Maswali Matatu Muhimu Ya Kujiuliza Kwenye Wazo Lako La Biashara.

Hakuna changamoto kubwa kama kupata wazo zuri la biashara na ambalo litakuwezesha kupata mafanikio na mafanikio makubwa.

Japo nimeshaandika mara nyingi sana jinsi ya kutengeneza wazo zuri la biashara, bado maswali mengo ninayopata kutoka kwa wasomaji ni wazo gani la biashara ni zuri na lenye faida.

Leo tutajifunza maswali matatu muhimu ya kujiuliza kwenye wazo lolote la biashara ili kujua kama litakuletea faida.

SOMA; Vitu VITATU Vinavyoathiri Kipato Chako Na Jinsi Ya Kukiongeza.

Muhimu ni kujua kwamba kila wazo la biashara ni zuri na linaweza kuleta faida. Changamoto ni jinsi gani unaweza kulitekeleza wazo hilo ili liweze kukuletea faida hiyo. Kupitia maswali haya matatu utaweza kuliweka wazo lako vizuri na hatimaye kuweza kutengeneza biashara kubw akupitia wazo hilo.

1. Je nawezaje kulipwa kwa wazo hili?

Jiulize swali hili muhimu sana kwamba unawezaje kulipwa kwa wazo ulilonalo. Unawezaje kulipwa kwa kile unachopenda kufanya?

Tuseme labda unapenda kuchora, je unawezaje kulipwa kwa kuchora? Hapa unaweza kupata majibu kama kuchora kazi za kisanaa, kuchora ramani za majengo, kuanzisha jarida la vibonzo na mengine mengi.

2. Je nitalipwa kiasi gani kutokana na wazo hili?

Kupata uhakika wa kulipwa kutokana na wazo bado hakutoshi wewe kujihakikishia biashara. Swali jingine muhimu la kujiuliza ni nitalipwa kiasi gani kwa wazo hili? Ni lazima ujue kiwango ambacho unaweza kulipwa kutokana na wazo lako. Na pia uone kiwango hiko unacholipwa kitakuwezesha kuendelea na biashara hiyo.

Kwenye mfano wetu wa kuchora hapo juu, huendakuchora vibonzo kunalipa, ila kuchora ramani za majengo kunaweza kulipa zaidi.

SOMA; Sheria NANE Za Kufanikiwa Kwenye Biashara Kutoka Kwa Warren Buffett.

3. Je kuna njia ambayo naweza kulipwa zaidi ya mara moja?

Wazo zuri la biashara ni lile ambalo unaweza kulipwa zaidi ya mara moja. Kama una biashara ambayo mtu akishanunua ndio imetoka na hawezi kurudi kwako tena ni vigumu sana kutengeneza biashara endelevu.

Ila kama utakuwa na njia ya kuweza kulipwa zaidi ya mara moja, au mteja kuja tena na tena utaweza kujenga biashara nzuri na yenye mafanikio makubwa.

Jiulize na kujijibu maswali hayo matatu na utaweza kulijenga wazo lako la biashara na likakuletea mafanikio makubwa sana.

TUPO PAMOJA.

SOMA; Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.

0 comments: