Kitu Hiki Kimoja Ni Lazima Kitokee Kwenye Maisha Yako, Japo Hukipendi.

Tukiangalia historia ya dunia tokea enzi na enzi, tunaona jinsi ambavyo watu wamepitia changamoto mbalimbali.
Tunaona jinsi ambavyo tawala kubwa kama Roma zilivyopigania ukuaji wa utawala wao na hata kufikia kufa kabisa.
Tumeona watu wakitokea kwenye maisha magumu, kujaribu vitu vipya kushindwa lakini kuwa vinganganizi na hatimaye wakafanikiwa.
Kitu kimoja ambacho naweza kukuhakikishia kitatokea kwenye maisha yako ni changamoto au vikwazo.
Haijalishi utapata elimu kiasi gani, haijalishi utakuwa na fedha kiasi gani na haijalishi utakuwana na hadhi kiasi gani. Kila ngazi utakayokuwa unapitia kwenye maisha yako utakutana na changamoto na vikwazo.
Tunaweza kusema changamoto hizi ni njia ya dunia kutupa mitihani ili tuoneshe kama kweli tuko tayari kupata kile tunachotaka.
Katika changamoto yoyote utakayopitia hata iwe kubwa kiasi gani, unaweza kufanya moja kati ya haya mawili;
1. Kukubali changamoto hiyo iwe ndio mwisho wako na kutoendelea na mapambano ya kupata kile ulichotaka.
2. Kutumia changamoto hiyo kukua zaidi na kukupa nguvu na hasira ya kupata kile ulichokuwa unataka.
Uchaguzi ni wako, kama utaamua kukubali kukata tamaa kila la kheri.
Kama utaamua kiendelea na mapambano licha ya changamoto unazokutana nazo weka email yako hapo juu ili uendelee kupata mbinu za kupambana na changamoto hizo.
TUPO PAMOJA.

0 comments: