Nilichojifunza Leo; Zoezi Moja Litakalobadili Maisha Yako Kabisa.

Nilichojifunza Leo

Leo nilipata wasaa wa kukutana na Mimi mwenyewe. Jana kabla ya kulala nilipanga appointment ya kukutana na Mimi mwenyewe asubuhi na mapema. Mbinu hii ya kukuta na mimi nilijifunza kwa rafiki yangu Amani Makirita . Nilipokutana na mimi tulijadili na kujifunza mambo kadha , kwa leo ngoja nikushirikishe nilijchojifunza kuhusu Mabadiliko.

Karibu kwenye somo

• You must change you self before changing others. The most difficult person to change is yourself
Ni rahisisi sana kumwambia mwenzako “unatakiwa ubadilike bwana” je umeshawahi kukaa peke yako ukajisemesha maneno hayo? Kumbuka ni rahisi kutamani kuona wengine wakibadilika, lakin wengi wetu hatuko tayari kubadilika sisi wenyewe. Kubadilika sio kitu kirahisi unahitaji nguvu ya ziada. Maana akili yako na mwili wako vilishakua na mazoea Fulani (status quo). Sasa katika kubadilisha mazoea hayo kuna kua na upinzani wa hali ya juu, Maana tunapenda kua katika hali tuliyoizoea maana hapo ndipo tunapokua comfortable. Sasa unapojaribu kutoka kwenye hiyo hali lazima uweke mikakati mizuri na uweze kuifutilia kuifanya mara kwa mara bila kujali unajisikia kufanya au hujisikii mpaka pale umepata yale mabadiliko unayoyatamani. Kumbuka ni rahisi kurudia hali ya mwanzo kuliko kufikia kwenye mabadiliko.
Mabadiliko ya kweli ni yale yanayokufanya kua mtu bora zaidi kuliko ulivyokua hapo awali. Katika mchakato wa mabadiliko utaumia, wakati mwingne utaona kama unajitesa vile. Lakini usiyatazame hayo Tazama kule unakotaka kufika, kama wewe ni Daudi, au John au jina lolote, mtazame Daudi au John unayetaka kumuona baada ya mabadiliko hiyo itakutia hamasa ya kuendelea mbele na mchakato wa kubadilika. Pia furahia kuona mabadiliko madogomadogo maana hayo ndiyo yatakayopelekea mabadiliko makubwa.

Fanya appointment na wewe binafsi, jipe muda wa kukutana na wewe mwenyewe. Jipe muda wa kujisikiliza. Mbona hua unapanga appointment na watu kibao. Lakin Je hua unapata wasaa wa kukutana na wewe binafsi? Au wewe sio wa muhimu kwako?

Nafikiri tukutane tena na tutaongelea zaidi jinsi ya kukutana na wewe na ni nini cha kusema unapokuna na wewe na faida zake.
Nakuachia hizi nukuu mbili za watu mahiri kabisa:

1. “Mabadiliko ya kweli lazima yaanze na wewe kubadilika. Kama hujabadilika wewe usijisumbue kumwambia mwingne abadilike” Daudi Mwakalinga

2. Change will not come if we wait for some other person or some other time. We are the ones we've been waiting for. We are the change that we seek. - Barack Obama

Hakuna lisilokua na mwisho. Kinachodumu ni mabadiliko. Nakutakia kila la kheri katika safari ya mabadiliko.

Daudi Mwakalinga
CC:
Makirita Amani
Unaweza pata kitabu kizuri sana kinachohusiana na Mabadiliko. Nashauri sana kitafute. tembelea hapa kujua zaidi JINSI YA KUFAIDIKA NA MABADILIKO YANAYOTOKEA.

Makala hii imeandikwa na Daudi  Mwakalinga.

0 comments: