Tofauti ya mtazamo Kati ya Mtu wa Hali ya kati na Mtu wa hali Juu.

Kuna tofauti nyingi sana kati ya tajiri na masikini jinsi wanavyofikiri na kuwa na mitazamo tofauti. Mitazamo chanya na kufikri kichanya zaidi kwa matajiri kunawafanya wajizidi kuwa juu ukilinganisha na masikini jinsi wanavyofikiria. Zifuatazo ni mitazamo mbalimbali kati ya tajiri(world class ) na watu wa kipato cha kati yaani (middle class).

RICHGROW

Masikini huwa wanaamini kuwa pesa ndio mzizi wa maovu yote lakini matajiri huwa wanaamini kuwa umasikini ndio mzizi wa maovu yote. Kwa hiyo amua kujivunia kuwa tajiri na dharau kauli za watu wa kipato cha chini wanaokuambia kuwa tajiri sio sahihi .

SOMA; Fanya Mambo Haya Matatu Na Usipokuwa Tajiri Ndani ya miaka 10, sahau kuhusu utajiri kwenye maisha yako.

Masikini huwa wanaamini kuwa pesa ni ngumu sana kuipata wakati matajiri huwa wanaamini kuwa pesa ni rahisi kuipata kama ukiitega.

Masikini huwa wanaamini kuwa kama wakiwa matajiri watapoteza marafiki wao lakini Matajiri huwa wanaamini kuwa na marafiki kutawaongezea mtandao mkubwa zaidi wa kuwa tajiri.

Masikini huwa wanawafundisha watoto wao jinsi ya kuishi lakini matajiri huwafundisha watoto wao jinsi ya kupata au jinsi ya kuwa tajiri.

Masikini huwa wanaamini kuwa pesa inambadilisha mtu Lakini Tajiri anaamini kuwa pesa inaonesha mtu alivyo.

Tajiri anaamini kuwa kuwajibika au kujituma ndio njia salama pekee ya kupata pesa wakati masikini huwa wanaamini kuwa kazi ndiyo njia salama pekee ya kupata pesa.

SOMA; Njia KUMI Za Kubana Matumizi Yako Mwaka Huu 2015.

Watu wa kipato cha kati huwa wanaamini kuwa na pesa nyingi inakutengenezea matatizo mengi lakini watu wa kipato cha juu yaani (world class) wenye uhuru wa kifedha wanaamini kuwa na pesa nyingi inakupunguzia kuwa na matatizo mengi au kuwa na matatizo machache.

Masikini huwa wanaamini kuwa ukipata fedha nyingi kutakupelekea kuwa na mawazo (stress) lakini tajiri anaamini kuwa na fedha nyingi inasaidia kupunguza mawazo (stress) au kutokuwa na mawazo .

Matajiri wanafikiri kirefu au kikubwa (think big) wakati masikini wanafikri kidogo u kifupi (think small).

Matajiri wanaishi chini ya kipato chao lakini masikini wanaishi juu ya kipato chao. Hii ndio sababu ambayo inawafanya watu wengi kutofikia malengo yao kwa sababu wanaishi juu ya kipato chao na kupelekea kuwa na madeni mengi.

Watu wa kipato cha kati wanaamini kuwa matajiri lazima wasaidie masikini lakini matajiri wanaamini katika kujitegemea.

Watu wa kipato cha kati wanaamini tajiri wana akili sana lakini watu wa kipato cha juu wanaamini kuwa na akili sana kuna uhusiano mdogo sana katika kupata utajiri au kuwa tajiri.

SOMA; Jambo Muhimu La Kila Mfanyabiashara Kufanya Kila Siku.

Watu wa kipato cha kati wanaamini kuwa na pesa ndio kutengeneza pesa lakini watu wenye uhuru wa kifedha wanaamini kuwa kupitia au kwa kutumia watu wengine kupata fedha au kutengeneza fedha.

Hizi ni baadhi tu ya mitazamo kati ya watu wenye kipato cha kati (middle class) na watu wenye uhuru wa kifedha ( world class).

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe deokessy.dk@gmail.com au tembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: