Hatua Saba (7) Za Kuweka Malengo Na Kuweza Kutimiza Ndoto Zako.

Kuweka malengo ni sawa na kuchora ramani ya sehemu uendako. Bila kuwa na ramani ni sawa na kutembea safari usiyoijua. Ni rahisi zaidi kufanikiwa katika hali ngumu ukiwa na malengo kuliko kufanikiwa katika hali rahisi bila malengo. Ni ngumu sana kufika uendako kama hujui njia. Bila malengo madhubuti ni ngumu sana kwako kufikia ndoto zako. Anza kuweka malengo yako leo, usichelewe kwani hakuna kesho ambayo imewahi kufika. Ukiweka malengo utapata msukumo kutoka ndani mwako na hivyo kuwajibika/kulazimika kutimiza ndoto zako.

clip_image002

1. Amua unachokihitaji katika maisha yako

Ili uweze kufanikiwa ni lazima uamue ni kipi cha kuwa nacho katika maisha yako. Kama unahitaji pesa jaribu kuweka kiasi ambacho unahitaji baada ya muda fulani. Mfano milioni moja kwa mwezi au milioni hamsini kwa mwaka. Hii itakufanya muda wote uone kama una deni na hivyo kufanya kila linalowezekana kufikia malengo yako. Weka malengo yako kama kuwa na afya njema, kujenga, biashara, siasa na kadhalika. Hakikisha vile unavyoamua kutoka moyoni ni vile vyenye faida kwako.

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

2. Andika malengo yako kenye karatasi/daftari

Baada ya kuamua unachokitaka maishani mwako sasa ni wakati wako wa kuweka malengo na kuandika kwenye karatasi au daftari dogo maarufu kama diary. Nakushauri uandike kwenye daftari maana ukiandika kwenye karatasi ni rahisi kupotea kuliko kwenye daftari dogo. Hakikisha unasoma vile ulivyoandika mara nyngi ili uweze kukumbuka na kuona kama deni kwako. Ukishaandika malengo yako ni kama umechora ramani ya vita, hivyo una sehemu ya kuanzia katika mapambano yako. Kuna siri kubwa iliyopo baina ya kuandika na ubongo wako.

3. Weka muda wa mwisho kwa kila lengo ulilojiwekea

Weka mwisho wa kila lengo ambalo utajiwekea, kama lengo ni kubwa inakubidi uligawanye katika vipande vidogo vidogo na hivyo kuwa rahisi kulimiza. Ukiweka muda wa mwisho (deadline) unapata msukumo kutoka ndani mwako. Weka muda wa mwisho kwa kila lengo. Usijiwekee malengo makubwa mno katika muda mfupi kwani ukishindwa kulitimiza unaweza kufa moyo.

4. Orodhesha vitu vitakavyokufanya ufikie lengo lako

Kila siku buni njia mpya zitakazokufikisha katika malengo yako. Waza na fikiria njia mpya kila mara. Orodhesha vitu na mawazo yako katika daftari dogo. Kumbuka bila kuandika vitu hivyo hutaweza kufikia lengo lako kwa urahisi. Orodha ya vitu vitakavyokufikisha katika ndoto zako ni sawa na barabara katika ramani.

SOMA; Sababu 10 Kwa Nini Hutafikia Malengo Yako 2015.

5. Chukua hatua/weka katika matendo

Baada ya hatua hizo nne sasa ni wakati wa wewe kuchukua hatua na kufanya katika matendo. Weka katika mpangilio kiasi kwamba unaanza na vile vyenye umuhimu zaidi mpaka vile vyenye umuhimu mdogo. Hii ni kwamba utaweza kutimiza vile vyenye kukufikisha katika kilele cha ubora wako. Ukianza kufanya vile visivyo na umuhimu kwanza basi utakuwa katika nafasi ngumu sana kufikia ndoto zako. Usiahirishe kwani uhairishaji (procrastination) hufanya usifanikiwe na hivyo kula muda wako bure. Chukua hatua leo kwani hakuna siku nyingine unayoijua zaidi ya leo.

7. Fanya jambo moja kila siku kutimiza malengo yako

Pengine hili ndilo jambo kubwa na la muhimu zaidi katika malengo yako kuweza kufikia ndoto zako. Ukiweka malengo bila kufanyia kazi itakuwa ni kazi bure. Fanya jambo moja kila siku ambalo litakupeleka hatua moja mbele zaidi ya jana. Maneno bila matendo ni kazi bure. Waswahili walisema ‘’maneno matupu hayavunji mfupa’’. Unatakiwa pia kuwa madhubuti na kuamua kutoka moyoni (commitment) mwako kufikia ndoto zako.

Ndugu msomaji nakuhimiza kuweka malengo yako leo na kuanza kufanyia kazi. Kama hutaweka malengo, ni sawa na kwenda vitani bila kuwa na ramani ya vita. Ni rahisi sana kushindwa bila ramani kwani kamwe hutajua unakoenda na hivyo utaishia usipopenda kuwepo.

Nakutakia kila la kheri katika kutimiza ndoto zako.

Makala hii imeandikwa na Nickson Yohanes

Unaweza kuwasiliana na nae kwa kwa: simu: 0712 843030/0753 843030

e-mail: nmyohanes@gmail.com

Pia unaweza kutembelea blog yake: www.lifeadventurestz.blogspot.com kujifunza zaidi

Pia unaweza kujiunga na email list yetu kwenye Life Adventures uweze kupata Makala kila zinapotoka.

0 comments: