Ushauri Kwa Waajiriwa Wapya Wote Wa Mwaka Wa Fedha 2014/2015

Habari mpenzi msomaji , na karibu tena katika usomaji wa makala kupitia tovuti hii kama ukitumia vema makala hizi za kila siku zinazotolewa na blog hii hakika utaboresha maisha yako kwa namna moja au nyingine.
Awali ya yote nitumie fursa hii kuwapongeza wote walioajiriwa mwaka wa fedha 2014/2015 katika sekta mbalimbali. Mara nyingi watu huwa wanajisahau sana pale tu wanapopata ajira. Leo napenda kukushauri mambo ya msingi ya kufanya ili uendelee kuboresha maisha yako.
Vitu ambazo unatakiwa kuvifanyia kazi ni;
1. Kuweka Akiba
Huwezi kufikia uhuru wa kifedha kama wewe ni mtu ambaye hujui kuweka akiba, mtu ambaye ukipata mshahara unatumia wote na kusubiri mwingine mwezi ujao. Hii ni tabia mbaya sana ambayo itakuletea athari kubwa sana mbeleni akiba haiozi hivyo basi ya kupasa kuweka akiba weka asilimia 10 ya mshahara wako katika akaunti maalumu ambayo itakusaidia ukiwa na dharura.
Umuhimu wa akiba utaujua pale tu utakapopata tatizo au dharura katika maisha kwani matatizo yapo kila siku na hakuna binadamu ambaye hana tatizo kila mtu ana matatizo yake hivyo basi anza sasa kuweka akiba ili ufikie mafanikio hapo mbeleni unapokuwa huna ajira.
SOMA; Kama Unataka Kumaliza Matatizo Yako Ya Fedha Fanya Kitu Hiki Kimoja.
2. Usitegemee Chanzo Kimoja Cha Mapato
Kuendelea kutegemea chanzo kimoja cha mapato yaani ajira ni hatari sana .hivyo basi nakushauri mbinu mbadala ya kuwa na vyanzo vingine vya mapato tofauti na ajira ambayo unayo kwa sasa buni miradi mbalimbali ambayo itakusaidia na kukupelekea kuwa na uhuru wa kifedha. Anza maandalizi sasa ya kuandaa kuwa na vyanzo vingine vya mapato tofauti na ajira.
3. Ishi Chini ya Kipato Chako
Hili limekuwa ni tatizo kwa watu wengi kuishi juu ya vipato vyao ,watu wamekuwa wanaishi maisha ya kuiga sana bila kuangalia kipato chake ni kidogo maisha ya kushindana ni mabaya sana. Kwa mfano unakuta mtu kipato chake ni laki mbili lakini mtu huyo anaishi maisha juu ya laki mbili hapo ndipo tatizo linapoanzia.
Kuishi juu ya kipato chako kitakupelekea kwenye madeni na kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo kabisa kwa sababu tu unaishi maisha ambayo siyo yako ishi maisha yako mwenye na wala hupaswi kuiga.
4. Kuwa na Nidhamu ya Pesa
Hata uwe na hela kiasi gani kama huna nidhamu na pesa ni tatizo sana, acha tabia ya kununua vitu kwa hisia kwa sababu tu Fulani kanunua na wewe unapata shauku ya kuwa nacho usitumie pesa ovyo tumia tu kwa mahitaji muhimu sana, punguza au acha kabisa starehe ambazo zinamaliza pesa zako kila siku acha kuwa mtumwa wa kisaikolojia wa uvutaji wa sigara, ulevi nakadhalika.
5. Endelea Kujifunza Kila Siku
Kumaliza shahada au stashahada siyo wa kusoma au mwisho wa kujifunza. Unahitajika kujifunza kila siku ,unahitajika kukua kila siku kesho uwe zaidi ya leo ulivyo sasa, ongeza maarifa chanya kila siku katika maisha yako. Chakula cha ubongo wako ni maarifa na akili yako ni kiwanda cha maarifa soma, soma, soma vitabu kadiri uwezavyo vitabadili maisha yako ,jifunze kwa waliofanikiwa utafika mbali kuliko kuendelea kuridhika na kujiona kuwa umeshamaliza chuo huna haja tena ya kujifunza.
SOMA; Kozi 1100 Unazoweza Kujifunza Bure Kupitia Mtandao.
Kwa hiyo , ili uweze kufika safari yako ya kimafanikio ya kupasa uwe na malengo na mipango juu ya maisha yako kuishi bila malengo ni sawa na kusafiri safari ambayo hujui unapokwenda ni wapi. Jali sana afya yako kwani katika safari ya mafanikio kitu cha kwanza cha kuzingatia ni afya. Kumbuka kujilipa pia 10% ya kipato chako pay yourself first hivyo basi zingatia kujilipa kwanza wewe kwani wewe ndio unafanya kazi na unawalipa watu wengi lakini unajisahau kujilipa na hela unayojilipa ifanyie uwekezaji ili ikusaidie.
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: