Jinsi ya kuzuia hatari ya kupata hasara kupitia uwekezaji katika hisa

Uwekezaji katika hisa ni kama biashara nyingine unaweza kupata hasara au faida, ila uwekezaji huu ni wa upekee ni jinsi ambavyo unafanyika. Ili uweze kukuza thamani ya pesa yako kupitia uwekezaji katika hisa na kuondoa hatari ya kupoteza pesa yako kuna vitu vya kuzingatia.

Jinsi ya kuzuia hatari ya kupata hasara kupitia uwekezaji katika hisa

1) Wekeza katika kampuni ambayo inafanya vizuri

Ili kuondoa hatari ya kupoteza pesa yako kupitia uwekezaji katika hisa ni kuwekeza katika kampuni ambazo zinafanya vizuri. Kuwekeza kwa kampuni ambazo zinafanya vizuri ni rahisi kukuza mtaji wako na kupata gawio lako. Katika somo lililopita tumeona jinsi ya kuchagua kampuni ambayo inafanya vizuri, kwa hiyo ni vizuri kwa mwekezaji kuwekeza katika kampuni ambayo inafanya vizuri.

SOMA; Kila Sehemu Utakayokwenda Utawakuta Watu Hawa.

2) Wekeza kwa muda mrefu

Unapoamua kuwekeza katika hisa ni vizuri ukawa na malengo ya kuwekeza kwa muda mrefu. Uwekezaji wa muda mrefu una manufaa makubwa kwa mwekezaji na unapunguza hatari ya kupata hasara. Huwezi ukawekeza kwa mwezi mmoja na ukasema wewe ni mwekezaji bali wewe ni mtu ambaye anabahatisha au mtu ambaye ana Bet. Kuonyesha jinsi gani kuwekeza kwa muda mrefu kuna manufaa kuna moja wa msomaji katika blogu yangu ya www.wekezamtanzania.blogspot.com alikiri kuwa alinunua hisa za kampuni ya SWIS mwaka 2013 kwa bei ya shilingi 2000 na mpaka sasa hisa za kampuni ya SWIS zinauzwa kwa shilingi 6,500. Bei ya hisa imeongezeka mara tatu ya bei ya mwanzo, kuwa na malengo ya kuwekeza kwa muda mrefu kuna manufaa makubwa kwa mwekezaji.

SOMA; BIASHARA LEO; Fukuza Wateja Hawa, Ni Mzigo Kwako.

3) Wekeza kampuni zaidi ya moja

Njia nzuri ya kulinda na kukuza uwekezaji wako ni kuwekeza kwenye kampuni zaidi ya moja katika soko la hisa. Ukiwekeza kwenye kampuni tatu au zaidi ikiwa kampuni moja haitofanya vizuri utafidiwa na ukuaji mzuri wa kampuni nyingine katika soko la Hisa. Hii ni njia mojawapo ambayo ina manufaa makubwa kwa mwekezaji. Ikiwa unataka kuwekeza unaweza ukatenga kiasi cha mwezi wa kwanza unanunua hisa katika kampuni ya SWIS, mwezi mwingine unanunua za CRDB na mwezi unaofuata unanunua za TBL. Au unaweza ukagawa kiasa sawa kwa kampuni ambazo umechagua kuwekeza mfano. SWIS 25%, CRDB 25%, TBL 25% na NMB 25% ni asilimia ishirini na tano ya akiba yako ya kuwekeza.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com/0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

SOMA; Haya Ndio Matumizi Mazuri Ya Mshahara Wako Ambayo Yatakuletea Furaha Na Mafanikio.

0 comments: