Hatua Saba (07) Muhimu Za Kukamilisha Malengo Yako Makubwa.

Watu wengi hufikiri kuwa na lengo lilio fasaha pamoja na kuwa na mtazamo chanya kuhusiana na ukamilishaji wa lengo ndio msingi mkuu wanaohitaji ili kuweza kuwa na furaha pamoja na kufanikiwa. Lakini kumbe hata kabla hujaanza safari yako ya kukamilisha lengo lako ni muhimu kuwa na mipango hatua kwa hatua inayokuhakikishia uwezekano mkubwa wa kukamilisha lengo lako.
Hapa ninakuletea hatua saba zitakazokuwezesha kukamilisha lengo lolote ambalo unajiwekea
1. Amua ni nini hasa unakihitaji katika kila eneo la maisha yako. Unahitaji kufafanua lengo lako katika lugha rahisi kiasi kwamba mtoto mdogo aweze kuelewa. Mfano unaweza kusema lengo lako ni kuwa na fedha nyingi, lakini uwingi wa fedha unazotaka haujaweka ni fedha nyingi kiasi gani. Sasa kutokuwa fasaha katika lengo kunakupelekea kutokuwa na hamasa na kufanya maamuzi ya kukamilisha lengo.
2. Andika lengo lako na lifanye liwe linaweza kupimika. Lengo ambalo halijaandikwa linakuwa ni lengo ambalo halijahuishwa au halijapewa nguvu ya kuwa hai. Ukilifanya lipimike maanake unakuwa umetengeneza tageti unayotaka kuifikia.
SOMA; Jinsi Ya Kutengeneza Kipato Cha Ziada Ukiwa Unaendelea Kufanya Unachofanya Sasa.
3. Weka ukomo wa kukamilisha. Unahitaji kuwa fasaha ni lini unahitaji kukamilisha lengo husika. Sehemu ya ubongo inayoitwa “subconscious” inapenda kuwa na ukomo na hii inakusaidia kuwa na nguvu na kukupa hamasa ya kuelekea kufanikisha lengo husika
4. Ainisha vikwazo ambavyo unahitaji kuvivuka ili kukamilisha lengo. Fahamu kitu gani kinaweza kwenda tofauti. Fahamu ni kitu gani kipo kati yako na lengo. Fahamu kwa nini bado haupo katika lengo lako.
5. Tambua maarifa na ujuzi wa ziada ambao utahitaji ili kuweza kufikia lengo lako. Ili kuweza kufanikiwa kukamilisha malengo ambayo hujawahi kuyakamilisha hapo kabla unahitaji kujifunza na kuwafanya vitu vya tofauti ambavyo hujawahi kufanya kabla.
6. Watambue watu ambao utawahitaji wakusaidie au waungane nawe ili uweze kufikia malengo yako. Kufikia malengo makubwa unahitaji kuwa natimu ya watu wengi wa kukusaidia. Kwa hiyo unahitaji kuwa na ufasaha ni watu wa aina gani hasa unaowahitaji ili uweze kuwa na timu ambayo itakupa msaada unaouhitaji.
7. Tengeneza orodha ya maelezo kwa kila kipengele ambavyo nimeanisha hapo juu na uweke mpangilio katika mfuatano yaani kipi kinaanza na kipi kinafuata na pia ni muhimu kuwa na kipaumbele. Ni muhimu kujua kipi unahitaji kwanza, kipi ni muhimu.
Baada ya kukamilisha hatua hizo saba ni muhimu kufanya kila siku japo kwa udogo sehemu ya kufikia lengo lako.
Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano:
Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blog yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.

0 comments: