Showing posts with label JIKINGE. Show all posts
Showing posts with label JIKINGE. Show all posts

Vyakula Vitano Ambavyo Vinaimarisha Afya Yako.

Sehemu kubwa ya magonjwa yanayotusumbua zama hizi yanatokana na mfumo wetu wa maisha. Magonjwa kama kisukari, presha ya kupanda na hata kansa yanatokana na mfumo wa maisha tunayoishi.

Vyakula tunavyokula, vitu tunavyokunywa na mtindo wa maisha tunaoendesha vimekuwa chanzo kikubwa cha magonjwa haya yanayosumbua watu wengi kwa sasa.

Ili kujikinga na magonjwa haya, kuna baadhi ya vitu unavyohitaji kubadili kwenye maisha yako. Leo tutajadili vyakula vitano ambavyo ukijenga tabia ya kuvitumia utajikinga na maginjwa mengi sana. Uzuri wa vyakula hivi ni kwamba vinapatikana kwa urahisi na havina gharama kubwa.

1. Nafaka ambazo hazijakobolewa.

Utumiaji wa nafaka ambazo hazijakobolewa unapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo. Pia nafaka hizi zinaondoa sumu kwenye mwili.

nafaka

2. Bisi(Popcorn).

Huenda umekuwa ukiziona bisi na kufikiri ni chakula cha watoto. Bisi zina virutubisho vinavyoitwa polyphenols ambavyo vinapambana na seli zinazosababisha kansa.

popcorn

3. Mayai.

Mayai yana virutubisho vinavyoitwa lutein ambavyo vinaondoa sumu mwilini. Virutubisho hivi vinaweza kuyalinda macho yako na upofu.

mayai

4. Maharage.

Maharage yana virutubisho vingi ambavyo vinaondoa sumu mwilini.

maharage

5. Sukari asili.

Vyakula vyenye sukari asili kama asali na sukari guru vina virutubisho vinavyoondoa sumu kwenye mwili.

asali

Fanya mabadiliko katika vyakula unavyokula ili uweze kuimarisha afya yako.

Kwa ushauri zaidi wa kiafya andika email kwenda afya@kisimachamaarifa.co.tz

KARIBU KWENYE MTANDAO WA AFYA IMARA

AFYA IMARA ni mtandao unaokupatia makala zinazohusiana na afya.
Kupitia mtandao huu utajifunza mbinu mbalimbali za kulinda na kuboresha afya yako.
Kama wote tunavyojua afya ni kiungo muhimu sana kwenye maisha yetu.
Bila kuwa na AFYA IMARA hatuwezi kufikia mipango na malengo tuliyojiwekea kwenye maisha yetu.
Tembelea mtandao huu kila siku ili uweze kujifunza kuhusu afya yako.

MAMBO UTAKAYOJIFUNZA KUPITIA AFYA IMARA.

Kupitia afya imara utajifunza mambo yafuatayo kuhusu afya;
1. Dalili za magonjwa mbalimbali.
2. Jinsi ya kujikinga na magonjwa.
3. Mazoezi na afya.
4. Lishe kwa makundi mbalimbali ya watu.
5. Afya kwa makundi mbalimbali kama watoto, wanawake na wazee.
MASWALI NA USHAURI ZAIDI.
Kama una tatizo la kiafya ambalo ungependa kupata ushauri zaidi unaweza kuandika na ukapewa ushauri wa kitaalamu. Andika email kwenda afya@kisimachamaarifa.co.tz
Tujenge AFYA IMARA ili tuweze kuwa na maisha bora.