Hiki Ndio Kitu Kitakachokuletea Mafanikio Ambacho Tayari Unacho.

Vitu vyote hapa duniani ambavyo tunaviona vilivyotengenezwa na binadamu, vimetokana na mawazo ya mtu, ambayo mawazo hayo yameweza kuleta mapinduzi makubwa hapa duniani. Mpaka leo mimi na wewe tunatumia vitu ambavyo vimetokana na mawazo ya watu .

Ukiwa na wazo au mawazo ya kutengeneza jambo Fulani basi wewe ni tajiri kama ukilifanyia kazi wazo lako kwa vitendo sio kuishia kuongea tu. Watu wote waliofanikiwa hapa duniani walianza kufikiria ,halafu wakapata wazo wakaweza kuthubutu na kuleta matokeo chanya katika jamii. Mfano simu au compyuta unayotumia leo kusoma makala hii yalikuwa ni mawazo ya mtu ambaye aliweza alithubutu kwa vitendo hatimaye akaleta matokeo chanya duniani.

SOMA; BIASHARA LEO; Kwa Nini Watu Hawawaambii Wengine Kuhusu Biashara Yako.

Hivyo basi hata wewe usife na wazo au mawazo yako mazuri uliyokuwa nayo ambayo yanaweza kuleta mabadiliko makubwa sana katika jamii yetu. Acha tabia ya kuhairisha mambo (procrastination) Anza SASA kuthubutu wazo lako na wewe najuwa utakuwa na mawazo mazuri sana ambayo ulikuwa nayo ungetamani kuyathubutu leo.

Ifuatayo ni kanuni ambayo inaonesha namna gani wazo au mawazo yako yanavyofanya kazi na kanuni hii kila mtu anaitumia pengine kwa kujua au kutokujua .

THOUGHTS (T) + FEELINGS (F) +ACTIONS (A) =RESULTS(R)

Ufafanuzi wake ni huu hapa MAWAZO +HISIA+VITENDO =MATOKEO

Kila kitu huwa kinaanza na mawazo ambayo yanazalishwa na akili yako kama tulivyoona hapo juu katika kanuni elekezi , na usemi huu unawezwa kudhihirishwa pia na mtunzi wa kitabu cha Secrets of the Millionaire Mind –T . Harv Eker ambaye alisema hivi ‘’everything begins with your thoughts which are produced by your mind ‘

SOMA; UKURASA WA 95; Fanya Kwa Kiasi.

Hisia (feelings), baada ya kuwa na wazo au mawazo ya kufanya jambo Fulani, kuna kitu kinakuja ndani yako kama tulivyoona katika kanuni elekezi ambacho kinakusukuma kufanya jambo hilo kwa shauku ,hisia nazo zinazalisha kitu kipya yaani hatua nyingine ya kuthubutu kufanya jambo hilo.

Vitendo (actions),baada ya kuwa na wazo ukapata hisia ya wazo lako hatua inayofuata ni vitendo ambapo hapa sasa ndio unaweza kuthubutu wazo lako na kupelekea hatua nyingine ambayo ni matokeo.

Matokeo (results) hapa ndio hitimisho la wazo lako, baada ya kuwa na wazo,ukapata hisia ya kufanya jambo hilo ukaweza kuthubutu kwa vitendo na hatimaye ukapata matokeo .

SOMA; NENO LA LEO; Mipango Sio Muhimu Kama Kitu Hiki.

Hivyo basi , tumeona kuwa kila kitu huwa kinaanza na mawazo hata wewe unaweza kutengeneza wazo lako zuri leo na kubadili kabisa fikra yako na kuwa na mtazamo chanya unaoweza kubadili maisha yako. Mtunzi wa kitabu cha The Magic of Think Big –David J.Schwartz ,ph.d anasema kuwa binadamu ni zao la mawazo yake mwenyewe , ‘’ A person is a product of his own thoughts’’

’ Your mind is a thoughts factory ‘’ – Akili yako ni kiwanda cha mawazo

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe (E-mail) deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea blog yake (tovuti) kwa kujifunza zaidi www.actualizeyourdream.blogspot.com

0 comments: