Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu Kinaitwa SELF-IMPROVEMENT 101.

Habari rafiki, ni matumaini yangu waendelea vizuri. Wiki hii tunaendelea na utaratibu wetu wa kushirikishana mambo 20 nilijifunza kwenye kitabu. Leo tunajifunza kutoka kwenye kitabu kinaitwa SELF-IMPROVEMENT 101. Kitabu kimeandikwa na mwandishi aliyebobea kwenye maswala ya uongozi, mwandishi anayeheshimika katika eneo lake la kutengeneza viongozi, sio mwingine mwandishi huyo ni John Maxwell.
Kitabu hiki kinahusu jinsi ya kujiboresha wewe binafsi, ukitaka biashara yako ikue lazima ukue wewe kwanza maana Biashara haiwezi kukua kukuzidi wewe mmiliki. Lakini pia mwandishi anasema kwamba unapojiboresha na vinavyokuzunguka ghafla vinakua bora. Na wengi hawatambui hili, wanahangaika kujaribu kuboresha wengine au biashara zao mwishowe wanashindwa. Sasa njia rahisi ya kufikia mafanikio ni kujiboresha wewe, na njia nzuri ni kuchagua kua mwanafunzi wa kudumu.
Usikome kujifunza, soma vitabu, majarida, hudhuria semina na tafuta mtu (mentor) aliyefanikiwa katika eneo unalotaka kujiboresha jifunze kwake. Heshimu mentor wako na pia fanyia kazi anachokuelekeza, usionyeshe kwamba una uwezo wakati unahitaji kujifunza. Mwishoni anasema gharama ya kutojiboresha ni kubwa sana kuliko ya kujiboresha. Lipa gharama sasa hivi, maana gharama ya baadaye ni kubwa sana.
Kwa ufupi kitabu hiki ni kizuri sana. Hupaswi kukosa mambo ya wiki hii.
Karibu tujifunze mambo mengine.
1. Ukuaji lazima uwe wa kukusudia, kama unataka kukua lazima ukusudie. Tunaweza kutamani maisha yetu yawe bora lakini tukaishia kutamani, tukifikiri ukuaji unatokea tu kama ajali. Kuna tofauti ya kutamani (wish) na kukusudia (intention). Kukusudia kunaambatana na utendaji. Growth must be intentional— nobody improves by accident.
2. Kila mtu anafikiria kuibadilisha dunia, na hakuna anayefikri kujibadilishe yeye mwenyewe kwanza. Watu wengi wanapambana na mabadiliko (fight against change) hasa kama yanawagusa kibinafsi. Unapaswa kutambua kwamba mabadiliko hayaepukiki, lakini pia kwa upande mwingine mabadiliko ni uchaguzi. Unaweza kuchagua kukua au kupambana na ukuaji. But know this: people unwilling to grow will never reach their potential.
3. Tofauti ya Waliofanikiwa na wasiofanikiwa haipo katika uwezo wao na watu wengi hawatambui hilo. Watu hawa Wanatofautiana kwenye shauku (desire) ya kufikia uwezo wao. Maana shauku hii ndiyo inayowasukuma kujifunza ili kukua kufikia uwezo wao. And nothing is more effective when it comes to reaching potential than commitment to personal growth.
4. Watu wengi hua tunasherehekea pindi tunapopata diploma au digrii (shahada) zetu na tunajisemea “Asante Mungu imepita hiyo” Ngoja sasa nipate kazi, maana nimemaliza kusoma/kujifunza. Lakini Fikra za mtindo huu hazitakupeleka mbali zaidi ya kuishia kua mtu wa wastani tu. Unapomaliza shule yako sio mwisho wa kujifunza, ndio kwanza kunakua kumekucha. Maana ukienda mtaani unagundua kumbe kuna vitu vingi sana ambavyo hukuweza kujifunza pindi ulipokua shuleni. If you want to be successful, you have to keep growing. The happiest people I know are growing every day.
5. Chagua maisha ya ukuaji (Choose a life of growth). Njia pekee ya kuboresha maisha yako ni kujiboresha wewe mwenyewe. Kama unataka kukuza shirika au kampuni lazima ukue kama kiongozi. Kama unataka kua na watoto bora lazima uwe baba bora kwanza. Kama unataka kupata mke/mume bora lazima wewe binafsi uwe bora kwanza. Hakuna njia ya uhakika ya kuwafanya watu wanaokuzunguka kua bora. Watu wengi wanasumbuka kweli kuboresha watu wanao wazunguka lakini wanashindwa. Kitu pekee ambacho kweli unao uwezo wa kukiboresha ni wewe mwenyewe. Na maajabu ni kwamba ukifanya kitu hicho (kujiboresha) kila kitu kinachokuzunguka ghafla kinakua bora. So the bottom line is that if you want to take the success journey, you must live a life of growth. And the only way you will grow is if you choose to grow.
6. Anza kukua leo. Sio kile utakachofanya, bali ni kile unachofanya sasa hivi ndio kinachojalisha. Usisubiri kuanza Kukua kesho, anza leo. Watu wengi ambao hawajafanikiwa wana ugonjwa unaoitwa “siku moja” nitafanya hiki au kile, wakati wangeweza kuanza mara moja kufanya vitu vyenye kuleta thamani kwenye maisha yao, lakini hawafanyi na kuishia kusema ipo siku nitafanya. The best way to ensure success is to start growing today. No matter where you may be starting from, don’t be discouraged; everyone who got where he is started where he was.
7. Ukuaji hautokei moja kwa moja (Growth is not automatic). Unaweza kua mdogo mara moja tu, lakini unaweza kua mchanga (Immature) kwa muda usiojulikana, hii ina maana ukuaji hauji automatic. Sio kwa vile umri unakwenda basi ufikiri ndio unakua, sio hivyo. Unaweza kua na miaka 50 lakini bado ukawa mchanga. Ukuaji unahitaji kuweka juhudi za dhati. The sooner you start, the closer to reaching your potential you’ll be.
8. Ukuaji wako wa leo ndio utakaofanya kesho yako iwe bora. Kila unachofanya leo kinajijenga kwenye kile ulichofanya jana, na vyote (vya jana na leo) ndivyo vitakavyoamua kesho yako itakua vipi. Growth today is an investment for tomorrow.
9. Ukuaji wako ni wajibu wako. Ulipokua mdogo wazazi wako walikua na wajibu kwako, hata elimu na ukuaji wako ilikua ni wajibu wao. Lakini sasa umeshakua mtu mzima, wewe ndio unabeba wajibu mzima wa maisha yako. Usipofanya ukuaji wako kua wajibu wako, basi ujue kamwe haitatokea.
10. Kamwe usiridhike au kubweteka na mafanikio uliyoyapata. Adui mkubwa wa mafanikio yako ya kesho ni mafanikio yako ya leo. Maana unapojiona umefanikiwa leo na kubweteka, unakua unahujumu mwenyewe mafanikio yako ya kesho. Kule kufikiri kwamba “umefika” unapofanikisha lengo kuna madhara sawa na kuamini kwamba unajua yote. Hii inaondoa hamasa au shauku ya kujifunza zaidi. Huu ni ugonjwa na watu wengi wanaumwa na huu ugonjwa. Lakini watu waliofanikiwa hawapumziki na kusema sasa nimefika, wanatambua kwamba kushinda kama ulivyo kushindwa ni jambo la muda kidogo (temporary), kwa hiyo wanafahamu fika wanapaswa kuendelea kukua zaidi na zaidi ili kuendelea kua na mafanikio. Don’t settle into a comfort zone, and don’t let success go to your head. Enjoy your success briefly, and then move on to greater growth.
11. Unapaswa kuwa mwanafunzi wa kudumu. Kama tulivyoona kwamba adui mkubwa wa mafanikio yako ya kesho ni mafanikio yako ya leo, ili kuweza kuvuka hiki kikwazo lazima uwe mwanafunzi wa kudumu. Ukiwa mwanafunzi wa kudumu hutabweteka na mafanikio uliyoyapata, utagundua kwamba vipo vingi sana vya kujifunza, na hapo ulipo bado sana hujaweza kufikia uwezo wako ulionao. Watu wengi walio fanikiwa wanasonga mbele kwenye mafanikio kwenye muda uleule ambao wengine wanaupoteza. Kumbuka unapopoteza muda, kuna mwingine muda huo anautumia kujiboresha na kusonga mbele, na kamwe hamtaweza kua sawa, lazima awe mbali tu.
12. Tengeneza mpango wa Kukua/kujiboresha (develop a plan for growth). Ufunguo wa kua na maisha ya kujifunza na kujiboresha bila kukoma umejificha kwenye mpango maalumu wa kujifunza. Weka mpango wa kila siku, andika mpango wako mahali, kwenye mpango wako andika vitu ambavyo unataka kujifunza, andika pia na njia utakazotumia kujifunza. Inaweza kua ni kwa kusoma, kuhudhuria semina, kufanya maongezi na wale waliofanikiwa kwenye eneo unalotaka kujifunza n.k Ukimaliza kazi iliyobaki ni kuwa na nidhamu ya kutendea kazi mpango huo. Usiruhusu udhuru. No excuse
13. Kama ulichokifanya jana bado kinaonekana ni kitu kikubwa basi ujue leo umefanya kidogo tu au haujafanya kabisa. Mara nyingi utasikia watu wakisifia uwezo wao au mafanikio yao ya siku za nyuma. Utasikia “ yaani mimi nilikua kichwa balaa, nilikua naongoza darasani” au “yaani enzi zangu ungenikuta kwenye ubora wangu nilikua ni shiiida” Sasa ngoja ni kwambie kitu Ukiona unajisifia kuhusu jana ujue leo hujafanya kitu.
14. Kwa kujiboresha wewe dunia nayo inakua bora. Usiogope unapokua kwa taratibu, cha kuogopa ni kusimama tu sehemu moja, au kudumaa. Sahau makosa uliyofanya lakini usisahau yale uliyojifunza kutoka kwenye hayo makosa. Jinsi gani unaweza kua bora kesho? Ni kwa kua bora leo. Anza kujiboresha leo
15. Wakati mzuri wa kupanda mti ulikua ni miaka ishirini iliyopita, ila wakati mwingine mzuri na sahihi wa kupanda mti ni leo. Yamkini unatamani ungeanza mapema , au pengine unatamani ungepataga mwalimu mzuri au mshauri mzuri miaka kadhaa iliyopita. Hakuna hata moja hapo lenye kuleta maana. Kuangalia nyuma na kuanza kulalamika hakutakusaidia wewe kusonga mbele. Muda ulionao sasa ndio una uwezo wa kuutumia kubadilisha maisha yako.
16. Adui mkubwa wa kujifunza ni kufahamu/kujua. Lengo la kujifunza ni kutenda na sio kufahamu/kujua, kwani ukishajua na kukaa nacho tu kina faida gani? Wengi wanaingia kwenye mtego wa KUJUA, pengine una digrii yako au masters yako, unafarijika kwamba unajua vitu vingi hivyo unaona huna cha kujifunza tena. Unaishia kusema kwa maneno mimi ni graduate au mimi nina master.. so what? Tunachotaka kuona ni utendaji na sio maneno yako. Unapojifunza zaidi ndipo unagundua kumbe hujui vingi na utaendelea kuwa na hamasa ya kujifunza. Huwa napenda kujifunza kutoka kwa tajiri Warren Buffet, japo ana umri zaidi ya miaka 84, na ni tajiri wa 3 wa ulimwengu, lakini haachi kujifunza kwa kubweteka kwa mafanikio aliyonayo, sasa wewe ni nani wakati hata kwenye kitongoji chako tu kwenye orodha ya watu matajiri haupo.
17. Kama unachokifanya hakina mchango kwako au kwa wengine basi hebu kaa chini uhoji uthamani wa hicho unachokifanya, na uhalali wa wewe kuendelea kukifanya kama hakina thamani kwako wala kwa wengine.
18. Wafanye marafiki zako kua waalimu wako, tengeneza marafiki ambao wanaokupa changamoto na kuongeza thamani kwako, na wewe pia ujitahidi kuongeza thamani kwao.
19. Kama wewe una kipaji sana, unaweza kua na wakati mgumu kufundishika. Kwanini? Kwa sababu watu wenye vipaji mara kadhaa hudhani kwamba wanajua kila kitu. Na hivyo kufanya vipaji vyao kushindwa kuongezeka/kutanuka zaidi. Kufundishika haina maana sana kuhusu uwezo au uwezo wa akili kama ilivyo kuhusu mtazamo. Kufundishika ni ile shauku au nia ya kusikiliza, kujifunza, na kutendea kazi. Ni kule kua na njaa ya kugundua na kukua. Teachability is the willingness to learn, unlearn, and relearn.
20. Kipaji peke yake hakitoshi kukufanikisha. Unaweza kuwa na kipaji na wala kisikusaidie. Tumeona watu wengi wenye vipaji ambao wameishia kuzika vipaji vyao kwa sababu moja kubwa ambayo ni Kutokufundishika. Wengi wamekua wakidhani ukiwa na kipaji basi mafanikio umepata. Kua na kipaji ni kitu kimoja tena cha kawaida sana, maana kwa taarifa tu ni kwamba kila mtu ana kipaji chake. Kua na kipaji ni kitu kimoja na kuweza kukifikisha kipaji chako hatua ya juu ni kitu kingine. Ujuzi ambao ni wa muhimu sana ambao unapaswa kua nao ni kujifunza jinsi ya KUJIFUNZA (learning how to learn), ukifaulu hapo lazima kipaji chako kitakupeleka hatua za juu.
Asanteni sana tukutane wiki ijayo. Kama utapenda kupata kitabu hiki Nitakupatia bure kabisa, niandikie email kupitia dd.mwakalinga@gmail.com
Makala hii imeandikwa na Ndugu Daudi Mwakalinga mwandishi, mhamasishaji na mshauri katika masuala ya kilimo. Unaweza kuwasiliana nae kwa simu 0763 071007 au email daudimwakalinga@yahoo.com au dd.mwakalinga@gmail.com Tembelea blog yake www.kilimobiasharablog.blogspot.com na ujifunze mengi kuhusu kilimo.

0 comments: