Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.

Kama mwaka huu 2015 umepanga kuanza biashara usifanye kosa moja ambalo huwa linafanywa na wafanyabiashara wengi wanapoanza.
Usianze biashara kama hujui miaka mitano ijayo biashara yako itakuwa imefika wapi.
Ni muhimu sana kuwa na picha kubwa ya biashara yako ili unapoanza usisahau ulipotaka kufika.
Kama utaanza biashara ukiwa hujui miaka mitano utakuwa wapi hutafika popote. Maana biashara itakapoanza kukuchanganya utajikuta ukihangaika na matatizo yanayokusonga na kusahau kukuza biashara yako.
Pata picha ya kule unakokwenda kabla hata ya kuanza safari.

0 comments: