Adui Yako Anaanzia Hapo Ulipo Na Anaanza hivi.

Adui yako ni wewe mwenyewe na anaanza na hofu zako...
Una hofu ngapi leo asubuhi?
Una hofu kama utakula leo mchana na jioni?
Una hofu kama mshahara utaingia kabla ya krismas?
Una hofu kama krismasi yako itakuwa nzuri?
Una hofu kama baraza la mawaziri litabadilishwa au halitabadilishwa?
Una hofu kama serikali itafanya maisha kuwa rahisi zaidi?
Una hofu kama 2015 chama unachokipenda kitashika madaraka?
Una hofu kama mpenzi/mwenza wako atakusaliti/atakuacha?
Una hofu kama hofu zako zitaosha??
Karibu hofu zote hapo juu hazina msaada mkubwa kwako au huwezi kuziathiri. Na kuendelea kuziendekeza ndio zinakuzuia ushindwe kufikiria mambo makubwa yatakayokuwezesha kufikia mafanikio makubwa.
Yaani kichwa kimoja chenye hofu zote hizo kitapata wapi nafasi ya kuweka jambo la muhimu?
Hofu hizi ndio adui mkubwa wa mafanikio kwako...
Usizipeleke hofu hizi 2015....

0 comments: