Mbinu 9 Za Kukuwezesha Kuamka Asubuhi Na Mapema Ukiwa Na Nguvu.

Kuamka asubuhi na mapema ni moja ya siri ya watu wenye mafanikio makubwa. Hii ni kwa sababu asubuhi na mapema akili inakuwa vizuri na hivyo kuweza kufanya majukumu yanayohitaji kutumia vizuri akili yako.

Pamoja na muda huu kuwa mzuri sana kwa kutekeleza majukumu, sio rahisi sana kuamka asubuhi. Watu wengi wamekuwa wakijaribu kuamka asubuhi lakini wanaishia kuzima alamu zao na kurudi kulala.

Leo hapa UTAJIONGEZA na mbinu 9 zitakazokuwezesha kuamka mapema na ukiwa na nguvu.

1. Soma kitabu au jarida dakika 30 kabla ya muda wa kulala.

2. Usile au kunywa pombe mda mfupi kabla ya kulala.

3. Weka simu au kompyuta yako mbali, mwanga wa simu na kompyuta hupunguza usingizi.

4. Usijiwekee majukumu mengi ya kufanya asubuhi. Fanya yale ambayo ni muhimu tu.

5. Panga kupata kifungua kinywa kizuri, hii itakuhamasisha kuamka mapema.

6. Fanya mazoezi, sio lazima yawe magumu.

7. Kunywa maji, itarudisha maji uliyopoteza kwa siku nzima.

8. Weka alarm yako kwenye chumba kingine ambapo utalazimika kuamka ili ukaifuate.

9. Pata jua la kutosha.

Unaweza kupitia mbinu hizi kwenye picha hapo chini.

how-to-wake-up-early

0 comments: