Aina TANO(5) za Uwekezaji Zinazoweza Kubadili Maisha Yako



Ili kuweza kuwa na utajiri endelevu katika maisha yako na unaojitosheleza ni muhimu ukawa mwekezaji. Uwekezaji upo wa aina nyingi. Hapa ninakuletea aina za uwekezaji unazoweza kuzifanya ili kukuwezesha wewe na wale watu wako wa karibu kuishi maisha ya utajiri wa kujitosheleza:
1.     Uwekezaji binafsi
Watu ambao wanatengeza utajiri wanafanya uwekezaji binafsi . hawa wanakuwa wasomaji kwa kujifunza. Daima huweka jitihada ya kujiboresha wao wenyewe siku hadi siku na kuongeza mipaka ya maeneo ambayo wanona wakijaribu watafanikiwa. Wanaongeza maarifa na uwezo wa kushawishi siku hadi siku. Na kiwango cha jitihada wanachoweka katika kujiboresha huwa kipo katika hali ya kukua siku hadi siku.
2.     Kuwekeza kwa wengine
Mwanamafanikio maarufu duniani Zig Ziglar alisema ukitaka kupata kitu chochote katika maisha ni vizuri uwasaidie wengine wapate vile wanavyovihitaji katika maisha yao. Watu wenye utajiri utagundua wamewekeza kuwasaidia wengine wafikie malengo yao na hivyo kusababisha na wao kufanikiwa kwa kuwafanikisha wenzao

3.     Wekeza katika taasisi
Katika taasisi unayofanya wekeza katika kuijenga taasisi hiyo ili iweze kuwa bora na taasisi inapoweza kuwa bora inawezesha kuongeza upataji wa mapato. Kuongezeka kwa mapato kwa taasisi kwa ujumla kunasaidia pia wale waliosababisha kuongezeka kwa mapato kuneemeka na hiyo faida. Kwa hivyo hili likifanyika katika kipindi chako cha kutumikia taasisi yako maanake utaongeza kujenga utajiri siku hadi siku.
4.     Wekeza katika mali zinazoongezeka thamani
Ubadilishaji wa fedha kwenda katika mali ambazo zinaongezeka thamani na zinafanya kazi badala yako siku hadi siku huongeza utajiri kwako. Mfano wa hili ni nyumba ambayo imejengwa kwa lengo la kupangasha au kukodisha. Sasa ile fedha uliyowekeza katika hiyo nyumba utaipata kwa kuendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka bila yaw ewe kufanya kazi.
5.     Wekeza katika mawazo
Vitu vingi tunavyoviona leo havikuanza moja kwa moja bila kupitia hatua Fulani, vingi vilianza kama wazo na kuendelezwa. Mawazo amabyo ni mazuri yakichanganywa na uchukuaji hatua wa kuyaweka katika matendo huleta matokeo mazuri ambayo yanaleta utajiri


Mwandishi: Goodluck Moshi
Mawasiliano:
Whatsapp: +255 753 201 994, Telegram: +255 658 201 994, Barua pepe: eng.gmoshi@gmail.com Facebook: Goodluck Moshi
Pia unaweza kutembelea blog yake www.stadizamafanikio.blogspot.com kujifunza zaidi.

0 comments: