Sifa Sita(6) Unazohitaji Ili Kuwa Mjasiriamali Bora.

Kumekuwa na maswali mengi sana katika mitazamo tofauti juu ya ujasiriamali kwa mfano ujasiriamali ni nini? Na mjasiriamali ni mtu mwenye sifa gani?. Basi mpenzi msomaji wa makala hii ya leo utapata kujua nini maana ya ujasirimali na sifa mjasiriamali ni zipi.

Ujasiriamali nini?

Ujasiriamali ni uwezo wa kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazojitokeza na kugeuza au kutumia changamoto hizo kama fursa. Kwa mfano eneo A kuna shida kubwa ya maji basi mjasiriamali atakabiliana changamoto hiyo kwa kuchimba kisima cha maji na hatimaye atakuwa ametupia changamoto hiyo ya maji na kugeuza kuwa fursa.

ujasiriamali 1

Sifa za kuwa mjasiriamali bora

  1. Uwezo wa Kuona Fursa

Mjasiriamali lazima uwe na jicho la kuona fursa au uwezo wa kuona fursa katika jamii yako inayokuzunguka. Mjasiriamali anatumia changamoto zinazojitokeza katika jamii yake na kutumia changamoto hiyo kama fursa kwake. Kwa mfano sehemu unayokaa watu wanauhitaji wa huduma za kibenki kama vile tigo pesa, m-pesa ,airtel money nk. Basi mjasiriamali anaona hiyo fursa kwake kwa kuanzisha vibanda hivyo vya kutolea huduma za kibenki.

SOMA; Njia Rahisi Ya Kutengeneza Matatizo Makubwa Kwenye Maisha Yako.

  1. Ubunifu

Kama mjasiriamali yakupasa uwe mbunifu. Baada ya kuona fursa sasa katika eneo Fulani buni kitu tofauti, kuwa wa kipekee kwa mfano kama unatengeneza chapati basi zifanye chapati hizo kuwa tofauti na za wengine. Mshawishi mteja onesha utofauti wako katika ubunifu wa bidhaa au huduma unayotoa.

  1. Kuwa Mvumilivu

Mjasiriamali siyo mtu wa kukata tama, mjasiriamali ni mtu mvumilivu. Tutambue kuwa hakuna mafanikio ya haraka na mafanikio hayatokei kama vile radi au ajali. Bali mafanikio katika jambo lolote lile yakupasa uwe mvumilivu sana, vilevile katika safari ya mafanikio kuna changamoto nyingi sana. Mafanikio yoyote yale yana changamoto hivyo basi uweke hili akilini mwako.

SOMA; Jambo Moja Muhimu La Kuzingatia Ili Uweze Kufikia Malengo Yako.

  1. Mtu Mwenye Malengo

Mjasiriamali ni mtu mwenye malengo. Lazima uwe na malengo ya muda mrefu na mfupi huwezi kuwa mjasiriamali bora kama huna malengo. Lazima ujiwekee malengo kwa mfano ndani ya mwaka mmoja unahitaji ufike wapi, kama umekosa kuwa na malengo umekosa sifa ya kuwa mjasiriamali bora.

  1. Ari ya Kufanya Kazi/Kujituma

Mjasiriamali unatakiwa kuwa mtu mwenye ari ya kufanya kazi au kujituma kwelikweli ,mtu wa kujitoa unahitaji masaa ya ziada katika kujitoa kwako . Ondoa uvivu, unabidi uweke juhudi ya kufanya kazi, lazima upende kazi yako usiwe mtu wa kusukumwa bali kuwa mtu wa kujituma.

SOMA; Upya Wa Biashara Mpya Na Unavyoweza Kuutumia Vizuri…

  1. Mtu Anayependa Kujifunza

Kama wewe ni mjasiriamali halafu huwezi kujifunza basi unapitwa na mengi sana. Mjasiriamali unatakiwa kujifunza kila siku kitu kipya, soma vitabu mbalimbali ,jifunze kwa watu waliofanikiwa kila siku kwani kujifunza hakuna mwisho na elimu haina mwisho, hudhuria semina mbalimbali upate maarifa mapya.

Hivyo basi,mjasiriamali anatakiwa awe mtu wa kuongeza thamani na mtu mwenye jicho la kuona fursa katika jamii inayomzunguka.

Makala hii imendikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: