Fanya Uwekezaji Huu Ambao Ni Rahisi Kwako Na Una Faida Kubwa.

Watu wengi wamekuwa wakitamani kufanya biashara au shughuli yoyote ambayo itakuza kipato chao, lakini wengi wao hukatishwa tamaa jinsi gani ataweza kusimamia biashara hiyo. Changamoto ya usimamizi wa biashara ni kubwa sana kwa watu wengi hasa wale ambao ni wafanyakazi katika serikali na kampuni binafsi. Na wengi ambao wamejaribu kufanya biashara wameshindwa kutokana na usimamizi mbovu wa biashara zao. Wengi wanatamani kukuza vipato kwa njia nyingine. Nini kifanyike?

Uwekezaji katika hisa ni suluhisho kwa wale wote ambao wanakutana na changamoto ya muda wa usimamizi wa biashara zao. Uwekezaji katika hisa ni rahisi, unahitaji muda mdogo wa usimamizi, unakua na kuongeza kipato kwa mwekezaji.

clip_image001

SOMA; Haya Ndio Mapinduzi Makubwa Tunayohitaji Ili Kufanikiwa Kwenye Kilimo.

Uwekezaji huu unafanyikaje?

Mtu yoyote Yule anaweza kuwa mwanahisa akiwa popote pale Tanzania. Unaweza kununua hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam kupitia mawakala wake ( Brockers) au kupitia Benki ya CRDB ukiwa mkoa wowote ule hapa Tanzania. Wasiliana wakala utapata utaratibu wowote jinsi ya kununua hisa. Unachotakiwa kuwa nacho ni pesa yako kwa ajili ya kununua hisa, akaunti yako ya benki na mawasiliano ya Mawakala wa soko la Hisa au Benki ya CRDB.

Kwanini uwekezaji huu ni rahisi?

Ni uwekezaji ambao unaweza kuufanya ukiwa katika mkoa wowote ule hapa Tanzania kwa gharama ndogo na wewe kuwa mmiliki wa hisa na kutengeneza faida. Ukihitaji kununua au kuuza hisa zako unachotakiwa kuwasiliana na mawakala wa soko la hisa ukiwa mkoani au sehemu yoyote ile kwa njia ya mtandao ( simu, barua pepe na benki). Utapata utaratibu wote kuhusu kuuza na kununua hisa.

Uwekezaji huu unahitaji muda mdogo wa usimamizi

Ukiwekeza katika hisa Mfano CRDB, TBL au SWIS hutahusika katika shughuli za kila siku za Kampuni. Wewe kama mwanahisa unahitajika kufuatilia utendaji wa Kampuni katika taarifa za fedha ambazo hutolewa kila baada ya miezi mitatu, sita na mwaka. Kama mwekezaji utasubiri katika kushiriki katika mkutano mkuu wa mwaka kwa ajili ya kutoa kushiriki katika vikao vya maamuzi ya wanahisa. Baada ya hapo unasubiri hisa zako kuongezeka thamani na kupata gawio.

SOMA; Huoni Kwa Sababu Hutaki Kuona.

Ni uwekezaji ambao unakua na mwekezaji anapata kipato

Ukiwa mwekezaji katika hisa, huku ukiwa unaendelea na kazi yako kama mwajiriwa au mfanyabiashara hisa zako zinaongezeka thamani na wewe mwekezaji utapata gawio kila baada ya miezi sita au mwaka. Utafaidika kwa haya ikiwa utaamua leo kwa kununua hisa za Kampuni ambazo zimesajiliwa katika soko la Hisa.

Faida ya Kuwa mmiliki wa Hisa

  1. Gawio

Ukiwa miliki wa hisa utapata gawio ikiwa Kampuni itapata faida katika kipindi hicho cha mwaka na wanahisa wakaridhia utoaji wa gawio. Gawio hutolewa mara mbili au moja kwa mwaka kutokana sera ya kampuni na maamuzi ya wanahisa.

  1. Ongezeko la thamani

Wanahisa pia huweza kupata faida itokanayo na ongezeko la thamani iwapo bei ya hisa itaongezeka kwenye soko la hisa. Ikiwa ulinunua hisa moja kwa Tsh 800 na baada ya mwaka hisa hizo sokoni zikauzwa kwa Tsh 1,400 basi unakuwa umepata ongezeko la thamani ya shilingi 6,00 kwa kila hisa. Hii ni faida tofauti na gawio, ikiwa utawekeza katika kampuni nzuri utapata gawio na ongezeko la thamani ndani ya mwaka mmoja. Vile vile ikiwa bei itashuka na kufikia Tsh 600 utapata hasara ya Tsh 200. Ila ukiwekeza katika kampuni nzuri ni vigumu kupata hasara na unakuwa na uhakika wa bei kuongezeka kwa 20% au 40% au zaidi kwa mwaka.

  1. Dhamana

Hisa  kwa mwekezaji anaweza kuzitumia kama dhamana anapohitaji kupata mkopo.

  1. Huokoa muda wa usimamizi

Ni uwekezaji ambao humpatia mwekezaji uhuru wa kufanya shughuli nyingine na kwa wale ambao hawana muda wa usimamizi katika biashara huu ni uwekezaji mzuri kwao.

  1. Ni mali inayohamishika kwa urahisi

Ni mali ambayo inahamishika ki urahisi na kwa haraka pale mwekezaji anapohitaji pesa yake kwa ajili ya shughuli nyingine.

  1. Akiba

Njia ya kujiwekea akiba kwa ajili ya baadaye.

  1. Ushiriki wa jamii katika Uchumi

Inasaidia kuongeza ushiriki wa jamii katika shughuli za kifedha na kukuza uchumi.

Kama unahitaji kushiriki katika Uwekezaji katika hisa kwa kununua hisa soma makala hii Hivi ndivyo unavyoweza kununua hisa katika soko la Hisa

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano: emmanuelmahundi@gmail.com au 0714 445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

0 comments: