Mambo KUMI Ya Kufanya Ili Usiishi Maisha Ya Majuto.

Maisha ya majuto sio maisha mazuri kuishi. Ni maisha ambayo yatakufanya ukose furaha na hivyo kuona maisha yako hayana thamani.

Lakini pia majuto mengi ambayo watu wanaishi nayo ni ya kujitengenezea wenyewe iwe kwa matendo yao au kwa mitazamo yao.

Leo utajiongeza na mambo KUMI unayoweza kuanza kufanya leo ili uweze kusihi maisha yasiyokuwa na majuto.

1. Jali afya yako. Hiki ni kitu muhimu sana, ukiwa na afya mbovu utajutia mambo yote ya hovyo uliyofanya yakakupeleka kwenye afya mbovu.

SOMA; NENO LA LEO; Acha Kujiandaa Kuishi…

2. Tenga muda wa kufanya vitu unavyovipenda. Hata kama una kazi ngumu kiasi gani, tenga muda kila siku wa kufanya vitu ambavyo unavipenda kweli kwa moyo wako.

3. Pata muda wa kupumzika, cheka , cheza.

4. Sema kile ambacho unataka kusema. Unafiki utakufanya ujute sana baadae.

5. Badili mtazamo wako.

6. Usiumizwe na yaliyopitwa, usiogopeshwe na yajayo, ishi leo.

SOMA; UKURASA WA 19; Ishi Leo..

7. Kubali kwamba kuna vitu huwezi kuvibadili.

8. Acha kukimbiza fedha na mali, toa huduma nzuri na fedha zitakufuata zenyewe.

9. Shukuru kwa maisha uliyonayo, hata kama ni magumu kiasi gani.

10. Onesha upendo kwa kila mtu anayekuzunguka.

Maisha ni yako na una uamuzi wa kuyaishi vile unavyotaka kama tu hauvunji sheria na taratibu. Chagua kuishi maisha ambayo utayafurahia kila siku ili uweze kuwa na maisha bora. Fanya mambo hayo kumi kuanzia leo na maisha yako yataanza kubadilika.

SOMA; Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..

0 comments: