Siri Moja Kubwa Ya Kufanikiwa Kwenye Ujasiriamali.

Unapokuwa mjasiriamali elimu yako ndio imeanza. Kwa kweli ili uweze kuwa juu kwenye ujasiriamali ni lazima uendelee kutafuta maarifa yatakayokufanya wewe na biashara yako kuwa bora zaidi.
Mjasiriamali anayeacha kujifunza ni mjasiriamali anayeacha kufaidika.
Wajasiriamali wanajifunza kupitia kusoma vitabu, kujifunza kuhusu watu waliofanikiwa, kusoma majarida yanayohusiana na wanachofanya, kuhudhuria semina na makongamano na njia nyingine nyingi.
Je wewe unatumia njia ipi kujifunza?

0 comments: