Hizi Ndizo Sifa Saba Za Kiongozi Bora.

Kila mtu ni kiongozi toka alivyozaliwa, yaani ni kipaji ambacho kila mtu huzaliwa nacho. Kila mtu ana uwezo wa kuwa kiongozi. Kila sehemu katika dunia hii huhitaji kiongozi, labda nikuulize swali, umewahi kuwa kiongozi? Jibu laweza kuwa ndiyo au hapana. Lakini hilo baki nalo kwa sasa. Niseme kwamba kama ukishindwa kuwa kiongozi wa watu wengi, utakuwa kiongozi wa familia yako kama baba au mama. Na kama hata hilo likikushinda basi wewe ni kiongozi wa maisha yako. Kuwa kiongozi wa maisha yako mwenyewe na usiruhusu mtu kuwa kiongozi na mwamuzi wa maisha yako. Kuwa bora au usiwe bora ni juu yako mwenyewe kuamua. Ukitaka kufanya chochote lazima ujifunze kuwa kiongozi bora kwani tayari umezaliwa kiongozi. Hizi ndizo sifa za kiongozi bora wa watu.

SOMA; Mahitaji Manne Ya Mtu Kuwa Kiongozi.

1. Kiongozi lazima awe na maono

Kiongozi ni lazima awe na maono ambayo ni tofauti wengine. Lazima awe na uwezo wa kuona vitu ambavyo watu wengine hawana uwezo kuviona. Ujue pia kuwa kiongozi alishawahi kuongozwa na akawa tofauti na watu wengine kwa kuona ambayo wao wameshindwa kuona.

2. Kiongozi huhitaji heshima

Kiongozi huhitaji heshima kutoka kwa watu wake na hata wa nje. Kiongozi lazima ajiheshimu ili aweze kuheshimiwa. Usilazimishe kuheshimiwa bali tengeneza mazingira ya kuheshimiwa.

SOMA; Nguzo Kuu Ya Uongozi; Tekeleza Kile Unachoahidi.

3. Kiongozi huona picha kubwa

Kiongozi lazima awe na uwezo wa kuona vitu vikubwa, maoni makubwa yaani picha kubwa. Kuna viongozi mfano wa Mwl. Nyerere, Mandela, Martin Luther King jr, Lincoln na wengineo, ni mfano wa viongozi waliokuwa na picha kubwa.

4. Kiongozi hujua ni wakati gani wa kubadili mwelekeo

Kuna wakati kiongozi hulazimika kubadili mwelekeo wa nguvu zake ama sera zake. Kama kiongozi bora kuwa na uwezo huo kutakusaidia sana katika kufanya maamuzi. Ni wakati gani wa kutumia nguvu kubwa, wakati gani utumie nguvu ndogo, wakati gani uache ama wakati gani wa kubadili mwenendo.

5. Kiongozi huweza kuona matatizo yalipo na kutafuta majibu

Kiongozi huweza kuona maeneo yenye matatizo na kuweza kutafuta suluhisho. Kujua tatizo lililopo sehemu ni nusu ya kulitatua. Ni dhahiri kuwa hutaweza kutatua tatizo usilolijua.

SOMA; Viongozi 100 Walioibadili Dunia.

6. Kiongozi lazima ajiamini na kuwa na mtazamo chanya

Kujiamini ni sifa kubwa katika kufanya mambo mengi. Ili uweze kujiamini ni lazima pia uwe na mtazamo chanya. Bila kujiamini na kuwa na mtazamo chanya na wenye kujenga sahau kuwa kiongozi mkubwa na bora. Kuwa na mtazamo chanya na mwenye kujiamini ili uweze kuaminiwa na wale unaowaongoza kwani hakuna mtu anayekubali kuongozwa na mtu asiyejiamini mwenyewe.

7. Kiongozi ni mwajibikaji

Kiongozi bora lazima aweze kuwajibika. Kuwajibika katika kutenda kazi na kusaidia watu. Pia kuwa tayari kung’atuka pale itakapoonekana kuwa umeshindwa kutekeleza matakwa ya watu wako. Kumbuka kuwajibika kwa nafasi yako kama kiongozi hata kama kosa hujalitenda kwako kwani hii itakuongezea sifa na heshima kwa watu wako. Usiwe king’ang’anizi wa madaraka pale utakapoona muda wako umeisha au hutakiwi na wale unaowaongoza.

Makala hii imeandikwa na Nickson Yohanes ambae ni mjasirimali na mhamasishaji.

Unaweza kuwasiliana na naye kwa : simu: 0712 843030/0753 843030

e-mail: nmyohanes@gmail.com

Pia unaweza kutembelea blogu yake: www.lifeadventurestz.blogspot.com kujifunza zaidi.

Makala imehaririwa kwa Kiswahili fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali Email: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

SOMA; Tabia Tatu Za Viongozi Dhaifu, Na Jinsi Ya Kuepuka Kuwa Mmoja Wao.

0 comments: