Njia Mbili Za Uhakika Za Jinsi Ya Kupata Fedha.

Fedha ni chombo cha muhimu sana kwa kila mtu anayeishi chini ya jua yaani Duniani kwa ajili ya kukidhi mahitaji muhimu ya kibinadamu. Fedha ni chombo kinachotumika kuhalalisha mambo baina ya pande mbili yaani mtoaji na mpokeaji katika kulinganisha mapatano yaliyofikiwa katika hali ya kuuza au kununua.

Ni chombo ambacho kila mtu anahitaji kuwa nacho usidanganyike kwamba utapata miuzija ya kifedha ikuangukie lahasha! Pesa zinatafutwa ,zinategewa mitego watu wamekuwa hawana kitu kwa kusubiri muujiza wa kifedha uwaangukie. fedha huleta jawabu la mambo yote na fedha ni ulinzi’’

NJIA ZA KUPATA FEDHA

1. KUWA MBUNIFU

Njia moja wapo ya kupata,kuongeza fedha ni kuwa mbunifu ,buni njia mbalimbali za kukuingizia kipato yaani miradi. Kadiri unavyotega mitego ndivyo unavyopata pesa au ndivyo unavyonasa fedha zaidi.

Fedha haina mwenyewe wala upendeleo ,tabia ya fedha hufuata pale ilipotegwa jifunze kutega mitego mbalimbali ( vyanzo vya mapato) mwisho wa siku ,wiki,mwezi au mwaka utasema umepata pesa . Huwezi kufanikiwa kama wewe ni mtu wa kukaa tu ,tafuta kazi itakayokupatia kipato na tumia kipato hicho kuanzisha chanzo chako cha mapato.

Kila kitu kina gharama au bei hivyo basi lipia gharama au bei upate huduma na kumbuka kuwa hakuna kitu cha bure “There is no free lunch

Kuwa bora katika kile unachofanya utalipwa fedha ,utapata fedha kulingana na ubora wa bidhaa au huduma unayotoa.

SOMA; Huu Ni Uwekezaji Wa Uhakika Ambao Hautakuangusha.

2. KUWA MSHINDANI

Kama unafanya biashara na hujui mshindani wako hilo ni tatizo .Lazima umjuwe mshindani wako katika biashara yako au katika kile unachofanya ,mwandishi wa kitabu cha The Entrepreneur Mind ,Kevin Johnson amesema tafuta adui wako yaani mshindani wako ‘find your enemy’na akatoa mfano wa kampuni mbili jinsi ngani zina ushindani wa miongo mingi na kampuni hizo ni ni Apple chini ya mwanzilishi wake Steve Jobs na Microsoft chini ya Bill Gates au kampuni ya cocacola na pepsi hizi kampuni zote zinapigania kutafuta masoko na kila mmoja anamjuwa adui wake yaani mshindani wake kama makampuni makubwa duniani yanaushindani hata wewe unabidi umtambue mshindani wako katika biashara yako ili uweze kuwa bora zaidi.

SOMA; NAFASI MOJA YA KAZI; Changamkia haraka.

Ubora wa kitu utamvutia mteja hata kama hakuwa amekuja kwa ajili ya bidhaa pengine alikuwa anapita tu kando lakin akashawishika baada tu ya kuona huduma unayotoa au bidhaa unayouza. Mfano wa kampuni za simu hapa Tanzania kama vile Tigo,Vodacom au Airtell zina ushindani kila siku huyu katoa hiki leo mwenzake naye kesho kaja na kingine ushindani huu unawafanya waendeshe kampuni zao katika hali ya ushindani inayoleta ufanisi wa kifedha na cha kushangaza wote wanapata wateja .

Ushindi unaonekana kwa Yule atakayekuwa amevutia wateja wengi zaidi na kupata kipato kikubwa zaidi na kudumisha kiwango cha juu cha ufanisi. Ukiwa mtu wa ushindani utatumia bidii kujifunza zaidi na wala hutokubali kushindwa utafanya vitu vyako katika hali ya ubora ili upate ufanisi zaidi maana hakuna mtu anayependa vitu /bidhaa feki ,kila mtu anapenda vitu bora

SOMA; Usianze Biashara Kama Hujui Kitu Hiki Kimoja.

Mwandishi wa Makala hii ni DEOGRATIUS KESSY ambaye ni mwandishi mhamasishaji na mjasiriamali unaweza ukawasiliana naye kupitia namba ya simu ya mkononi 0717101505 au kupitia barua pepe deokessy.dk@gmail.com

0 comments: