Vitu Vitatu Vinavyoathiri Kipato chako Kwenye Chochote Unachofanya.

Katika uchumi tunaoishi, kipato chako kitategemea vitu vitatu;

  1. Nini unafanya. Kama unachofanya ni muhimu sana, basi hata kipato chako kitakuwa kikubwa.
  2. Unakifanya kwa kiwango gani. Kama unafanya kwa viwango vya juu sana basi kipato chako kitakuwa kikubwa. Kama unafanya kawaida basi kipato chako kitakuwa cha kawaida.
  3. Ugumu wa kukubadilisha. Kama ni vigumu kupata mtu mwingine anayefanya kama wewe basi thamani yako itakuwa kubwa na kipato chako kitakuwa kikubwa pia. Kama ni rahisi kupata mwingine, yaani unachofanya kila mtu anaweza kukifanya thamani yako itakuwa ndogo na kipato chako kitakuwa kidogo pia.

Hii ni sahihi kwenye kazi, biashara na hata shughuli yoyote ya kiuchumi unayofanya. Jitahidi uwe bora zaidi na kipato chako kitakuwa kikubwa sana. Haijalishi ni kazi au biashara gani unayofanya, kinachojali ni ubora unaotoa.

Dunia inalipa ubora.

0 comments: