NENO LA LEO; Njia Isiyokuwa Na Foleni.
There are no traffic jams along the extra mile. –Roger Staubach
Hakuna foleni unapokwenda mbali zaidi.
Unapofanya kile ambacho kila mtu anafanya utakutana na ushindani mkubwa sana.
Unapofanya kitu chenye ubora mkubwa na wa kipekee utakuwa mwenyewe na hakutakuwa na ushindani.
Mara zote nenda maili ya ziada, fanya zaidi ya wengine na utapata zaidi.
Nakutakia siku njema.
12/30/2014 07:48:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachohitaji Ili Kufanikiwa.
In order to succeed, your desire for success should be greater than your fear of failure. –Bill Cosby
Ili kufanikiwa, hamu yako ya mafanikio inabidi iwe kubwa kuliko hofu yako ya kushindwa.
Kinachokufanya mpaka sasa hujafanikiwa ni hofu ya kushindwa. Una hofu kwamba ukijaribu kitu fulani unachokifikiria utashindwa.
Ili ufanikiwe inabidi uweze kuishinda hofu hiyo na utaweza kuishinda kama kiu yako ya kufanikiwa ni kubwa kuliko hofu ulizo nazo.
Nakutakia siku njema.
12/29/2014 07:15:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Hapa Ndio Pa Kuanzia, Hasa kwa mwaka 2015…
The way to get started is to quit talking and begin doing. –Walt Disney
Njia ya wewe kuanza ni kuacha kuongea na kuanza kufanya.
Ni rahisi sana kuongea, kila mtu anaweza kuongea..
Ni rahisi sana kupanga, kila mtu anapenda kupanga na kupanga tena baada ya kupanga.
Lakini kuongea na kupanga hakutofanya lolote, hakutokufikisha popote.
Kufanya ndio kutakutoa hapo ulipo, vitendo na sio maneno au mipango.
Acha kupanga na kuongea kila siku, 2015, maneno kidogo vitendo vingi..
Nakutakia siku njema.
12/28/2014 12:31:00 PM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Hiki Ndio Unachokiishi
Too many of us are not living our dreams because we are living our fears. –Les Brown
Wengi wetu hatuishi ndoto zetu kwa sababu tunaishi hofu zetu.
Acha sasa kuzuiwa na hofu na anza kuishi maisha ya ndoto zako. Hakuna kinachoshindikana kama kweli utakuwa umedhamiria.
Nakutakia siku njema.
12/19/2014 10:38:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Huwezi Kuanguka Kama Hutafanya Hivi.
You can’t fall if you don’t climb. But there’s no joy in living your whole life on the ground. –Unknown
Huwezi kuanguka kama hutopanda. Lakini hakuna furaha kwenye maisha kama utaishi maisha yako yote ukiwa chini.
Anza sasa kupanda na kuwa bora zaidi, ndio unaweza kuanguka ila utajifunza mengi na utaweza kufikia juu zaidi.
Ukiendelea kuogopa kuanguka, utaendelea kubaki hapo ulipo.
Nakutakia siku njema.
12/18/2014 08:13:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Hiki Ndio Chanzo Cha Furaha.
Happiness is not something readymade. It comes from your own actions. –Dalai Lama
Furaha sio kitu ambacho kimetengenezwa tayari. Furaha inatokana na matendo yako mwenyewe.
Kama utakuwa na matendo yenye maana kwako na kwa wanaokuzunguka ni lazima yatakuletea furaha. Furaha hupewi na mtu mwingine.
Soma; HII NI HAKI YAKO YA KUZALIWA, USITEGEMEE KUPEWA NA WENGINE.
Nakutakia siku njema.
12/12/2014 07:30:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Mlango Mpya Wa Furaha
When one door of happiness closes, another opens, but often we look so long at the closed door that we do not see the one that has been opened for us. –Helen Keller
Mlango mmoja wa furaha unapojifunza, mlango mwingine unafunguka, lakini tunaishia kuangalia mlango uliojifunza kwa muda mrefu na hivyo kushindwa kuona mlango mpya uliofunguka.
Acha kuangalia matatizo yako tuu, angalia pembeni na utaona fursa nyingi za kubadili na kuboresha maisha yako.
Nakutakia siku njema.
12/10/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Ni Mara Ngapi Unahitaji Kusimama Tena?
Fall seven times and stand up eight. –Japanese Proverb
Anguka mara saba, nyanyuka mara ya nane.
Haijalishi ni mara ngapi umeshindwa, cha msingi ni kuendelea tena.
Kukata tamaa ni mwiko kama kweli unataka kuyafikia mafanikio makubwa.
Nakutakia siku njema.
12/09/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Jambo Kubwa Na La Kushangaza.
We can easily forgive a child who is afraid of the dark; the real tragedy of life is when men are afraid of the light. –Plato
Tunaweza kumsamehe mtoto mdogo anayeogopa giza; ila jambo kubwa na la kushangaza kwenye maisha ni pale mtu mzima anapoogopa mwanga.
Ni kipi unachokiogopa kukifanya kwenye mwanga? Maana hiko ndio kinachokuzuia wewe kufikia mafanikio makubwa.
Nakutakia siku njema.
12/08/2014 07:12:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Hapa Ndio Unapoweza Kuanzia Na Hiki Ndio Unachoweza Kufanya.
Start where you are. Use what you have. Do what you can. –Arthur Ashe
Anzia hapo ulipo. Tumia hiko ulicho nacho. Fanya unachoweza.
Usipoteze tena muda kufikiri ni wapi pa kuanzia, uanze na nini au ufanye nini. Unachohitaji ni kuanza kupiga hatua na mambo mengine yote yatakwenda vizuri.
Nakutakia siku njema.
12/07/2014 08:17:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Chochote Unachotaka Kuwa Kipo Huku
Everything you’ve ever wanted is on the other side of fear. –George Addair
Chochote ambacho umewahi kutaka kipo upande wa pili wa hofu.
Acha sasa kuwa na hofu na chukua hatua kupata kile unachotaka.
Kumbuka hakuna kingine zaidi ya kuchukua hatua.
Nakutakia siku njema.
12/06/2014 07:45:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Umepangiwa Kuwa Mtu huyu…
The only person you are destined to become is the person you decide to be. –Ralph Waldo Emerson
Mtu pekee uliyepangiwa kuwa ni yule unayeamua kuwa.
Kama unaamua kuwa na mafanikio utakuwa nayo kweli na kama unaamua kuwa wa hovyo utakuwa wa hovyo.
Maamuzi ni yako, uchaguzi ni wako.
Nakutakia siku njema.
12/05/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Maana Halisi Ya Vikwazo.
Obstacles are those frightful things you see when you take your eyes off the goal. –Henry Ford
Vikwazo ni yale mambo ya kutisha unayoyaona pale unapoondoa macho yako kwenye malengo yako makubwa.
Ukishaweka malengo na mipango yako usiangalie tena pembeni, utaona mambo mengi ambayo yatakukatisha tamaa.
Nakutakia siku njema.
12/04/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Njia Moja Ya Uhakika Ya Kuepuka Kupingwa.
There is only one way to avoid criticism: do nothing, say nothing, and be nothing. –Aristotle
Kuna njia moja pekee ya kuepuka kupingwa; usifanye chochote, usiseme chochote na usiwe chochote.
Vinginevyo chochote utakachofanya lazima kuna mtu atakupinga au kukukosoa.
Fanya kile unachoona ni sahihi kufanya na komaa nacho mapaka ufikie mafanikio.
Nakutakia siku njema.
12/03/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Jinsi Ya Kuua Hofu
If you hear a voice within you say “you cannot paint,” then by all means paint and that voice will be silenced. –Vincent Van Gogh
Kama unasikia sauti ndani yako inayokuambia huwezi kuchora basi kwa njia yoyote ile hakikisha unachora na sauti hiyo itanyamazishwa.
Usikubali kukatishwa tamaa na nafsi yako mwenyewe. Fanya kile unachohofia na hofu itakufa yenyewe.
Natutakia siku njema.
12/02/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Kisasi Bora
The best revenge is massive success. –Frank Sinatra
Kisasi bora ni mafanikio makubwa.
Kama mtu amekufanyia jambo baya na unataka kulipa kisasi, kisasi bora kulipa ni kuhakikisha unafanikiwa sana.
Nakutakia siku njema.
12/01/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Uwekezaji Unaolipa Riba Kubwa Sana
An investment in knowledge pays the best interest. –Benjamin Franklin
Uwekezaji kwenye elimu/ujuzi ndio uwekezaji unaolipa riba kubwa sana.
Anza sasa kuwekeza kwenye ujuzi na elimu yako, jifunze mambo mapya na yafanyie kazi.
Jinsi unavyojifunza zaidi ndivyo unavyoongeza thamani yako na hivyo kuongeza kipato chako.
Nakutakia siku njema.
11/30/2014 08:08:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Siku Mbili Muhimu Sana Kwenye Maisha Yako.
The two most important days in your life are the day you are born and the day you find out why. –Mark Twain
Siku mbili muhimu sana kwenye maisha yako ni siku uliyozaliwa na siku uliyojua kwa nini ulizaliwa.
Najua wengi tunajua siku tulizozaliwa ila ni wachache sana wanaojua kwa nini walizaliwa.
Kama bado hujajua kwa nini ulizaliwa kwaribu tusaidiane kujua kwa nini ulizaliwa, yaani ni nini hasa unatakiwa kufanya na maisha yako.
Andika email yenye kichwa cha habari KWA NINI NILIZALIWA na maelezo mengine muhimu kuhusu wewe kisha tuma kwenye email ushauri@kisimachamaarifa.co.tz
Nakutakia siku njema.
11/29/2014 09:52:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Kuhusu Kuendesha Siku Au Kuendeshwa na Siku.
Either you run the day, or the day runs you. –Jim Rohn
Kwenye siku yako ni labda unaiendesha siku au siku inakuendesha wewe.
Unaiendesha siku pale ambapo unakuwa na malengo na mipango yako ambayo unaifuata.
Unaendeshwa na siku pale ambapo unafanya kile kinachotokea mbele yako.
NINAJUA UNAJUA UNACHOTAKIWA KUFANYA, FANYA SASA, LEO HII ILI UWEZE KUIENDESHA SIKU YAKO.
Nakutakia siku njema.
11/28/2014 07:20:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments
NENO LA LEO; Unachohitaji Ili Kubadili Maisha Yako.
You can never cross the ocean until you have the courage to lose sight of the shore. –Christopher Columbus
Huwezi kuivuka bahari mpaka pale utakapokuwa na ujasiri wa kupoteza taswira ya ufukwe.
Tunapenda vitu vizuri lakini tunaogopa kupoteza tulivyo navyo. Huwezi kupata vitu vipya kama hutaacha hivyo ulivyonavyo sasa.
Nakutakia siku njema.
11/27/2014 07:00:00 AM | Labels: NENO LA LEO | 0 Comments