Huyu Ni Mjasiriamali Mwenye Hamasa Kubwa sana. Unaweza kujifunza kila kitu kutoka kwake.

Moja ya vitu ambavyo vitakuwezesha wewe kufanikiwa kwenye ujasiriamali ni kupend akile unachokifanya. Kama kweli unapenda unachofanya, utakuwa na hamasa kubwa sana ya kukifanya.

Hamasa hii ndio inakuwezesha kuvuka vikwazo, kuwa mbunifu na kuweza kufikia mafanikio makubwa sana.

Kuna mjasiriamali mmoja mkubwa sana duniani ambaye ana hamasa kubwa sana ambayo huwa inawashangaza wengi. Pamoja na mafanikio makubwa aliyonayo, bado haoni shida kufanya mambo madogo madogo ambayo yanamfanya azidi kufikia mafanikio makubwa.

Mjasiriamali ninayemzungumzia ni Richard Branson. Huyu ni raia wa uingereza na anamiliki kampuni kubwa ya Virgin Group ambayo ina kampuni zaidi ya 400 chini yake. Huyu ni mmoja wa watu matajiri sana duniani, akikadiriwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 4.9.

branson

Leo hapa utajiongeza na baadhi ya mambo anayofanya Branson ambayo yatakufanya na wewe uwe na hamasa zaidi kwenye ujasiriamali unaofanya.

Katika ufunguzi wa hotel mpya chini ya kampuni yake ya Virgin, kulikuwa na tetesi kwamba Richard alikuwa anawatembelea wateja wake usiku na kuwafurahisha zaidi.

branson 2

Tetesi hizo zilithibitishwa na Branson mwenyewe pale alipowatembelea wateja chumbani kwao na kuwasomea hadithi wakati wa kulala. Kama ambavyo wazazi huwa wanawasomea watoto wao hadithi.

branson 3

Unaweza kuona ni kitu kidogo ila kinajenga picha kubwa sana kwake na kwa biashara zake. Hii inaonesha jinsi anavyojali biashara zake na anavyotoa huduma bora kwa wateja.

Angalia video ya tukio zima hapo chini;

0 comments: