Mambo 20 niliyojifunza Kwenye Kitabu LITTLE BETS.

Habari rafiki, ni matumaini yangu waendelea vizuri. Karibu sana katika utaratibu wetu wa kushirikishana mambo 20 niliyojifunza kwenye kitabu. Leo tunajifunza kutoka kwenye kitabu kinachoitwa LITTLE BETS. Kitabu hiki kimeandikwa na Peter Sims

LITTLE

1. Matatizo hupelekea kupata shuluhisho mpya ambazo hukuwahi kufikikiria. Unapokumbana na matatizo au changamoto chukulia kama vile ni fursa ya wewe kugundua njia mpya.

2. Unapopoteza mwelekeo usikate tamaa kamwe hakikisha unatafuta njia mpya kwa kutumia uzoefu ulio nao... kama alivyofanya SteveJob. katika kuanzisha kampun nyingne ya next computer baada ya kufukuzwa kwenye kampuni ya apple aliyoianzisha

3. Ukianza biashara ukiwa na mtaji mdogo ukafeli ni rahisi kuinuka kuliko kuanzisha biashara ukiwa na mtaji mkubwa ukafeli.

4. Waweza kuanza na wazo dogo. Wazo dogo laweza zaa matokeo makubwa, hakikisha unafanyia kazi wazo lako.

SOMA; Kuna Jambo Moja La Ziada La Kufanya.

5. Kubali kuwa kuna mawazo hayatafikia mafanikio lakini usiache kuwaza. Unapojizoesha kuwaza mawazo ya biashara, mwanzoni utakua unapata mawazo ya kawaida, na pengine mengi hayatafikia kwenye mafanikio, Lakini baada ya muda akili inaanza kuleta mawazo mazuri zaidi.

6. Kukosea ni moja ya hatua ya kufanikiwa. Ukiwa unakwepa kukosea au kushindwa itakuwia vigumu kufika unakotaka kwenda maana hutajaribu kwa hofu ya kushindwa.

7. Ubunifu ni kuunganisha vitu unavyovijua... unganisha doti za uzoefu wako

8. Unaposhindwa usichukilie kushindwa bali chukulia kwamba umefahamu njia ambayo haitkufikisha, alafu tafuta njia nyingne

9. Mafanikio yanaficha matatizo

10. Maswali ni majibu mapya, ukiwa na utaraibu wa kujiuliza maswali na kujaribu kuyajibu kwa utendaji kutakupelekea kupata majibu mapya. Kabla ya majibu hutangulia maswali ubora wa majibu unategemea ubora wa maswali.

SOMA; Hii Ndio Hatari Kubwa Kuliko Zote.

11. Katika mafanikio hakuna njia ya mkato, lazima uzingatie kanuni na ukubali kwenda hatua kwa hatua

12. Tafuta msaada kwa waliokutangulia...hakuna anayefanikiwa peke yake

13. Kujaribu mara kwa mara kunasahihisha makosa, na pia kunapelekea kwenye jibu sahihi. Jaribu tena na tena

14. Sio lazima ujue kila kitu ndio uanze biashara. Hata kama utajua kila kitu yapo mambo ya mapya (surprises) utakuna nayo kwenye biashara unayotaka kufanya. Kama ni hivyo basi ukishafahamu yale ya msingi anza mara moja, mengine utajifunza kwa vitendo zaidi ya nadharia.

15. Usikatishwe tamaa na wasikilizaji au watu wa pembeni, ukishinda hakuna hata mmoja atakayekumbukwa, bali wewe ndiye utakayekua shujaa. Wako wapi waliomkatisha tamaa Nyerere wakati akipigania uhuru wa Tanganyika, walikuwepo waliomkatisha tamaa, lakini leo hii hakuna anayekumbukwa hata mmoja. Follow your heart

16. Ugunduzi mdogo unaweza kukupelekea kua na biashara kubwa sana.

SOMA; Kinachoamua Maisha Yako Sio Unachozungumza, Bali Hiki…

17. Ukamilifu ni kizuizi cha ubunifu. Kusubiri mpaka ukamilike kunafanya watu wengi wanashindwa kua wabunifu maana wanatamani muda wote waonekane wamekamilika

18. Mipango mizuri hujengwa ama hubomolewa na mazungumzo na kukutana na watu wengne. Unapokua na wazo au mipango yako jua ni nani wa kumshirikisha

19. Wajasiriamali wanofanikiwa ni wale wenye mtazamo wa majaribio. Hufanya majaribio mapya kila wakati. Hujaribu mawazo mapya bila kujali ni madogo kiasi gani. Katika kujaribu huko ndiko kunako wapa uwezo wa kutambua njia sahihi ni ipi

20. Akili au ubongo unakua kwa kujifunza vitu vipya kila siku. Unapojifunza vitu vipya seli za ubongo wako zinakua. Uwezo wa kufikiri pia unakua.

Asanteni sana. Tukutane wiki ijayo

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana naye kwa simu 0763 071007 au barua pepe daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com

0 comments: