Haya Ndio Matumizi Mazuri Ya Mshahara Wako Ambayo Yatakuletea Furaha Na Mafanikio.

Mshahara ni makubaliano ya malipo kati ya mwajiri na mwajira kulingana na kazi anayofanya mwajiriwa. Malipo haya yanakuwa kwa muda au kipindi fulani kutokana na mkataba wao waliojiwekea.

Wakati mwingine unafanya kazi na kupata mshahara lakini hujui au hufahamu sehemu au makundi unayoweza kuugawa mshahara wako.

Zifuatazo ni bahasha tano ambazo unaweza kuugawa mshahara

1.SADAKA(Tithe Fund)

Unapopata mshahara wako asilimia kumi ya kipato chako yaani mshahara weka katika bahasha hii au mfuko huu wa sadaka. Kutoa asilimia kumi ya mshahara wako ni mwongozo wa kuufuata lakini siwezi kukulazimisha uamuzi uko mikononi mwako BO SANCHEZ katika kitabu chake cha My Maid Invest in the Stock Market alikuwa akiwaambiwa wafanyakazi wake yani wasaidizi wake hivi ‘’ You will grow in abundance think’’ usemi huu wa BO SANCHEZ una maanisha kuwa kuna faida sana pale unapotoa sadaka kama alivyonena hapo juu,  utakuwa katika uwezo mkubwa wa kufikiri’

SOMA; Tabia KUMI Za Watu Waliofanikiwa Sana(PICHA)

2. MATUMIZI ( Expense Fund)

Haya ni yale matumizi ya kila siku ya mahitaji ya nyumbani (daily needs) ambapo pia unaweza ukatenga fungu lingine la mshahara wako au kipato chako na kuweka katika bahasha hii ya matumizi.Hii itakusaidia sana kutotumia hela vibaya na kuwa na nidhamu ya pesa katika mshahara wako na itakusaidia kujuwa kwa mwezi matumizi yako yanagharimu kiasi gani.

3. MSAADA ( Support Fund)

Katika jamii zetu kusaidiana ni jambo la kawaida msaada huo unaweza ukatoa kwa ndugu,jamaa,marafiki na nk. Pengine ni kumsaidia mtaji wa kuanzisha biashara au kuboresha biashara na mengine mengi kuhusiana na msaada. Hivyo weka sehemu ya mshahara wako katika bahasha hii ya msaada hii itakusidia kutoharibu bajeti zako nyingine.

SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

4. DHARURA (Emergence Fund)

Katika maisha yetu ya kibinadamu huwa tunapatwa na dharura sana,na ubaya wa dharura unakuja pale umepatwa na tatizo halafu huna hela ya haraka ya kutatua jambo hilo lakini kama ukiwa umeweka sehemu ya kipato chako katika bahasha hii wala hutopata shida ya kulitatua. Dharura ni nyingi katika maisha na zinatokea kwa ghafla bila taarifa kama vile ajali, radi au kifo kinavyotokea. Ukiwa na fedha ya dharura itakusaidia kuwa na amani ya akili (Peace of Mind).

5. KUSTAAFU (Retirement Fund)

Hii ni njia moja nzuri ya kuweka akiba na kustaafu ukiwa milionea. Weka ,tenga akiba katika bahasha ya kustaafu na iwekeze hela hii katika soko la hisa . Hela hii weka katika bahasha ya kustaafu na usiitumie bali iwekeze katika soko la hisa na mwisho wa siku una staafu ukiwa milionea.

SOMA; Hivi ndivyo unavyoweza kununua Hisa katika soko la Hisa la Dar es salaam (DSE)

Gawa mshahara wako katika mafungu haya matano na utakuwa na maisha yenye furaha na mafanikio makubwa. Kwa kutoa sadaka utakuwa vizuri kiimani, kwa kutoa msaada utakuwa vizuri kijamii na kwa kuweka akiba na kuwekeza kwenye soko la hisa utajiandaa kwa maisha yako ya baadae.

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi Mhanasishaji na Mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba namba 0717101595 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com

0 comments: