Hii Ndio Njia Moja Muhimu Ya Kufikia Mafaniko Makubwa.

NJIA MOJAWAPO YA MAFANIKIO NI KUWA MWENYE BIDII

Katika kila jambo kunahitajika bidii. Bidii ni nguvu ambayo inamwezesha mtu kufikia malengo yake aliyojiwekea ili aweze kufanikiwa.

Mpendwa msomaji wa makala hii ukitaka ufaulu katika jambo lolote lile lazima ujijengee tabia ya kujituma ,maana maendeleo yoyote yale katika jambo lolote yanahitaji mtu anayejituma.

SOMA; Kama Tayari Una Ndoto Hiki Ndio Unatakiwa Kufanya.

Mawazo ya mtu mwenye bidii siku zote huelekea utajiri tu. Utajiri unakuja baada ya kufanyia kazi mawazo yako kwa bidii. Mtunzi wa kitabu cha Who will Cry When You Die-Robin Sharma anasema ‘’ Live your life in such away that when you die the world cries while you rejoice’’ maana yake ‘‘ ishi maisha yako kiasi kwamba siku ukifa dunia nzima italia wakati wewe unafurahia’’ hivyo basi usemi huu unatuasa tuweke bidii ili tuweze kufanikiwa na kuleta matokeo chanya katika jamii.

SOMA; Njia Moja Ya Uhakika Ya Kuishinda Hofu.

Hivyo basi, mafanikio yeyote duniani katika nyanja yeyote ile yanaletwa na bidii yako katika jambo hilo unalowekea bidii, bidii inatumika katika biashara, elimu, michezo, uongozi nakadhalika.

‘’ You can not see, what you don’t look for’’ maana yake huwezi kuona kwa kile ambacho hukitafuti ‘’ mtunzi wa kitabu cha The Compound EffectDarren Hardy amedhihirisha hilo katika usemi wake hapo juu. Hivyo basi, tunapaswa kuwa wenye bidii katika kazi, masomo, biashara nakadhalika ili tuweze kufanikiwa katika maisha yetu na kuleta mabadiliko chanya katika jamii zetu tunazoishi.

SOMA; Kitu Hiki KImoja Kitakufanya Ushindwe Kwenye Biashara.

’Mawazo ya mwenye bidii huelekea utajiri tu bali mwenye pupa huelekea uhitaji’’

Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi mhamasishaji na mjasiriamali unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe (E-mail) deokessy.dk@gmail.com

Makala imehaririwa kwa Kiswahili fasahanaRumishael Peterambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na MjasiriamaliEmail: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

0 comments: