Showing posts with label UONGOZI. Show all posts
Showing posts with label UONGOZI. Show all posts

Sifa Unazotakiwa Kuzitambua Kwa Kiongozi Anayeweza Kuleta Mabadiliko.



Habari na karibu ndugu mpenzi msomaji wa blogu hii ya JIONGEZE UFAHAMU. Ni matumaini yetu umekuwa na wiki ya mafanikio sana.
Leo tutaangalia sifa unazotakiwa kuzitambua kwa mtu unayetaka awe kiongozi au unamtegemea awaongoze.
  1. Tabia
Mtu mwenye tabia nzuri au njema anakuwa na uaminifu, utiifu, nidhamu, kutegemewa, uvumilivu, kujitambua na pia anakuwa na bidii katika kazi. Wakati kwa upande mwingine mtu asiye na tabia njema au nzuri anakuwa hana uwezo wa kuwajibika kwa matendo yake, hawezi kukamilisha kazi kwa wakati, na pia hatimizi ahadi au majukumu yake.
  1. Kuhamasisha
Mtu ambaye anajua wapi anaelekea anakuwa na uwezo wa kuhamasisha wengine wafuatane nae kutokana na ahadi au mambo mazuri yanayopatikana kule anakoelekea. Kwa hiyo unahitaji kuangalia mtu Yule ambaye anafuatwa na watu wazuri na sio wale walio wa kawaida kabisa pia angalia huyu mtu anamtazama nani kama mtu anayemhamasisha bila shaka kwa Yule anayefaa kuwa kiongozi utamkuta anamfuatilia mtu ambae pia ni kiongozi na ana sifa njema


  1. Mtazamo chanya
Tafuta mtu Yule ambaye hana vizuizi katika akili yake kwa kuona jambo Fulani haliwezekani bali awe ni Yule mwenye nia ya kujaribu pamoja na kuwaza chanya kuwa atafanikiwa katika lile atendalo na anakuwa hazuiwi na vikwazo binafsi.
  1. Ufanisi mzuri katika kuwasiliana
Viongozi wazuri ni wale ambao wanaweza kuwasiliana vema, wanakuwa wanajihusisha vema na wale wanaoongea nao kwa kuweza kumtazama ana kwa ana pamoja na kuwa na tabasamu kwa Yule anayeongea naye. Kiongozi mzuri si Yule anayeweza kuwasilisha ujumbe wake lakini pia anakuwa na uwezo mzuri wa kusikiliza pia wale anaowaongoza.
  1. Kujiamini
Bila kujali hali gani katika wakati husika kiongozi pamoja na kundi wanapitia , kiongozi mzuri ni Yule anayekuwa anayejiamini na kuwa na ujasiri kuwa yeye pamoja na timu anayoiongoza wanaweza kusogea hatua kutoka walipofika
  1. Nidhamu

Kiongozi ni Yule mwenye nidhamu anayeweza kutawala hisia zake na pia ana uwezo wa kusimamia au kutawala muda wake jinsi ya kuutumia ili kumsaidia kupata mafanikio kwa ajili yake na timu anayoiongoza
  1. Rekodi nzuri ya mafanikio
Ni vizuri ukacheki historia yake ya nyuma ya utendaji wa mtu. Na kiongozi mzuri utakuta ana rekodi nzuri ya utendaji

Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano:
Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blog yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.

Jinsi ya Kuwaandaa Kuongoza Viongozi Watarajiwa (Chipukizi)

Habari na karibu ndugu mpenzi msomaji wa blogu hii ya JIONGEZE UFAHAMU. Ni matumaini yetu umekuwa na wiki ya mafanikio sana.
Leo nitazungumzia namna ya kuwaandaa watu wenye sifa za uongozi ambao umewatambua upo nao katika timu yako katika taasisi. Kuwaandaa viongozi hawa watarajiwa kunahusisha wewe ambaye tayari ni kiongozi pamoja na hao viongozi watarajiwa , nah ii inaweza kulinganishwa kwa kiasi Fulani kama unawawapatia mafunzo.

1.     Tengeneza Mahusiano na Viongozi Chipukizi Unaowaandaa
Viongozi chipukizi ambao umeshawatambua unahitaji kuwafahamu, kuwasikiliza historia za maisha yao ili uweze kuwajua zaidi ya vile unavowajua tu kiofisi. Huhitaji kujua kuhusu uwezo au ubora wao tu bali unahitaji pia kujua kuhusu madhaifu yao pia ili uweze kujua namna ya kuwafanya wakamilifu kwa hayo mapungufu uliyoyatambua. Na ukiweza kujenga mahusiano mazuri maanake utafanya wakupende na pia kuongeza nia na kiu kwao kujifunza kutoka kwako

SOMA; Hatua 6 za Kuwalea Viongozi Watarajiwa (Chipukizi)


2.     Washirikishe ndoto yako
Wakati unaendelea kuwafahamu usiwaache wao peke yao tu wakuambie ya kwao, na wewe pia unahitaji kuwashirikisha pi historia ya maisha yako na unahitaji kwenda hatua ya ziada kwa kuwashirikisha ndoto yako kuhusiana na taasisi ambayo unaiongoza. Na hii itawasaidia kujua ni wapi unataka kwenda na hivo kujiunga kujitoa kufuatana nawe mpaka mwisho wa safari yako
3.     Waombe utayari wao kujitoa kiuongozi
Moja ya kiungo muhimu ambacho kinaweza kumfanya kiongozi chipukizi kuwa kiongozi mwenye mafanikio, ni utayari wa kujitolea kiuongozi. Ni muhimu sana kwa hawa viongozi chipukizi unaowaandaa wawe wamejitoa kwa ajili ya uongozi pamoja na taasisi. Na unahitaji kuwaeleza gharama ambayo itawachukua kwa wao kuwa viongozi, na jambo la muhimu ni uwe mkweli kuhusu mambo ambayo watahitaji kuzingatia au kuyajua hata kabla ya hatua yenyewe ya kufanya maamuzi ya kukubali kuweza kujitoa kiuongozi.
4.     Weka malengo kwa ajili ya ukuaji
Viongozi hawa chipukizi wanahitaji kujua malengo yaliyo fasaha ambayo wanatakiwa kuyapigania au kuyafanikisha, nah ii itawasaidia kujua ni nini wnatakiwa kufanya na pia ni vitu gani vinatarajiwa kutoka kwao. Jambo muhimu zaid la kuzingatia ni unapoweka malengo zingatia malengo yawe yako wazi, fasaha na yanayoeleweka. Malengo yawe ni sahihi kwao lakini pia yawe yanaweza kupimika. Baada ya kuyafahamu hayo malengo ni vizuri yawekwe katika maadnishi ili kila mmoja aweze kujitoa kikamilifu katika malengo hayo
5.     Weka mambo ya msingi sawa
Ni muhimu sana kuweka misingi kwa kuwaelewesha majukumu yao na wayafahamu kwa undani. Weka kwa ufasaha mategemeo yako kwao lakini pia na wao wajue vipaumbele ni vipi katika majukumu yao. Na uhakikishe wanaweza kujua tofauti kati ya kazi iliyo ya umuhimu sana na ile kazi yenye umuhimu kiasi.
6.     Mfumo wa ufundishaji unaofaa
Kuna hatua tano muhimu zinazoweza kukupatia matokeo mazuri hasa inapohusisha kuwaandaa kiuongozi viongozi chipukizi
                               i.            Kuwa mfano kwanza kwa kila unachotaka waweze kukifanya
                             ii.            Wafundishi au waelekeze
                          iii.            Simamia maendeleo ya kile unachowaelekeza
                          iv.            Wahamasishe
                             v.            Wape fursa pia ya kutengeneza viongozi kati yao viongozi chipukizi
7.     Simamia maendeleo yao bila kuacha
Ni muhimu ukawa na mikutano iliyo rasmi na isiyo rasmi pia ili kuweza kujua mahitaji, matatizo ambayo wanakumbana nayo pia. Na hii itakusaidia kuwapatia vifaa sahihi zaidi na kuendelea kuwapa ujasiri na kuwahamasisha.

Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano:
Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blog yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.