Kijana Punguza Mambo Haya Ili Uweze Kupata Mtaji Wa Kuanza Biashara -1

Vijana wengi wamekuwa wakilalamika ni wapi wanaweza kupata mtaji na kuweza kufanya biashara ili kuboresha maisha yao. Lakini vijana hao ndio watu wa kwanza wanaongoza kwa matumizi mbalimbali yasiyo na tija na kufanya starehe sana bila kujua kuwa hizo starehe wanazofanya wangezipunguza au kuacha kabisa na kuweka hiyo hela ili waweze kupata mtaji wa kufanya biashara wanazopenda .

Punguza Mambo Haya ili uweze kupata mtaji

1. Kamari (Kubeti)

Watu wazima hata vijana wengi siku hizi wanapoteza sana rasilimali muda katika kucheza kamari. Huwezi kuwa na uhuru wa kifedha (tajiri) kwa kucheza kamari, watu waliofanikiwa duniani na wenye uhuru wa kifedha hawajafanikiwa kwa kucheza kamari kama wewe unavyodhania na kuendelea kubeti kila siku na kuliwa kila siku katika mchezo huo.

SOMA; Hii Biashara Inaliangamiza Taifa, Tujiepushe Nayo.

Watu wengine wanaweza kubeti kwa siku zaidi hata ya elfu 20 kwa siku akitegemea atashinda hela nyingi na mambo humwendea mrama bila mafanikio yoyote. Kesho pia anajaribu tena kubeti akiwa na imani kuwa ipo siku ataweza kushinda. Mchezo huu wa kubeti anayefaidika ni Yule anayemiliki hiyo kampuni na siyo wewe bali wewe ndio una mtajirisha bila wewe kujua.

Je unaweza kujiuliza tokea uanze kubeti mpaka leo umepoteza shilingi ngapi?

Je kama ungeweza kuwekeza hela zako hizo kila siku bado tu hujapata mtaji? Mpaka hapo hujaweza kujiajiri?

Ni vema sana na ni bora sana ukaitumia fedha hiyo unayopoteza kila siku katika kamari na kuiwekeza fedha hiyo katika soko la hisa na kuendelea kupata faida bila kupoteza hela yako kama ulivyokuwa unapoteza katika kamari au kama unavyoendelea kupoteza fedha yako katika kamari.

Huu ni ushauri wa bure ambao unaweza ukautumia na kujikomboa kuliko kuendelea kucheza kamari.

SOMA; Hawa Ndio Wateja Rahisi Kuwapata Kwenye Biashara Yako.

2. Ulevi

Kitu chochote ukizidisha ni sumu, ulevi wa kupindukia ni sumu pia, siwezi kukuzuia kunywa ila kunywa kiasi punguza pombe au vilevi unavyotumia kila siku na kutumia hela hiyo unayopunguza kupitia pombe hizo unazonunua kila siku na kuweka akiba yako ili uweze kupata mtaji wako wa kufanya biashara halali unayoipenda na kuweza kupata kipato chako .

Vijana wengi wamekuwa ni watu wa starehe kupita kiasi ambayo baadaye inakuletea madhara makubwa utakuja kushtuka pale ambapo huwezi tena kufanya kazi. Ni vema ukautumia muda huu kufanya mabadiliko, amka kijana, amka Mtanzania ili uweze kuhalalisha ndoto yako.

Kama una uwezo wa kunywa bia tano au zaidi kwa siku kwa bei ya sasa ya bia moja na ukijinyima kwa mwezi bado hujapata mtaji?

Usisubiri mpaka upate mtaji mkubwa sana anza na mtaji mdogo na Ujasiriamali mdogo mdogo ambao utakupeleka juu kufikia mafanikio makubwa. Tunaweza kupata mfano kwa bilionea kutoka Afrika Alihaji Aliko Dangote ukisoma wasifu wake yaani wasifu wake alianza kupenda ujasiriamali tokea yuko darasa la tatu na alikuwa anauza pipi au peremende je leo yuko wapi?

SOMA; Ni Lipi Dhumuni Lako Kwenye Maisha? Langu Ni Hili Hapa.

Angalia mapinduzi anayofanya Mtwara kujenga bandari na kujenga kiwanda cha saruji ni jinsi gani mtu huyu ataweza kuwakomboa watanzania wa mahali husika ambapo anajenga vitu hivyo na kuleta mabadiliko chanya mengi. Hivyo usidharau kidogo anza nacho leo kipende na ujifunze utafanikiwa.

Mpenzi msomaji wa makala hii asante kwa muda wako na endelea kufuatilia tena mwendelezo wa makala hii wiki ijayo siku kama ya leo (Jumatatu).

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

Makala imehaririwa kwa Kiswahili fasaha na Rumishael Peter ambaye anatafsiri/kuhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali barua pepe: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422. tovuti http://rumishaelnjau.wix.com/editor

0 comments: