Sababu Zinazokufanya Wewe Kushindwa Kuthubutu Wazo Lako

Watu wengi wamekuwa na mawazo mazuri sana ya kuthubutu ndoto zao, licha ya kuwa na mawazo mazuri sana ambayo yangeweza kuleta mabadiliko chanya katika jamii yetu ya leo kuna changamoto au sababu zinazowafanya washindwe kuthubutu ndoto zao. Nazo ni;

1. Woga / Hofu,

Woga au hofu siku zote huja pale mtu anaposhindwa kujiamini kuwa anaweza kufanya jambo fulani katika jamii husika . Hii ni sababu inayowafanya watu wengi kufa na mawazo yao mazuri ,kushindwa kuthubutu wazo zuri alilokuwa nalo pia kushindwa kuwa mbunifu katika kazi, biashara na hali kadhalika woga unamfanya mtu kuendelea kuwa mtumwa wa jambo fulani, kwa nini nasema kuwa mtumwa? Kufanya kitu chochote ambacho hukipendi ni utumwa hivyo basi ukitaka kuwa na mafanikio fanya kile unachopenda. Woga ni mbaya hatupaswi kuupa shukrani

SOMA; Ukweli Kuhusu Maisha Ambao Kila Mtu Anapaswa Kuujua.

2. Kutoamua kufanya Jambo hilo kwa Hamasa na Wakati

Ukishakuwa na wazo la kufanya jambo chanya ambalo litakuletea mabadiliko katika maisha yako anza hapo hapo ulipo usisubiri mpaka hamasa iliyokuwa ndani yako ya kufanya jambo hilo lipotee kabisa, ikishapotea hamasa basi na wazo lako litakufa kwa kushindwa kuthubutu kwa wakati. Usipoteze wakati au muda kwani muda ndiyo rasilimali tuliyopewa sawa sio kwa masikini au tajiri wote tuna muda sawa hakuna upendeleo katika hili.

3. Kuahirisha Mambo (procrastination)

Wengi wanashindwa kufanya mabadiliko katika maisha yao, wanashindwa kuthubutu mawazo yao kila siku kwa sababu ya kuahirisha mambo, tabia hii ya kusema nitafanya badaye ndio inakufanya wewe ushindwe kutimiza ndoto yako kwa wakati.

Mtunzi wa kitabu cha procrastinationTimothy anasema ‘’ ukitaka kufanya jambo Fulani anza kulifanya ‘’ Just start’’. Hivyo basi ili kuondokana na hali ya kuahirisha mambo kila siku anza kulifanya jambo hilo usisubiri itakusaidia kuthubutu ndoto yako .

Mpenzi msomaji wa makala hii ili uweze kufanikiwa na kuthubutu mawazo yako mazuri ambayo ulikuwa nayo au unayo kwa muda mrefu huu ndio muda wa kuthubutu kwa vitendo.

SOMA; Mara Zote Sema Ukweli, Ni Rahisi Kukumbuka.

4. Kuomba Ushauri kwa Watu Walioshindwa

Ukitaka kufanikiwa, kuthubutu mawazo ambayo unayo usiombe ushauri kwa mtu aliyeshindwa kwa sababu atakukatisha tamaa, omba ushauri kwa yule aliyefanikiwa ambaye alikuwa na mawazo mazuri kama uliyonayo wewe akaweza kuthubutu hatimaye kufanikiwa.

5. Kutojifunza kwa Bidii

Mafanikio yoyote yanatokana na kujifunza kwa bidii, kama wazo ni kuhusu biashara fulani jifunze sana kuhusiana na hiyo biashara, utakuwa bora na utaweza kutimiza ndoto yako.

Mtunzi wa kitabu cha The Entrepreneur MindKevin D.Johnson anasema, ili uweze kuwa mjasiriamali bora jifunze sana katika kile unachofanya tumia mbinu ya ‘’Ignorance can be bliss’’ Ujinga utakufanya kuwa na furaha kama ukijifunza.

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi,mhamasishaji na majasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au barua pepe (Email) deokessy.dk@gmail.com.au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

SOMA; Usiweke Maanani Unachoambiwa Na Mtu Aliye Kwenye Hali Hizi Tatu.

0 comments: