Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara - 2

Habari mpenzi msomaji wa mtandao huu wa JIONGEZE UFAHAMU. Natumaini unaendelea vema na karibu tena katika mwendelezo wa makala hii sehemu ya pili. Kama hukuisoma sehemu ya kwanza ya makala hii unaweza kuisoma hapa; Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara –1

Karibu kwenye sehemu ya pili ya makala hii ili upate kujifunza mengi zaidi.

3. Sigara

Ukiangalia paketi ya sigara wameandika uvutaji wa sigara ni hatari kwa maisha yako lakini watu bado hawasikii, mwingine anavuta hata paketi moja ya sigara kwa siku.

Lakini mtu huyo pengine hana hata mtaji wa biashara anaendelea kulalamika na kukaa vijiweni .Kumbe angeweza kuacha au kupunguza kuvuta sigara kila siku na kuweka akiba ya hela hiyo hatimaye kupata mtaji na kuanza biashara ndogondogo.

4. Matumizi ya Simu (vocha)

Mawasiliano ni muhimu sana ndio hatukatai je mawasiliano hayo yana tija kwako?

Kama kweli unataka kujikomboa na kupata mtaji wako punguza matumizi ya vocha kwa mwezi au miezi mitatu uone ni kiasi gani cha fedha unachoweza kupata na kufanya kuwa mtaji wako.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyojitengenezea Dharura.

Vijana wamekuwa na matumizi ya kununua vocha kila siku wengine zaidi hata ya elfu 2000 kwa siku je vocha hiyo inakuingizia? Au mawasiliano hayo yanakuingizia yanabadili maisha yako? yana tija kwako jiulize mwenyewe utapata jibu halafu fanya maamuzi haraka ya kubadilika , punguza matumizi hayo ya vocha kila siku iwekeze hiyo hela unayonunua nayo vocha kila siku uweke akiba ili upate mtaji na uache kulalamika kila siku mtaji uko mikononi mwako amka kijana.

Hivyo basi, kuna mambo mengi sana unaweza kuyapunguza yanayohusiana na somo hili ,punguza safari zisizokuwa na tija ,ununuaji wa vitu hovyo mfano unanunua nguo mpya kila mtindo mpya unapotoka jiulize una nguo ngapi ambazo huzivai na unanunua nyingine ? mtaji uko mikononi mwako ukiamua kupunguza na kuwekeza pesa hiyo utafika mbali.

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: