutengeneza pesa lakini watu wenye uhuru wa kifedha wanaamini kuwa kupitia au kwa kutumia watu wengine kupata fedha au kutengeneza fedha.
Hizi ni baadhi tu ya mitazamo kati ya watu wenye kipato cha kati (middle class) na watu wenye uhuru wa kifedha ( world class).
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com
5/04/2015 07:30:00 AM | Labels: FEDHA, MBINU ZA MAFANIKIO | 0 Comments
Jambo Moja Muhimu La Kuzingatia Ili Uwe Tajiri.
Kabla ya kitu chochote hakijaweza kuwa katika hali yake ya uhalisia huanza katika wazo. Nyumba haiwezi kujengwa kabla ya kuanza kuwa na mchoro unaongoza ujenzi wa hiyo nyumba. Katika maana nyingine rahisi unaweza kusema tunafikiri kwanza halafu tunafuata utekelezaji au kuweka katika matendo kile tunachokifikiri.
Jaribio rahisi ambalo linaweza kukufanya ujue kama mtu ataishia kuwa tajiri au tayari ni tajiri ni kwa kutazama yale mambo anayoyafanya kwa kuwa yale anayoyafanya yanaweza kutabiri matokeo yanayotarajiwa. Mambo anayoyafanya mtu huyafanya kutokana na mwongozo anaopata kutoka katika kiwanda chake cha kuzalisha mawazo.
Jaribio lenyewe ni kutazama mawazo ambayo anayatengeneza kupitia jinsi anavyoilisha akili yake. Chunguza ni mambo gani au vitabu vya aina gani au majarida ya aina gani au makala za aina gani huyo mtu anasoma. Katika hivyo vitabu au majarida mwangalie vipengele gani ambavyo anavyovisoma na pia uangalie vipengele gani katika majarida au vitabu hivyo hivyo huwa havipi mkazo kuvisoma. Katika vile vipengele anavyovisoma chunguza anavisoma katika mpangilio gani au mfuatano upi?
Jaribio hili unaweza kulifanya hata kwako binafsi kama kweli una kiu ya kubadili hali yako ya sasa kuwa tajiri au kama tayari ni tajiri basi kuufanya utajiri wako ukue zaidi. Watu ambao ni matajiri walio kaa chini kutafakari na kuamua kwa kusudia kuwa wanataka kuwa matajiri tofauti na wale ambao labda wameshinda bahati nasibu au wamerithishwa mali huchagua vitabu au majarida ambayo yanaongeza thamani katika utajiri wao, huchagua vipengele katika majarida au vitabu ambavyo kweli vinaongeza thamani katika maisha yao, havipi mkazo vipengele vile ambavyo haviongezi thamani na katika haya majarida au vitabu utagundua huwa wanasoma vipengele vinavyohusiana na fedha au biashara kwanza kabla ya kusoma vipengele vingine.
SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.
Ukitaka kuwa daktari ni muhimu sana usomee udaktari, au ukitaka kuwa msanifu majengo ni muhimu sana usome kuhusu masuala ya usanifu majengo ili uwe na uwezo wa kufanya kazi yako kwa ufanisi na usiwe mbabaishaji katika eneo husika ulilolichagua. Matajiri wote ambao wamechagua kwa makusudi kuwa matajiri wamejifunza kwa njia mbalimbali kuhusu utajiri. Mmoja wa wana mafanikio maarufu duniani Jim Rohn hupenda kusema ukihitaji furaha nenda ujifunze furaha, ukihitaji uhuru wa kifedha nenda ujifunze kuhusu uhuru wa kifedha, ukihitaji afya bora nenda ujifunze kuhusu afya bora, orodha hii inaweza kuendelea zaidi lakini Jim alihitimisha kwa kusema kila kitu unachokihitaji ni kujifunza, ndiyo maana nikasema kama unataka utajiri jifunze utajiri. Kujifunza huku sio kwa kukaa darasani kwa sababu mifumo yetu ya elimu haina mitaala inayowaelekeza watu namna ya kuwa matajiri bali ina mitaala ambayo inawaandaa watu kuwa waajiriwa. Matajiri wengi waliamua kujiendeleza binafsi kwa kusoma makala, vitabu na majarida ambayo yanawapatia maarifa ambayo hayajawekwa katika mitaala ya mifumo wa elimu tulio nao.
Mafunzo makubwa ambayo wamejifunza ni namna ambavyo matajiri wengine kabla yao jinsi wanavyowaza kwa kudhibiti malighafi inayotumika katika kiwanda cha mawazo kupitia ulishaji wa akili zao kwa yale wanayoyasoma, wamejifunza namna matajiri waliotangulia wanavyofanya kazi, wanavyokula, wanavyoishi , wanavyoweka akiba, wanavyowekeza katika vitega uchumi mbalimbali. Wamejifunza kwa kujaribu kuongea na watu matajiri ili kuwapa mbinu za kufanikiwa kwa upande mmoja na kwa upande mwingine kuwaelekeza mambo ambayo wanatakiwa kuchukua tahadhari ili kuepuka kutetereka. Wamejifunza kwa kuuliza maswali sahihi, maswali sahihi ni yale maswali ambayo ukiuliza yanaenda kugusa na kubadili maeneo maisha yako moja kwa moja. Wamesoma mahojiano mbalimbali ambayo hawa matajiri waliotangulia wameyafanya, wamesoma kuhusu wasifu wa hawa matajiri waliotangulia. Hayo ndio masomo ambayo wanajifunza katika chuo cha utajiri.
SOMA; Jinsi Ya Kuondokana Na Tabia Ya Kuahirisha Mambo.
Kama kweli umeamua kwa makusudi kabisa unahitaji kuwa tajiri ni lazima ujiendeleze kwa kuwa na uelewa pamoja na maarifa ya kujitosheleza kuhusu utajiri.
Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano: Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blogu yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.
4/30/2015 07:30:00 AM | Labels: FEDHA, MBINU ZA MAFANIKIO | 0 Comments
Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.
Inawezekana umefika katika hatua ambayo unaona kama ungekuwa na kiasi fulani cha fedha basi matatizo yako yote ambayo yamekuwa yanakusumbua au yanakukabili bila kujali yana umri kiasi gani yangekuwa yamepatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Kama ingekuwa kuwa na fedha ni kupata ufumbuzi wa matatizo tuliyonayo ina maana tungetarajia watu wenye fedha nyingi wangekuwa hawana matatizo kabisa. Lakini katika maisha ya leo baadhi ya hawa watu ambao wana fedha sana ndiyo ambao wana matatizo zaidi kama ya magonjwa, kukosa furaha n.k ukiwalinganisha na wale ambao hawana fedha au wana fedha kiasi kidogo.
SOMA; Najua Umeshasikia Hili Mara Nyingi, Sio Vibaya Ukasikia Tena Na Leo.
Kwa mfano fedha haiwezi kukulinda usiumwe lakini inaweza kukusaidia kupata huduma bora zaidi ya kiafya baada ya kuumwa. Kwa hiyo tungekosea sana kusema kwa kuwa una hela basi umeshapona mara baada ya kugundua unaumwa, bali unapokuwa unaumwa hatua ya kwanza ni kuanza kufikiri namna ya kukupatia huduma ya afya inayoweza kutibu ugonjwa unaokusumbua halafu hatua ya pili inafuata namna ya kutumia kiasi cha fedha uliyonayo kupata huduma husika kutatua tatizo linalokukabili. Kwa hiyo fedha huja katika hatua ya mbele sana na siyo hatua ya kwanza katika utatuzi wa tatizo bali ni kitu kinachowezesha utatuzi wa tatizo.
SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.
Kwa maana nyingine fedha haina ubaguzi kwamba wewe ni wa rangi gani au umetoka katika kundi gani la uchumi (mtu masikini au mtu wa daraja la kati au mtu tajiri) au wazazi wako walikuwa na hali gani ya kifedha au hata unafikiri kuwa wewe ni nani (nafasi yako katika jamii).
Fedha haiwezi kubagua kwa kuwa haijui mambo mengi yanayomhusu yule anayemiliki kiasi husika cha fedha. Fedha haijui una kiwango gani cha elimu au maarifa, fedha haina masikio wala macho wala uwezo wa kuhisi. Bali fedha ipo kwa ajili ya kutumiwa, kuwekwa akiba, kuwekezwa.
Kila mmoja wetu anayo haki na fursa sawa kuweka jitihada ya kupata fedha zaidi bila kujali jana yako ilikuwaje. Inawezekana ukaona ni ngumu na kuna changamoto na vikwazo zaidi lakini inawezekana kufanya na kuibadili maisha yako.
SOMA; Njia TANO Rahisi Za Kutangaza Biashara Yako.
Kwa hiyo ni muhimu sana kukaa chini na kutafakari na kufafanua kwa kina ni nini hasa kusudi la wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji. Kuwa na ufafanuzi au maana sahihi ya wewe kuwa na kiasi cha fedha unachokihitaji itakusaidia kuendana vema na tabia hizo kuu tatu za fedha nilizoziainisha hapo juu (kutumiwa, kuwekwa akiba na kuwekezwa).
Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano: Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blogu yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.
Makala imeangaliwa muundo na lugha fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na MjasiriamaliEmail: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.
4/23/2015 07:30:00 AM | Labels: FEDHA | 0 Comments
Haya Ndio Matumizi Mazuri Ya Mshahara Wako Ambayo Yatakuletea Furaha Na Mafanikio.
Mshahara ni makubaliano ya malipo kati ya mwajiri na mwajira kulingana na kazi anayofanya mwajiriwa. Malipo haya yanakuwa kwa muda au kipindi fulani kutokana na mkataba wao waliojiwekea.
Wakati mwingine unafanya kazi na kupata mshahara lakini hujui au hufahamu sehemu au makundi unayoweza kuugawa mshahara wako.
Zifuatazo ni bahasha tano ambazo unaweza kuugawa mshahara
1.SADAKA(Tithe Fund)
Unapopata mshahara wako asilimia kumi ya kipato chako yaani mshahara weka katika bahasha hii au mfuko huu wa sadaka. Kutoa asilimia kumi ya mshahara wako ni mwongozo wa kuufuata lakini siwezi kukulazimisha uamuzi uko mikononi mwako BO SANCHEZ katika kitabu chake cha My Maid Invest in the Stock Market alikuwa akiwaambiwa wafanyakazi wake yani wasaidizi wake hivi ‘’ You will grow in abundance think’’ usemi huu wa BO SANCHEZ una maanisha kuwa kuna faida sana pale unapotoa sadaka kama alivyonena hapo juu, utakuwa katika uwezo mkubwa wa kufikiri’
SOMA; Tabia KUMI Za Watu Waliofanikiwa Sana(PICHA)
2. MATUMIZI ( Expense Fund)
Haya ni yale matumizi ya kila siku ya mahitaji ya nyumbani (daily needs) ambapo pia unaweza ukatenga fungu lingine la mshahara wako au kipato chako na kuweka katika bahasha hii ya matumizi.Hii itakusaidia sana kutotumia hela vibaya na kuwa na nidhamu ya pesa katika mshahara wako na itakusaidia kujuwa kwa mwezi matumizi yako yanagharimu kiasi gani.
3. MSAADA ( Support Fund)
Katika jamii zetu kusaidiana ni jambo la kawaida msaada huo unaweza ukatoa kwa ndugu,jamaa,marafiki na nk. Pengine ni kumsaidia mtaji wa kuanzisha biashara au kuboresha biashara na mengine mengi kuhusiana na msaada. Hivyo weka sehemu ya mshahara wako katika bahasha hii ya msaada hii itakusidia kutoharibu bajeti zako nyingine.
SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.
4. DHARURA (Emergence Fund)
Katika maisha yetu ya kibinadamu huwa tunapatwa na dharura sana,na ubaya wa dharura unakuja pale umepatwa na tatizo halafu huna hela ya haraka ya kutatua jambo hilo lakini kama ukiwa umeweka sehemu ya kipato chako katika bahasha hii wala hutopata shida ya kulitatua. Dharura ni nyingi katika maisha na zinatokea kwa ghafla bila taarifa kama vile ajali, radi au kifo kinavyotokea. Ukiwa na fedha ya dharura itakusaidia kuwa na amani ya akili (Peace of Mind).
5. KUSTAAFU (Retirement Fund)
Hii ni njia moja nzuri ya kuweka akiba na kustaafu ukiwa milionea. Weka ,tenga akiba katika bahasha ya kustaafu na iwekeze hela hii katika soko la hisa . Hela hii weka katika bahasha ya kustaafu na usiitumie bali iwekeze katika soko la hisa na mwisho wa siku una staafu ukiwa milionea.
SOMA; Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)
Gawa mshahara wako katika mafungu haya matano na utakuwa na maisha yenye furaha na mafanikio makubwa. Kwa kutoa sadaka utakuwa vizuri kiimani, kwa kutoa msaada utakuwa vizuri kijamii na kwa kuweka akiba na kuwekeza kwenye soko la hisa utajiandaa kwa maisha yako ya baadae.
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi Mhanasishaji na Mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba namba 0717101595 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com
3/23/2015 07:30:00 AM | Labels: FEDHA | 0 Comments
Njia Mbili Za Uhakika Za Jinsi Ya Kupata Fedha.
Fedha ni chombo cha muhimu sana kwa kila mtu anayeishi chini ya jua yaani Duniani kwa ajili ya kukidhi mahitaji muhimu ya kibinadamu. Fedha ni chombo kinachotumika kuhalalisha mambo baina ya pande mbili yaani mtoaji na mpokeaji katika kulinganisha mapatano yaliyofikiwa katika hali ya kuuza au kununua.
Ni chombo ambacho kila mtu anahitaji kuwa nacho usidanganyike kwamba utapata miuzija ya kifedha ikuangukie lahasha! Pesa zinatafutwa ,zinategewa mitego watu wamekuwa hawana kitu kwa kusubiri muujiza wa kifedha uwaangukie. “ fedha huleta jawabu la mambo yote na fedha ni ulinzi’’
NJIA ZA KUPATA FEDHA
1. KUWA MBUNIFU
Njia moja wapo ya kupata,kuongeza fedha ni kuwa mbunifu ,buni njia mbalimbali za kukuingizia kipato yaani miradi. Kadiri unavyotega mitego ndivyo unavyopata pesa au ndivyo unavyonasa fedha zaidi.
Fedha haina mwenyewe wala upendeleo ,tabia ya fedha hufuata pale ilipotegwa jifunze kutega mitego mbalimbali ( vyanzo vya mapato) mwisho wa siku ,wiki,mwezi au mwaka utasema umepata pesa . Huwezi kufanikiwa kama wewe ni mtu wa kukaa tu ,tafuta kazi itakayokupatia kipato na tumia kipato hicho kuanzisha chanzo chako cha mapato.
Kila kitu kina gharama au bei hivyo basi lipia gharama au bei upate huduma na kumbuka kuwa hakuna kitu cha bure “There is no free lunch”
Kuwa bora katika kile unachofanya utalipwa fedha ,utapata fedha kulingana na ubora wa bidhaa au huduma unayotoa.
SOMA; Huu Ni Uwekezaji Wa Uhakika Ambao Hautakuangusha.
2. KUWA MSHINDANI
Kama unafanya biashara na hujui mshindani wako hilo ni tatizo .Lazima umjuwe mshindani wako katika biashara yako au katika kile unachofanya ,mwandishi wa kitabu cha The Entrepreneur Mind ,Kevin Johnson amesema tafuta adui wako yaani mshindani wako ‘find your enemy’na akatoa mfano wa kampuni mbili jinsi ngani zina ushindani wa miongo mingi na kampuni hizo ni ni Apple chini ya mwanzilishi wake Steve Jobs na Microsoft chini ya Bill Gates au kampuni ya cocacola na pepsi hizi kampuni zote zinapigania kutafuta masoko na kila mmoja anamjuwa adui wake yaani mshindani wake kama makampuni makubwa duniani yanaushindani hata wewe unabidi umtambue mshindani wako katika biashara yako ili uweze kuwa bora zaidi.
SOMA; NAFASI MOJA YA KAZI; Changamkia haraka.
Ubora wa kitu utamvutia mteja hata kama hakuwa amekuja kwa ajili ya bidhaa pengine alikuwa anapita tu kando lakin akashawishika baada tu ya kuona huduma unayotoa au bidhaa unayouza. Mfano wa kampuni za simu hapa Tanzania kama vile Tigo,Vodacom au Airtell zina ushindani kila siku huyu katoa hiki leo mwenzake naye kesho kaja na kingine ushindani huu unawafanya waendeshe kampuni zao katika hali ya ushindani inayoleta ufanisi wa kifedha na cha kushangaza wote wanapata wateja .
Ushindi unaonekana kwa Yule atakayekuwa amevutia wateja wengi zaidi na kupata kipato kikubwa zaidi na kudumisha kiwango cha juu cha ufanisi. Ukiwa mtu wa ushindani utatumia bidii kujifunza zaidi na wala hutokubali kushindwa utafanya vitu vyako katika hali ya ubora ili upate ufanisi zaidi maana hakuna mtu anayependa vitu /bidhaa feki ,kila mtu anapenda vitu bora
SOMA; Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.
Mwandishi wa Makala hii ni DEOGRATIUS KESSY ambaye ni mwandishi mhamasishaji na mjasiriamali unaweza ukawasiliana naye kupitia namba ya simu ya mkononi 0717101505 au kupitia barua pepe deokessy.dk@gmail.com
3/16/2015 07:30:00 AM | Labels: FEDHA, MBINU ZA MAFANIKIO | 0 Comments
Sababu 5 Zinazokufanya Wewe Kuishia Kukopa Kila Siku.
Watu wamekuwa wakifanya kazi kila siku ili kuweza kupata pesa ya kuendesha maisha yao ya kila siku . lakini wengi wao wamekuwa na desturi ya kuwa na madeni kila siku na kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo .Kuna madeni ya aina mbili nayo ni madeni ya Mabaya na mazuri .Mazuri ni yale unayokopa kwa ajili ya kuanzisha mradi Fulani na mabaya ni yale ya kukopa kwa ajili ya kula na siyo kuzalisha .Hivyo basi madeni haya ndio yana kufanya wewe kubaki kuwa masikini na kushindwa kufanya shughuli za uzalishaji.
Tuangalie sababu hizo ni zipi zinazokufanya wewe kila siku unaishia kukopa .
1. KUTOWEKA AKIBA.
Wahenga wanasema hivi Akiba haiozi ,hivyo basi kumbe kujiwekea akiba itakusaidia wewe kuondokana na madeni ya kila siku na kuachana na kukopa kabisa.Unaweza kujiwekea akiba kila siku kulingana na kipato chako ambacho una kipata kupitia biashara yako au mshahara wako wa mwezi .Haijalishi una kipato kikubwa kiasi gani kama wewe ni mtu wa kutumia tu bila kuweka akiba wewe ni masikini,
FAIDA ZA KUWEKA AKIBA
· Itakusaidia kwenye dharura ya ghafla inayoitaji hela
· Itakusaidia kupata mtaji
· Akiba haiozi
· Akiba ni ulinzi wako
SOMA; Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.
2. KUTEGEMEA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO
Hili ni tatizo kwa watu wengi kutegemea chanzo kimoja cha mapato mfano,mtu anategemea chanzo kimoja tu cha mapato yaani Ajira .Huwezi kufikia katika eneo la kujidai ,eneo la kuwa na uhuru wa kipesa (comfort zone)kwa kutegemea chanzo kimoja cha mapato.Ili kuepukana na madeni kila siku ambayo hayana tija kwako .Anza leo kuwa na vyanzo vya mapato yaani ’’ multiple streams of income ,money machines’’.
Fanya vyanzo vyako vya mapato kuwa kama matawi ya mti utakuwa na uhuru wa kifedha.
3. KUISHI JUU YA KIPATO CHAKO
Hili ni tatizo kwa watu wengi ,kujiingiza katika gharama zisizo za kilazima mfano ,mtu anapokea mshahara laki na nusu halafu matumizi yake ni zaidi ya laki tatu.
Je unafikiri mtu atayaepuka madeni ya kila siku? jibu ni hapana. Anza kuishi chini ya kipato chako leo ,acha tabia ya kuigaiga Fulani amenunua simu mpya na wewe unataka ununue ili mradi tu na wewe uonekane upo kwenye chati kumbe unajimaliza mwenyewe bila kujijua. Haijalishi unakipato kikubwa kiasi gani yakupasa uishi chini ya kipato chako. “whatever your income live below your means”
SOMA; Hii Ndio Sababu Kwa Nini Watu Wanafurahia Pale Unapoanguka...
4. KUTOJILIPA
Watu wengi wanafanya kazi sana na wana walipa watu wengine lakini wanajisahau kujilipa wao kwanza .Wewe ndio mfanyaji kazi unatakiwa kujilipa kwanza wewe.
“pay yourself first” jilipe kwanza wewe 10% ya kipato chako hii itakusaidia sana kujiwekea akiba na kuondokana na kukopa kila siku.Anza leo kujilipa kama ulikuwa haujui hii fungua akaunti maalumu kwa ajili ya kuhifadhi pesa yako na usiiguse ndani ya miaka miwili utakuw mtu mwingine.
SOMA; Nafasi Ya Wewe Kuwa Bora Kila Siku… NA ZAWADI YA TSH 365,000/=
5. KUISHI BILA YA KUJIWEKEA BAJETI YA MATUMIZI YAKO
Kuishi bila ya kuwa na bajeti ya matumizi yako kwa mwezi ,wiki, siku ni sawa na kusafiri bila ya kujua unapokwenda. Ukiwa na bajeti itakusaidia kujua matumizi yako ya kila siku na kuweza kujiepusha na kukopa hivyo basi anza leo kuwa na bajeti yako ya matumizi.
‘’ ukijua unapokwenda katika safari yako utafika uendako’’
Makala hii imeandikwa na DEOGRATIUS KESSY ambaye ni mwandishi,mjasiriamali na mwamasishaji unaweza kuwasiliana naye kwa kupitia simu namba 0717101505 au kwa barua pepe (Email) deokessy.dk@gmail.com
ASANTE !
3/02/2015 07:35:00 AM | Labels: FEDHA, MBINU ZA MAFANIKIO, MBINU ZA MAISHA | 0 Comments
Maazimio Matano Muhimu Ya Fedha Kwa Kila Kijana Kuweka Mwaka Huu 2015.
Bado tupo kwenye msimu wa mwaka mpya na huu ni wakati muhimu wa kuweka maazimio na malengo mbalimbali ili kuboresha maisha yetu zaidi.
Huenda tayari umeshaweka malengo na mipango yako ya mwaka 2015, leo tutakumbushana mambo machache ambayo ni ya muhimu sana kuyajumuisha kwenye malengo yako ya mwaka huu 2015.
Kama bado hujaweka malengo mpaka leo bado hujachelewa, unaweza kukaa chini leo na kuandika malengo yako kwenye karatasi na kuanza kuyafanyia kazi.
Kama huna mpango wa kuweka malengo kabisa kwa mwaka huu pole…
Yafuatayo ni maazimio muhimu kuweka kwenye malengo yako ya kifedha kwa mwaka huu 2015;
1. Weka akiba zaidi ya ulivyoweka mwaka jana.
Kama mwaka jana ilikuwa unaweka akiba, mwaka huu ongeza kiwango cha akiba unachoweka. Kama huna utaratibu wakujiwekea akiba kabisa anza na kuweka pembeni asilimia 10 ya kile unachopata. Ukipata elfu kumi, weka elfu moja pembeni. Ukipata laki moja weka elfu kumi pembeni. Baada ya muda mfupi utaona mabadiliko makubwa ya kifedha kwenye maisha yako.
2. Punguza madeni yako.
Madeni ni mzigo, madeni ni utumwa, mtu anayekudai anaweza kunyanyasa utu wako muda wowote. Mwaka huu weka azimio la kupunguza madeni yako na kama ikiwezekana lipa yote kabisa. Kaa chini na wale wanaokudai na wape pendekezo la njia rahisi kwako kuwalipa kisha anza kuwalipa. Utanunua uhuru wako ulioupoteza.
3. Tengeneza, badilisha bajeti yako.
Ni muhimu sana kuishi kwa bajeti, kama mpaka sasa huna bajeti tafadhali sana tengeneza bajeti yako leo. Amua ni kiasi gani utakachoishi nacho kwa siku, wiki na hatimaye mwezi. Na jitahidi sanakuishi kwa kiasi hiko, usinunue vitu kwa tamaa tu, nunu kile ulichopanga kwenye bajeti. Kama umepanga mwezi huu hununui nguo, usishawishike kununua nguo hata ukikutana nayo nzuri kiasi gani, nguo nzuri huwa haziishi. Siku ambayo bajeti yako inaruhusu utapata nzuri kuliko uliyokutana nayo.
4. Jifunze kuhusu uwekezaji.
Bila shaka uwekezaji ni somo gumu sana kwa vijana. Wengi hawapendi kusikia kitu hiki na huona ni kitu kinachohitaji elimu kubwa. Ukweli ni kwamba uwekezaji ni rahisi na ni njia rahisi kwako kukuza kipato chako. Kuna aina nyingi za uwekezaji, kuna uwekezaji wa kununua mali, uwekezaji wa fedha na kadhalika. Unaweza kuanza kujifunza hapa hapa kwa kubonyeza maandishi haya
Soma; Hivi ndivyo unavyoweza kutajirika kwa kuanza na shilingi elfu moja.
5. Jijengee nidhamu ya fedha.
Kama hutakuwa na nidhamu ya fedha, yote tuliyojadili hapo juu hayataweza kukusaidia. Mara zote tumia pungufu ya unachokipata, yaani matumizi yako yasizidi mapato yako. Na pia kwenye kuweka akiba weka akiba na inayobaki ndio ufanye matumizi. Ukifanya matumizi ili inayobaki ndio uweke akiba hutabakiwa na kitu.
Wewe kama kijana ni muhimu sana kwako kujijengea misingi imara ya kifedha na kiuchumi. Weka maazimio hayo matano muhimu mwaka huu 2015 na anza kuyafanyia kazi.
1/12/2015 11:20:00 AM | Labels: FEDHA, SOKO LA HISA(DSE) | 0 Comments
Kuhusu Uwekezaji Tanzania
Kupitia mtandao huu utajifunza fursa mbalimbali za uwekezaji na pia kupata taarifa zinazohusu uwekezaji.
AINA ZA UWEKEZAJI TANZANIA.
Kwa bahati nzuri sana kuna aina nyingi sana za uwekezaji Tanzania. Kuna kila rasilimali na fursa mbalimbali za uwekezaji. Ugunduzi wa mafutra na gesi unaoendelea kufanyika Tanzania unaifanya Tanzania kuwa moja ya nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi sana.Kuna aina mbalimbali za uwekezaji zinazoweza kufanyika Tanzania.
1. Uwekezaji wa mali.
Tanzania kuna arhi kubwa sana ambapo mtu anaweza kununua na kuendeleza kwa kujenga majengo ya kibishara na hata makazi.Pia ardhi hii inaruhusu kilimo na hivyo mtu unaweza kuwekeza kwenye kilimo cha biashara.
2. Bishara.
Kwa kuwa uchumi wa tanzania unakua kwa kasi sana mtu yeyote anayweza kuwekeza kwenye biashara anaweza kuapata faida kubwa. Biashara za bidhaa na huduma zinakua kwa kasi sana kutokana na ongezeko la watu na muingiliano wa kimataifa.3. Uwekezaji katika maliasili na gesi.
Tanzania ina gesi nyingi sana ambayo bado haijachimbwa. Hii inatoa fursa kubwa sana ya uwekezaji.4. Uwekezaji wa hisa na vipande.
Hii ni fursa nzuri ya uwekezaji kwa watu ambao wana miotaji kidogo. Soko la hisa la dar es salaa limeorodhesha makampuni mbalimbali ambayo mtu anaweza kununua hisa.Pia dhamana ya uwekezaji UTT, inatoa fursa kwa watu kununua vipande na vipande hivyo kuongezeka thamani na hivyo kunufaika zaidi.
Kuna fursa nyingi sana za uwekezaji ambazo utajifunza kupitia mtandao huu.
11/02/2014 04:58:00 PM | Labels: BIASHARA, DHAMANA YA UWEKEZAJI(UTT), FEDHA, HABARI ZA UWEKEZAJI, SOKO LA HISA(DSE), UCHUMI, UWEKEZAJI WA MALI(PROPERT) | 0 Comments
