Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Huu ni wakati ambao karibu kila mtu anahitaji kuingia kwenye biashara. Haijalishi mtu ameajiriwa au hana ajira, haijalishi kiwango cha elimu mtu alichonacho na wala haijalishi umri wa mtu, kwa sasa kila mtu anahitaji kuwa kwenye biashara.

Ajira zimekuwa za shida kupatikana na hata wale wanaozipata bado haziwawezeshi kuyamudu maisha. Changamoto ni nyingi sana. Njia ya uhakika ya kuweza kupambana na changamoto hizi ni kuingia kwenye biashara,

Mazingira ya kuingia kwenye biashara nayo yamebadilika pia. Tofauti na zamani ambapo ilihitaji mtu kuwa na uwezo mkubwa sana wa kifedha ndio aweze kuingia kwenye biashara, sasa hivi unaweza kuingia kwenye biashara kwa mtaji kidogo sana.

Pamoja na umuhimu huu wa kuingia kwenye biashara na urahisi wa kufanya biashara, bado kuna changamoto kubwa sana wkenye biashara. Biashara nane kati ya kumi zinazoanzishwa zinakuwa zimeshakufa ndani ya miezi 18. Na hata zile ambazo zinapona kipindi hiki, nyingi hazifikii mafanikio makubwa.

Watu wengi wanaweka juhudi kubwa sana kwenye biashara ila bado hawaoni mafanikio waliyotarajia. Hili linawaangusha wengi sana na wengi kukata tamaa.

Matatizo haya mengi yanatokana na kukosekana kwa elimu sahihi ya biashara, kukosa mtazamo sahihi wa kufanikiwa kwenye biashara, kutokujua mbinu za mafanikio kwenye biashara na kufanya biashara kwa mazoea.

Ili kuwasaidia wafanyabiashara na wale ambao wanapanga kuingia wkenye biashara kuweza kuondokana na changamoto hizi, AMKA CONSULTANTS imeandaa SEMINA YA MAFANIKIO KWENYE BIASHARA 2015. Semina hii itakupatia wewe elimu sahihi, mbinu muhimu na mtazamo sahihi utakaokuwezesha kufanikiwa kwenye biashara yako.

Hii sio semina ya kukosa kwa sababu imejaa mambo mengi ambayo hujawahi kuyapata sehemu nyingine yoyote.

Semina hii imeandaliwa kuweza kukidhi mahitaji ya kufanikiwa kwenye biashara kwa mazingira yetu ya kitanzania. Semina hii itakuwezesha wewe kutoka hapo ulipo sasa na kupiga hatua kubwa sana kibiashara.

Semina hii itaendeshwa kwa njia ya mtandao na itaendeshwa kwa kipindi chote cha mwezi wa tano.

Washiriki wa semina hii watatumiwa email ya mafunzo kila siku asubuhi, kupata nafasi ya kuisoma na kuweza kuuliza swali popote ambapo hajaelewa. Email hizi zitakuwa na mafunzo yaliyofanyiwa utafiti w akina pamoja na mifano ambayo itamwezesha mshiriki kpata mawazo tofauti anayowez akuyatumia kwenye biashara yake na akafanikiwa sana.

Semina hii itafundisha mambo yafuatayo;

SEMINA YA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA.

Anza, kuza na fanikiwa kupitia biashara.

Yatakayofundishwa;

1. Utangulizi

1.1. Huu ni wakati mzuri wa wewe kuwa kwenye biashara.

1.2. Unawezakufanikiwa kwenye biashara.

1.3. Utakachokipata kwenye kozi hii.

2. Wazo la biashara

2.1. Biashara sahihi kwako kufanya

2.2. Jinsi ya kupata wazo bora la biashara

2.3. Jinsi ya kuboresha wazo lako la biashara

2.4. Baadhi ya mawazo ya biashara.

3. Mchanganuo wa biashara.

3.1. Umuhimu wa mchanganuo

3.2. Vitu muhimu vya kuweka kwenye mchanganuo wako

3.3. Udhaifu na uimara wako

3.4. Utafiti wa biashara yako

3.5. Ushindani.

3.6. Kuajiri wasaidizi bora kwenye biashara yako.

4. Mtaji na vyanzo vyake.

4.1. Aina za mtaji unaohitaji kwenye biashara

4.2. Mtaji wa fedha na vyanzo vyake

4.3. Njia bora za wewe kupata mtaji wa biashara.

5. Urasimishaji wa biashara

5.1. Umuhimu wa kusajili biashara yako.

5.2. Aina za usajili na faida zake

5.3. Hatua za kusajili biashara yako

5.4. Umuhimu na jinsi ya kulinda biashara yako.

6. Thamani ya biashara yako

6.1. Maandalizi ya bidhaa au huduma

6.2. Upatikanaji na upakiaji wa bidhaa au huduma

6.3. Upangaji wa bei.

7. Masoko na uuzaji.

7.1. Chagua soko la biashara yako

7.2. Mpango bora wa kutangaza biashara yako.

7.3. Njia rahisi za kutangaza biashara yako.

7.4. Mbinu za kuongeza mauzo kwenye biashara yako.

8. Mzunguko wa fedha.

8.1. Mauzo na faida.

8.2. Gharama muhimu za biashara

8.3. Gharama za kuepuka kwneye biashara

8.4. Kujilipa wewe mwenyewe.

8.5. Hesabu za fedha na umuhimu wa mhasibu.

9. Huduma kwa wateja.

9.1. Lengo la biashara ni kutengeneza wateja.

9.2. Jinsi ya kutoa huduma bora kwa mteja.

9.3. Mfanye mteja atangaze biashara yako.

9.4. Mteja ni mfalme na mwisho wa ufalme wake.

10. Changamoto za biashara.

10.1. Changamoto zinazoua biashara nyingi

10.2. Umuhimu wa mabadiliko

10.3. Mbinu za kufufua biashara inayokufa.

11. Mafanikio ya biashara yako

11.1. Jifunze kila siku

11.2. Matumizi mazuri ya muda

11.3. Kujihamasisha mwenyewe

11.4. Mafunzo kwa wafanyakazi wako

11.5. Usimamizi mzuri wa biashara yako.

11.6. Kununua uhuru wako kutoka kwenye biashara yako.

Gharama za kushiriki semina hii ni tsh elfu 30(30,000/=), ili kupata nafasi ya kushiriki semina hii tuma fedha za kushiriki kwa Mpesa 0755953887 au tigo pesa/airtel money 0717396253 kisha tuma majina yako na email kwenye moja ya namba hizo na utaandikishwa kwenye semina hii. Uandikishaji unaanza leo tarehe 20/04/2015 na utasitishwa tarehe 01/05/2015. Wahi kujiandikisha mapema kwani nafasi ni chache na zitakapojaa utakosa nafasi hii adimu ya kupata maarifa ya kukuwezesha kufanikiwa kwenye biashara yako.

Kumbuka semina inafanyika kwa njia ya mtandao hivyo popote ulipo Tanzania na hata nje ya Tanzania unaweza kushiriki semina hii.

Semina itaanza rasmi tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima.

Karibu kwenye semina hii ambayo itakupatia kila unachohitaji ili kufanikiwa kwenye biashara yako.

Kumbuka maarifa ni nguvu, pata maarifa sahihi kupitia semina hii ili uweze kuwa na nguvu za kutosha na zitakazokuletea mafanikio makubwa.

Karibu sana na hakikisha hukosi semina hii kwa sababu yoyote ile.

TUPO PAMOJA.

Makirita Amani 

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

kitabu-kava-tangazo4322

0 comments: