Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu UNPROFESSIONAL.

Habari rafiki, ni matumaini yangu waendelea vizuri. Wiki hii tunaendelea na utaratibu wetu wa kushirikishana mambo 20 nilijifunza kwenye kitabu.  Leo tunaangazia kitabu kinachoitwa UNPROFESSIONAL. Kitabu kimeandikwa na Jack Delosa. Kitabu hiki kinaonyesha jinsi gani kijana Jack Delosa mwenye miaka 26 alivyoacha chuo na kuanzisha biashara na kua milionea mdogo katika nchi ya Australia. Unprofessional haimanishi kufanya mambo ya hovyo au kufanya mambo ya kudharauliwa, Unprofessional ni njia ya kutoa changamoto kwa maisha ya mazoea au kutoa changamoto kwa fikra za mazoea. Unprofessional ni Kubuni au kuvumbua njia yako katika kusonga mbele kutengeneza kesho yako nzuri.

Karibu tujifunze mambo mengine

1.     Usikubali sauti yako ya ndani uzimwe na makelele ya sauti za watu huko nje. Hizo sauti za watu wa nje zinataka uishi kama wao wanavyotaka...  Jifunze kujisikiliza, kuisikiliza sauti yako ya ndani ni muhimu sana.

2.     Mjasiriamali anayefanikiwa sana ni yule anayeweza kutengeneza vizuri ulimwengu ambao haukuwepo. Ni yule anayeweza kutengeneza bidhaa au huduma ambazo hazikuwahi kuwepo toka kuwepo kwa ulimwengu.

3.     Kuna mambo mengi ya muhimu katika dunia hii zaidi kuliko yale unayopaswa kujifunza shuleni. Usifungwe kwenye kile ulichojifunza shule peke yake. Yapo ya muhimu na mazuri sana ambayo hukuweza kujifunza shuleni. Kwa hiyo usiache kujifunza kisa eti una degree 1 au 2 au 3….. Hata profesa anajua vichache sana, ukilinganisha na vitu  vilivyomo….

4.     Biashara haiwezi kukua kuzidi mwanzilishi wake.  Ukitaka biashara yako ikue, lazima uanze kukua wewe kwanza. Ukiona biashara  inadorora ujue mwanzilishi/mmiliki wake naye kadorora.  Kiwango chako cha kujifunza ndicho kitakachoamua umbali gani biashara yako itafika.

5.     Ukiwa mjasiriamali lazima uwe mchunguzi, mara zote uwe unavumbua  mipaka mipya ya fursa. See things invisible

6.     Kitu kikubwa katika dunia ya leo ni kuongeza thamani kwenye maisha ya wengine na kuibadilisha dunia kua sehemu nzuri zaidi, Ukiweza kufanya hivyo watu hawajali au hawataangalia kama una sifa rasmi au hauna, hawaangalii wewe umesoma shule kiasi gani, kinachojalisha ni thamani gani unayoongeza kwa watu na dunia.

7.     Uhai wa biashara yako utategemea thamani unayowapa wateja wako. Don’t let anyone, especially the professionals, tell you any different

8.     Usisubirie upewe ruhusa au kibali, jiruhusu mwenyewe. Ruhusa/Kibali chako cha biashara ni uwezo wa kua na ndoto ya vitu ambavyo havikuwahi kuwepo awali, na ujasiri wa kuvijaribu.

9.     Kisababisho  cha kwanza  kikubwa  kinachosababisha kushindwa kwa biashara nyingi  hasa zinazoanza ni kukosa lengo (focus). Waanzilishi wa biashara hizo wanataka kugusa kila kitu, kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja, matokeo yake hawafanyi vizuri kwenye jambo lolote. Stick to the three rules of start-up: Focus. Focus. Focus.

10.                       Mjasiriamali unapaswa uzungukwe na watu nadhifu/makini kukuzidi wewe.  Unatakiwa wewe ndio uwe kilaza katika watu wanaokuzunguka. Wengi wetu tunapenda kuwepo kwenye makundi ya watu ambao wanakubali na ambao tumewazidi uwezo wa kiakili au kiuchumi . Kwa kawaida tunataka tukiwa kwenye makundi hayo sisi ndio tuonekane vichwa, na tunapenda sisi ndio tuwe tunamiliki mazungumzo.

11.                       Watu wa leo hakuna anayetaka kuuziwa, watu wanataka kununua na siyo kuuziwa, unachotakiwa kufanya ni kumsaidia mteja wako aweze kununua. Usijikite katika kuongea tu kuhusu biashara yako ili kumshawishi mtu anunue bidhaa au huduma yako, bali  mpe nafasi mteja aeleze hitaji lake.  It’s not about ‘selling’; it’s about providing the necessary leadership to enable your customers to buy.


12.                       Katika mwanzo wa biashara  mpya au mradi wowote mpya usiwekeze kwa kiwango kikubwa kwenye kitu chochote kabla ya kujihakikishia kwamba huduma au bidhaa unayotaka kuitengeneza ndiyo kitu wateja wanataka.

13.                       Kama unaweza kupata kundi la watu ambao wanatafuta kile unachotaka kuzalisha, basi kama ni vita basi umeshapata ushindi nusu. Nusu iliyobaki itategemea na ubora wa bidhaa utakayo wapatia

14.                       Wafahamu wateja wako vizuri. Katika biashara jinsi unavyowafahamu/unavyowaelewa vizuri wateja wako, ndivyo utakavyoweza kuwahudumia vizuri, na hii ndiyo itakayopelekea mafanikio ya biashara yako. Jitahidi kujua kwa nini wananunua kwako, je wanapata wapi taarifa, Week end zao hua wanakwenda wapi, marafiki zao ni kina nani, mara ngapi wananunua kutoka kwako, kwanini wanapendelea bidhaa au huduma zako kuliko za washindani wako,  ndoto zao ni zipi, hofu za pia ni zipi, wao wenyewe wanajionaje,  wanatamani kua nani. You need to get to know them better than they know themselves. Kinyume na hapo utafunga biashara, au utaishia kua na biashara ya kawaida sana.

15.                       Anza kabla hujawa tayari. Hua hakuna muda muafaka wa kuanzisha biashara,  hakuna siku ambapo utakua na muda wa kutosha,  fedha au taarifa za kutosha kuanzisha biashara, hakuna wakati ambapo utasema sasa niko tayari kila kitu kipo sawa.  Wajasiriamali halisi ni wale wanaonza kuchukua hatua kabla hawajawa tayari. Wakati wengine wanahangaika na kuweka mipango, kufanya utafiti au kusubiri, wajasiriamali halisi wao wanaendelea kusonga mbele tu.

16.                       Maono yako yanapokua makubwa ndio inakua rahisi kuyatekeleza. Mara kadhaa tumekua tukijidanganya kwa kuamini kwamba tunapokua na malengo madogo ndio inakua rahisi kuyafikia, lakini uzoefu umedhibitisha kwamba kinyume chake ndio ukweli. Ukweli ni kwamba unapokua na maono makubwa ndiyo yanakua rahisi kutekeleza, kwa sababu utapata watu ambao kweli watahamasishwa na maono hayo na kutamani kua miongoni mwa maono hayo. Hakuna anayetaka kua sehemu ya vitu vinyonge.


17.                       Kikwazo kikubwa katika ukuaji wa kampuni au mashirika ni pale waanzilishi/wamiliki wanapokua bado wanafikiri na kutenda vilevile kama walipokua wakianzisha biashara hizo. Hii itakua kikwazo cha ukuaji mpaka pale wamiliki watakapotambua kwamba wanasimamia kampuni au shirika ambalo linahitaji uongozi wa tofauti kabisa na wakati wa uanzishwaji wake..

18.                       Njia nzuri yenye ufanisi katika kujenga mahusiano mazuri na soko lako unalolilenga ni kuwaelimisha wateja wako kuhusu suluhisho ambalo wanafuata kwako kununua. Hii haimaanishi kuwaelimisha kuhusu biashara yako, bali kuwaelimisha kuhusu suluhisho wanalokuja kutafuta kwako (bidhaa au huduma unayouza). Kufanya hivyo utajenga imani kati ya wateja na biashara yako. Regardless of what business you are in, today you are in the business of education.

19.                       Katika ulimwengu wa kibiashara ushawishi unajengwa kwa kuzalisha kitu chenye maudhui makubwa (great content). Kama wewe ni mwandishi hakikisha unayoandika yana uwezo wa kuongeza thamani kwa msomaji. Ukifanikiwa kuandika vitu vyenye thamani, ushawishi kwa watu utakuja tu, utatengeneza hadhira kubwa.


20.                       Unapokua unataka kufanya ushirikiano wa kibishara wa kimkakati (strategic partnership), kwanza fahamu ni kitu gani mwenzako atanufaika nacho. Katika huo ushirikiano ni thamani gani uanyoweza kuitengeneza mwenzako anufaike?  Katika mwanzo wa mazungumzo kitu cha msingi unapaswa kuonyesha jinsi gani huyo mshirika wa kibiashara atanufaika kwanza. Ukitanguliza maslahi yako mbele hutafanikiwa. What you want out of the partnership should be secondary.

Asanteni sana
Tukutane wiki ijayo

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana naye kwa simu 0763 071007 au barua pepe daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com


0 comments: