Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu Cha Megaliving -By Robin Sharma

Habari msomaji wa jukwaa la jiongeze ufahamu, Ni matumaini yangu unaendelea vizuri katika safari hii ya mafanikio. Katika safari ya mafanikio kujifunza kila wakati ndio njia ya uhakika ya kukufikisha kwenye mafanikio, na ndio lengo la Jiongeze Ufahamu. Katika kuhakikisha kwamba tunajiongeza ufahamu kwelikweli kila wiki tutakua tunashirikishana kwa ufupi mambo 20 niliyojifunza kutoka kwenye kitabu kimoja kati ya 2 ninavyosoma. Wiki hii tutaanza na kujifunza kutoka kwenye kitabu kizuri sana cha Megaliving kilichoandikwa na mwandishi mashuhuri duniani Robin Sharma.

Karibu sana:

1. Mafanikio ya nje yanaazia na mafaniko ya ndani.

2. Kama unataka kuongoza kampuni lazima ujifunze kujiongoza wewe kwanza.

3. Watu wengi ni wafungwa wa maisha yao ya nyuma. Lazima tufike mahali tuachane na kua wafungwa wa maisha yaliyopita ili kuanza maisha mapya mazuri

4. Mawazo yangu ya leo ndio yatakayotengeneza ndoto zangu za kesho.

5. Kitu cha kwanza kuepukana na utumwa wa mawazo, ni uelewa. Kwanza anza kwa kutambua mawazo ambayo yamekua yakikurudisha nyuma. Tafuta karatasi yaandike mambo hayo. Halafu weka mikakati ambayo utaitumia kuondokana na mawazo hayo.

SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Na Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi.

6. Orodha ya ndoto. Andika chini orodha ya ndoto ambazo unatamani zitimie maishani mwako

7. Tumezungukwa na utajiri mwingi tu, na wanaoweza kuupata ni wale tu wanaotambua hilo na kua na fikra chanya ambazo zinawasaidia kuona fursa mbalimbali zinazowapelekea kuupata utajiri huo

8. Usijilinganishe na wengine. Kimbia mbio zako mwenyewe

9. Kinachowatenganisha waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni hiki; Waliofanikiwa wanayo njaa au kiu kubwa sana ya kupata wazo jipya na maarifa mapya, wakati wasiofanikiwa wanabweteka na hali walio nayo, hawana kiu ya kujifunza vipya.

10. Wasomaji ni viongozi, utakua kiongozi mkubwa pale tu utakapojijengea tabia ya kujiendeleza wewe binafsi kwa kusoma vitabu vizuri kwenye Nyanja husika.

11. Huwezi kuwa mtu mkubwa katika Nyanja yeyote mpaka umeanza kuhisi kua wewe ni mkubwa

12. Washindi ni watu wenye nidhamu ya hali ya juu

13. Watu wenye mawazo chanya ndio wanao ongoza kila sehemu, kama baishara, uongozi, familia, elimu n.k. Hii ina maana kama una mawazo hasi hutaweza kushindana na mwenye mawazo chanya…

14. Washindi hua wanatengeneza mikakati ya kunufaika kutokana na changamoto wanazokabiliana nazo, wanahakikisha wanashinda kwa gharama yeyote. Washindi lazima wapate njia tu.

15. Hakuna kitu kinachoweza kumzuia mtu aliyekataa kuzuiliwa.

SOMA; Fursa katika Kilimo cha Bustani

16. Hakuna kinachoweza kumzuia mtu mwenye mtazamo sahihi wa kiakili asiweze kufikia malengo yake, lakini pia hakuna kitu chochote hapa duniani kinachoweza kumsaidia mtu mwenye mtazamo hasi.

17. Malengo ni msingi wa muhimu sana katika maisha. Kama huna malengo huwezi kujua unakokwenda, yaani utaenda kila mahali maana hujui unakotaka kwenda hasa.

18. Kusudi la Maisha ni Maisha yenye kusudi.

19. Vikwazo vinavyokuzuia wewe kupata vile amabavyo ungeweza kuvipata ni vile ulivyojiwekea mwenyewe kwenye mawazo yako.

20. Hata ukimuomba Mungu ufanikiwe kama huta chukua hatua sahau kuhusu kufanikiwa. Wengi wanafikiri wakimuomba Mungu awafanikishe ni kwamba atawateremshia mafanikio toka mbinguni na wao wakiwa wamekaa hapohapo walipo. Kwanza Jua ni nini unataka kisha Muombe Mungu sawa kabisa, lakini chukua hatua zinazostahili.

Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana nae kwa simu 0763 071007 au 0658 587029 au email daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com

0 comments: