Jinsi ya kuchagua Kampuni ya kuwekeza katika Soko la Hisa

Unapohitaji kuingia kwenye uwekezaji katika Hisa swali la kwanza utajiuliza je ni kampuni gani inafaa kuwekeza. Swali hili ni zuri kwa mwekezaji kwa sababu anahitaji kuweka pesa yake katika sehemu salama na ambayo itafanya biashara yake izidi kukua. Kuchagua kampuni inayofanya vizuri katika soko la ni jambo gumu kwa watu wengi hasa ambao hawana ujuzi kuhusu uwekezaji katika Hisa. Leo tutaangalia mbinu ambazo zitamsaidia mtu ambaye hana ujuzi kuhusu uwekezaji ili aweze kuchagua kampuni ya kuwekeza katika soko la Hisa.

SOMA; Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)

Kwa kuanza kuwekeza sasa ndipo unapoanza kujifunza kuhusu uwekezaji katika Hisa. Na ukiendelea kusoma makala kama hizi utaendelea kukuza uelewa katika uwekezaji katika Hisa na kuweza kuwekeza bila wasiwasi.

Kampuni ambazo ni nzuri kwa ajili ya kuwekeza kwa mtu ambaye ana ujuzi mdogo

1. Wekeza katika Kampuni ambayo unaipenda/unaifahamu

Katika kampuni ambazo zimesajiliwa katika soko la Hisa kuna kampuni ambayo utakuwa unaipenda. Anza kuwekeza toka katika Kampuni hiyo kwa sababu unaipenda hata kama haitafanya vizuri utakuwa mvumilivu na kusubiri kwa kipindi kijacho.

2. Wekeza katika kampuni kubwa

Katika soko la Hisa kuna Kampuni kubwa na ndogo, kwa mwekezaji ambaye anafuatilia taarifa katika soko la Hisa ni rahisi kufahamu kampuni kubwa na kampuni ndogo ambazo zimesajiliwa katika soko la Hisa, Ukiwekeza katika kampuni kubwa una hatari ndogo kuweza kupoteza mtaji wako.

SOMA; Weka Pamoja Vitu Hivi Vitatu Na Tayari Wewe Ni Mjasiriamali Mwenye Mafanikio Makubwa.

3. Wekeza kwa Kampuni ambayo inauza hisa zake kwa mara ya kwanza (IPO)

Njia nzuri kwa mwekezaji ambaye anao ujuzi mdogo kuweza kuwekeza katika soko la Hisa. Ni vizuri kuanza kuwekeza katika Kampuni ambazo zinauza Hisa zake kwa mara ya kwanza katika soko. Mara nyingi bei zake huwa chini ya thamani halisi hivyo ni rahisi bei kuongezeka zikisajiliwa katika soko. Nunua hisa kwa kampuni ambazo zinakaribia kusajiliwa katika soko la Hisa. Ili kufahamu kampuni ambazo zinauza hisa zake kwa mara ya kwanza tembelea www.dse.co.tz au nitakuwa natoa taarifa kupitia blog hii ya Jiongeze ufahamu au www.wekezamtanzania.blogspot.com .

SOMA; Maswali Matatu Kwa Anayetaka Kuwa Mjasiriamali Kujiuliza Kutoka Kwa Richard Branson.

Jinsi kuchagua kampuni inayofanya vizuri

Ufanisi wa Kampuni husika

Hapa tunaangalia ufanisi wa kampuni yenyewe kutokana na taarifa zake za fedha. Kwa mwekezaji anayeanza ataangali vitu vifuatavyo katika taarifa za fedha za kampuni

· Revenue/Sales/Interest income (Ukuaji wa mauzo)

· Net Income (Faida baada ya kutoa gharama zote pamoja na kodi)

· Earnings per share (kwa kiasi gani kila hisa imepata toka kwenye faida ya kampuni)

· Share Price (Bei za hisa kwa kipindi fulani)

· Dividend (Ukuaji wa gawio)

Kwa vitu ambavyo nimevionyesha hapo juu utaangalia katika taarifa za fedha za kampuni kupitia website ya DSE na kama unapata shida unaweza kunitafuta kwa mawasiliano nitakayoweka hapo chini.

Ili uweze kufanya kwa urahisi utaandaa table kama iliyopo hapo chini ili kuweza kujua ni kampuni ipi imefanya vizuri. Ili uweze kufanya uamuzi sahihi unatakiwa kulinganisha kampuni ambazo zinafanya biashara inayofanana.

2012

2013

MAKAMPUNI

Details

Ongezeko %

Nafasi

NMB

Interest income

287,923

355,686

23.5

3

Net Income

97,401

133,906

37.5

2

Earnings per share (EPS)

195

267.81

37.3

1

Share Price

1,120

2,620

133.9

1

DCB

Interest income

18,600

24,665

32.6

2

Net Income

1,908

3,711

94.5

1

Earnings per share (EPS)

50

55

10

3

Share Price

620

490

-20.9

3

Mabadiliko ya bei kwa kampuni zilizo katika soko la Hisa

Ni vizuri ukawa na taarifa ya mabadiliko ya bei za Hisa kwa Kampuni ambazo zipo katika soko la Hisa kwa miaka miwili nyuma. Ili uweze kufahamu ongezeko la bei za Hisa katika soko. Taarifa hizi zitakuasidia kujua kama kampuni bei zake zinaongeze, zinapungua au zinashuka kwa miaka miwili. Taarifa hizi utazipata kupitia website ya DSE.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

0 comments: