Weka Pamoja Vitu Hivi Vitatu Na Tayari Wewe Ni Mjasiriamali Mwenye Mafanikio Makubwa.

Kama tayari una kundi la watu wanaokufuata, na wanaosikiliza unachosema, ila huna cha kuwauzia, huna biashara.

Kama una bidhaa au huduma unayouza ila hakuna mtu yuko tayari kununua huna biashara.

SOMA; Sifa TATU Unazohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Kama una bidhaa au huduma unayouza na watu wapo tayari kununua ila huna njia rahisi ya wateja kuweza kukulipa huna biashara.

Kama ukiwa na bidhaa au huduma unayouza, ukawa na watu ambao wako tayari kuinunua, na ukawa na mfumo mzuri wa watu kukulipa ili kuipata, hongera una biashara kubwa ambayo itakuletea mafanikio.

Kwa kuweza kufikia vigezo hivyo vitatu na kuviweka pamoja wewe ni mjasiriamali mwenye mafanikio.

Kila la kheri.

SOMA; Huyu Ni Mjasiriamali Mwenye Hamasa Kubwa sana. Unaweza kujifunza kila kitu kutoka kwake.

0 comments: