Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Na Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi.

Majukumu mengi sana yameongezeka sasa ukilinganisha na zamani. Kuna wakati watu tunahisi kama masaa yamekuwa yakienda haraka kupita zamani. Usiku ni mfupi na mchana ni mfupi pia. Ukiamka saa mbili basi ujue saa kumi na mbili jioni ipo karibu, saa kumi na mbili ikifika haujakaa vizuri saa nne usiku tayari unahitaji kulala na kesho uamke asubuhi mapema ili uendelee na mikiki mikiki ya maisha. Ukweli ni kwamba masaa ni 24 kama zamani na hakuna hata saa moja iliyopunguzwa na Mungu. Majukumu yamekuwa mengi, kumekua na maendeleo ya kiteknolojia na hivyo ndivyo vinavyofanya siku ,wiki, mwezi hata mwaka kuonekana mfupi na kujikuta hatujatimiza majukumu yetu kama tunavyotarajia.

clip_image001

SOMA; Siri Itakayokuwezesha Kufanya Chochote.

Hebu tupitie ratiba za wengi wetu katika ulimwengu huu wa sasa wa utandawazi,unaamka asubuhi kitu cha kwanza ni kuchukua simu yako ya kisasa (smartphone) na kuangalia ujumbe mfupi whatssap, baadaye telegram, ukimaliza, twitter baadaye kidogo unaingia facebookuonewaliowekapicha na habari mpya. Wakati huo umewasha TV yako ukisikiliza ni jambo lipi jipya limejiri. Bado hujaenda youtube kutafuta video, nyimbo mpya. Hivi kwa mtindo huu siku si itaisha hata hujakumbuka kusali wala kuangalia majukumu yako kijamii na kifamilia? Kwa namna hii ndoto zako utaishia kuota tuu au kupanga mipango bila kuwa na utekelezaji.

clip_image002

SOMA; Hiki Ndio Kitu Muhimu Sana Kwenye Maisha Yako. Na Sio Chakula Au Hewa.

Umeshajiandaa na unataka kufanya jambo la maana unasikia mlio mtu katuma ujumbefacebookunajifariji naangalia hii ya mwisho, unaona habari LULU atoa mpya. Unaingia mtandaoni kuona ni mpya ipi. Katika kuchunguza unaona ni kitu cha kawaida tuu, wakati unafikiri kuendelea na shughuli zako unaona habari nyingine Diamond kapata kashfa (scandal) unajifariji uchungulie dakika moja lakini haiwi hivyo. Unaenda nyingine hadi nyingine mpaka siku inaisha. Ufanye nini sasa? Tuungane pamoja wiki ijayo ili kujua ni namna gani unaweza kupanga majukumu yako vizuri ingawa kuna vitu vingi sana vinavyoweza kusonga ratiba zetu na majukumu yetu na kutufanya tuwe nje ya mstari.

MWANDISHI: ESTHER NGULWA

MAWASILIANO: 0767 900 110 / 0714 900 110

estherngulwa87@gmail.com

0 comments: