Jambo Moja Muhimu La Kuzingatia Ili Uweze Kufikia Malengo Yako.

Afya siyo neno geni kabisa katika akili yako. Na wala siyo mara yako ya kwanza kuliona neno hili au kusikia watu wakiongelea kuhusu afya kupitia vyombo vya habari kama vile radio, Luninga (TV) na nk.

Nini maana ya afya ?

Afya ni hali ya kuwa mzima kiakili,kimwili,kijamii na kiuchumi pia. Hivyo basi, kama binadamu yakupasa uwe na afya bora ili uweze kufikia malengo yako uliyojiwekea kwa sasa au kwa baadaye.

Wamiliki wa vyombo vya moto kama vile gari, pikipiki na nk. Wamekuwa wakifanyia huduma au service vyombo vyao vya moto kila baada ya muda Fulani. Kwanini wanafanyia vyombo vyombo vyao service au huduma?

Wanafanyia sevirce au huduma kwa sababu ili visiharibike na viendele kuwasaidia katika maisha yao ya usafiri wa kila siku. Wasipo vifanyia service au huduma vitakufa au kuharibika kabisa.

SOMA; USHAURI; Usianzishe NGO Anzisha Kampuni.(Usianzishe Msaada Anzisha Biashara)

Swali, je kwa binadamu wa kawaida tunafnayia service au huduma miili yetu? Kumbe basi , watu wanapasa kutunza afya zao sana kuliko kitu chochote .Ukiwa na afya mbaya na usipojali mwili wako utadhoofika na kushindwa kutimiza malengo au mipango yako uliyojiwekea kufikia sehemu fulani ya maisha unayohitaji kufikia.

Tunahitaji kula vizuri na kwa wakati ili tuwe na afya bora. Kula vizuri kuna hitaji mlo kamili wa chakula ambacho kinajenga mwili na siyo kubomoa. Je vyakula unavyokula vinajenga mwili au vina bomoa mwili? Nafikri jibu unalo mwenyewe.

Tunahitaji tunywe maji mengi kwa siku ,tunahitaji pia tupate muda wa kupumzika ili kufanya afya yako iwe nzuri katika Nyanja zote , tafiti nyingi zinasema kuwa binadamu anatakiwa kulala masaa 7-8 kwa usiku. Pia unahitaji upate muda wa kupumzika mchana ,unaweza ukasinzia kwa dakika 10-15-30 na pumzika pale mwili unapohitaji kupumzika usijilazimishe kufanya kazi wakati mwili umechoka.

SOMA; BIASHARA LEO; Kuhusu Wateja Wasionunua Kwako.

Faida za kuwa na afya bora

Ø Inakuongezea ufanisi wa kazi

Ø Unakuwa imara kiakili na kimwili

Ø Unakuwa mchangamfu

Ø Unakuwa na furaha

Hizi ni miongoni mwa faida chache kati ya nyingi za wewe kuwa na afya bora. Kumbuka kuwa huwezi kufikia au kutimiza malengo yako uliyojiwekea kam hauna afya bora, hivyo basi jail sana afya yako na fanyia huduma au service mwili wako mara kwa mara.

Makala hii imendikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: