Maswali ambayo huulizwa mara nyingi kuhusu uwekezaji katika hisa.

Watu wengi wanatamani kufanya uwekezaji katika hisa na kufahamu jinsi ambavyo uwekezaji huu unavyofanyika ila kuna vitu vingi hawavifahamu katika uwekezaji. Maswali haya yatakufungua mwanga jinsi ya kutambua uwekezaji katika hisa, jinsi ambavyo unafanyika na jinsi ambavyo mwekezaji atapata manufaa katika uwekezaji huu.

1. Nini ushiriki wa soko la hisa (DSE) katika kupanda na kushuka kwa thamani ya Hisa?

Soko la Hisa (DSE) haihusiki kabisa katika kuchangia kupanda na kushuka kwa thamani ya hisa. Vitu ambavyo vinasababisha kushuka na kupanda kwa za hisa ni nguvu ya soko (yaani wanunuzi na wauzaji). Wanunuzi wakiwa wengi katika hisa ya kampuni Fulani hupelekea kupanda kwa bei kwa sababu watashindana kwa bei ili kila mtu aweze kununua hisa hizo.

2. Wapi unaweza kupata bei za hisa?

Ili uweze kupata taarifa za bei ya hisa za kila siku tembelea tovuti yao ambayo ni www.dse.co.tz. Katika tovuti yao utaweza kufahamu bei za kampuni ambazo zimeongezeka na kampuni ambazo bei zake zimeshuka.

SOMA; Changamoto Inayokusumbua Kwenye Biashara.

  1. Naweza kununua hisa kuanzia ngapi?

Kiwango cha chini cha kununua hisa katika soko ni hisa 100 ila mwekezaji unaweza kununua hisa chini ya mia moja kwa lugha kingereza huitwa odd lots board. Kwa hiyo mwekezaji yoyote anaweza kununua hisa chini ya mia moja katika soko la hisa yaani unaweza nunu hisa 5, 10, 20 au zaidi.

4. Hisa zinauzwa wapi?

Hisa zinauzwa sehemu mbili i) katika soko la wali, hapa ni pale kampuni ambapo inauza hisa zake kwa mara ya kwanza kabla ya kusajiliwa katika soko la hisa. ii) Hisa zinauzwa kwa madalali wa soko la Hisa au unaweza nunua katika tawi la benki ya CRDB lolote lile. Anwani za madalali wa soko la Hisa zinapatikana katika tovuti ya DSE au soma makala hivi ndivyo unavyoweza kununua hisa.

5. Nalipia hisa mara moja tu au ni kila mwezi kwenye Kampuni husika?

Ukinunua hisa pesa unatoa mara moja tu, ikiwa utahitaji kununua hisa zingine utalipia kwa hisa ambazo unaongeza. Baada ya kununua hisa zako hakuna gharama nyingine zaidi ya kusubiri hisa zako kuongezeka thamani na kupata gawio. Ikiwa utahitaji kununua hisa nyingine utalipia kwa bei ambayo ipo sokoni.

SOMA; KITABU; Jinsi Ya Kufaidika Na Mabadiliko Yanayotokea Kwenye Maisha.

  1. Kwa sisi tulioko mikoani tunawezaje kununua hisa?

Mmoja wa madalali wa soko la Hisa ameingia ubia na benki ya CRDB kwa hiyo popote lililopo tawi la benki ya CRDB unaweza ukanunua hisa. Vile vile kuna kampuni nyingine za madalali ambalo watafanya utaratibu wa kununua hisa.

  1. Je unaweza kupata taarifa za utendaji na ufanisi wa kampuni unapokuwa mwanahisa?

Kampuni yoyote ambayo imesajiliwa katika soko la hisa ni lazima iweke taarifa zake muhimu kuhusu utendaji wake na taarifa za fedha za kila mwaka, miezi mitatu na miezi sita. Kama mwekezaji taarifa hizi zitakusaidia kujua kampuni ambayo inafanya vizuri na ambayo haijafanya vizuri ili uweze kuchagua kampuni bora ya kuwekeza.

  1. Hisa zinapatikana muda wote au ni kwa muda Fulani tu?

Kuna aina mbili ya masoko ya hisa, soko la awali ambapo hisa huuzwa kwa mara ya kwanza na kwa kipindi maalumu tu na kuna soko la upili ambapo soko la hisa halina kipindi maalum unaweza kununua na kuuza muda wowote iwe tu ni siku ya kazi (Jumatatu hadi Ijumaa). Katika soko la upili ndipo soko la Hisa linapofanya kazi zake kila siku ya kazi ambapo mwekezaji atanunua na kuuza hisa zake.

SOMA; Haya Ndio Matumizi Mazuri Ya Mshahara Wako Ambayo Yatakuletea Furaha Na Mafanikio.

  1. Je gawio hutolewa mara ngapi na kampuni kwa wawekezaji?

Gawio hutolewa kulingana na sera ya kampuni husika. Kuna kampuni ambazo hutoa gawio mara mbili kwa mwaka na kuna kampuni ambazo hutoa gawio mara moja kwa mwaka. Ukiwa mmiliki wa hisa unayo haki ya kupata gawio ikiwa kampuni itatoa gawio hilo kulingana idadi ya hisa ambazo unamiliki.

  1. Je nikifariki hisa zako atamiliki/atarithi nani?

Soko la hisa limeandaa utaratibu ambao kila mwekezaji ambaye ananunua hisa katika fomu ambazo unapewa utajaza mrithi wako. Mrithi wa hisa unaweza kumchagua mtu yoyote Yule ambaye wewe ungependa awe mrithi wako.

Endelea kutembelea mtandao huu kuendelea kupata makala nzuri kuhusu uwekezaji katika Hisa na mfulululizo wa maswali na majibu kuhusu bidhaa ya Hisa.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano emmanuelmahundi@gmail.com simu 0714445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania.blogspot.com

Makala imehaririwa kwa Kiswahili fasaha na Rumishael Peter ambaye ni Mhariri wa vitabu/makala za Kiswahili na Mjasiriamali Email: rumishaelnjau@gmail.com simu 0713 683422.

0 comments: